Hamza Mwapachu, Abdulwahid Sykes na Chief Michael Lukumbuzya

Hamza Mwapachu, Abdulwahid Sykes na Chief Michael Lukumbuzya

Swadakat Mkuu Kambaresharubu.
Maalim MS ahsante kwa kutuunganisha na kikubwa tunapata historia halisa ya wazee wetu sasa kama watu wanaumia matumbo sidhani kama hiyo ndiyo nia yetu, nimeelezwa kwamba aliyepakatwa kwenye hiyo picha mkono wa kulia ni Dada Ghania Chaurembo pia kwenye hiyo picha wapo Kaka zetu Idd Chaurembo, Mohamed Chaurembo, Salum Chaurembo,Mzee Dossa Aziz, Mohamed Ngarawa,Shariff Badawi, Mzee Abbas Sykes na mjomba Said Mahfoudh. Kama alivyoeleza Maalim MS hii picha ilipigwa Mtoni kwa Sheikh Chaurembo
a80fe48301fc46e41b965cb694cddebf.jpg

Naendelea kupata maelezo na In Shaa Allah kila nitakachopata nitakileta hapa Barzani
Mtebetini,
Ahsante sana kwa taarifa hii.
 
Unajua Wikipedia nini? Naweza ku upload taarifa wewe na ritz ni mtu na mumewe ikawa validated.
Hiyo link niliyoweka ina picha ya Nyerere akicheza bao. Nayo huiamini? Kama ambavyo hutaki kuamini kuwa hao wazee walipomkaribisha Nyerere walikuwa tayari hata jina la TANU wameshalitunga zamani.
 
Mohamed Said hatuwezi kwenda mbele kwa kutumia side mirror. Hizi hekaya zako zitatusaidia endapo kama taifa nia yetu ni kurudi nyuma na si kwenda mbele.
...Manzese,
Mimi kilichonisukuma kuandika maisha ya Abdul Sykes ni ile kugundua
kuwa historia yake na ya wazee wetu wengine waliounda TANU na kisha
kupigania uhuru wa Tanganyika imefutwa.

Sidhani kama kuna ubaya kuandika historia na wala hii sioni kama ni kurudi
nyuma.
 
Kuna kimtu kinaitwa Poscali na kijitu kinaitwa Yatco vinathubutu kusema MZEE SHEIKH ULAMAA MUHAMED SAID eti murongo.
Du vijitu vingine sijui vimesoma wapi hata kupambambanua vitu havijui.
Nasijui viko wapi muda mrefu sijaviona sijui vimekimbilia wapi Magu au Maswa?
Sahimtz,
Hiki kitabu cha Abdul Sykes wala kisingechapwa London endapo
isingekuwa uoga wa ''publishers,'' wa hapa nyumbani.

''Publisher'' wa kwanza niliyemuendea aliposoma mswada wa kitabu
alipata mshtuko.

Alinisaili kutaka kujua vipi nimeyajua hayo yote niliyoandika.

Nilimjibu kuwa wengi katika niliowataja ni wazee wangu na wengine
nimezungumzanao ana kwa ana.

Kitu alichoniambia ni kuwa nina mgodi wa dhahabu lakini aliogopa
kukichapa.

Niliwafuata Oxford University Press, Nairobi na wao pia walisema wao
hawataweza kukichapa ingawa walikiri ni kitabu kizuri.
 
Nguruvi3, Mag3, Mzee Mwanakijiji, Pasco, Yericko Nyerere, Nanren, Uncle Jei Jei na wanao fanana nao wameingia mitini.

Siwashangai, maana hakuna swali walilokuja nalo, tena kwa kebehi, ambalo halijapata jibu la uwazi na ukweli usiopingika.

Mimi nnawaomba sana watueleze historia ya wazee wao katika hizo harakati za uhuru, watutupie na vipicha vya hapa na pale na kama hawawezi basi wasikimbie kwa tahayuri, waje kuujuwa ukweli.

Wasiuogope ukweli, ukweli utawaondoa kwenye kifungo cha fikra walichofungwa bila kujijua.
 
