Handeni: Walimu wanaoga vichakani kwa kukosa bafu

Handeni: Walimu wanaoga vichakani kwa kukosa bafu

peno hasegawa

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2016
Posts
14,255
Reaction score
23,949
Walimu wanaofundisha Shule ya Msingi Gole iliyopo Kata ya Kang’ata wilayani Handeni mkoani Tanga, wameiomba Serikali kuwasaidia ujenzi wa vyoo vya walimu kwa kuwa wanajisaidia na kuoga kwenye vichaka kwa kukosa vyoo bora.

Wakizungumza shuleni hapo juzi walisema kuna muda inabidi waingie kujisaidia kwenye vyoo vya wanafunzi kwa sababu choo wanachotumia kwa majira ya mchana hawawezi kuingia kwani hakina mlango rahisi mtu akipita kumuona aliye ndani.

Mwalimu Mkuu swa shule hiyo, Said Mbelwa alisema licha ya ukosefu wa bafu na vyoo vya walimu, pia kuna walimu wanne wanaoishi kwenye nyumba moja jambo linalowanyima faragha na familia zao.

Mwalimu Jackson Mwakalukwa alisema athari nyingine ambayo ipo kutokana na adha hiyo ni kukosa mwalimu wa kike kwenye shule yao,hivyo imekuwa ni changamoto kwa wanafunzi wa kike kukosa mtu wa kumueleza matatizo yao hasa yanayohusu nasuala ya kike.

Naye Ofisa Elimu Msingi wilayani hapo, Goodluck Mwampashe alikiri kuwepo changamoto ya vyoo vya walimu kwenye shule hiyo na kueleza kuwa mpango wa kujenga upo ila kwa kutumia mfuko wa wafadhili.

Akiwa katika kijiji hicho, kwenye mkutano wa hadhara Mkuu wa Wilaya ya Handeni Siriel Mchembe, aliendesha harambee kijijini hapo ili kupata vifaa vya kuanzia ujenzi.
 

Attachments

Walimu wanaofundisha Shule ya Msingi Gole iliyopo Kata ya Kang’ata wilayani Handeni mkoani Tanga, wameiomba Serikali kuwasaidia ujenzi wa vyoo vya walimu kwa kuwa wanajisaidia na kuoga kwenye vichaka kwa kukosa vyoo bora.

Wakizungumza shuleni hapo juzi walisema kuna muda inabidi waingie kujisaidia kwenye vyoo vya wanafunzi kwa sababu choo wanachotumia kwa majira ya mchana hawawezi kuingia kwani hakina mlango rahisi mtu akipita kumuona aliye ndani.

Mwalimu Mkuu swa shule hiyo, Said Mbelwa alisema licha ya ukosefu wa bafu na vyoo vya walimu, pia kuna walimu wanne wanaoishi kwenye nyumba moja jambo linalowanyima faragha na familia zao.

Mwalimu Jackson Mwakalukwa alisema athari nyingine ambayo ipo kutokana na adha hiyo ni kukosa mwalimu wa kike kwenye shule yao,hivyo imekuwa ni changamoto kwa wanafunzi wa kike kukosa mtu wa kumueleza matatizo yao hasa yanayohusu nasuala ya kike.

Naye Ofisa Elimu Msingi wilayani hapo, Goodluck Mwampashe alikiri kuwepo changamoto ya vyoo vya walimu kwenye shule hiyo na kueleza kuwa mpango wa kujenga upo ila kwa kutumia mfuko wa wafadhili.

Akiwa katika kijiji hicho, kwenye mkutano wa hadhara Mkuu wa Wilaya ya Handeni Siriel Mchembe, aliendesha harambee kijijini hapo ili kupata vifaa vya kuanzia ujenzi.
 

Attachments

Yaani, bafu ya kuogea inawapigisha yowe walimu? Hivi wameshindwa kukata hiyo miti ya hivyo vichaka wakajenga ua(bafu-maliwato), wakakata majani wakayatandaza chini, wakaoga, kama wapo New York? Eti choo walimu hakina mlango, huku ni kuitia aibu taaluma ya ualimu? Hiyo shule haina mwalimu wa stadi za kazi, au haiba?

