Braza Kede
JF-Expert Member
- Nov 1, 2012
- 3,840
- 6,844
- JF, Insta, facebook na magazeti vyote, vingejaa picha na jumbe za Tanzia.
- Akaunti nyingi za kijamii hasa za watu maarufu kama wanamuziki wasanii wanasiasa mainfluencers zingesimama kufanya kazi.
- Baa kubwakubwa na sehemu nyingi za starehe zingefungwa maana wamiliki na baadhi ya wahudumu nguli hawajiwezi tena wamerudishwa makwao kwa uangalizi wa afya zao au wameshatangulia mbele za haki.
- Mitaa na vichochoro vingi vingejaa matenti ya wadau wakishiriki shughuli za wapendwa wao.
- Nyumba nyingi zingekuwa na walau mgonjwa mmoja mwenye ugonjwa usioeleweka.
- Nyumba nyingi zingebaki chini ya uangalizi wa watoto maana wazazi hawajiwezi au wameshatangulia mbele za haki.
- Ambulance na mahospitali yangekuwa bize kushughulikia wahanga, homa zingine zingasahaulika kwanza.
- Baadhi ya Ofisi kubwakubwa za serikali bunge mahakama na za binafsi zingefungwa kwa kupoteza watendaji wake muhimu au wahusika kuhudhuria mazishi ya mfanyakazi mwenzao.
- Humu Jf nyuzi za mambo ya mahaba zingepungua kama sio kwisha kabisa.
- Humu Jf nyuzi za kutukuza na kusifu utukufu mkuu wa muumba zinģetamalaki na kupata mashiko ya hali ya juu.
- Kungekuwa na misururu mikubwa ya costa za abiria hasa kutoka Dar kwenda mikoani zikisafirisha wapendwa wao wakiwa wagonjwa au wafu kwenda maeneo mbalimbali ya nchi.
Wakuu HIV ipo, tujilinde!
- Akaunti nyingi za kijamii hasa za watu maarufu kama wanamuziki wasanii wanasiasa mainfluencers zingesimama kufanya kazi.
- Baa kubwakubwa na sehemu nyingi za starehe zingefungwa maana wamiliki na baadhi ya wahudumu nguli hawajiwezi tena wamerudishwa makwao kwa uangalizi wa afya zao au wameshatangulia mbele za haki.
- Mitaa na vichochoro vingi vingejaa matenti ya wadau wakishiriki shughuli za wapendwa wao.
- Nyumba nyingi zingekuwa na walau mgonjwa mmoja mwenye ugonjwa usioeleweka.
- Nyumba nyingi zingebaki chini ya uangalizi wa watoto maana wazazi hawajiwezi au wameshatangulia mbele za haki.
- Ambulance na mahospitali yangekuwa bize kushughulikia wahanga, homa zingine zingasahaulika kwanza.
- Baadhi ya Ofisi kubwakubwa za serikali bunge mahakama na za binafsi zingefungwa kwa kupoteza watendaji wake muhimu au wahusika kuhudhuria mazishi ya mfanyakazi mwenzao.
- Humu Jf nyuzi za mambo ya mahaba zingepungua kama sio kwisha kabisa.
- Humu Jf nyuzi za kutukuza na kusifu utukufu mkuu wa muumba zinģetamalaki na kupata mashiko ya hali ya juu.
- Kungekuwa na misururu mikubwa ya costa za abiria hasa kutoka Dar kwenda mikoani zikisafirisha wapendwa wao wakiwa wagonjwa au wafu kwenda maeneo mbalimbali ya nchi.
Wakuu HIV ipo, tujilinde!