Sahimtz,

Ngoja nimnukuu kiduchu Mwalimu Nyerere kwenye hotuba yake.

"Wakanichagua President wa African Association. Tanganyika African Association... Ndipo tukaanza sasa shughuli za kujaribu kuandika katiba mpya ya TAA kusudi tuipe madhumuni ya shahaba ya kuleta uhuru."

"Mwaka uliofuata 1954 ndio tuka, kwa kweli mimi nilidhani tutachukua katiba tu wenzangu wakasema hapana, tukibadili katiba tubadili na jina".

"Tukahaingaika sana kupata jina na hao hao kina Abdul Sykes, jina lile hatukuligundua. Wao walikuwa wamelifikiria zamani wakina Abdul Sykes hao. Walikuwa Burma alikuwa askari na kule waliwahi kufikiria kuanzisha chama..."Kusema kweli wao waliwahi kufikiria kabisa Tanganyika African National Union."Kwa hiyo wakati tunahangaika hangaika pale tuchukuwe jina gani tuchukue Tanganyika African Union wakasema hali itafanana na Kenya African Union. Watadhani nao ni Maumau. Tunataka kuanzisha Maumau yetu. Ndio wakina Abdul Sykes wakakumbuka jina lao walilokuwa wameliunda walipokuwa Burma, wakasema tuite Tanganyika African National Union, ndio tukaanzisha..."

"Wazee wa Dar es Salaam wakaniamini upesi sana, kijana mdogo nikawa na uhusiano mkubwa sana na wazee wa Dar es Salaam. Mkubwa sana, watu wazima, mimi mdogo. Wadogo wenzangu wengine walikuwa ni hao Abdul Sykes kina Abbas Sykes wakina Dossa. Lakini wengine wote walikuwa watu wazima...".

Hii hotuba ilikuwa inaendelea ngoja tufanye juhudi tuipate yote.

Wazee wetu Mwenyezi Mungu hawajaze kheri kwa nia zao nzuri kwa taifa letu.
Mkuu Ritz shukran jazirah ukipata yote tuwekee tupate kusikia kutoka kwa kiywa cha mwalim labda wenzetu wataelewa.
 
Dah hii story is so amazing yan.. Ila mbona zimefichwa jaman.?
Bakar..,
A fascinating and amazing story in deed!

Kisa cha kukataliwa historia ya Abdul Sykes ni kuwa ikiwa utamleta Abdul
katika historia ya TANU itabidi urudi nyuma miaka miaka 50 kupata asili yao
ya Kizulu vipi walikuja Tanganyika.

Utakwenda hadi Kwa Likunyi Mozambique ambako Sykes Mbuwane babu
yake Abdul alikotokea.

Hiki kijiji kipo Imhambane na ndipo Von Wissman alipokwenda kuchukua
jeshi la mamluki wa Kizulu kuja Tanganyika kupigana na Abushiri bin
Salim
na Chief Mkwawa miaka ya mwisho ya 1800.

Ally Sykes mwaka wa 1952 alichukua likizo na akaenda hadi kwao kwa
Likunyi kuona alikotoka babu yake.

Nimeandika kitabu cha maisha ya Ally Sykes, ''Under the Shadow of British
Colonialism.''

Huu mswada haujachapwa sasa karibu mwaka wa ishirini.

Humo ndimo aliponieleza safari tatu muhimu kwake wakati wa kudai uhuru.

Safari ya kwanza hii ya Mozambique 1952, safari ya pili Ghana kuadhimisha
uhuru wa Ghana 1947 tena hakupanda ndege kenda kwa nchi kavu na safari
nyingine ya Rhodesia 1953 alipokamatwa na Makaburu.

Safari hii TAA ilialikwa Northern Rhodesia na Kenneth Kaunda raia wa African
National Congress na alifatana na Denis Phombeah.

Ukielezwa aliyoshuhudia Ally Sykes katika hizi safari utajua nini maana ya ukoloni.

