Hamza Mwapachu, Abdulwahid Sykes na Chief Michael Lukumbuzya

Hamza Mwapachu, Abdulwahid Sykes na Chief Michael Lukumbuzya

Mashujaa kwa lipi!? Inawezekana walikuwa wacheza bao nje ya ofisi za TANU, au wakereketwa tu, kama walivyo manyumbu wengine wa vyama vya siasa.....!

Hawana mchango wowote zaidi ya ushabiki, hivyo kutokea kwenye picha haina maana kuwa ulichangia chochote katika harakati za ukombozi...! Hata wewe unaweza kuingia kwenye kundi la wachezaji wa Yanga kushangilia ushindi, ukatokea kwenye picha! Hiana maana kuwa na wewe ulikuwa uwanjani.!

Haijawahi kutokea babuyo akaweko kwenye hizo picha kwa bahati nzuri? Zitazame vizuri...

Kuhusu bao wala isiwe mwao...
https://upload.wikimedia.org/wikipedia/sw/4/4d/Nyerere_bao_butiama.jpg

Birds of a feather...
 
Mkuu Mshume Kiyate
Naweka picha ya hawa wazee wanaoitwa wacheza bao na baadhi ya majina yao ambao mi sijawahi kusoma kwenye somo la historia shuleni. Tunachosema hapa tunawekewa sawa kumbukumbu anaebisha atuambie hawa wazee hata mmoja wao katajwa wapi kwenye historia inayofundishwa shuleni
1466702299320.jpg

WAZEE WALIOANZISHA VUGUVUGU LA KUSAKA UHURU

Kutoka kulia waliosimama.
1. Abdallah Shomari (Tandamti no. 3)
2. Nassoro kalumbanya (simba str.)
3. Said Chamwenyewe (Aggrey/Congo str.)
4. Mtoro Ally (Muhonda str.)
5. John Rupia (Misheni kota)
6. Julius Nyerere(Pugu Sekondari) 7. Said Chaurembo (Congo/ Mkunguni str.)
8. Jumbe Tambaza(Upanga)
9. Sheikh Suleiman Takadir (Mafia /Swahili)
10. Dossa Aziz (Mbaruku/Somali kipande)
11. Mshume Kiyate (Tandamti)
12. Juma Sultan (Kitchwele karibu na kanisa dogo )
13. Maalim Shubeti (Masasi/ Likoma)
14. Rajab Simba ( kiungani str.)
15. Waziri Mtonga (Kilosa no.18, Ilala)
16. Mwinjuma Mwinyikambi (Mwananyamala)
17. Maxi Mbwana (Aggrey/Kongo)
18. Yosia Omari(Sungwi Kisarawe)
19. Sheikh Issa Nassir ( Bagamoyo)
 
Wanaukumbi.

Mkipata wasaa japo kiduchu msikilizeni Mwalimu Nyerere, akiwaongelea hawa wazee wetu "wacheza bao" kama wanavyoitwa na ndugu zetu hapa barzani.

Ni kapande cha hotuba ya kuaga mwaka 1985 pale Diamond Jubilee, akiongea na Wazee wa Dar es Salaam...

https://m.soundcloud.com/faraj-mohammed-1/nyerere-audio.

Hicho ni kapande kidogo cha hotuba ilikuwa ndefu lakini Abdulwahid Sykes, katajwa na Mwalimu Nyerere, zaidi ya mara tano lakini humu barzani watu hawataki kabisa Abdulwahid Sykes, watu wamtaje daah!!
 
Kwanini mada za mwalimu mohd said watu wa upande flani zinawachoma sana
 
Wanaukumbi.

Mkipata wasaa japo kiduchu msikilizeni Mwalimu Nyerere, akiwaongelea hawa wazee wetu "wacheza bao" kama wanavyoitwa na ndugu zetu hapa barzani.

Ni kapande cha hotuba ya kuanga mwaka 1985 pale Diamond Jubilee, akiongea na Wazee wa Dar es Salaam...

https://m.soundcloud.com/faraj-mohammed-1/nyerere-audio.

