Hans Poppe: Hali ya kiuchumi Simba SC si nzuri

Shida ya viongozi wa Simba shule ndogo! Wanaongoza timu kizamaaaani mpaka wanapokwama ndo wanagundua tatizo! Fukuza wote!
 


viongozi wana michongo ya jezi alafu wauze kama simba wapi na wapi mpwa

tatizo wengi waligombania wakijua wanarudisha hela zao na kuweka vitega uchumi sasa azam tv kawamaliza we utaona kama hanshope atagombania ,,sasahvi anatamani uongozi muda uishe kesho alah
 
Mkuu vuta subira, soon mkwanja utatua.

Mkuu,hizo zikitua ni balaa badala ya neema. Kazi itakuwa kulipa madeni halali na fake humohumo. Wapigaji hawatacheza mbali.
Usije shangaa watu wanatoana macho
 
simba walikataa mkataba mkubwa sana toka zuku kwa sababu ya aden rage tamaa zake kwa kweli ni aibu timu kama simba ikalipwa sawa na singida kitu kingine wadai uwiano wa mechi uwe sawa kwani mechi nyingi zinazoonywesha ni za simba na yanga lakini mapato sawa halafu mauzo ya jezi hayaeleweki yanaenda wapi cha ajabu mbeya city wameweza kudhibiti mauzo ya jezi zao wakati simba wanahangaika
 
Wamlipe kwanza Tambwe ndipo wakajifie huko!

Sasa nimeamini ile habari iliyoletwaga humu kuwa mikia wanapiga mechi za mchangani huko Shinyanga sijui Mwanza kutafuta hela ya kulipia kambi. Mikia walikuja juu wakidai ni uzushi kumbe timu iko hoi bin taabani
 

Mkuu hebu nielimishe zaidi hapo kwa red, Yanga wao wananufaika vipi na azam TV? manake si mechi zao wanaonyesha?
 

Kuhusi mbeya city kidhibiti mapato ya jezi sikubaliani na ww...kuna mtu namfaham anaprint jezi feki za timu zote ikiwemo mbeya city na anauza kama kawa na pesa anakunja
 
Mkuu hebu nielimishe zaidi hapo kwa red, Yanga wao wananufaika vipi na azam TV? manake si mechi zao wanaonyesha?
Rudia tena kusoma utamwelewa.
 

Tuwasamehe bure msimu ujao watakuwa pamoja na yanga kusaini milioni mia 9....vinginevyo azam waoneshe mechi za costi na african sports
 

Hao wachache wanaoenda uwanjani ndio wanamoyo w2akwenda kuisapoti timu,yani hata mechi zisingekuwa zinaonyeshwa luningani watu wasingeenda uwanjani kwa pafomansi mbovu waliyonayo
 
Halafu nimeona kwenye maelezo yake kwa "simba na yanga wanaathirika," angeisema timu yake ...yanga hatujaathirika ndo mana hatudaiwi mshahara na wala hatujacheza ndondo kusaka pesa za mshahara,aizungumzie litim lake
 
Mkuu hebu nielimishe zaidi hapo kwa red, Yanga wao wananufaika vipi na azam TV? manake si mechi zao wanaonyesha?

Tangu Azam TV waanze kuonesha mechi za ligi kuu, Yanga haijawahi kuchukua hata senti 1 ya udhamini huo. Mechi za Yanga zimeendelea kuoneshwa bure. Ni heri mechi zioneshwe bure kuliko udhamini feki wa 100m/=, huo ndio msimamo wa Yanga.

Ni furaha iliyoje Simba kuanza kulia njaa! Naamini mwakani wataungana na Yanga kuibana TFF ili udhamini wa Azam TV uboreshwe.
 
Mkuu vuta subira, soon mkwanja utatua.

Seembo...unakumbuka kipindi kile unaongelea habar ya pesa za Etoel ukaanza na kuota ndoto za alnacha kuhusu uwanja wa bunju..pole bana hizo ndo timu zetu..zina wenyewe sio mm wala ww...kuna taarifa nusu ya fedha iliishapigwa zamaaan na viongozi waliopita
 

Aisee nilikuwa silijui hili, asante kwa ufafanuzi mkuu Makoye Matale
 
Last edited by a moderator:
Kiukweli inauma sanaaa yanga na simba kuwa taabani kimapato timu zina zaidi ya nusu Karne mipango mi bovu kila siku kulia njaa
.Kungekuwa na mipango thabithi hata ya kuwashawishi wapenzi wa vilabu hivi pendwa walau kununua gazeti la yanga imara au ngurumo za simba wasingekuwa hapo wapenzi wanaambiwa hununui khabari tu bali pia unakuwa umechangia klabu sidhani kama wangekwama ila wapenzi wanaona viongozi wapigaji.
 
Na bado timu inapigwa faini kwa makosa ya kijinga kama kugomea kuingia kwenye vyumba huku si kupoteza vijisenti vinavyopatikana.
 

Mkuu nakumbuka walipokuja Etoile kucheza na Yanga, kuna mwandishi wa Gazeti la Mwananchi alimuuliza kiongozi wa Etoile, kuwa ni lini watawalipa Simba hela zao.. Kiongozi alijibu kua hivi sasa wana hali mbaya kiuchiumi ila watalipa tu.. Nadhani tuendelee kuvuta subira.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…