Halima Mdee na wenzake 18 wapanga kuihujumu BAWACHA, washitukiwa

Halima Mdee na wenzake 18 wapanga kuihujumu BAWACHA, washitukiwa

Makamanda mnapitia wakati mgumu sana kisiasa, miezi kadhaa nyuma mmesumbua sana na maneno yenu ya mipasho bila hata kuweka akiba ya maneno, haya ndo malipo ya matusi na usaliti wenu dhidi ya taifa, na nadhani kuna kitu mtajifunza.
 
Basi, kama ni muigizaji kiasi kile anastahili tuzo ya uigizaji.

Mtu kuigiza hadi unavunjwa viuongo kikwelikweli; sijawahi ona mwigizaji wa namna ile.

Niliposikia Mbowe akisema angependa mrithi wake awe ni kutoka BAWACHA, nilidhani alikuwa akimlenga Halima; kunbe sio? Nani basi?

Juhudi zote zile alizokuwa akizifanya hadi Bungeni, ilikuwa ni maigizo?

Lakini pia tukubali kuwapa sifa zao watu wa CCM waliofanikiwa kumrubuni. Kwanza mtu ungeanzia wapi kumsogelea Halima na kuanza kulainisha kirahisi vile? Yaani kukosa ubunge tu, tena kwa kunyang'anywa kwa nguvu, ndiyo ikawa sababu rahisi ya kumlainisha kirahisi vile Halima na akina Ester wawili?

Hawa mabinti wameingia katika historia ya usaliti, itakayowaandama maisha yao yote. Sasa wanazidi kujidhalilisha kwa haya wanayoendelea kuyafanya, huku wakiwa nje ya chama.

Matumaini ya wengi baada ya mkasa huu wa Halima na wenzake ni kwamba CHADEMA imefuzu. Imeviruka vihunzi vyote kwa ufanisi mkubwa. Chama hakijawahi kujitakasa kuliko kilivyojitakasa wakati huu. Kazi kwenu sasa kuzidi kukiimarisha chama hasa huko vijijini na mitaani.
Sasa hivi hakuna asiyejua uwepo wa CHADEMA tena ndani ya nchi hii.

Mwisho: ushauri wangu. Tazameni kwa makini sana sera zenu. Kuna baadhi ya sera hizo haziuziki kabisa kwa jamii ya waTanzania. Zitazameni kwa makini mzirekebishe panapotakiwa.
Chadema inapokea maoni kutoka kila mahali , wasilisha sera mbovu zifanyiwe kazi
 
makamanda mnapitia wakati mgumu sana kisiasa, miezi kadhaa nyuma mmesumbua sana na maneno yenu ya mipasho bila hata kuweka akiba ya maneno, haya ndo malipo ya matusi na usaliti wenu dhidi ya taifa, na nadhani kuna kitu mtajifunza.
Matusi kwa tafsiri ya kwenu ni nini ?
 
CHADEMA kinasimamia kikamilifu mchakato wa kifo chake.

Wananchi walikinyima kura lakini enewei sikio la kufa....
Kilichofanyika kwenye uchaguzi tumekiona kwa macho yetu, usiwasingizie wananchi. Ule haukuwa uchaguzi, bali maonyesho ya ujinga wa mtu mweusi kwenye box la kura.
 
Yaani watu wanao shabikia upinzani hua ni kama punguani tu,ni afadhari kukaa kama sisi bila vyama vya siasa,sasa hapa hao CCM wanakujaje? Kutwa kucha ni visingizio tu,chama cha siasa kimesha jichanga lakini shutuma zinaenda kwa kundi jingine,wapuuzi kweli ninyi

CCM ndiyo dola (serikali) yenyewe iliyojipa madaraka ya kudhibiti uwanja mzima wa shughuli za kisiasa. Upinzani ni sauti/mawazo mbadala kwa serikali.

Usipokubaliana na kinachosemwa na upinzani, basi umekubaliana na matendo na kinachosemwa na serikali. Ni suala la kuona kweli iko wapi na kusimama nayo. CCM/Serikalini? au katika upinzani?

Kujiita “sisi bila vyama vya siasa” hapa Tanzania ni ubatili (void) - si kweli. Ni uongo ulio dhahiri kabisa. Ni ama umesimama na dola au na upinzani. Neutral doesn’t exist here.
 
Makamanda mnapitia wakati mgumu sana kisiasa, miezi kadhaa nyuma mmesumbua sana na maneno yenu ya mipasho bila hata kuweka akiba ya maneno, haya ndo malipo ya matusi na usaliti wenu dhidi ya taifa, na nadhani kuna kitu mtajifunza.
 
Hatukatai kupata hizo pesa shida ni uhalali wa kuingia huko bungeni inaenda kuwa kituko cha bunge linavyo endeshwa dunianzima
Sasa ndio tayari wabunge, nyie chadema mmepoteza wao covid wamepata
 
Chadema inapokea maoni kutoka kila mahali , wasilisha sera mbovu zifanyiwe kazi
Nikupe mfano mmoja ulio wazi:
Sera ya majimbo haiiongezei chochote Tanzania. Na hata kama CHADEMA wanaing'ang'ania kwamba ndiyo sera yao kuu na muhimu sana, basi italazimu jambo hilo liamuliwe na wananchi wenyewe kwa kura ya maoni na sio wao CHADEMA kuingia tu na kubadili muundo mzima wa kiserikali kwa vile tu wameshinda uchaguzi kwa kumpata Rais. Hata bungeni inawezekana ikawa ni vigumu kupitisha jambo kama hilo.

Kwa hiyo sera ya majimbo haiwezi kutekelezwa kwa vile tu CHADEMA wameshika serikali. Ni lazima jambo hilo lipitie Bungeni na hata wananchi washirikishwe kwa kupiga kura ya maoni.

Huo ni mfano mmoja wa mambo magumu yanayofanya baadhi ya wananchi kusita kuiunga mkono CHADEMA.
Hatakueleza sababu za lazima kubadilisha muundo uliopo hazieleweki vyema na wananchi wengi.

Yapo mengine kadhaa yanayotia shaka juu ya CHADEMA na hatma ya Tanzania yanayowafanya waTanzania wengi kusita kuwaunga mkono moja kwa moja.
 
Utashangaa siku hilo baraza likiitwa wanachadema nyomi watahudhuria. Hapo ndo utajua hali halisi
 
Back
Top Bottom