'Hangover' ya propaganda za utawala wa Magufuli zitadumu kwa baadhi ya watu milele

'Hangover' ya propaganda za utawala wa Magufuli zitadumu kwa baadhi ya watu milele

Hii paragraph ya 5 ndio imefanya niwe na shaka KUBWA na Wewe kusema tunadhani SERKALI NA MAFISADI wanatuibia? Aisee kwahiyo ESCROW kwako ni halali, MELEMETA ni Safi kwako, upigaji bandari hadi gauge ya kupima mafuta kuchezewa ni SAWA kabisa, .
Wewe ni nani?
Hizlo zote unazoongea zilikuwa uongo was Magufuli alifanya maigizo ili wajinga wamsifu eti amegundua wizi bandarini , kweli wajinga ndo waliwao
 
Alianzisha miradi hiyo kibwege kwa kukurupuka bila utaalamu wa project management matokeo yake mpaka anakufa hakuna hata mmoja uliofika 40% mpaka anakufa. Ni ubwege pia kumsifia kwa kuanzisha mradi halafu haujamalizika

Angekuwa na akili nzuri angejikita na mradi mmoja kwanza say SGR pengine leo ingekuwa imemalizika na inaingiza fedha
Alikuwa mshamba sana au pengine mweupo kwenye nadharia na falsafa za maendeleo. Alifikiri maendeleo ni majengo, barabara, madaraja na vitu vingine vinavyoonekana; yaani maendeleo ya vitu. Upeo wake kiuongozi ulikuwa mdogo sana, hakustahili kuwa kiongozi wa nchi hii; ndiyo maana hatimaye ilibidi kutokea yaliyotokea.
 
No doubt Magufuli alimaster sana the art of propaganda. Alizishika media zote, hadi za nje kuna wakati ikatangazwa kwamba hazipaswi kurusha maudhui ya ndani bila kibali.

Media zote nchi, binafsi na zile za serikali hadi zile ambazo ziko tu online ambazo hazina usajili wa serikali zilijaa woga kumtaja Magufuli katika namna ambayo isingempendeza. Media nchini ziliimba mapambio ya kumsifu na kumtukuza mawizo mpaka machweo.

Propaganda za Magufuli zinanikumbusha propaganda za Adolf Hilter, Joseph Stalin na Mao Ze Dong. Hawa watu walikuwa na uwezo mkubwa sana wa kuaminisha mambo ambayo hayapo, walikuwa na uwezo wa kupandikiza nadharia zao na imani zao juu ya kadamnasi na ikaamini vivyo, huku nyuma ya pazia wakiwa na mauzauza yao kibao.

Magufuli alitupiga wapi? Kwanza alijifanya Rais wa wanyonge, akijua kwamba watanzania wengi over 40% tuko chini ya mstari wa umasikini wa $1 kwa siku, masikini wengi tulimpenda sana tukidhani ni mwenzetu lakini katu, hakuwa mwenzetu, JPM alikuwa tajiri sana.

Magufuli alijua kwamba watanzania hatupendi mafisadi, wengi tunadhani umasikini wetu kuna watu wanatuibia serikalini. JPM akaona atangaze nao vita kali, tukamsahau yeye ambaye alijilimbikizia mali nyingi sana, huku tukijua kwamba anapambana na mafisadi kwa ajili yetu, kumbe ni kwa ajili yake kwani kila alipotaifisha mali zao, zikawa zake na jamaa zake.

JPM master the art of public manipulation. Kwenye ziara zake alisimama barabarani, alizungumza na watu, akatoa fedha hadharani kwa watu wa hali ya chini, alitembelea hospitali na kutoa misaada hadharani kwa watu waliokuwa na hali ngumu huku kila media ikimulika. Vitendo vile vimewalevya wengi kudhani kwamba JPM was saviour, tukasahau kabisa na yeye ni mwanadamu mwenye tamaa na uchu, aliweza kufanya chochote pasi nasi kujua kuwa mali zetu zinaibwa na kuwekezwa kwenye hotels zake, real estate, mashamba na kuficha fedha nje ya nchi. Mtoto wa dada yake, aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya fedha Dotto James alifanya kazi kubwa sana kusafirisha fedha za mjomba wake nje.

Naona leo wakimkumbuka sana. Nasikitika sana kuona wengi wakimkumbuka JPM pasi na wao kujua kwamba bado wamo kwenye dimbwi la mning'inio wa propaganda za JMP. Ila kama tungejua uozo na madudu aliyofanya nyuma ya pazi, pengine tungezinduka kutoka kwenye hangover hiyo. Tuishie hapo.
Mimi ningependekeza itungwe sheria kali ya kuhakiki mali za viongozi wakuu wa serikali wanapoingia, na wanapotoka uongozini. Kuwe na mfumo ambao ni fool proof, na wale watakaobainika kuiba mali ya umma wapate adhabu kali hata kifungo miaka mingi gerezani.
Leo mkuu wa nchi anatamka kuna pesa za umma ziliibwa na kuhifadhiwa China, lakini si ajabu suala hili litapotezewa hivi hivi. Ni aibu kwetu kama taifa.
 
