Hakuna ubaya wowote wala ajabu yoyote Marais kupanda pamoja! Tulipanda basi moja na Rais Mkapa nchini Sweden

Hakuna ubaya wowote wala ajabu yoyote Marais kupanda pamoja! Tulipanda basi moja na Rais Mkapa nchini Sweden

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
53,857
Reaction score
121,995
Wanabodi

Hii issue ya Rais Samia kupandishwa basi moja na viongozi wengine wa Afrika kwenye mazishi ya Malkia, imegubikwa maneno mengi, ujuaji mwingi, na kujua kwingi, lakini ukweli wennyewe halisi, tatiza ni ushamba tuu mwingi zaidi ya uhalisia!. Watu wakimuona Rais lazima apande benzi na kutembea na msafara, basi wanadhani Rais akipanda basi anakuwa sio Rais au amedharauliwa!. Nini basi, watu tumewaona marais wanatembea kwa miguu na wengine wanatumia baiskeli kwenda kazini!

Natoa wito kwa sisi Wabongo tupunguze ushamba jameni!, hakuna kitu cha ajabu yoyote kwa viongozi kupanda usafiri wa pamoja wa basi as long as issue za kiusalama zimezingatiwa. Viongozi wa Africa kuwekwa basi moja, sio ubaguzi, ni kuwaweka like people close together, Asian nao waliwekwa basi lao, European nao na lao etc ili kule wazungumze mfano Mama Samia was close to Ruto!.

Mwaka 1998, Katika ziara yake nchini Sweden, rais Benjamin Mkapa na ujumbe wake na mwenyeji wake, Waziri Mkuu wa Sweden, na sisi waandishi wa habari, wote tulipanda basi moja kutoka Stockholm kwenda Uppsala. Hivyo ni jambo la kawaida sana, when in Rome, do as the Romans does! Misafara ya viongozi inachosha, inatesa na kurudisha nyuma maendeleo, IGP Sirro peleka Traffic Sweden kujifunza misafara ya wenzetu, Time is Money!

Mwaka 1995 tulisafiri ndege moja na Waziri Mkuu Fredric Sumaye, kwenda South aboard Alliance Air. Ndege ikafika few minutes ahead of schedule, hivyo kushuka abiria wote mnaingia kwenye zile basi trums za airport, hivyo tukashuka na Sumaye na mkewe na walinzi wote kwenye basi na halina siti!, hivyo tunapanda basi moja na Waziri Mkuu wa nchi yako halafu anashika mchuma!

Ile trum inaondoka ndipo motorcade ya kumpokea inaingia hapo uwanjani, huku balozi Ami Mpungwe behind the stearing wheel akiendesha mwenyewe, anashuka na kupungia mkono trum lisimame, ndipo Waziri Mkuu wetu na msafara wake wakaachia mchuma na kupokelewa!

Kiukweli sisi wabongo kwa kushadadia mambo madogo madogo yasiyo na maana yoyote!, nilidhani watu wangenote organization ya msiba, watu wanavyolia kizungu! Hakuna watu kughalaghala na kukanyagana, hakuna Red Cross walio busy kubeba watu waliozimia.

Misiba TV zetu huku misiba ya viongozi ni nyimbo za maombolezo, TV za wenzetu msiba wa kiongozi ni documentaries za her legacy!. Full time ni interviews kumhusu Malkia, sikuona kiongozi yoyote akihojiwa hata Waziri Mkuu wao!, huku ni mihotuba na mihotuba ya viongozi kuchoshana tuu bure!

Msafara wa mwili just 5 cars piki piki tatu mbele, mbili nyuma, ingekuwa ni huku!. Kunapotokea misiba kama hii, ya wenzetu walio staarabika, we should use them as a learning experience, sisi tunashikia bango Rais wetu kupanda basi as if Mama Samia ni katope, angeyeyuka!

Mbona viongozi kupanda mabasi ya pamoja ni kawaida, hili jambo linafanyika kila siku kwenye mikutano ya nchi za Jumuiya ya Madola and in fact its a good thing viongozi wana ji mix na ku mingle!