Ikiwa utaeleza haya na mengine mengi ambayo hapa hakuna nafasi ya kuyaeleza
utakuja na sura nyingine kabisa katika historia ya TAA, TANU na harakati za uhuru.

Itabidi ueleze vipi hawa akina Sykes walijuana na Kenneth Kaunda, Jomo
Kenyatta
,viongozi wa Fabian Society kama John Hatch kabla hata
Nyerere hajawajua.

Itakubidi pia ueleze vipi baba yao aliasisi African Association (AA) 1929 na
Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika 1933.

Vipi aliweza kujenga nyumba hiyo ilipozaliwa TANU na kujenga shule jengo
ambao lipo hadi leo.

Itabidi pia ueleze viongozi wa wakati ule na michango yao katika jamii hasa
machifu kama Chief Kidaha Makwaia, Chief Abdallah Said Fundikira na
Thomas Marealle ambao wakijuana vyema na akina Sykes na kustahiana
sana.

Hizi ndizo zilikuwa siasa za nyakati ule.
Haya hayakutakiwa.

Waandishi na watafiti wa Kivukoni College waliona hii itapunguza umuhimu wa
Nyerere katika historia ya TANU.

Tatizo likawa historia ya TANU lazima ianze na Mwalimu Nyerere.
Hili ndilo likasababisha matatizo mengi katika uandishi wa historia ya TANU.

Hivi ndivyo tulivyofikishwa hapa leo tuko barzani tunajadili na wengine kama
akina Nguruvi3 wanajadili kwa hamaki wakidai ati Mwalimu Nyerere
anakashfiwa.

Na ''kashfa,'' yenyewe ni kule kuandika historia ya TANU kama ilivyokuwa.
 
Duh nazidi kuchanganyikiwa. Minadhani tumuulize na Kaunda, si bado yupo. Kwa hiyo pale Lumumba ni kwa Sykes
 
Duh nazidi kuchanganyikiwa. Minadhani tumuulize na Kaunda, si bado yupo. Kwa hiyo pale Lumumba ni kwa Sykes
Onyx,
Huna haja ya kuchanganyikiwa wala kumtafuta
Kaunda.

Mimi sikwenda Zambia kuyajua haya yote.

Unachotakiwa kufanya ni kupitia Sykes Papers.

Hebu soma hapo chini:
''In his capacity as the secretary of TAGSA, Ally
Sykes
had established contact with the Secretary
-General of the Pan African Congress of Northern
Rhodesia, Kenneth David Kaunda.'' [1]


[1] K.D. Kaunda to A.K. Sykes, 28 th December,
1953. Sykes Papers.

Kutoka kitabu cha Abdul Sykes...
 
Wanaukumbi.

Mkipata wasaa japo kiduchu msikilizeni Mwalimu Nyerere, akiwaongelea hawa wazee wetu "wacheza bao" kama wanavyoitwa na ndugu zetu hapa barzani.

Ni kapande cha hotuba ya kuanga mwaka 1985 pale Diamond Jubilee, akiongea na Wazee wa Dar es Salaam...

https://m.soundcloud.com/faraj-mohammed-1/nyerere-audio.

Hicho ni kapande kidogo cha hotuba ilikuwa ndefu lakini Abdulwahid Sykes, katajwa na Mwalimu Nyerere, zaidi ya mara tano lakini humu barzani watu hawataki kabisa Abdulwahid Sykes, watu wamtaje daah!!
mkuu Ritz kwa hotuba hii wale waliokuwa wanabisha kuwa jina la TANU sio wazo la Mwalimu ila jina hilo wazee wetu walikuwa nalo kabla mwalimu hajajiunga TAA watakuwa wameshapata majibu kongole Mzee MS hakika wewe ni kisima cha historia yetu japokuwa kuna wengine wachache hawataki kuukubali ukweli
 
mkuu Ritz kwa hotuba hii wale waliokuwa wanabisha kuwa jina la TANU sio wazo la Mwalimu ila jina hilo wazee wetu walikuwa nalo kabla mwalimu hajajiunga TAA watakuwa wameshapata majibu kongole Mzee MS hakika wewe ni kisima cha historia yetu japokuwa kuna wengine wachache hawataki kuukubali ukweli
Wa Ukae,
Mimi siku zote huwaambia watu kuwa si kama mimi nina akili kuzidi
wengine ila Allah mwenyewe alijaalia kuwa nilizaliwa katika kipindi
kile cha siasa za utaifa wa Tanganyika na watu wale ambao walikuwa
katika wimbi lile.

