DOKEZO Halmashauri Mbeya imetuuzia maeneo yenye Mwekezaji anayehatarisha afya zetu kwa kutumia baruti

DOKEZO Halmashauri Mbeya imetuuzia maeneo yenye Mwekezaji anayehatarisha afya zetu kwa kutumia baruti

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Mwanongwa

JF-Expert Member
Joined
Feb 15, 2023
Posts
611
Reaction score
567
Mimi kama mkazi wa Jiji la Mbeya kuna kitu sikielewi kutoka kwa Viongozi wa Jiji hasa Idara ya Ardhi na Watu wa Mazingira wa NEMC.

Huku Mbeya katika Kata ya Nsalaga, Bonde la Uyole, Uongozi wa Halmashauri ulianzisha mradi wa viwanja vipya na kuhamasisha sana Wananchi wajitokeze kununua viwanja hivyo, kweli tulijitokeza na kununua.
Lakini kinachoendelea hivi sasa katika eneo hilo la mradi huo wa viwanja ni balaa tupu na hatari kwetu Wananchi wa maeneo hayo.

Kuna raia mmoja mwenye asili ya Uarabuni anayemiliki kampuni ya ukandarasi, naye amepewa kibali cha kuchimba mawe katika maeneo hayo, amefunga na mitambo yake ya kusaga mawe.
DSC_0117.JPG
Kibaya zaidi siyo kuchimba tu bali anapiga baruti kwaajili ya kuvunja miamba hiyo ya mawe maana mawe ya juu tayari amekwisha yamaliza na sasa ni mwendo wa baruti tu.

Sisi tulionunua viwanja kwaajili ya kujenga tutawezaje kujenga eneo hilo wakati kuna shughuli za uchimbaji zinaendelea karibu na maeneo yetu, pia baruti ni hatari sana sababu zinarusha mawe, hivyo zinahatarisha maisha ya Watu na viumbe wengine.
DSC_0090.JPG
Mitambo yake ya kusaga mawe inachafua hali ya hewa kila siku sababu vumbi muda wote zinatapakaa kwenye makazi ya watu na kusababisha magongwa mbalimbali kikiwemo kikohozi pamoja na mafua yasiyoisha.

Najiuliza hapa hivi wakati mamlaka zinampatia kibali huyo mwekezaji mwenye kampuni hiyo inayoitwa Narmo, ilitegemea sisi tunajengaje sasa maeneo hayo?
DSC_0092.JPG
Upande wa pili ninyi NEMC inamaana hamuoni kama jamaa anaharibu mazingira kwa kuchimba mawe tena kwa kupiga baruti muda wote wa shughuli.

Baruti hizo zimesababisha nyufa kwenye nyumba nyingi tu za Wananchi waishio karibu na maeneo hayo ya mradi huo wa mgodi wa mawe kama wanavyouita.
DSC_0115.JPG
Kulikuwa na ulazima gani wa kutoa kibali kuendesha shughuli hiyo ya uchimbaji wakati mnajua fika kuwa italeta shida kwa sisi Wananchi ambao tumenunua viwanja maeneo hayo.

Siyo siri Viongozi wa Halmashauri hasa Idara ya Ardhi mmetukosea sana Wananchi, pesa zetu mmechukua na mmetuletea majanga maana hatuwezi kabisa kujenga kutokana na baruti zinazopigwa, moja zinaweza kuangusha nyumba na pia tutakuwa tunalazimika kutoka kwa muda katika nyumba zetu ili kupisha baruti kupigwa.
DSC_0102.JPG
Watu wa Reli wakague reli yao
Ndugu zangu wa mamlaka ya reli nawakumbusha kupita kukagua njia yenu ya treni sababu imepita maeneo hayo ambayo zoezi la uchimbaji wa mawe kwa njia ya kupiga baruti linaendelea, hivyo ni vyema kupita na kuikagua njia hiyo mara kwa mara ili mbeleni yasije yakatokea majanga.

Mtafutieni huyo mwekezaji eneo lingine nje ya mji ndiyo akachimbe hayo mawe na siyo hapa katika eneo ambalo mmetuuzia viwanja.
 

Attachments

  • DSC_0107.JPG
    DSC_0107.JPG
    1.3 MB · Views: 10
Sasa hivi naona mradi wa viwanja umeingizwa kwenye mfumo wa Tausi-Tamisemo na watu wanaendelea kununua...
 
Nsalaga kumbe viwanja vimesogezwa Hadi kule mlima nyoka? Nina karibu miaka 7 tangu nimetoka mbeya
 
Mimi kama mkazi wa Jiji la Mbeya kuna kitu sikielewi kutoka kwa Viongozi wa Jiji hasa Idara ya Ardhi na Watu wa Mazingira wa NEMC.

Huku Mbeya katika Kata ya Nsalaga, Bonde la Uyole, Uongozi wa Halmashauri ulianzisha mradi wa viwanja vipya na kuhamasisha sana Wananchi wajitokeze kununua viwanja hivyo, kweli tulijitokeza na kununua.
Lakini kinachoendelea hivi sasa katika eneo hilo la mradi huo wa viwanja ni balaa tupu na hatari kwetu Wananchi wa maeneo hayo.