Hicho ni kapande kidogo cha hotuba ilikuwa ndefu lakini Abdulwahid Sykes, katajwa na Mwalimu Nyerere, zaidi ya mara tano lakini humu barzani watu hawataki kabisa Abdulwahid Sykes, watu wamtaje daah!!
Ritz..Mwalimu Jkn ktk hii hotuba ametamka wazee wazee wazee wa DSM kama mara 10 hivi na anewataja kina sykes mara kadhaa.
Ivi hawa watu wanao sita kuamini kauli na maadishi ya Sheikh Muhamed Said wanataka wapewe ushahidi gani tena wa ukweli na ithibati zaidi ya haya?
Cha ajabu kuna mtu eti na yeye katunga kitabu kujibu vitabu vya Sheikh Muhamed sasa anajibu nini kama Mwalimu Jkn mwenyewe anatamka wazee wazee wa Dsm na kina sykes?
 
Ritz..Mwalimu Jkn ktk hii hotuba ametamka wazee wazee wazee wa DSM kama mara 10 hivi na anewataja kina sayks mara kadhaa.
Ivi hawa watu wanao sita kuamini kauli na maadishi ya Sheikh Muhamed Said wanataka wapewe ushahidi gani tena wa ukweli na ithibati zaidi ya haya?
Cha ajabu kuna mtu eti na yeye katunga kitabu kujibu vitabu vya Sheikh Muhamed sasa anajibu nini kama Mwalimu Jkn mwenyewe anatamka wazee wazee wa Dsm na kina sayks?
Sahimtz,

Ngoja nimnukuu kiduchu Mwalimu Nyerere kwenye hotuba yake.

"Wakanichagua President wa African Association. Tanganyika African Association... Ndipo tukaanza sasa shughuli za kujaribu kuandika katiba mpya ya TAA kusudi tuipe madhumuni ya shahaba ya kuleta uhuru."

"Mwaka uliofuata 1954 ndio tuka, kwa kweli mimi nilidhani tutachukua katiba tu wenzangu wakasema hapana, tukibadili katiba tubadili na jina".

"Tukahaingaika sana kupata jina na hao hao kina Abdul Sykes, jina lile hatukuligundua. Wao walikuwa wamelifikiria zamani wakina Abdul Sykes hao. Walikuwa Burma alikuwa askari na kule waliwahi kufikiria kuanzisha chama..."Kusema kweli wao waliwahi kufikiria kabisa Tanganyika African National Union."Kwa hiyo wakati tunahangaika hangaika pale tuchukuwe jina gani tuchukue Tanganyika African Union wakasema hali itafanana na Kenya African Union. Watadhani nao ni Maumau. Tunataka kuanzisha Maumau yetu. Ndio wakina Abdul Sykes wakakumbuka jina lao walilokuwa wameliunda walipokuwa Burma, wakasema tuite Tanganyika African National Union, ndio tukaanzisha..."

"Wazee wa Dar es Salaam wakaniamini upesi sana, kijana mdogo nikawa na uhusiano mkubwa sana na wazee wa Dar es Salaam. Mkubwa sana, watu wazima, mimi mdogo. Wadogo wenzangu wengine walikuwa ni hao Abdul Sykes kina Abbas Sykes wakina Dossa. Lakini wengine wote walikuwa watu wazima...".

Hii hotuba ilikuwa inaendelea ngoja tufanye juhudi tuipate yote.

Wazee wetu Mwenyezi Mungu hawajaze kheri kwa nia zao nzuri kwa taifa letu.
 
Mkuu Mshume Kiyate
Naweka picha ya hawa wazee wanaoitwa wacheza bao na baadhi ya majina yao ambao mi sijawahi kusoma kwenye somo la historia shuleni. Tunachosema hapa tunawekewa sawa kumbukumbu anaebisha atuambie hawa wazee hata mmoja wao katajwa wapi kwenye historia inayofundishwa shuleniView attachment 359432
WAZEE WALIOANZISHA VUGUVUGU LA KUSAKA UHURU

Kutoka kulia waliosimama.
1. Abdallah Shomari (Tandamti no. 3)
2. Nassoro kalumbanya (simba str.)
3. Said Chamwenyewe (Aggrey/Congo str.)
4. Mtoro Ally (Muhonda str.)
5. John Rupia (Misheni kota)
6. Julius Nyerere(Pugu Sekondari) 7. Said Chaurembo (Congo/ Mkunguni str.)
8. Jumbe Tambaza(Upanga)
9. Sheikh Suleiman Takadir (Mafia /Swahili)
10. Dossa Aziz (Mbaruku/Somali kipande)
11. Mshume Kiyate (Tandamti)
12. Juma Sultan (Kitchwele karibu na kanisa dogo )
13. Maalim Shubeti (Masasi/ Likoma)
14. Rajab Simba ( kiungani str.)
15. Waziri Mtonga (Kilosa no.18, Ilala)
16. Mwinjuma Mwinyikambi (Mwananyamala)
17. Maxi Mbwana (Aggrey/Kongo)
18. Yosia Omari(Sungwi Kisarawe)
19. Sheikh Issa Nassir ( Bagamoyo)
Hawa ndio Muwalimu JKN alio wataja ktk hotuba aliyo weka ustaadh Ritz.
WAZEE WAZEE WAZEE WA DSM.
 