Hata siku ya Uhuru pale uwanja wa taifa, mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao, wanakuja pale Karimjee wanakuwa dropped off, kisha wanapanda usafiri wa pamoja, wanapelekwa uwanja wa Taifa na mabasi maalum, baada ya shughuli mabasi yanawarudisha Karimjee ndipo kila mmoja anapeperusha tena bendera yake kwenye magari yao!

Kipi cha ajabu jameni?, ushamba ukizidi nao ni issue. Natoa wito kwa Venus Nyota, fanya utaratibu wa kusafiri na few private media ili wakati wewe unatuma press release za hard news, hao private media watume color stories, Watanzania wapatiwe exposure na wajue mambo mengine ya mambo ya kimataifa.

Paskali

Rejea Ukiwa Rais katika nchi za Kiafrika unapewa utukufu uliopitiliza
 
Hatushangai peke yetu, Kiongozi wetu pia ameonekana kwenye basi akishangaa kupandishwa humo na kutofurahia kuchukuliwa picha!

Kama ni kweli ni jambo la kawaida kupanda basi, mbona hawapandi mabasi special kwenda Dodoma bungeni Ili kupunguza gharama na kuachana V8?
 
Nafikiri you don’t get the logic, karibia kila mtu anajua kwamba siyo ishu kupanda basi, ishu ni kwamba kwa nini huku kwetu hilo haliwezekani? Umeshaona msafara wa Waziri wa Fedha Mwigulu? Kwa nini tusimamishwe masaa 2 kupisha mkubwa apite?

Bora hata zamani ilikuwa ni raisi, Makamu wake na Waziri Mkuu basi, nakumbuka hata Mkuu wa Majeshi tulikuwa naye foleni, lkn leo hii kila mtu anapewa msafara, sasa kwa nini? Mbona huko kwa Wazungu mnakoomba hela mnapanda basi kutunza mazingira na kubana matumizi?
 
Sawa tunakubali kaka. Siye tumeona yawezekana viongozi wetu wanaweza bana matumizi kwenye shughuli kama hizo. Iwe mikutano ya chama. Kumpokea rais kutoka nje. Na hafla nyingine zozote kubwa. Yawezekana wakakwea hiace. Coaster na hata daladala. Kumbuka nchi yetu maskini wa kutupa. Kuna ubaya gani viongozi wetu wenye weledi wakaamuwa kufanya hivyo kama Ulaya?

Ya nini kumpa shida zaidi mlalahoi wakati yawezekana?
 
Umetumia nguvu nyingi kuelezea jambo lililo wazi. Nadhani hakuna anayeshangaa viongozi hao kupanda basi huko Uingereza. Kilichowakera wengi ni ule ukweli kwamba kwa nini viongozi hawa hawa wanaoonekana "humble" wamekaa kwenye basi huko kwa wazungu wakiwa huku nyumbani wanahitaji msafara wa ma-vieite 50+? Kama kwa matajiri huko convoy ya kiongozi inakuwa na gari zisizozidi tano (tena gari za kawaida tu), kwa nini hao viongozi wetu wakija huku wanahitaji mamisafara hayo makubwa yasiyo na faida? Umetaja Norway sijui Sweden, misafara ya viongozi huko ikoje?

Kuwa mwangalifu sana kuita watu wajinga na sijui washamba. Mara nyingi ukichunguza vizuri utakuta kuna mantiki kubwa imejificha katika "ujinga" na "ushamba" wao.
 
Mimi nilitamani viongozi wa Africa ndo wapandishwe Yutong. Maana kiukweli hamna wanachotusaidia zaidi ya wizi na kutupa ahadi za Uongo na kuweka vitu vinavyotukandamiza kisha tukihoji tunajibiwa majibu yanayokaribiana na kejeli au unapotezwa!

Wenye umuhimu wamepewa kipaumbele kabisa VVIP.

Watu kama viongozi wa East Africa kwa kweli wangewapandisha tlhata Saratoga au Adventure na Champion! simjui vizuri baharia William Ruto !! wangejichagua miongoni mwao nani aendeshe basi!

Heshima inatengenezwa bhana , sio kitu kila mtu anastahili

Na ngoja warudi maana tulivyowananga mtandaoni 😁😁😁
 
Back
Top Bottom