Kuna raia mmoja mwenye asili ya Uarabuni anayemiliki kampuni ya ukandarasi, naye amepewa kibali cha kuchimba mawe katika maeneo hayo, amefunga na mitambo yake ya kusaga mawe.
Kibaya zaidi siyo kuchimba tu bali anapiga baruti kwaajili ya kuvunja miamba hiyo ya mawe maana mawe ya juu tayari amekwisha yamaliza na sasa ni mwendo wa baruti tu.

Sisi tulionunua viwanja kwaajili ya kujenga tutawezaje kujenga eneo hilo wakati kuna shughuli za uchimbaji zinaendelea karibu na maeneo yetu, pia baruti ni hatari sana sababu zinarusha mawe, hivyo zinahatarisha maisha ya Watu na viumbe wengine.
Mitambo yake ya kusaga mawe inachafua hali ya hewa kila siku sababu vumbi muda wote zinatapakaa kwenye makazi ya watu na kusababisha magongwa mbalimbali kikiwemo kikohozi pamoja na mafua yasiyoisha.

Najiuliza hapa hivi wakati mamlaka zinampatia kibali huyo mwekezaji mwenye kampuni hiyo inayoitwa Narmo, ilitegemea sisi tunajengaje sasa maeneo hayo?
Upande wa pili ninyi NEMC inamaana hamuoni kama jamaa anaharibu mazingira kwa kuchimba mawe tena kwa kupiga baruti muda wote wa shughuli.

Baruti hizo zimesababisha nyufa kwenye nyumba nyingi tu za Wananchi waishio karibu na maeneo hayo ya mradi huo wa mgodi wa mawe kama wanavyouita.
Kulikuwa na ulazima gani wa kutoa kibali kuendesha shughuli hiyo ya uchimbaji wakati mnajua fika kuwa italeta shida kwa sisi Wananchi ambao tumenunua viwanja maeneo hayo.

Siyo siri Viongozi wa Halmashauri hasa Idara ya Ardhi mmetukosea sana Wananchi, pesa zetu mmechukua na mmetuletea majanga maana hatuwezi kabisa kujenga kutokana na baruti zinazopigwa, moja zinaweza kuangusha nyumba na pia tutakuwa tunalazimika kutoka kwa muda katika nyumba zetu ili kupisha baruti kupigwa.
Watu wa Reli wakague reli yao
Ndugu zangu wa mamlaka ya reli nawakumbusha kupita kukagua njia yenu ya treni sababu imepita maeneo hayo ambayo zoezi la uchimbaji wa mawe kwa njia ya kupiga baruti linaendelea, hivyo ni vyema kupita na kuikagua njia hiyo mara kwa mara ili mbeleni yasije yakatokea majanga.

Mtafutieni huyo mwekezaji eneo lingine nje ya mji ndiyo akachimbe hayo mawe na siyo hapa katika eneo ambalo mmetuuzia viwanja.
Mkuu, viwanja hivyo vinauzwa sh ngapi?
Na vinasimamiwa na ofisi ipi hapo Mbeya?
 
Binafsi huwa naumia sana kutapeliwa na mamlaka za serikali kwa sababu malengo yake ni chanya siku zote mfano kustawisha maisha ya wananchi.

Sasa kuna baadhi ya watendaji wanatapeli kwa mgongo wa serikali na hakuna anayejali. Watu wamesoma mambo ya ardhi miaka minne halafu washindwe kupanga miji kweli mpaka kuwaweka watu kwenye baruti na makazi?!!!
 
Kiukweli nime pita Sana eneo lile na huwa Nina shangazwa kuona kazi kama ile inafanyika kwenye eneo la mji unao kuwa kwa Kasi Kama ule

Niwakati sasa mamlaka kuangalia namba nyingine ya kufanya ili kupata mawe au kokoto na kuondokana na eneo Hilo Kama mgodi Tena kwani mji umesha kuwa tayali na hayo ni makazi ya watu kwa Sasa
 
Kiukweli nime pita Sana eneo lile na huwa Nina shangazwa kuona kazi kama ile inafanyika kwenye eneo la mji unao kuwa kwa Kasi Kama ule

Niwakati sasa mamlaka kuangalia namba nyingine ya kufanya ili kupata mawe au kokoto na kuondokana na eneo Hilo Kama mgodi Tena kwani mji umesha kuwa tayali na hayo ni makazi ya watu kwa Sasa
Kabisa
 
Ni
Binafsi huwa naumia sana kutapeliwa na mamlaka za serikali kwa sababu malengo yake ni chanya siku zote mfano kustawisha maisha ya wananchi.

Sasa kuna baadhi ya watendaji wanatapeli kwa mgongo wa serikali na hakuna anayejali. Watu wamesoma mambo ya ardhi miaka minne halafu washindwe kupanga miji kweli mpaka kuwaweka watu kwenye baruti na makazi?!!!
Hatari
 
Kabisa yaani
Kiukweli nime pita Sana eneo lile na huwa Nina shangazwa kuona kazi kama ile inafanyika kwenye eneo la mji unao kuwa kwa Kasi Kama ule

Niwakati sasa mamlaka kuangalia namba nyingine ya kufanya ili kupata mawe au kokoto na kuondokana na eneo Hilo Kama mgodi Tena kwani mji umesha kuwa tayali na hayo ni makazi ya watu kwa Sasa
 
Back
Top Bottom