Sahimtz,

Ngoja nimnukuu kiduchu Mwalimu Nyerere kwenye hotuba yake.

"Wakanichagua President wa African Association. Tanganyika African Association... Ndipo tukaanza sasa shughuli za kujaribu kuandika katiba mpya ya TAA kusudi tuipe madhumuni ya shahaba ya kuleta uhuru."

"Mwaka uliofuata 1954 ndio tuka, kwa kweli mimi nilidhani tutachukua katiba tu wenzangu wakasema hapana, tukibadili katiba tubadili na jina".

"Tukahaingaika sana kupata jina na hao hao kina Abdul Sykes, jina lile hatukuligundua. Wao walikuwa wamelifikiria zamani wakina Abdul Sykes hao. Walikuwa Burma alikuwa askari na kule waliwahi kufikiria kuanzisha chama..."Kusema kweli wao waliwahi kufikiria kabisa Tanganyika African National Union."Kwa hiyo wakati tunahangaika hangaika pale tuchukuwe jina gani tuchukue Tanganyika African Union wakasema hali itafanana na Kenya African Union. Watadhani nao ni Maumau. Tunataka kuanzisha Maumau yetu. Ndio wakina Abdul Sykes wakakumbuka jina lao walilokuwa wameliunda walipokuwa Burma, wakasema tuite Tanganyika African National Union, ndio tukaanzisha..."

"Wazee wa Dar es Salaam wakaniamini upesi sana, kijana mdogo nikawa na uhusiano mkubwa sana na wazee wa Dar es Salaam. Mkubwa sana, watu wazima, mimi mdogo. Wadogo wenzangu wengine walikuwa ni hao Abdul Sykes kina Abbas Sykes wakina Dossa. Lakini wengine wote walikuwa watu wazima...".

Hii hotuba ilikuwa inaendelea ngoja tufanye juhudi tuipate yote.

Wazee wetu Mwenyezi Mungu hawajaze kheri kwa nia zao nzuri kwa taifa letu.
Kuna kimtu kinaitwa Poscali na kijitu kinaitwa Yatco vinathubutu kusema MZEE SHEIKH ULAMAA MUHAMED SAID eti murongo.
Du vijitu vingine sijui vimesoma wapi hata kupambambanua vitu havijui.
Nasijui viko wapi muda mrefu sijaviona sijui vimekimbilia wapi Magu au Maswa?
 
Mohamed Said hatuwezi kwenda mbele kwa kutumia side mirror. Hizi hadithi zako zitatusaidia kama nia yetu kama taifa ni kurudi nyuma na sio kwenda mbele.
 
CtOKRwRzrB5mBzQ5Cb9hS_jD8pN0sOFV1B9UckVYU8i70_Q_XEgdcQvlLqtXwNIGW3VWYaLF4a3otlgbC7K9Em0h3Ei39ed7tspSVQ5gtgrZL5rX2su_TqGlyreZorkWRdRYWBJm9Hn-QodC4i5vw06b46UkgySmTNjczP8cj6bmXb4RA6T3qSC_BRU6IEc8Uk75bpciUYbt_YdFaT-dh7hXKdN7cAdD9DHdB4xKJnFGYL4kk1Re5KOjQb6dQbt6-W2QvuYpX7q_3wE2ayyasqEFYWkowgSSkAVFoSq7jL6StW7uicmeAbddSAD_lW0f1GKpvu4xqI9a4PI-bYpm_24kxvl6H8PB1jGH53J9kAbmKXXFPW9YH4qAATIs8DSUScqrg8cJFiy35i4w8jl_JY9uTugl2Aw44difR64FY7bDSEaxEnvJoAwt7M-fxGIG15Umq6XOPqn2rzgSW-lp0fZFNQw9Psx1PGIaIrPRkMAm9PszJcCMiwBkZ9tPSxmQbYeMWxj0yL1lzzPXdNCcTFcoGpAmatJ1uOku2ZCcVz5Si6WIiO58WJjxk8cC3pX-kibj3Y1fBK5co9QGLfLHjSh0zHTOmAOH=w579-h657-no

Chief Michael Lukumbuzya wa Ukerewe​

Nilikuwa naitafuta picha ya hayati Chief Michael Lukumbuzya kwa miaka mingi bila mafanikio. Sababu ya kuitafuta picha ya Chief Lukumbuzya ni kisa alichonihadithia Bi. Mwamvua biti Masha mke wa marehemu Abdulwahid Sykes maarufu akijuikana kwa jina la mwanae wa kwanza Daisy hivyo tukimuita Mama Daisy.