Nitake nisitake ikawa lazima historia hii nitaijua nje ndani, ndani nje.
Hii hotuba ni katika moja ya bahatii mbaya sana kwa Mwalimu Nyerere.

Ni katika hotuba hii aliposema kuwa hakumbuki Abdul Sykes alikua na
nafasi gani katika uongozi wa TAA.

Kama hili halikutosha ndiyo kwa mara ya kwanza Nyerere anasikika kwa
mara ya kwanza akimtaja Abdul Sykes kwa ulimi wake hadharani.

Hotuba hii ilirushwa mubashara kutoka Diamond Jubilee Hall na mimi
nilikuwa nasikiliza.
 
Maalim Mohamed Said Salaam Aleykum
Nimekuwa nikikisikiliza kipande cha hotuba ya Mwalimu Nyerere ambayo hakukamilika aliyoileta
Al-alama Ritz na katika pita pita yangu humu kwenye Jamvi nikakuta uzi ambao umeandikwa na jamaa yetu, naomba niweke huo uzi hapa muone

Mwalimu Nyerere alifanya kosa kujiunga na TAA, angebaki na TAWA yake itupe UHURU

Maalim naona katika maelezo ya wachangiaji wa huo uzi wa hapo juu kulitolewa ombi la kuileta hii hotuba ya maneno badala ya maandiko,mi nauliza mleta bandiko alileta hii hotuba ya maneno Barzani? kama hakuleta naomba aombwe ailete maana ameiandika kwa urefu, badala ya Al-alama Ritz kuhangaika kuitafuta.
 
Maalim Mohamed Said Salaam Aleykum
Nimekuwa nikikisikiliza kipande cha hotuba ya Mwalimu Nyerere ambayo hakukamilika aliyoileta
Al-alama Ritz na katika pita pita yangu humu kwenye Jamvi nikakuta uzi ambao umeandikwa na jamaa yetu, naomba niweke huo uzi hapa muone
sifa
Mwalimu Nyerere alifanya kosa kujiunga na TAA, angebaki na TAWA yake itupe UHURU

Maalim naona katika maelezo ya wachangiaji wa huo uzi wa hapo juu kulitolewa ombi la kuileta hii hotuba ya maneno badala ya maandiko,mi nauliza mleta bandiko alileta hii hotuba ya maneno Barzani? kama hakuleta naomba aombwe ailete maana ameiandika kwa urefu, badala ya Al-alama Ritz kuhangaika kuitafuta.
Mtebetini,
Mimi ningeweza kuchangia katika bandiko hilo kwa nia ya kuelimisha
ila kwa kasoro moja kubwa sana.

Huyo aliyefungua uzi hana moja alijualo katika si historia ya AA, TAA
wala TANU.

Baya zaidi anamkopi Mohamed Said kisha anabadilisha hapa na pale
anavyopenda mwenyewe na kibaya sana ananitukania wazee wangu.

Angekuwa huyu ni msomi wa haja mathalan katika viongozi na waasisi
wa AA, TAA na TANU yeye anawabadilisha na kuwapa sifa ambazo si zao
angelikuwa na ushahidi lakini hana lolote ni maneno tu.

Historia ya TAA katika mwaka wa 1950 palipofanyika mapinduzi ya kuwatoa
Mwalimu Thomas Plantan na Clement Mohamed Mtamila, Judith
Listowel
katika kitabu chake: The Making of Tanganyika (1965) kaeleza
lau kwa ufupi mchango wa Schneider Abdillah Plantan.

Mohamed Said ndiye aliyekuja na maelezo kamili ya nini kilitokea katika
kuuweka uongozi mpya madarakani.

