DOKEZO Hali ni mbaya sana kwa walemavu tuliosoma, Si Serikali wala kampuni binafsi ambazo ziko tayari kutuajiri. Tunabaguliwa

DOKEZO Hali ni mbaya sana kwa walemavu tuliosoma, Si Serikali wala kampuni binafsi ambazo ziko tayari kutuajiri. Tunabaguliwa

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Unadhani hata wasio walemavu hali zao zipo poa ? Mkuu ni pote tu na sio Afrika tu bali duniani nguvu kazi is no longer required; Ingawa kwa Tanzania yetu tungeweza kutokuwa na shida hii kutokana na kwamba tuna resources za kumwaga..; na sasa hivi nyie walemavu mnalalamika kesho tutakuwa na wazee ombaomba sio kwamba wanalalamika tu bali kila tukipiga tambo watakuwa wanatusimamisha na kutuomba omba

 
Pole sana mkuu.

Umejaribu kupitia ajira portal ?.
Huko private nina-uzoefu nako ni kugumu sana kwa watu wenye ulemavu kukupokea na sometime huwezi kuwalaumu, wale wanaangalia faida zaidi kuliko hali zetu. Na baadhi ya taasisi za serikali hawazingatii kabisa izo 3% na 50% ufaulu za walemavu kwenye ajira zao sijui kwanini.

Kuna group kubwa la whatsap la watu walemavu, nile namba PM wakuunge.
Hii 3% ingekuwa inatekelezwa hii Tatizo lingepungua sana!!

Mfano mtu ambaye hatekelezwi kanuni hio anafungiwa leseni yake ya biashara au analipishwa faini kubwa!! Tatizo lingepungua
 
Niende kwenye mada moja kwa moja!!.

Nimekuwa moja ya wahanga wa hili Tatizo kwa muda mrefu sana

Kati ya watu wanaosoma kwa mateso makubwa sana ni watu wenye ulemavu, kuanzia shule za msingi mpaka sekondari, hii inatokana na miundo mbinu mingi kuwa tofauti na Hali zetu watu wenye ulemavu.

Wakati mtu mwenye ulemavu anapambna akiamini kuwa yeye hawez kulima, kutembeza mitumba, Wala kufanya kazi ngumu za ujenzi akitegemea akili yake tu ya darasani angalau impe mwanga wa maisha.

Baada ya ajira huyu mtu mwenye ulemavu anaanza kuzunguka na baiskeli yake au magongo yake kweny interview mbalimbali, wakati mwingine hufanyika mikoani, au kwenye majengo yasiyo na lift.
Wengi wanaishia kukata tamaa sana.

Kuna sehemu niliwahi kataliwa kabisa kisa mimi ni mlemavu kwamba siwezi kufanya hio kazi kwasababu nitakuwa naenda sana hospitali, yaani trip kazini trip hospitali. Wanahisi labda sisi ni wagonjwa fulani hivi,

Inaumiza sana sana, naongea kwa niaba Yao sana.

Wengi walioajiriwa ni sababu za kisiasa, ili ionekane hawabaguliwi hasa kwenye sekta zinazohusiana na walemavu ndio huko wamejazwa!

Nina watu nawajua ni walemavu, wanapitia kipindi kigumu sana lakini wakiwa na elimu Yao kichwani! Yaani huu unyanyapaa huwezi ona kwa jicho la kawaida! Ni dhamira za watu.

Kitanda usicholalia huwezi jua kunguni wake!! We feel pain sana sana

Natimiza mwaka wa saba(7) tangu nimalize digrii yangu ya usimamizi wa fedha..

Serikali haitujali tena, zaidi ya kutulazimisha tukope pesa tuu.

Wadau wapo kimaslahi na kisiasa zaidi wapate attention wakati wanatoa misaada.

Hata vyama vya walemavu sasa hawana la kusema baada ya kulamba sukari

Sisi tukimbilie wapi zaidi yenu wadau wa hapa JF, tusaidieni kupaza sauti sisi walemavu tuliopambana kusoma kwa bidii, tunatamani kubeba tofali angalau tupate mkate wa kila siku lakini Hali zetu hazituruhusu.

Tuliamini katika elimu nayo imetusaliti, nchi imetutenga, tuna hari mbaya sana
pole sana naamini ujumbe umefika kwa wahusika.
tusisahau hujafa hujaumbika na kila mmoja wetu ni mlemavu mtarajiwa.
 
Niende kwenye mada moja kwa moja!!.

Nimekuwa moja ya wahanga wa hili Tatizo kwa muda mrefu sana

Kati ya watu wanaosoma kwa mateso makubwa sana ni watu wenye ulemavu, kuanzia shule za msingi mpaka sekondari, hii inatokana na miundo mbinu mingi kuwa tofauti na Hali zetu watu wenye ulemavu.

Wakati mtu mwenye ulemavu anapambna akiamini kuwa yeye hawez kulima, kutembeza mitumba, Wala kufanya kazi ngumu za ujenzi akitegemea akili yake tu ya darasani angalau impe mwanga wa maisha.