Nilikuwa kila nikipata fursa ya kuwa na mama yangu Bi. Mwamvua, yaani Mama Daisy nikipenda kumdodosa mambo yalivyokuwa wakati wa ukoloni walipokuwa wanapambana na Muingereza, kwanza kichinichini katika miaka ya mwanzo ya 1950 wakati wa TAA kisha wakipambana na mkoloni dhahiri baada ya kuunda TANU mwaka wa 1954.

Bi. Mwamvua
alikuwa wakati mwingine bila kutegemea akiniangushia habari muhimu kupita kiasi. Mfano siku aliponiambia kuwa nafasi ya president wa TANU nafasi ile ilikuwa ya Chief Kidaha Makwaia lakini alikataa ndipo bahati ikamuangukia Julius Nyerere.

IMG-20160406-WA0111%2B%25281%2529.jpg

Chief David Kidaha Makwaia​

Iko siku akanieleza taharuki iliyotokea nyumbani kwa Abdul Sykes baada ya Nyerere kula chakuka kilichomfanya tumbo limkate na ikadhaniwa kuwa amelishwa sumu.

Mkasa huu ulitokea wakati mama yake Nyerere, Bi. Mugaya Nyangombe yuko na Mama Maria Nyerere vilevile wamekaa uani na akina mama wengine na Abdul Sykes, Nyerere na viongozi wengine wako nyumba kubwa wanapanga mipango ya kupeleka harakati mbele.

Mama yake Nyerere alianza kulia akiamini kabisa kuwa mwanae katiliwa sumu katika chakula. Mama Daisy alikuwa na habari nyingi sana za nyakati zile. Historia ya TANU kama zilivyo nyaraka na picha zake nyingi zimo mikononi mwa watu.

Mfano mwingine ni wa mkutano wa kwanza wa Wanawake wa TANU uliokuwa ukifanyika Arnautoglo Hall na yeye alikuwa yuko nyumbani anafanya shughuli zake. Anasema, ‘’Aliporudi nyumbani Bwana Abdul kanikuta nimekaa, akaniuliza wewe hukwenda mkutanoni? Wenzako wote wako Arnautoglo…’’ Bi. Mwamvua anasema hapo hapo akachukua baibui lake na kuelekea mkutanoni.

Wasemaji wakuu walikuwa Bi. Titi Mohamed na Bi. Tatu biti Mzee. Huu ndiyo mkutano wa kwanza wa wanawake wa TANU.

toW0HLKw0_eZRKHUURD38LIxZWcW5RXD7goNoYJWFVWEj8kMEyL1bPXqHWB5CmfrXmD1mA=w329-h566-no

Kushoto Mama Daisy na mbele yake ni Bi. Titi Mohamed
na Bi. Zainab mke wa Tewa Said Tewa

Katika mazungumzo kama haya ndipo siku moja akanihadithia habari za Chief Luumbuzya. Anasema walitoka Dar es Salaam yeye mumewe kwenda Nansio, Ukerewe kumtembelea Hamza Mwapachu.

Anasema walipanda meli Mwanza pamoja na Chief Lukumbuzya kuelekea Nansio. Lukumbuzya alikuwa anatokea Makerere Uganda alipokuwa anasoma anarudi nyumbani likizo. Abdul Sykes na Michael Lukumbuzya hawakuwa wanajuana.

Hamza Mwapachu alikuwa amekusanya wananchi na kikundi cha ngoma kuja kumpokea bandarini Nansio President wa TAA Abdulwahid Sykes. Lukumbuzya alishangazwa kukuta sherehe bandarini akifanyiwa mtu ambae yeye hakuwa anamjua na akiuliza anaambiwa ni mgeni kutoka Dar es Salaam.

