Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Baada ya Mdau wa JamiiForums.com kudai kuna kuna baadhi ya Mafisa wa Halmashauri ya Kibaha Mji wamekuwa wakiwasumbua Wananchi wa Matuga, Kibaha Vijijini kwa kuwatishia ili kuwaondoa kwenye makazi yao, Kibaha Mji imetoa ufafanuzi wa kinachoendelea.
Innocent Byarugaba, ambaye ni Afisa Mawasiliano wa Halmashauri ya Kibaha anajibu hoja za Mdau huyo ambaye alidai kuwa licha ya kuwa wao wapo Kibaha Vijijini lakini wamekuwa wakisumbuliwa na Maafisa wa Kibaha Mji.
Malalamiko ya Mdau soma hapa ~ Maafisa wa Kibaha Mji wanatumia Mgambo na Askari mwenye bastola kututisha ili watuondoe katika Makazi yetu
Byarugaba anaelezea:
Matuga haipo Kibaha Mjini, sisi hatuhusiani na ugomvi wa huko, pili ni kweli kuna maafisa wetu walipigwa picha wakiwa na gari la ofisi yetu walipoenda eneo hilo.
Kwenye hilo eneo kuna sehemu mbili, kipande ni eneo la Kibaha Mjini na Kipande.
Eneo ambalo linamilikiwa na Abdulkadir kuna eneo ambalo lipo Mtaa wa Zegereni zaidi ya Ekari 250, sasa mzee anayeonekana kwenye picha kwa mbele ni Mkuu wa Idara ya Mifugo, Uvuvi na Kilimo sio mpima ardhi ila na yeye ana kiwanja chake maeneo ya Visiga.
Maafisa wa Kibaha Mji.
Gari la Kibaha Mji lililopigwa picha na Wananchi maeneo ya Matuga.Kilichokuwa kinafanyika kwenye picha hiyo ambayo inasambaa mitandaoni ikiwaonesha Maafisa wetu eneo hilo, ni kuwa Afisa wetu mmoja alienda kuonesha eneo analolimiliki kihalali upande wa Kibaha Mjini.
Siku hiyo alienda kuonyeshwa eneo ambalo amelinunua kihalali, mwingine anayeonekana kwenye picha alikuwa na vifaa vya kutambua mipaka, kwa kuwa lile eneo limepimwa siku nyingi na tumetoka kwenye mvua, majani yamekuwa mengi, hivyo vifaa alivyokuwa navyo vinasaidia kumuonesha mipaka ilipo.
Kuhusu wao kutumia gari la ofisi, Wakuu wa Idara na vitengo wanaruhusiwa kutembelea magari ya ofisi.
Kuhusu Wananchi hao kwenda kulalamika hadi kwa Mkuu wa Wilaya ijulikane kuwa DC ana Kibaha Vijijini na Mjini, hivyo kwenda kulalamika kwake ni halali yao (Wananchi wa Matug) kwa kuwa kiongozi huyo ndio mwakilishi wa Rais ngazi ya Wilaya.
Hivyo, walioenda kulalamika walitimiza wajibu wao kwa uhalali na ni haki yao.
Itambulike kuwa shamba au eneo linalozungumzwa ni la mtu binafsi na Halmashauri haihusiki kwa aina yoyote.
Wananchi wa Matuga wanaolalamika maeneo yao kuvamiwa na Maafisa wa Kibaha Mji.
Innocent Byarugaba, ambaye ni Afisa Mawasiliano wa Halmashauri ya Kibaha anajibu hoja za Mdau huyo ambaye alidai kuwa licha ya kuwa wao wapo Kibaha Vijijini lakini wamekuwa wakisumbuliwa na Maafisa wa Kibaha Mji.
Malalamiko ya Mdau soma hapa ~ Maafisa wa Kibaha Mji wanatumia Mgambo na Askari mwenye bastola kututisha ili watuondoe katika Makazi yetu
Byarugaba anaelezea:
Matuga haipo Kibaha Mjini, sisi hatuhusiani na ugomvi wa huko, pili ni kweli kuna maafisa wetu walipigwa picha wakiwa na gari la ofisi yetu walipoenda eneo hilo.
Kwenye hilo eneo kuna sehemu mbili, kipande ni eneo la Kibaha Mjini na Kipande.
Eneo ambalo linamilikiwa na Abdulkadir kuna eneo ambalo lipo Mtaa wa Zegereni zaidi ya Ekari 250, sasa mzee anayeonekana kwenye picha kwa mbele ni Mkuu wa Idara ya Mifugo, Uvuvi na Kilimo sio mpima ardhi ila na yeye ana kiwanja chake maeneo ya Visiga.
Maafisa wa Kibaha Mji.
Gari la Kibaha Mji lililopigwa picha na Wananchi maeneo ya Matuga.
Siku hiyo alienda kuonyeshwa eneo ambalo amelinunua kihalali, mwingine anayeonekana kwenye picha alikuwa na vifaa vya kutambua mipaka, kwa kuwa lile eneo limepimwa siku nyingi na tumetoka kwenye mvua, majani yamekuwa mengi, hivyo vifaa alivyokuwa navyo vinasaidia kumuonesha mipaka ilipo.
Kuhusu wao kutumia gari la ofisi, Wakuu wa Idara na vitengo wanaruhusiwa kutembelea magari ya ofisi.
Kuhusu Wananchi hao kwenda kulalamika hadi kwa Mkuu wa Wilaya ijulikane kuwa DC ana Kibaha Vijijini na Mjini, hivyo kwenda kulalamika kwake ni halali yao (Wananchi wa Matug) kwa kuwa kiongozi huyo ndio mwakilishi wa Rais ngazi ya Wilaya.
Hivyo, walioenda kulalamika walitimiza wajibu wao kwa uhalali na ni haki yao.
Itambulike kuwa shamba au eneo linalozungumzwa ni la mtu binafsi na Halmashauri haihusiki kwa aina yoyote.
Wananchi wa Matuga wanaolalamika maeneo yao kuvamiwa na Maafisa wa Kibaha Mji.