Halmashauri ya Wilaya ya Ubungo tusaidieni hili la taka Sinza, hali ni mbaya

Halmashauri ya Wilaya ya Ubungo tusaidieni hili la taka Sinza, hali ni mbaya

tripleec

Senior Member
Joined
Oct 19, 2022
Posts
169
Reaction score
159
Nikiwa kama mwananchi nimeona nitumie jukwaa hili maana naamini wahusika wengi wapo humu na wengi wanaweza saidi kupaza sauti.

Nimepita eneo la Sinza kumekucha karibu na kanisa la KKKT kiukweli hali ya usalama wa afya ni mbaya kwa wakazi hao.

Nilifanya mahojiano na baadhi ya wakazi wa maeneo hayo nini kimewasibu wakasema yapata kama miezi 2 gari la kuzoa taka hawajawahi kuliona licha ya kuwa wanalipa pesa ya huduma hiyo.

Nikawauliza je mmeshatembelea ofisi za Serikali ya mtaa majibu niliyopewa ni kuwa mwenyekiti na katibu wamekuwa wakiwapa majibu tofauti mmoja anasema linakuja tangulia mwingine anajibu gari haliji tena.

Nikajiuliza sasa kama hakuna gari kwanini waasitafute tenda nyingine , mwananchi mmoja akanijibu kuwa wameambiwa mpaka tenda ya huyu wa sasa iishe mwakani ndiyo watatafuta mtu mwingine.

Ifike mahala wale wa mikokoteni waachiwe kazi hii maana watu wapo tayari kulipia huduma lakini mzoaji hayupo mwisho wa siku nachelea au naogopa kama wakiamua kuziacha barabarani na hali hii ya mvua ni hatari kwa miundo mbinu lakini npia na magonjwa ya mlipuko.

Nimemabatanisha picha katika moja ya mtaa unaitwa Chuma nyuma ya kanisa la KKKT sizna kumekucha.


WhatsApp Image 2023-11-24 at 08.27.37 (1).jpeg
WhatsApp Image 2023-11-24 at 08.27.37 (2).jpeg
WhatsApp Image 2023-11-24 at 08.27.37.jpeg
WhatsApp Image 2023-11-24 at 08.27.38 (1).jpeg
WhatsApp Image 2023-11-24 at 08.27.36.jpeg
 
Njooni kijijini. Huku kwetu nanjilinji hakuna tabu ya takataka, mafuriko, kelele ya mamuziki, changudoa, wala chakula au maji. Hewa safiii, baridiiiii
 
na makanisa ya kilokole tana kelele mbaya kabisa kule mitaa ya LION ni shidaaa makelele mekeleleeeeeeeee uwwiiiiiiiiii
 
Mbunge anahusika na usafi pamoja na kero zote jimboni kwake. Mbunge anaweza kuwasilisha kwa waziri wa TAMISEMI utendaji mbovu wa Mkurugenzi wa Halmashauri.
Mkuu kama kupokea maoni ya wananchi na kuyawakilisha kwa baraza la halmashauri au Bungeni sni sawa ila sio kazi yake wala ya diwani. Hiyo ni kazi ya Mwenyekiti, Mtendaji na mkuu wa wilaya.
 
Nikiwa kama mwananchi nimeona nitumie jukwaa hili maana naamini wahusika wengi wapo humu na wengi wanaweza saidi kupaza sauti.

Nimepita eneo la Sinza kumekucha karibu na kanisa la KKKT kiukweli hali ya usalama wa afya ni mbaya kwa wakazi hao.

Nilifanya mahojiano na baadhi ya wakazi wa maeneo hayo nini kimewasibu wakasema yapata kama miezi 2 gari la kuzoa taka hawajawahi kuliona licha ya kuwa wanalipa pesa ya huduma hiyo.

Nikawauliza je mmeshatembelea ofisi za Serikali ya mtaa majibu niliyopewa ni kuwa mwenyekiti na katibu wamekuwa wakiwapa majibu tofauti mmoja anasema linakuja tangulia mwingine anajibu gari haliji tena.

Nikajiuliza sasa kama hakuna gari kwanini waasitafute tenda nyingine , mwananchi mmoja akanijibu kuwa wameambiwa mpaka tenda ya huyu wa sasa iishe mwakani ndiyo watatafuta mtu mwingine.

Ifike mahala wale wa mikokoteni waachiwe kazi hii maana watu wapo tayari kulipia huduma lakini mzoaji hayupo mwisho wa siku nachelea au naogopa kama wakiamua kuziacha barabarani na hali hii ya mvua ni hatari kwa miundo mbinu lakini npia na magonjwa ya mlipuko.

Nimemabatanisha picha katika moja ya mtaa unaitwa Chuma nyuma ya kanisa la KKKT sizna kumekucha.


View attachment 2822917View attachment 2822918View attachment 2822919View attachment 2822920View attachment 2822916
Marekebisho:
Ubungo ni Halmashauri ya Manispaa na siyo Halmashauri ya Wilaya.
 
Watu wa dsm wanaishi tu hili wasife lakini hawana furaha
 
Hizo taka mbona zimekaa sahihi.

Mwananchi ana wajibu wa kufanya usafi na kuhifadhi taka kwenye vyombo na asubiri gari la taka lije kuzibeba.

Hapo sijaona kosa. Au ulitaka wakati wanafagia basi gari iwe hapo mtaani?

Siyo kila kitu ni kibaya. Mimi ninaona taka zimehifadhiwa vizuri tu.

Sinza ni moja ya kata zenye mazingira safi za Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo.
 
Issue siyo kuhifadhiwa Kiongozi nilichokikuta ni kuwa wameweka kusubiri gari ila zimekaa muda mrefu na hakuna namna yoyote kwamba zitachukuliwa wananchi wao wamejitahidi ziweka ili gari lipite ila ni muda mrefu wanasema gari halijapita na kumbuka bado kuna taka zingine ambazo zitahitajika nazo kuzolewa mwisho wa siku wakizidi ziweka hivi mazingira ndiyo yatakuwa hatarishi zaidi.
 
Back
Top Bottom