Mimi ningependekeza itungwe sheria kali ya kuhakiki mali za viongozi wakuu wa serikali wanapoingia, na wanapotoka uongozini. Kuwe na mfumo ambao ni fool proof, na wale watakaobainika kuiba mali ya umma wapate adhabu kali hata kifungo miaka mingi gerezani.
Leo mkuu wa nchi anatamka kuna pesa za umma ziliibwa na kuhifadhiwa China, lakini si ajabu suala hili litapotezewa hivi hivi. Ni aibu kwetu kama taifa.
Hivi haiwezekani rais Samia alazimishwe kuweka hadharani taarifa ya ule ukaguzi alioagiza ufanywe b.o.t wa transactions za January to march 2021
 
Jibu liko wazi kwa sababu mnamchukia, we fikiria hivyo vifo vya kuokota maiti za kwenye viroba ni kipi kilichofanya hadi hivyo vifo vihusishwe na Magufuli? Utagundua ni chuki tu ndio hufanya mumpa hiyo tuhuma.

Kuna wengine wanakwambia alikufa kwa corona ila hana sababu yeyote ya msingi ya kushawishi kuwa kweli alikufa kwa corona na ajabu unakuta mtu anaamini hivyo na humwambii kitu, unagundua hii ni athari ya chuki yani mtu anaona kusema Magufuli kufa na corona ni jambo la kumdharirisha ni kama adhabu.
Tangu afariki sijawahi kusikia mtu katekwa, kauawa au maiti imeokotwa ikiwa ndani ya kiroba.
 
Tangu afariki sijawahi kusikia mtu katekwa, kauawa au maiti imeokotwa ikiwa ndani ya kiroba.
Kwahiyo una maana ya kwamba uhalifu wa watu kutekwa umekuja kipindi chake tu kwamba huko nyuma hakukuwa na uhalifu wa watu kutekwa Tanzania? Kwamba Tanzania hakuna uhalifu wa watu kuuliwa?

Kama ni hivyo basi Tanzania ilihitaji kupongezwa maana ni jambo kubwa kuweza kudhibiti uhalifu wa aina hiyo kwa 100%.
 
No doubt Magufuli alimaster sana the art of propaganda. Alizishika media zote, hadi za nje kuna wakati ikatangazwa kwamba hazipaswi kurusha maudhui ya ndani bila kibali.

Media zote nchi, binafsi na zile za serikali hadi zile ambazo ziko tu online ambazo hazina usajili wa serikali zilijaa woga kumtaja Magufuli katika namna ambayo isingempendeza. Media nchini ziliimba mapambio ya kumsifu na kumtukuza mawizo mpaka machweo.

Propaganda za Magufuli zinanikumbusha propaganda za Adolf Hilter, Joseph Stalin na Mao Ze Dong. Hawa watu walikuwa na uwezo mkubwa sana wa kuaminisha mambo ambayo hayapo, walikuwa na uwezo wa kupandikiza nadharia zao na imani zao juu ya kadamnasi na ikaamini vivyo, huku nyuma ya pazia wakiwa na mauzauza yao kibao.

Magufuli alitupiga wapi? Kwanza alijifanya Rais wa wanyonge, akijua kwamba watanzania wengi over 40% tuko chini ya mstari wa umasikini wa $1 kwa siku, masikini wengi tulimpenda sana tukidhani ni mwenzetu lakini katu, hakuwa mwenzetu, JPM alikuwa tajiri sana.

Magufuli alijua kwamba watanzania hatupendi mafisadi, wengi tunadhani umasikini wetu kuna watu wanatuibia serikalini. JPM akaona atangaze nao vita kali, tukamsahau yeye ambaye alijilimbikizia mali nyingi sana, huku tukijua kwamba anapambana na mafisadi kwa ajili yetu, kumbe ni kwa ajili yake kwani kila alipotaifisha mali zao, zikawa zake na jamaa zake.

JPM master the art of public manipulation. Kwenye ziara zake alisimama barabarani, alizungumza na watu, akatoa fedha hadharani kwa watu wa hali ya chini, alitembelea hospitali na kutoa misaada hadharani kwa watu waliokuwa na hali ngumu huku kila media ikimulika. Vitendo vile vimewalevya wengi kudhani kwamba JPM was saviour, tukasahau kabisa na yeye ni mwanadamu mwenye tamaa na uchu, aliweza kufanya chochote pasi nasi kujua kuwa mali zetu zinaibwa na kuwekezwa kwenye hotels zake, real estate, mashamba na kuficha fedha nje ya nchi. Mtoto wa dada yake, aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya fedha Dotto James alifanya kazi kubwa sana kusafirisha fedha za mjomba wake nje.

Naona leo wakimkumbuka sana. Nasikitika sana kuona wengi wakimkumbuka JPM pasi na wao kujua kwamba bado wamo kwenye dimbwi la mning'inio wa propaganda za JMP. Ila kama tungejua uozo na madudu aliyofanya nyuma ya pazi, pengine tungezinduka kutoka kwenye hangover hiyo. Tuishie hapo.
Ukiona mtu anavunja Katiba iliyomweka madarakani,huyo siyo kiongozi bali ni mtawala,JPM aliishi kiutawala zaidi na uongo ili kuwapumbaza wasio na mawazo ya mbali katika kufikiri kwa vile eneo analotokea wajinga ni wengi sana.
 