Lukumbuzya alipigwa na butwaa kuona mapokezi ya watu wake wa Ukerewe wakiwa katika nderemo wakati yeye chief hakuna hata mtu alikuwa anajua kuwa yumo katika meli ile ile. Baadae Hamza Mwapachu alimfahamisha yule mgeni waliokuja kumpokea pale alikuwa nani katika siasa za Tanganyika.

proxy

Hamza Kibwana Mwapachu​

Simulizi kama hizi zilinifikirisha sana katika kutaka kuwajua wazalendo wa wakati ule. Hamza Mwapachu alikuwa anafanya haya ya kukusanya wananchi kumpokea kiongozi wa Waafrika chini ya pua za Waingereza bila kujali nini kitampata licha ya kuwa yeye kupewa uhamisho kupelekwa kisiwani Ukerewe peke yake ilikuwa ni adhabu, kwa hakika ni kifungo khasa cha kumtia kuzuizini asiweze kuenedeleza mipango yake ya kuunda chama cha siasa.

Uhuru ulipopatikana Chief Michael Lukumbuzya alipelekwa nje ambako alikuwa balozi na mwisho akawa balozi Canada ambako huko ndiko umauti ulikomfika.

6La5FUdYcnEadMYf6JSIrrWhkpElkSUYiAFTlRs_Bz4mDSXPmSD4EMzk4gTvEnMGuvf8pxy__jBGacnsvJHLYxP_wyS0OA25OYba8__txYHDI2z5TOfGkl7O_IoMO3NAleFvmru20T-YQF39hdK_UD7K79l2x2k40bDIMbiMoIB_ArerygwQ5oIGK11itARq1AoviA_D4OZrLGJZ-mOTiDWEC0pNQPmQPCS-cXzyWVr9raFuGLLKTwCz1GYMrJwsoBIeqCiy_AoHfwRMiTgHgBNRPHowAkwTnbtPxlJ_q9CTx_Ny6xhgBxkIMIBwc9Y79KJA7DXbYcODNB5X-lEL7SxzUEASzHc9r77_ByOVTHcN0j-HCDs2tr7oGw85M3YPXBv0OHG_2pnc_yZefK7n9_UyaxLXX1pmIeP1p01hc6LGf1QcrRusRSirpgfDZrxPMGTwr3EcKUjvY8vh1Kj2_zL9VnkUc-uHdQCSgUi6JBUaZrDi_2LVFAy1ImbD9BwIspcf8aHvXSBLQFSWfC2m3EGmjIMKOU2CDUXZv8NTjsn7UCfaBiWfrRT4ab3OSNhVpvB2GqLU1Rgk5_YjnfJgAxeKukdqeFoc=w476-h657-no

Abdulwahid Sykes​
Mohamed Said hatuwezi kwenda mbele kwa kutumia side mirror. Hizi hekaya zako zitatusaidia endapo kama taifa nia yetu ni kurudi nyuma na si kwenda mbele.
 
Mohamed Said hatuwezi kwenda mbele kwa kutumia side mirror. Hizi hadithi zako zitatusaidia kama nia yetu kama taifa ni kurudi nyuma na sio kwenda mbele.
Unapo hitaji kwenda mbele lazima ungalie UMETOKA WP UPO WAPI UNAKWENDA WAPI.
Na unapo kuwa mtu mkamilifu lazima ujue historia ya familia yako na taifa lako.
Bila kujua haya ukamilifu wako utakuwa na mushkel/mashaka.
Ivi hujui watu wanakaa mashule na vyuoni kwa miaka kusoma haya unayo yaona ww yanaturudisha nyuma?
 
Mtebetini,
Nakuomba pia mtafute kaka Idd Churembo lazima atawajua
waliokuwa kwenye picha.

Mimi pia nikimfahamu Sheikh Bilal Mshoro na kitu kimoja Allah
alichomjaaliwa ni kuwa na watoto wenye akili nzuri sana darasani.

Alikuwapo mwanae mmoja Idara ya Uchumi Chuo Kikuu Mlimani
na yeye sasa ni marehemu.

Said Mahfoudh hata mimi namfahamu toka utoto wangu.

Yeye ni mpwa wa Mwalimu Adam aliyekuwa akisomesha Al Jamiatul
Islamiyya Muslim School.

Kwa hisani yako ukipata hizo taarifa tafadhali tuletee hapa Majlis na sisi
tufaidi.
Nadhani huyu Mjomba Said Mahfoudh anaishi keko nyumbani kwake ni karibu na Natonal Hotel zamani Chang'ombe Village.
 
