Hamisa Mobeto ni kiini macho tu, Aziz Ki anafidiwa pesa aliyoikataa kwingine

SAYVILLE

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
7,895
Reaction score
12,975

Inahitaji jicho la kiinteligensia kujua baadhi ya mambo yanayoendelea nchi hii.

Watu wameshangaa inakuwaje Aziz Ki akatae zaidi ya milioni 90 kwa mwezi, tofauti labda ya zaidi ya milioni 60 ya pesa anayolipwa sasa. Likatengenezwa picha eti mlimbwende Hamisa Mobeto ndiyo kama kamshawishi abaki kwa sababu tu ya "penzi".

Kwa Deportivo de Utopolo ninayoijua mimi na kwa jicho langu la kiinteligensia, ninachojua mimi hawajataka kuweka wazi malipo sahihi wanayomlipa huyu Mbukinabe ili isije kuwaletea shida katika mahusiano kati ya wachezaji wenyewe katika kikosi au kumpa pressure kubwa mbele ya mashabiki. Pia hawakutaka aibu ya kuondokewa na mchezaji mwingine kwa sababu ya kuzidiwa kete na timu nyingine. Mobeto katumika kama kiini macho tu kuwahadaa Waswahili wasiopenda kuchakata bongo zao.

Kuna watu wamechota bilioni sehemu huko wamemlipa chini ya meza kufidia zile alizoziacha za Waarabu.
 
Kwani umekuwa shida Yangu kuendelea na Aziz Ki. Mbona nyie kina dada mnaachana na wenye pesa mnaenda kuanzisha mahusiano na wasio na chochote.

Kabla ya pesa Kuna mahusiano, Kuna mambo ambayo sio ya kifedha. Kuna kulinda jina pia hivyo hata kama Azizi amekubali offer ndogo Yanga, nakuhakikishia msimu ujao atakuwa na Furaha zaidi kuliko hata angeenda Al ahly.

Muukize Mayele atakuambia, muukize Micqson, kilichomrudisha cChama Simba ni kitu Gani?
 
Ela alizotaka Mayele na alizotaka Aziz Ki ni zipi nyingi? Kams Mayele tu aliyekuwa ndiye star wa timu alitaka mshahara wa milioni 48 na hakupata, sembuse hizo milioni 90?
 
Hakuna aliyetaka kumpa hizo ml 90 yes alitakiwa ila dau hazikuwekwa wazi so kama kabaki ni kakubaliana na matakwa ya Yanga Wala hakuna ziada.

Kama hizo deal zingekuwepo Faisal, Mayele na wachezaji wengine wakali sana tena wanaotaka hela ya kawaida wangeletwa.
 
Mbumbumbu kwenye heka heka zisizo na faida
 
Hii nchi ni kama wananchi wote darasa la saba tu.Yanachotwa mabilioni mangapi kulea timu kama mtu amleavyo manunu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…