Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 8,870
- 14,258
Wakati saa ikisoma sifuri baina ya 2023 na 2024 mara Hamas wakaanza kurusha makombora kwa mtindo wao ule wa kama mvua ambapo Iron Dome huwa zinashindwa kujua ianze na lipi kati ya mengi yanayokuja.
Sauti za ving'ora zilizofuata hazikuwa ni zile za kuukaribisha mwaka mpya bali za kuwaonya watu wakimbilie kwenye mahandaki yao. Kizaazaa hicho kilikuwa ni kwa nchi nzima kuanzia mji mkuu wa TelAviv.
Kijana Gabriel Zemelman, 26 amesema sote tuliogopa tukiwa tumejibanza kwenye vipembe na nyoyo zikitudunda.
Naye Ran Stahl, 24 amesema kila akitaka kucheza anashindwa akimkumbuka rafiki yake aliyekuga oktoba 7 kwenye tamasha la muziki la Nova.
Kila akitaka kuinua mguu anajihisi mkosa huku rafiki yake huyo akimjia machoni.
Sauti za ving'ora zilizofuata hazikuwa ni zile za kuukaribisha mwaka mpya bali za kuwaonya watu wakimbilie kwenye mahandaki yao. Kizaazaa hicho kilikuwa ni kwa nchi nzima kuanzia mji mkuu wa TelAviv.
Kijana Gabriel Zemelman, 26 amesema sote tuliogopa tukiwa tumejibanza kwenye vipembe na nyoyo zikitudunda.
Naye Ran Stahl, 24 amesema kila akitaka kucheza anashindwa akimkumbuka rafiki yake aliyekuga oktoba 7 kwenye tamasha la muziki la Nova.
Kila akitaka kuinua mguu anajihisi mkosa huku rafiki yake huyo akimjia machoni.