Ligi Kuu ya Tanzania kwa mzunguko huu wa lala salama, hakuna Klabu ya mpira yenye uwezo wa kuifunga
Simba SC kutokana ubora wa kikosi.
••Watafanya Nini Sasa Uwezo Hamna
Simba SC imekuwa ikitandaza gozi la ng'ombe vema kabisa kwa viwango vya juu, huku wakipiga pasi za maana zilizothibitishwa na
Shirikisho la soka Afrika (CAF) na kusababisha
Simba SC kupata matokeo chanya.
Klabu hiyo ya
Wekundu wa Msimbazi wao wanachokifanya ni kutiririka tu kwenye mtelemko wa kuzoa pointi tatu kila mchezo, Yanga kachukua kidude 1-0 Uwanja wa Taifa, African Lyon kagaragazwa 3-0 Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Azam FC kachapwa 3-1 Uwanja wa Taifa, klabu ambazo kidogo zilikuwa zikitegemewa kuleta upinzani wa kupata walau sare, kwa mukhadha huo hakuna kwa sasa timu ambayo itaifunga
Simba SC kwenye TPL.
••Mwana Kulitaka Mwana Kulipewa
Katika mwendelezo wa kukusanya pointi tatu tatu kila sehemu, kwa sasa kituo kinachofuta ni Ipogolo mkoani Iringa ambapo Lipuli watalazimika kushuka katika eneo lao nakuacha pointi tatu huku safari ya
Watakatifu Simba ikiendelea.
Klabu ya Simba imeondoka leo kuelekea mkoani Morogoro ambapo leo jioni watafanya mazoezi kisha kesho asubuhi wataanza safari kuelekea mkoani Iringa ambako Jumanne itakipiga na
Wanapaluhengo Lipuli FC.
Niiii
Ghazwat kwa niaba ya
sembo OKW BOBAN SUNZU Shunie King Ngwaba Sapta Sapta Tui tunawaambia watani zetu
Sibonike Mwana Mtoka Pabaya Shadeeya Prince Kunta Kila timu ishinde mechi zake..!
View attachment 1030312View attachment 1030313View attachment 1030314
Sent using
Jamii Forums mobile app