Kwahiyo una maana ya kwamba uhalifu wa watu kutekwa umekuja kipindi chake tu kwamba huko nyuma hakukuwa na uhalifu wa watu kutekwa Tanzania? Kwamba Tanzania hakuna uhalifu wa watu kuuliwa?

Kama ni hivyo basi Tanzania ilihitaji kupongezwa maana ni jambo kubwa kuweza kudhibiti uhalifu wa aina hiyo kwa 100%.
Yah. Tunapaswa kumshukuru Mungu kwa tukio lile la march '21.
 
No doubt Magufuli alimaster sana the art of propaganda. Alizishika media zote, hadi za nje kuna wakati ikatangazwa kwamba hazipaswi kurusha maudhui ya ndani bila kibali.

Media zote nchi, binafsi na zile za serikali hadi zile ambazo ziko tu online ambazo hazina usajili wa serikali zilijaa woga kumtaja Magufuli katika namna ambayo isingempendeza. Media nchini ziliimba mapambio ya kumsifu na kumtukuza mawizo mpaka machweo.

Propaganda za Magufuli zinanikumbusha propaganda za Adolf Hilter, Joseph Stalin na Mao Ze Dong. Hawa watu walikuwa na uwezo mkubwa sana wa kuaminisha mambo ambayo hayapo, walikuwa na uwezo wa kupandikiza nadharia zao na imani zao juu ya kadamnasi na ikaamini vivyo, huku nyuma ya pazia wakiwa na mauzauza yao kibao.

Magufuli alitupiga wapi? Kwanza alijifanya Rais wa wanyonge, akijua kwamba watanzania wengi over 40% tuko chini ya mstari wa umasikini wa $1 kwa siku, masikini wengi tulimpenda sana tukidhani ni mwenzetu lakini katu, hakuwa mwenzetu, JPM alikuwa tajiri sana.

Magufuli alijua kwamba watanzania hatupendi mafisadi, wengi tunadhani umasikini wetu kuna watu wanatuibia serikalini. JPM akaona atangaze nao vita kali, tukamsahau yeye ambaye alijilimbikizia mali nyingi sana, huku tukijua kwamba anapambana na mafisadi kwa ajili yetu, kumbe ni kwa ajili yake kwani kila alipotaifisha mali zao, zikawa zake na jamaa zake.

JPM master the art of public manipulation. Kwenye ziara zake alisimama barabarani, alizungumza na watu, akatoa fedha hadharani kwa watu wa hali ya chini, alitembelea hospitali na kutoa misaada hadharani kwa watu waliokuwa na hali ngumu huku kila media ikimulika. Vitendo vile vimewalevya wengi kudhani kwamba JPM was saviour, tukasahau kabisa na yeye ni mwanadamu mwenye tamaa na uchu, aliweza kufanya chochote pasi nasi kujua kuwa mali zetu zinaibwa na kuwekezwa kwenye hotels zake, real estate, mashamba na kuficha fedha nje ya nchi. Mtoto wa dada yake, aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya fedha Dotto James alifanya kazi kubwa sana kusafirisha fedha za mjomba wake nje.

Naona leo wakimkumbuka sana. Nasikitika sana kuona wengi wakimkumbuka JPM pasi na wao kujua kwamba bado wamo kwenye dimbwi la mning'inio wa propaganda za JMP. Ila kama tungejua uozo na madudu aliyofanya nyuma ya pazi, pengine tungezinduka kutoka kwenye hangover hiyo. Tuishie hapo.
Ndio maana tunataka hao jamaa zake ambao wapo hai wapelekwe Mahakamani na pesa zirejeshwe maana tumeshajulishwa zimewekwa huko China. ! Bila kufanya hivyo hizi zote ni porojo kama za Abunuwas !! Watanzania sio mazuzu wa kudanganywa danganywa kama ulivyoeleza !! Watanzania wana akili timamu na wanajua mchele upi na pumba ni zipi !!
 
Yah. Tunapaswa kumshukuru Mungu kwa tukio lile la march '21.
Mwaka 2022 hadi huu 2023 kumekuwa na matukio ya ajabu ajabu watu wanauwana kikatili,kumekuwa na unyanyasadi na mabalaa mbalimbali mwanzo kabisa tulianza na panya road hali iliyotishia usalama wa watu na mali zao.

Hayo mabalaa na mitihani yote imetokea kipindi ambacho Magufuli ameshafariki hayupo.
 
Pumzika kwa Amani Kipenzi chetu! Mungu akusamehe makosa yako, na familia yako ipone kwa maumivu kama haya yanayosambaa kwa kasi Nchini.
 
Vile mwendakuzimu amefurahia uzi wako huu kutokea huko kuzimu😁😁😁
downloadfile-4(1).jpg
 
Back
Top Bottom