Hamza Mohamed Hassan azikwa makaburi ya Kisutu, Dar. Mazishi yachelewa kutoa risasi zilizokwama mwilini

Hamza Mohamed Hassan aliyefanya mauaji pale Selender bridge anazikwa leo na waislamu na rafiki na ndugu zake.

Tukio liko mubashara Global tv!
Nchi ya Tanzania ina wapumbavu wengi. Hivi watu hawajui privacy? Hivi watu hawajui mazishi ni mambo ya kifamilia? Huwa nashangaa kuona mtu amefiwa yuko kwenye uchungu na hawa makanjanja wa TV za online wamemzunguka eti wanamhoji!
 
Amesema amempigania Allah kwa kujitoa mhanga?!

Hivi Mungu kama ni mwenye nguvu anatakiwa ajipiganie mwenyewe au afanye kupiganiwa na Wanadamu?

Sasa hapo mkubwa atakuwa ni nani? Mwanadamu au Mungu?
 
unakumbuka lile tukio la kutengeneza kwamba kuna mwanajeshi mstaafu amepigwa risasi siku moja baada ya Tundu Lissu kushambuliwa?
Nalikumbuka vizuri sana, ili ku justify kuwa yoyote anaweza kushambuliwa na majambazi, [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Sijui walilimaliza vp lile tukio.
 
Hamza anajinasibu kumpigania Allah, jamaa lilikua kichwa maji jamani

Hivi watu wa aina hii wanamjua kweli Mwenyezi Mungu na mapenzi yake? Huyu Mungu anayeruhusu uzaliwe na ufe, ndio anakuruhusu ukaue mtu mwingine innocent?
Kuna watu hawajui wanalofanya. Hamza imekula kwake
 
Acha stori zako ndugu
Hamza ni kada mtiifu na chama tawala kinamtambua, watuambie wamemtenda nini?
Gaidi gani anamiliki silaha kihalali?

Ina maana mnataka kuivua nguo serikali kwamba ilifanya poor vetting ndo maana Hamza akaruhusiwa kumiliki silaha??
 
Alichokifanya Hamza nakifananisha kiasi na alichowahi kukifanya Said Mwamwindi kwa RC Dr Kleruu.
Probably Mwamwindi had an issue with the RC. Ingawa njia ya kutatua tatizo haikuwa sahihi kabisa, Wale vijana aliowauwa Hamza walikosa nini?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…