Hali ya kutokupenda ujulikane wewe ni kabila gani maofisini ni uzalendo au ni usaliti?

Magufuli ndio alikuwa anaongoza kuuliza makabila ya watu, afadhali alikufa
 
Hii nchi haina ukabila ndio maana watu hawaoni haja yakuongea kikabila, hasa huku mijini.
So yupo sahihi.
Chamsingi unatakiwa uje umuulize kabila lake ndio utajua kama anaogopa kujulikana kabila lake au haoni umuhimu wakuongea kilugha chake mbele ya kadamnasi.
 
Mi huwa nawajibu mi ni mjaluo wanasema hamna mjaluo muarabu basi tunaishia kucheka.Mambo ya kuulizana makabila ni aina ya ushamba na Uchawi tu.
 
Haya
mimi kabila langu ni Mgagagigikoko, nawe sema la kwako.
 
Mtoa mada na mwigulu nchemba nadhani wote mna traits zinaendana
 
We ndo mshamba,sisi wote ni watanzania,kabila kabila my foot? Fanya kazi acha Majungu,ukijua kabila lake ndo utamfanyeje sasa?,kabila has nothing to do with your job or his/her's.,
 
Kinachojadiliwa hapa ni pale unapoonekana ni aibu kubwa kujulikana kabila lako, hadi ukashindwa kuwa na amani ofisini kwako kisa eti kaja mtu wa kwenu kakuoongelesha kikwenu, unaongea huku ukiangalia chini utafikiri kakuletea ugoro kutoka shamba sasa unashindwa namna ya kuupokea ukihisi utachekwa na wenzako.
 
2022 bado watu wanaongelea makabila πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜­
 
90% Hawajiamini.

Mbona kuna watu ndani ya siku mbili utajua tuu ni kabila gani na hawaoni shida kujulikana... kimsingi hapo makabila yanayodharaulika au yenye sifa Fulani mbaya ndio maana wengi hukosa kujiamini
Makabila karibu yote TZ yanafanana katika mambo mengi tu...Umasikini,Ujinga n the like
 
Huyo ni mhaya kama sijakosea.
Ni bora kutojua kabila la mtu...maana mtu akishajua kabila lako ndo anaanza kukudefine...
Hata ukifanya kosa dogo utaadhibiwa kulinganishwa na tabia za kabila lako...
Tens zile mbaya zitapewa kipaumbele hasa ukitokea kwenye makabila makubwa yenye mafanikio makubwa mfano wachaga, wahaya, wanyakyusa NK..
Vikabila tofauti na hayo hujifeel inferior mbele ya hizo jamii...so akikutana mtu kutoka jamii hizo tabia zote mbaya hupambikiwa mhusika...


So kuepusha hayo bora ummute Tu kabila lako




Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app
 
Mara nyingi wanaoulizia makabila thinking capacity yao ni ndogo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…