Hapa ndipo utatupenda sisi watu weusi


Hahah mkuu umelenga mulemule, huwa nashangaa sana wabongo wenzangu muda wote wanasema Tz ina rasilimali nyingi so ni tajiri so wageni wanaionea wivu! Utafikiri nchi zingine hazina hayo wanayoyasema, kwa ujumla rasilimali kubwa zaidi ya kibinadamu ni akili ya kutawala mazingira yake na kufanya hayo mawe, madhahabu, magesi, mafuta, maji, mamichanga, nk, na kuwa uwezo wa kuyabadilisha yawe pesa, mali, madawa, barabara, maflyover, mahuduma bora ya jamii, nk nk. Hii ndio rasilimali muhimu ambayo watu weusi tumenyimwa.

Kwa sasa kila mtu mweusi anajua maisha yake yatabadilika kwa miujiza, yani atakesha kwa maombi kwenye makanisa ya wanaojiita manabii na mitume, na wengine kwa sangomaz kulishwa uchafu wakijua nyota intang'aa baada ya hapo na pesa zitatiririka kama bomba na kukubalika. Tumepotezwa njia na tukapotea kweli, kizazi hiki kinachoshindania dini za wazungu na waarabu kama mpira wa Simba na Yanga kinatakiwa kupita kwanza then kinachokuja na kingine kinaweza kupata akili ya kujua namna gani transformation zinafanyika. Baada ya wazazi na watoto wa kiafrika kuacha kushindana kusomesha watoto kupata nafasi ya kwanza kwa kukariri na kuachia ufahamu wao utawale mawazo yao na kufanya uumbaji kwa fikra zao bado tutabaki kukopa kila siku tujenge vituo vya afya. Tunapomaliza kulipa hakuna kituo kinakuwa bado kipo tunakopa tena kukirepair tena hadi kizazi hiki kifutike!

Peter Botha aliwahi kutoa kijimessage kwamba South Africa haijajangwa kwa wishful thinking (ambayo ndo weusi tunayo) wakati makaburu wanatawala, baadaye wamechukua weusi ukitazama SA imerudi kuwa km nchi zingine za waafrika, vilivyofanywa na makaburu ndo kimebaki, weusi tunajua kula na kuzaana! Sorry km nimemkwaza mtu yeyote.
 

Great philosophers km kina Gallileo na wengine kina Newton hawakutaka historia ili wafanye mapinduzi waliyofanya. Walitumia mazingira na wanachoona in real time kubadilisha maisha yao na hatimaye wakabadilisha maisha ya binadamu wote! Historia ikufundishe kukwepa wanaoua ndoto zako tu sio kukariri na kufikiri kuna miujiza ukisema una uhusiano na wayahudi! Ni kujilisha upepo tu
 
Tena hapa ndio huwa wananifikirisha Sana nikiangalia picha za misafara ya watumwa,yaani Babu zetu mashababi kabisa Kama thelathini wamekamatwa na waarabu wawil legelege,Sasa najiuliza hivi walikuwa sawa kweli?
Hujawahi kuona jamaa mdogo mdogo hata mwili hana ila mibaba mikubwa kumi inamtii? Akili ikishakubali kwamba mimi ni inferior inaleta effect mpaka kwenye mwili ndivyo ilivyo ni ishu ya psychology tu
 
Alfu huyu kijana umughaka analeta Uzi za kusadikika😂
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…