Lady Whistledown
JF-Expert Member
- Aug 2, 2021
- 1,147
- 2,008
Halima Mdee
Alikuwa Mbunge wa Kawe kuanzia 2010 hadi 2020 (CHADEMA) akiwa miongoni mwa Wanawake wachache walioweza kuingia Bungeni kwa kupitia vyama vya Upinzani. Aliwahi pia kuwa mwenyekiti wa BAWACHA
Dorothy Semu
Mwaka 2020 aliteuliwa kuwa Makamu Mwenyekiti Bara na Chama cha ACT-Wazalendo, huku Machi 2024 akichaguliwa kuwa Kiongozi wa Chama hicho
Dkt. Dorothy Gwajima
Mwaka 2020 aliteuliwa kuwa Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto. Dkt. Gwajima amekuwa mstari wa mbele katika masuala ya Kijinsia na afya, hasa akisisitiza Usawa na nafasi za Wanawake katika jamii
Tunapowatazama Wanawake kama Halima Mdee, Dorothy Semu, na Dkt. Dorothy Gwajima, tunapata nguvu na msukumo mpya wa kushiriki katika siasa na nafasi za uongozi.
Kwa ujasiri na uvumilivu wao, wameweza kuvunja mipaka, kushinda changamoto, na kuwa sauti ya mabadiliko ndani ya jamii zetu.
Halima alionesha ujasiri wa kupaza sauti ya wanyonge, Dorothy aliongoza kwa kuweka wanawake na vijana mstari wa mbele, na Dkt. Gwajima alitoa mchango mkubwa katika sekta ya afya kwa maslahi ya wananchi.
Wanawake hawa ni ushahidi kuwa hakuna lisilowezekana kwa mwanamke anayeamini katika uwezo wake. Tunapoyaona mafanikio yao, tunahamasika kujiamini, kujiunga katika mijadala ya kisiasa, na kutumia sauti zetu kuleta mabadiliko tunayoyataka.
Hivyo basi, kwa wanawake na wasichana wa Tanzania, simama na uamini kuwa unao uwezo wa kuleta mabadiliko - jiunge katika siasa na simama kama sauti ya mabadiliko katika taifa letu
Alikuwa Mbunge wa Kawe kuanzia 2010 hadi 2020 (CHADEMA) akiwa miongoni mwa Wanawake wachache walioweza kuingia Bungeni kwa kupitia vyama vya Upinzani. Aliwahi pia kuwa mwenyekiti wa BAWACHA
Dorothy Semu
Mwaka 2020 aliteuliwa kuwa Makamu Mwenyekiti Bara na Chama cha ACT-Wazalendo, huku Machi 2024 akichaguliwa kuwa Kiongozi wa Chama hicho
Dkt. Dorothy Gwajima
Mwaka 2020 aliteuliwa kuwa Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto. Dkt. Gwajima amekuwa mstari wa mbele katika masuala ya Kijinsia na afya, hasa akisisitiza Usawa na nafasi za Wanawake katika jamii
Tunapowatazama Wanawake kama Halima Mdee, Dorothy Semu, na Dkt. Dorothy Gwajima, tunapata nguvu na msukumo mpya wa kushiriki katika siasa na nafasi za uongozi.
Kwa ujasiri na uvumilivu wao, wameweza kuvunja mipaka, kushinda changamoto, na kuwa sauti ya mabadiliko ndani ya jamii zetu.
Halima alionesha ujasiri wa kupaza sauti ya wanyonge, Dorothy aliongoza kwa kuweka wanawake na vijana mstari wa mbele, na Dkt. Gwajima alitoa mchango mkubwa katika sekta ya afya kwa maslahi ya wananchi.
Wanawake hawa ni ushahidi kuwa hakuna lisilowezekana kwa mwanamke anayeamini katika uwezo wake. Tunapoyaona mafanikio yao, tunahamasika kujiamini, kujiunga katika mijadala ya kisiasa, na kutumia sauti zetu kuleta mabadiliko tunayoyataka.
Hivyo basi, kwa wanawake na wasichana wa Tanzania, simama na uamini kuwa unao uwezo wa kuleta mabadiliko - jiunge katika siasa na simama kama sauti ya mabadiliko katika taifa letu