Hamisi Shaban Taletale aka Babu Tale, fanya hima ujenge kwenu hii nyumba ni aibu kuu

Hamisi Shaban Taletale aka Babu Tale, fanya hima ujenge kwenu hii nyumba ni aibu kuu

Sijaelewa, huyo aliyefariki ni mke wake,kwahiyo msiba ulifanyika nyumbani kwao Tale au nyumbani kwa marehemu mke wake?
 
Nimekuelewa, ila kwa mtu ambaye ana uwezo wake mzuri kwanini ushindwe kujenga mjini na kijijini?

Hii ndo sababu inasababisha maendeleo pia yasienee kijijini maana watu hawaoneshi kujali umuhimu wa walipozaliwa
Safi! Umeongea bonge la point. Mijitu mingi haitaki kuwekeza vijijini na ni miongoni mwa sababu vijiji kudumaa. Niliona kuna familia fulani walimsakama sana ndugu yao kwa kuamua kujenga ghorofa kijijini kwao mkoani Tabora huko.
Inashangaza sana. Hata sisi wahaya tunajitahidi, lakini si kwa kasi sana.
 
Je status zetu ni sawa na wao?..kinachomponza tale hapa ni ustaa, then vile wanavyotuaminishaga kwamba pale WCB pesa Mingi.
 
Mmmmh.. ni wapi hapo nje ya nchi watu hawathamini kumiliki nyumba?

Tena nje ya nchi, watu ndo wanakuwaga na dream za ku own nyumba (real estate), sema shida ni kwamba kumiliki nyumba ni gharama sana ndo mana wengi wanaishia kupanga mpaka wanakufa.

Sioni kama ni akili kuwa na mihela mingi kwenye account halafu usiwe na nyumba, ni kukosa akili.. pesa hii hii ambayo ikitokea inflation inakuwa haina tofauti na makaratasi?

Mtu yoyote mwenye akili popote pale lazima uwaze kumiliki nyumba, at some point in your life... Hakuna ufahari wa kutokuwa na nyumba nzuri.

Refere basic needs
- Food
- Shelter (Housing)
- Cloth

Hivi ndo vitu vitakupa heshima duniani.. How you eat (become healthy), Where you live (Good House), what you wear (Good Clothes).. sijui kama umenisoma mkuu
Unachosema ni kweli kabisa.. lakini usipende sana kuishi kwa kutafuta heshima kutoka kwa watu... Kuna watu wengine hawapendi hustling za kujenga na kusumbuana na mafundi, wanaamua kupanga nyumba nzuri wanayoweza kumudu
 
Aibu kwa kweli halafu huwa wanajiita matajiri, hata kuweka curtains tu kumemshinda? Kashindwa kuendeleza kwao ndio huyu anataka ubunge? Au anataka ubunge ili anufaike ? Aibu hii. Maisha ya social media bwana........
Hamna aibu yoyote, yeye yupo kazini. Aibu tunaona sisi tunaoamini maisha yake ya kujulikana. Ustaa unaendana na kuficha uhalisia wa maisha, mwanasiasa lazima uwe muongo, fundi garadge lazima awe mchafu, kondakta lazima ajue kuongea sana, mzibua vyoo atanuka kinyesi.
Msanii lazima ataigiza maisha sawa na hao mapromota sijui mameneja.
 
aisee watu wanaofanya kazi za kisanii hawatabiriki.
Mimi nilivyoona wanavuma sana nikajua kwao kuna magorofa na nikajua ana maisha safi kumzidi diamond.
Kumbe hamna kitu kabisa,makelele mengii
Aibu kwa kweli halafu huwa wanajiita matajiri, hata kuweka curtains tu kumemshinda? Kashindwa kuendeleza kwao ndio huyu anataka ubunge? Au anataka ubunge ili anufaike ? Aibu hii. Maisha ya social media bwana........
 
aisee watu wanaofanya kazi za kisanii hawatabiriki.
Mimi nilivyoona wanavuma sana nikajua kwao kuna magorofa na nikajua ana maisha safi kumzidi diamond.
Kumbe hamna kitu kabisa,makelele mengii
Tatizo social media imetoa plate-forme kwa kila mtu awe nani awe nani. Kufake kwingi.
 
Kwa tafsiri yako wewe utajiri ni nini?
Naam. Sisi watu masikini tuna shida sana. Yaani tunashindana kuvaa, kula, nyumba... Ndio maana ukikaa Uswahilini, majirani watakuchukia kwa vitu kama kula mayai mara kwa mara! Akina Mo, Bakhresa... watapata wapi muda wa kumtazama jirani anavaaje? Ukisoma maoni mengi hapa, utaona jinsi wengi tulivyo masikini (mali na akili).
 
Back
Top Bottom