Kufaragua kimlango cha majani mkajisitiri kwa raha zenu, kumewashinda? Sasa watoto wetu mnawafundisha nini? Eti mna changia choo na wanafunzi kisa choo chenu hakina mlango! Ndiyo maana mkuu wa wilaya wa Bukoba mjini, mheshimiwa Mnari, enzi za utawala wa mzee wa Msoga, aliwachapa kisawasawa.

Nasaha zangu kwa TAMISEMI(ofisi ya Rais); rudisheni EK (elimu ya kujitegemea) mashuleni, kuepuka hizi fedheha kwenye vyombo vya habari na mitandao ya kijamii na taifa letu kwa ujumla katika viunga vya kimataifa.
 
Choo na bafu wangejenga TU wenyewe, mambo mengine sio lazima serikali serikali nakat mshahara wanao, nguvu wanazo!!

Kwamba wamekosa hata namna ya kujichangisha hela kuweka mlango wanaona Bora waende machakani na kushare vyoo na watoto was shule??!

Huu Ni uvivu wa kufikir na ubahili wa kupindukia!!
 
Choo na bafu wangejenga TU wenyewe, mambo mengine sio lazima serikali serikali nakat mshahara wanao, nguvu wanazo!!

Kwamba wamekosa hata namna ya kujichangisha hela kuweka mlango wanaona Bora waende machakani na kushare vyoo na watoto was shule??!

Huu Ni uvivu wa kufikir na ubahili wa kupindukia!!
Hapo ndo mnakosea. Je kodi zinazolipwa kwa ajili ya kujenga hizo bafu zinaenda wapi? V8 moja tu ya wilaya inajenga vyoo vyote vya iyo wilaya. Ndo maana hatuendelei.
 
Hapo ndo mnakosea. Je kodi zinazolipwa kwa ajili ya kujenga hizo bafu zinaenda wapi? V8 moja tu ya wilaya inajenga vyoo vyote vya iyo wilaya. Ndo maana hatuendelei.
Serikali ya nchi yako Ni bichwa la mwendawazimu!

Mambo mengine Ni kufunika kombe mwanaharamu apite!.

Ni Jambo la kushangaza Sana, kwa watu wenye family zao kujisaidia na kuoga vichakani kwa sababu wanasubir serikali iliyojaa ufisadi, na wizi wa Mali za Umma ije iwajengee bafu na choo!
 
Yaani, bafu ya kuogea inawapigisha yowe walimu? Hivi wameshindwa kukata hiyo miti ya hivyo vichaka wakajenga ua(bafu-maliwato), wakakata majani wakayatandaza chini, wakaoga, kama wapo New York? Eti choo walimu hakina mlango, huku ni kuitia aibu taaluma ya ualimu? Hiyo shule haina mwalimu wa stadi za kazi, au haiba?

Kufaragua kimlango cha majani mkajisitiri kwa raha zenu, kumewashinda? Sasa watoto wetu mnawafundisha nini? Eti mna changia choo na wanafunzi kisa choo chenu hakina mlango! Ndiyo maana mkuu wa wilaya wa Bukoba mjini, mheshimiwa Mnari, enzi za utawala wa mzee wa Msoga, aliwachapa kisawasawa.

Nasaha zangu kwa TAMISEMI(ofisi ya Rais); rudisheni EK (elimu ya kujitegemea) mashuleni, kuepuka hizi fedheha kwenye vyombo vya habari na mitandao ya kijamii na taifa letu kwa ujumla katika viunga vya kimataifa.
Mkuu hayo yalifanyika kipindi kile ualimu ulipokuwa wito. Sasahivi ualimu si wito tena ni kuganga njaa na kutafuta tonge baada ya kukosa kwa kuelekea kupata tonge.

Mimi binafsi naungana na hawa waalimu kwa kuelezea hii changamoto kwakuwa haya ni matokeo ya mfumo ambao watawala wenyewe wanaujenga. Mfumo usio na mlinganyo ki utu na kimaslahi, kuna watu kwenye mfumo wanamasilahi mpaka yana mwagika wakati wengine kama waalimu maslahi yao ni duni hata kukosa huduma tu za msingi za kibinadamu, kama hivi.

