Halmashauri ya Kibaha yasema imetumia Milioni 410 ya Mapato ya Ndani kununua Madawati na Meza 4000

Halmashauri ya Kibaha yasema imetumia Milioni 410 ya Mapato ya Ndani kununua Madawati na Meza 4000

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
WhatsApp Image 2024-10-25 at 17.12.58_0b783ea3.jpg
Halmashauri ya Mji Kibaha imeendelea kutekeleza kwa Vitendo maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.Samia Suluhu Hassan kwenye Sekta ya Elimu baada ya kufanya hafla ya kugawa Madawati 2000,Viti na Meza 2000 zenye thamani ya Shilingi 410,000,000 zilizotokana na Mapato ya ndani.

Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini, Silvestry Francis Koka aliyekuwa Mgeni rasmi ametoa rai kwa Wananchi na wawekezaji wote kulipa Kodi stahiki kwa wakati kwani fedha hizo Sasa wanashuhudia zikirudi kwenye Jamii kwenda kuondoa kero kwa watoto wetu wanaosoma shule za Msingi na Sekondari za Serikali huku akikemea vikali kuziita shule za Kayumba kutokana na uwekezaji mkubwa unaowekwa na Serikali.
WhatsApp Image 2024-10-25 at 17.12.58_d0a3045d.jpg

WhatsApp Image 2024-10-25 at 17.12.59_da097a03.jpg
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kibaha Dkt.Rogers Jacob Shemwelekwa ameeleza kuwa Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Dkt.Samia Suluhu Hassan imeendelea kuboresha miundombinu ya Elimu ambapo Madarasa 217 na Matundu ya vyoo 232 yenye thamani ya Shilingi 4,358,551,560 yamejengwa kwa shule za msingi na Sekondari.

Aidha,Dkt.Shemwelekwa ameongeza kuwa Halmashauri ya Mji Kibaha imepokea Shilingi 5,179,017,622 kwa ajili ya kugharamia Elimu bila Malipo na kutoa rai kwa wadau wa Sekta ya Elimu kuunga mkono jitihada za Serikali kwenye Sekta hii muhimu kwa ajili ya kuandaa Wataalam watakaolitumikia Taifa baadaye

Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Mhe.Nikkson Simon John pamoja na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Kibaha Mhe.Mussa Abdallah Ndomba wamempongeza Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kutoa fedha nyingi kuimarisha Sekta ya Elimu.
WhatsApp Image 2024-10-25 at 17.12.58_1da41237.jpg

WhatsApp Image 2024-10-25 at 17.13.00_a2909b31.jpg
Aidha,wametumia fursa hiyo Kumpongeza Dkt.Shemwelekwa na menejimenti kwa utendaji mzuri wa kusimamia Mapato na kuweza kutatua changamoto ya Madawati iliyokuwa kero ya muda mrefu.

Kwa upande wao Swaumu Bakari na Margreth Chuwa kwa niaba ya Wanafunzi wamemshukuru Rais Samia kwa kuendelea kuwajali kwenye sekta ya Elimu na kuahidi kusoma kwa bidii hasa Masomo ya Sayansi.

Halmashauri ya Mji Kibaha yenye jumla ya Wanafunzi 17,424 ina shule 66 za Serikali kati yake za Msingi ni 46 na Sekondari 20.
 
Safi sana hapo wameongeza kiwango cha Elimu kwa kiwango kikubwa saba Big up kwao haya ndio tunatakiwa kusikia kutoka kwenye vyanzo vya mapato yetu..
 
Milioni 410 ukigawa kwa hiyo 4000 unapata milioni moja na ishirini na tano elfu. Hilo nalo la kuliangalia. Mitano tena kwa mama ikiwa atadhibitisha ni sawa
 
Inasikitisha sana kuna watu hata hesabu ya kugawanya hawajui. Bad enough hata kujiongeza kutumia hiyo calculator ya simu zao napo holaaa!

Mmoja anasema dawati moja ni milioni moja, mwengine anasema dawati moja ni milioni moja na ishirini na tano elfu.

Kulaleki kwa hivi vichwa vya 1+1=55 safari bado tunayo 😂
 
Kila dawati moja kwa laki moja.. sio mbaya.. ila tumepigwa kizungu
 
Inasikitisha sana kuna watu hata hesabu ya kugawanya hawajui. Bad enough hata kujiongeza kutumia hiyo calculator ya simu zao napo holaaa!

Mmoja anasema dawati moja ni milioni moja, mwengine anasema dawati moja ni milioni moja na ishirini na tano elfu.

Kulaleki kwa hivi vichwa vya 1+1=55 safari bado tunayo 😂
Premij hiyo vieite yako hapo mbweni haijambo?
 
VX moja jipya la DED ni zaidi ya 400m
VX moja jipya la DC ni zaidi ya 400m

Kwangu mimi huo ununuzi wa viti, meza na madawati 4000 ungetosha kugharamiwa na pesa za kununua VX moja jipya la DED au DC.

Note:
Karibu kila baada ya miaka mitano, ununuzi wa VX jipya la DED hufanyika.
 
Back
Top Bottom