Aliyetoa maelezo haya alikuwa Waziri Dossa Aziz tena nyumbani kwake
Mlandizi mbele ya Ally Sykes.

Mohamed Said anaona shida kuchangia uzi wa mtu ambae haijui historia
ya Tanganyika.

Kuhusu hiyo hotuba ya Mwalimu Nyerere.

Kwa sasa sitosema kitu hadi tumeisikiliza sote hapo nitakuonyesheni wapi
katia mkono wake kubadili maneno.

Lakini ikiwa unataka kuona jinsi historia ya TANU ilivyopotezwa na kujua
vipi Dr. Kyaruzi aliingia katika uongozi wa TAA nakusihi uingie hapo chini:
Mohamed Said: WAJUE SHEIKH HASSAN BIN AMIR, SCHNEIDER PLANTAN, HAMZA MWAPACHU, ABDUL SYKES NA DR. VEDASTO KYARUZI KATIKA HISTORIA YA TANU

<iframe width="420" height="315" src="" frameborder="0" allowfullscreen></iframe>
 
Maalim Mohamed Said Salaam Aleykum
Nimekuwa nikikisikiliza kipande cha hotuba ya Mwalimu Nyerere ambayo hakukamilika aliyoileta
Al-alama Ritz na katika pita pita yangu humu kwenye Jamvi nikakuta uzi ambao umeandikwa na jamaa yetu, naomba niweke huo uzi hapa muone

Mwalimu Nyerere alifanya kosa kujiunga na TAA, angebaki na TAWA yake itupe UHURU

Maalim naona katika maelezo ya wachangiaji wa huo uzi wa hapo juu kulitolewa ombi la kuileta hii hotuba ya maneno badala ya maandiko,mi nauliza mleta bandiko alileta hii hotuba ya maneno Barzani? kama hakuleta naomba aombwe ailete maana ameiandika kwa urefu, badala ya Al-alama Ritz kuhangaika kuitafuta.
Akhui Mtebetini,

Ukipata wasaa pitia hapa chini kwenye huu uzi vyombo vimo humo huyu mleta mada alikimbia mwenyewe pamoja na wenzake uzi ulikua hatari.

Uchochezi wa Mohamedi Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar
 
Maalim Mohamed Said
Nimekusoma na uliyonieleza ni dhahir shahir mleta ule uzi anabandika/anabadilisha taarifa za vyanzo vyake vya habari. Nimeleta uzi huo hapa Barzani ili kuweka kumbukumbu sawa kwani kwenye uzi huo mleta uzi aliombwa kuleta Audio mimi nakumbusha alete tuisikie,Audio iliyoletwa na Al-alam Ritz ni kipande kidogo nikilinganisha na maelezo aliyoandika mleta huo uzi.
 
Maalim Mohamed Said
Nimekusoma na uliyonieleza ni dhahir shahir mleta ule uzi anabandika/anabadilisha taarifa za vyanzo vyake vya habari. Nimeleta uzi huo hapa Barzani ili kuweka kumbukumbu sawa kwani kwenye uzi huo mleta uzi aliombwa kuleta Audio mimi nakumbusha alete tuisikie,Audio iliyoletwa na Al-alam Ritz ni kipande kidogo nikilinganisha na maelezo aliyoandika mleta huo uzi.

Huyo anaejiita Yericko Nyerere katika uzi aliobandika link Ritz alijidai ataenda "nyumbani" Msasani atuletee mkanda wa video wa hotuba ya Nyerere, tukambana akijidai ataenda nyumbani Butiama tukambana sana kwa uongo wake mpaka akaja kushushuliwa na mtoto wa kwanza wa Mwalimu Nyerere ambae ni mwana JF pia aitwae Andrew Nyerere.

Huyo ni muongo wa ajabu anafanya plagiarism za kijinga, tena achunge sana asije akashitakiwa kwa kuchukua kazi za watu na kujifanya zake huku akiandika hovyo hovyo, chini kabisa ya kiwango chochote cha uandishi.

Ni mtu hatari sana.
 
Back
Top Bottom