Kujenga choo cha shule kwa ajili ya waalimu si kitu kigumu kwa waalimu kumi lakini kuna kitu kinakosekana kuwafanya wafanye hivyo nacho ni uzalendo. Uzalendo huu haupotei tu bali husababishwa na mfumo usio na mlinganyo hata waweze kuona kwanini wahangaike na jambo ambalo wenye mamlaka hawako tayari kuhangaikanalo na ukizingatia wao wapo sehemu inayojumuisha wakandamizwaji.

Mtoto umleavyo ndivyo akuavyo na hizi ni daily tu kuwa sasa kila mtu afanye yake, afanye yanayo muhusu na ampende anaependeka, hakuna sababu ya kujitoa kwa mfumo usio na mlinganyo na usio jali wengine bali matumbo yao na familia zao wao waliokwenye nafasi zao.
 
Hapo ndo mnakosea. Je kodi zinazolipwa kwa ajili ya kujenga hizo bafu zinaenda wapi? V8 moja tu ya wilaya inajenga vyoo vyote vya iyo wilaya. Ndo maana hatuendelei.

Ndo maana siupendi ujamaa, unahimiza uvivu hata wa kufikiri jambo la kawaida tu na kulitolea maamuzi.

Hapo unawaza V8 iuzwe ili lijengwe bafu. Akili za kijamaa kabisa yaani, uvivu tu kutaka serikali ifanye ila mwanachi akae tu sababu yeye ni mnyonge na masikini.

Kwann hujawaza wajiunge waanzishe mradi wa kijiji wa "tokomeza magonjwa jenga choo na bafu" kisha wakawasiliana na viongozi wapate sapoti?

Wakirusha tu kwenye social media wanachofanya wangepata attention ya mbunge, mkuu wa wilaya, mkoa na ingevuka hata mipaka na wangepata sapoti.
 
Naona vyoo na maji sio muhimu kwa nchi zetu

Yaani bora wanunua madege yenye hasara lakini mwalimu na wanafunzi kujisaidia porini kama wanyama karne hii ya 21 ni sawa tu kwa serikali
 
Cha ajabu nini? Mimi mwenyewe nilioga sana tu vichakani kwenye shule moja iliyoko Moshi vijijini, kata ya Arusha Chini, sikuwa mwalimu muoga kwa viongozi wa elimu na halmashauri kwa nilichoona si cha kawaida nilipiga kelele mpaka nikaona utekelezaji ukifanywa ikiwemo nyumba za kisasa za walimu na madarasa bora kwa wanafunzi.
 
Yaani, bafu ya kuogea inawapigisha yowe walimu? Hivi wameshindwa kukata hiyo miti ya hivyo vichaka wakajenga ua(bafu-maliwato), wakakata majani wakayatandaza chini, wakaoga, kama wapo New York? Eti choo walimu hakina mlango, huku ni kuitia aibu taaluma ya ualimu? Hiyo shule haina mwalimu wa stadi za kazi, au haiba?

Kufaragua kimlango cha majani mkajisitiri kwa raha zenu, kumewashinda? Sasa watoto wetu mnawafundisha nini? Eti mna changia choo na wanafunzi kisa choo chenu hakina mlango! Ndiyo maana mkuu wa wilaya wa Bukoba mjini, mheshimiwa Mnari, enzi za utawala wa mzee wa Msoga, aliwachapa kisawasawa.

Nasaha zangu kwa TAMISEMI(ofisi ya Rais); rudisheni EK (elimu ya kujitegemea) mashuleni, kuepuka hizi fedheha kwenye vyombo vya habari na mitandao ya kijamii na taifa letu kwa ujumla katika viunga vya kimataifa.
Ma bwege Sana hawa walimu wa sasa
 
Mkuu kama kweli wewe ni Mwalimu na ulishindwa hata kujijengea mwenyewe kibafu hata cha miti na kuweka mawe kwenye sakafu na hapa unajisifia.......inasikitisha
Cha ajabu nini? Mimi mwenyewe nilioga sana tu vichakani kwenye shule moja iliyoko Moshi vijijini, kata ya Arusha Chini, sikuwa mwalimu muoga kwa viongozi wa elimu na halmashauri kwa nilichoona si cha kawaida nilipiga kelele mpaka nikaona utekelezaji ukifanywa ikiwemo nyumba za kisasa za walimu na madarasa bora kwa wana
 
Back
Top Bottom