Hali ya maisha kwa wananchi ni ngumu kweli!? Ama tulizoea Dezodezo

ni hayo tu

Mkuu ni kweli mambo mengi yamebadilika sikuhizi "kila falme na nyakati zake"

Kuna baadhi ya mabadiliko inatubidi tu-comply tu hatuna budi kufanya hivyo.

Kwahiyo mkuu unataka kutuambia kua inatupasa kuwajibika katika baadhi ya mambo sisi kama Wananchi.
 
Mkuu sijawahi ona awamu watu wananunua mandinga ya kifahari kama hii, kama hali ngumu ni kwako tu na watu wa mtaan kwenu ila watu wanaenjoy maisha balaa, we angalia kwenye magari namba D zilichukua miaka mingap na hii namba E haina hata miaka miwili ila ishafika EJA now famasiala nini
 
Oya sio powa ndinga nyingi sana.
 
Kuna watu watakwambia eti hao ndio wale kila urefu utakula kamba kwa mbuzi yakeπŸ€”
 
Wabongo wavivu? Ushaona hata ikitokea ajira moja ya kupata ujira wa bei ya kutupa watu wangapi wanajitokeza ? Am Sorry to say hii ni kauli ya mtu ambaye ameamu kufumba macho au ya aliyeshiba hence hamjui mwenye njaa....

View attachment 3023270
Watu wametafuta kazi kwa bidii kubwa ila wakipata wanaanza kufiwa kila baada ya week wanasubiria week end utafikili wameajiriwa ili wasuburie week end
 
Wewe kama sio Msukuma sijui..,yaani awamu ya 5 unafananisha na ya 4!! Eti maisha yalikuwa mazuri!!
 
Hakuna wakati ambao ulishawahi kuwa mwepesi au mgumu. Ni mikakati yako tu na matumizi yako tu. Hv walioishi kipindi Cha Nyerere watasemaje??? Usafiri shida, umeme, maji, chakula shida, vituo vya afya shida.
 
Watu wametafuta kazi kwa bidii kubwa ila wakipata wanaanza kufiwa kila baada ya week wanasubiria week end utafikili wameajiriwa ili wasuburie week end
Kwahio ajira zenye ujira ni nyingi kuliko wahitaji ? Hivi unajua watu wapo tayari kuhonga hata mishahara yao ya mwanzo ili wapate kazi na bado hawapati ? Hivi unajua Tanzania hii kuna walinzi wanalinda kwenye hizi kampuni za mifukoni mwaka mzima bila off wala sikukuu kwa ujira wa ambao haufiki laki mbili bila benefits zozote na hawana pa kwenda wala Serikali haina cha kuwafanya yaani atleast hawa wamejaribu kuwapa hata hizo 150k

Kuna dogo alikuwa yupo town anabangaiza hana hata pa kulala akaomba kwa jamaa awe analala kibarazani kwake huku analinda linda akiamba asubuhi akapige dayworker...

Mkuu in short hali ngumu kwa majority usipende kuangalia vitu kwa macho au hali yako bali angalia majority na uhalisia ni kwamba middle income class is shrinking tunatengeneza taifa la wachache wanaokula na kusaza wakati majority hata harufu ya chakula hawaipati....
 
Utajiri na unafuu umebaki Kwa akina mwigulu mchemba and the like!!! Labda na watumishi wa hizi agencies kama TRA,Tarura,Bot,nk haki huku tamisemi ni balaaa Hali ni ngumu mno!! Wafanyabiashara ndio usiseme!!!
Nafikiri sera mbovu za uchumi na viongozi kukosa vision
 
Kumbe wenzetu watumishi kwao mambo safi... Wakati wengine wakihimizwa wajiajiri wasitegemee ajira wengine wanajipimia kamba ndefundefu.

Alie nacho anaongezewa asiye nacho hata kile alichonacho ananyanganywa,


Hali hii ni common sana hapa Tanzania.

Kupitia connection kuna familia kuanzia baba mama mjomba binamu kaka mdogo mtu wote wako vitengo kiufupi hakuna anailia shida kwenye familia...

Ila sasa kuna familia ukoo mzima shida tupu hakuna aliyewahi kutoboa kusema atawashika mkono wezake baadae anakuja kuibuka mmoja kwa mbinde sana ukoo mzima unamtumainia huyo,

kasoma sasa apate ujira angalau, kijana wa watu, anapiga miaka 7 hadi 9 bila bila, anakubali matokeo anapiga kifua maisha ya naendelea.
 
Ndo maisha mzee
 
Awamu ya sita mambo yameharibika sana na kufanya maisha kuwa magumu sana.mimi kama Mimi awamu ya Tano nilikuwa napata sana pesa sababu ya mazingira kuwa mazuri ya biashara.Mama kaivuruga biashara hadi sasa sipati tena pesa nyingi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…