Nadhani huyu Mjomba Said Mahfoudh anaishi keko nyumbani kwake ni karibu na Natonal Hotel zamani Chang'ombe Village.
Swadakat Mkuu Kambaresharubu.
Maalim MS ahsante kwa kutuunganisha na kikubwa tunapata historia halisa ya wazee wetu sasa kama watu wanaumia matumbo sidhani kama hiyo ndiyo nia yetu, nimeelezwa kwamba aliyepakatwa kwenye hiyo picha mkono wa kulia ni Dada Ghania Chaurembo pia kwenye hiyo picha wapo Kaka zetu Idd Chaurembo, Mohamed Chaurembo, Salum Chaurembo,Mzee Dossa Aziz, Mohamed Ngarawa,Shariff Badawi, Mzee Abbas Sykes na mjomba Said Mahfoudh. Kama alivyoeleza Maalim MS hii picha ilipigwa Mtoni kwa Sheikh Chaurembo
a80fe48301fc46e41b965cb694cddebf.jpg

Naendelea kupata maelezo na In Shaa Allah kila nitakachopata nitakileta hapa Barzani
 
1466631354457-jpg.359148


Mbetini,
Kwanza nakushukuru kwa kuileta picha hii hadharani.
Mimi ndiye mtu wa kwanza kuiona picha hii nje ya wenyewe.

Hii picha nilipewa na watoto wa Sheikh Abdallah Chaurembo
katika miaka ya 1980 na mimi nnilifanya mipango ipatikane nakala
yenye ubora na hilo lilifanyika.

Picha hii ilipigwa 1956 shambani kwa Sheikh Abdallah Chaurembo
Mtoni Dar es Salaam.

Ukoo wa Chaurembo una kawaida ya kufanya hawli kila mwaka na hii
inaendelea hadi leo

Katika hawali ya mwaka ule Mwalimu Nyerere alialikwa.
Pamoja na Nyerere kuna watu wengi maarufu katika picha hiyo.

Nyerere amekaa katika ya Liwali Ahmed Saleh kushoto na Sheikh
Bilal Mshoro
kulia.

Yupo Rajab Diwani, Liwali Ahmed Saleh, Sheikh Bilal Mshoro
kutoka Tabora, Sheikh Ramadhani Abbas, Saleh Muhsin huyu alikuwa
TANU kisha akatoka pamoja na Zuberi Mtemvu kuunda Tanganyika
African Congress (ANC) mwaka wa 1958 kufuatia Uchaguzi wa Kura Tatu,
katika watoto waliokaa chini yuko Said Mahfoudh mmoja wa vijana wa
kwanza kuingia Chuo Kikuucha Dar es Salaam katika miaka ya awali ya
1960.

Hii picha ilipotea kwa miaka zaid ya 20 hata wenyewe akina Chaurembo
wakawa hawana nakala ya picha hii.

Nimefurahi kuiona tena hii picha.
Alhamdulilah.

Nimeiweka picha hii katika blog yangu:
Mohamed Said: KUTOKA JF: HAKUNA PICHA INAYOELEZA HISTORIA YA WAISLAM NA MWALIMU NYERERE KAMA HII

Sheikh Mohamed Said akhsante Kwa darsa Inshaalah MwenyeeziMungu akuzidishie afya Na kila la kheri Kwa sadaka yako Kwa umma.
Je Saidi Mahfudhi anashughulika Na nini?
Shukran jazeelah
 
Duh Mtebetini Hii dunia ndogo.Angalia darsa inavyo kutanisha watu.
Waswahili husema Mwenyezi Mungu anashani yake, wee ukiwa na yako Mwenyezi Mungu amepanga yake huwezi kupangua mi nimejikuta naunganishwa na watu wala sikutegemea kugongana nao humu kwa ID zetu za kujibanza usijulikane,kasoro Maalim Mohamed Said yeye ni verified user.
Naomba turudi tafadhali kwenye mada tusimuharibie uzi wake na tukamkosea adabu Maalim MS
 
Sheikh Mohamed Said akhsante Kwa darsa Inshaalah MwenyeeziMungu akuzidishie afya Na kila la kheri Kwa sadaka yako Kwa umma.
Je Saidi Mahfudhi anashughulika Na nini?
Shukran jazeelah
Mgogoone,
Amin kwa sote.

Juzi nimemuona Said Mahfoudh kwenye mazishi ya Abdulrahman Lukongo
Sijui anafanya nini kwa sasa.
 
Back
Top Bottom