Halmashauri ya Wilaya ya Ubungo tusaidieni hili la taka Sinza, hali ni mbaya

Halmashauri ya Wilaya ya Ubungo tusaidieni hili la taka Sinza, hali ni mbaya

Kipindi cha mvua huko dampo pa kutupa taka hakuingiliki

Ova
 
Nipeni tenda nilete magari ya taka
Kabla hamjapata magonjwa hebu jiongezeni kwanza msafishe na kuzoa taka mkazitupe halafu ndio mpaze sauti kila sehemu
 
Nikiwa kama mwananchi nimeona nitumie jukwaa hili maana naamini wahusika wengi wapo humu na wengi wanaweza saidi kupaza sauti.

Nimepita eneo la Sinza kumekucha karibu na kanisa la KKKT kiukweli hali ya usalama wa afya ni mbaya kwa wakazi hao.

Nilifanya mahojiano na baadhi ya wakazi wa maeneo hayo nini kimewasibu wakasema yapata kama miezi 2 gari la kuzoa taka hawajawahi kuliona licha ya kuwa wanalipa pesa ya huduma hiyo.

Nikawauliza je mmeshatembelea ofisi za Serikali ya mtaa majibu niliyopewa ni kuwa mwenyekiti na katibu wamekuwa wakiwapa majibu tofauti mmoja anasema linakuja tangulia mwingine anajibu gari haliji tena.

Nikajiuliza sasa kama hakuna gari kwanini waasitafute tenda nyingine , mwananchi mmoja akanijibu kuwa wameambiwa mpaka tenda ya huyu wa sasa iishe mwakani ndiyo watatafuta mtu mwingine.

Ifike mahala wale wa mikokoteni waachiwe kazi hii maana watu wapo tayari kulipia huduma lakini mzoaji hayupo mwisho wa siku nachelea au naogopa kama wakiamua kuziacha barabarani na hali hii ya mvua ni hatari kwa miundo mbinu lakini npia na magonjwa ya mlipuko.

Nimemabatanisha picha katika moja ya mtaa unaitwa Chuma nyuma ya kanisa la KKKT sizna kumekucha.


View attachment 2822917View attachment 2822918View attachment 2822919View attachment 2822920View attachment 2822916
Hizi picha mbona ni za Lagos Nigeria?
 
Leo niliona nipite tena kwa ndugu zangu wa juzi nione nini kimeendelea naona lalamikomlao limechukuliwa hatua na kama kunamdau humu au muhusika basi nami sina budi kumshukuru kwa kuwaona hawa ndugu zetu na kujali afya zao.Taka zimetolewa na wanasema ilikuja maalum kwa ajili ya eneo hilo. Nimefarijika jukwaa hili kuona hatua imechukuliwa.
picha 2 (3).jpeg
picha 2 (2).jpeg
 
Kwa Manispaa ya Ubungo takataka ni kila sehemu kwa sasa, hata Mabibo barabara ya ubungo maziwa to kigogo wananchi wameamua kuzirundika barabarani pembezoni mwa mifereji ya maji ya mvua ikitokea mvua kubwa itazisomba na kuziingiza mto msimbazi zote, zipo muda kila tukipita barabara hiyo twazikuta.
 
Back
Top Bottom