Baada ya ajira huyu mtu mwenye ulemavu anaanza kuzunguka na baiskeli yake au magongo yake kweny interview mbalimbali, wakati mwingine hufanyika mikoani, au kwenye majengo yasiyo na lift.
Wengi wanaishia kukata tamaa sana.

Kuna sehemu niliwahi kataliwa kabisa kisa mimi ni mlemavu kwamba siwezi kufanya hio kazi kwasababu nitakuwa naenda sana hospitali, yaani trip kazini trip hospitali. Wanahisi labda sisi ni wagonjwa fulani hivi,

Inaumiza sana sana, naongea kwa niaba Yao sana.

Wengi walioajiriwa ni sababu za kisiasa, ili ionekane hawabaguliwi hasa kwenye sekta zinazohusiana na walemavu ndio huko wamejazwa!

Nina watu nawajua ni walemavu, wanapitia kipindi kigumu sana lakini wakiwa na elimu Yao kichwani! Yaani huu unyanyapaa huwezi ona kwa jicho la kawaida! Ni dhamira za watu.

Kitanda usicholalia huwezi jua kunguni wake!! We feel pain sana sana

Natimiza mwaka wa saba(7) tangu nimalize digrii yangu ya usimamizi wa fedha..

Serikali haitujali tena, zaidi ya kutulazimisha tukope pesa tuu.

Wadau wapo kimaslahi na kisiasa zaidi wapate attention wakati wanatoa misaada.

Hata vyama vya walemavu sasa hawana la kusema baada ya kulamba sukari

Sisi tukimbilie wapi zaidi yenu wadau wa hapa JF, tusaidieni kupaza sauti sisi walemavu tuliopambana kusoma kwa bidii, tunatamani kubeba tofali angalau tupate mkate wa kila siku lakini Hali zetu hazituruhusu.

Tuliamini katika elimu nayo imetusaliti, nchi imetutenga, tuna hari mbaya sana
Mkuu pole sana. Nenda gran melia hotel -Arusha. Geti la tatu dogo la juu kabisa kulia kama unaelekea philips kutokea round about ya impala ( au kama unatokea philips ni geti la kwanza kushoto) . Kuna kitengo pale kinatoa ajira kwa walemavu sikumbuki jina kinaitwaje.. ila nenda pale wale wazungu wana ajiri walemavu tuu kwa asilimia 99%
 
Pole sana Kwa hiyo changamoto Mkuu

Nafikiri watu wanaajiriwa Kwa kuzingatia weledi na tija ambayo unaweza kuongeza kwenye Taasisi husika.

Unaweza kuajiriwa ukiwa ni mlemavu wa ngozi/viungo ama chochote na ukawa na tija kwenye eneo husika.

Tuishi tukijua Kila mtu ni mlemavu mtarajiwa

Unaweza kuwa mzima sasa, lakini Bodaboda utakayopanda kesho ikakupa ulemavu keshokutwa
Asante mkuu
 
Pole sana mkuu.

Ni swali tu ambalo nahitaji uelewa, hivi kwenye usaili hasa serikalini, swala la ulemavu ni kigezo au ni kipaumbele katika kupata ajira? Naomba kujuzwa.

Kwa sababu kwa hali iliyopo sasa sidhani kama issue ni walemavu vs wasiokuwa walemavu, unless otherwise uwe competent na bado ufanyiwe figisu kutokana na hali yako. Ninachofahamu Issue ya ajira ni janga la kitaifa.

I stand to be corrected.
Nafikiri wameweka tu Kama kigezo, lakn utekelezaji wake umekua kinyume! Ukiweka ulemav ni Kama umejipalia makaa ya moto
 
Pole sana ndgu! Kuna asasi za kiraia zinahusika na mikopo yenye masharti nafuu,,,, ungeenda huko walau , hizi ajira bila connection n changamoto sana ! Very sorry pal
 
A
Pole sana Kwa hiyo changamoto Mkuu

Nafikiri watu wanaajiriwa Kwa kuzingatia weledi na tija ambayo unaweza kuongeza kwenye Taasisi husika.

Unaweza kuajiriwa ukiwa ni mlemavu wa ngozi/viungo ama chochote na ukawa na tija kwenye eneo husika.

Tuishi tukijua Kila mtu ni mlemavu mtarajiwa

Unaweza kuwa mzima sasa, lakini Bodaboda utakayopanda kesho ikakupa ulemavu keshokutwa
Asante mzee wetu kwa nasaha nzurii...nikiwa Kama shuhuda wa ajari barabarani mwaka Jana na kuvunjika mguu so kwa muda wa zaidi ya miezi 7 nimeishi Maisha ya ulemavu..

Nikaanza kutembea kwa kujifunza muda mwingine nilikua nawaonea wivu watu walio kua wanatembea sikujua Kama ntaweza kutembea Tena na kwa Sasa mwezi huu wa pili nafikisha mwaka mmoja..now naweza kutembea Tena

Shukrani sanaa mkuu.
 
Back
Top Bottom