Happy birthday Mtume na nabii wa mwisho wa Soka Saint Gaucho

Happy birthday Mtume na nabii wa mwisho wa Soka Saint Gaucho

Gang Chomba

JF-Expert Member
Joined
Feb 29, 2008
Posts
20,649
Reaction score
4,786
ronaldinho-ronaldinho-178428_1024_768.jpg

Mnamo tarehe 21 ya mwezi wa 3 mwaka 1980 hukoo Porto Alegre nchini Brazil, alizaliwa mtume na nabii wa mwisho wa Soka.

Ujio wake ulitarajiwa, kwani ishara nyingi zilishajionesha kuwa mbarikiwa atakaekuja kutambulisha skills zinazopatikana katika ligi haswa ya Mbinguni yu karibu kuzaliwa.

Kuzaliwa na kukua kwake kulikuwa ni kwa kibinaadamu zaidi na alisoma na kupata malezi kama watoto wengine mpaka alipotimiza miaka 13 ndipo matendo ya kinabii yakaanza onekana.

Akiwa na umri huo Dinho aliisaidia timu yake ya mtaa kupata ushindi wa goli 23-0 magoli ambayo yote aliyatupia yeye.

Huyu ndie Ronaldo de Assis Moreirra almaarufu kama Ronaldinho Gaucho the saint ambae akiwa uwanjani basi Malaika huacha shughuli zao na kuanza kumtazama.
 
Hakudumu sana na PSG kwani Barca walikuwa ktk mipango ya kuijenga timu yao. Pesa wanayo, uwanja wanao, ila kuna kitu wakawa wamekosa. Na hapa sasa ndipo ikawalazimu wamchukue mtu ataekuja kufanikisha kuiunda na kuipa mafanikio na ndipo msemo "DINHO MADE BARCA AND BARCA MADE MESSI" unapothibitika.
hatimae Dinho akatua Nou Camp na kuanza ujenzi wa timu.
 
Acha kufananisha vijana wa vijiweni na vyeo vya heshima kama hivyo. Kama wewe huna dini usitake kugusa imani za wenzako kwa mizaha kama hii.

Lugha ziko nyingi za kuwasilisha unachokiamini ni kizuri lakini sio kwa staili hii.
 
Barca ikawa timu ya ushindani badala ya ushiriki.

Barca ikaanza kupata ushindi mfululizo ktk mashindano yote, barca ikaanza kujaza uwanja kwani habari za miujiza ya soka anayofanya Saint Gaucho zilitapakaa ulimwenguni kote
 
Barca wakaanza kupata vikombe na makombe. Barca wakafanikiwa hata kupata ushindi nyumbani kwa hasimu wao Real Madrid, na moja kati ya mechi ya kukumbukwa ni ile ambayo Dinho alitupia kamba mbili na kupelekea washabiki nguli wa los blancos kuinuka kwenye viti vyao na kuanza kumpigia makofi. Kitendo hiki cha kishujaa kiliwahi kumtokea pia Diego Maradona baada ya kuwashikisha adabu Madrid hapo Bernabeu.

No one else
 
THE SAGGA CONTINUA...

Mnamo mwaka 2008 Dinho alielekea nchini Italy ili kwenda kukamilisha kazi aliopewa.

Dinho alitua ktk uwanja wa ndege mkubwa na wakisasa zaidi uliopo ktk mkoa wa Milan.

Dinho alilakiwa na maelfu ya washabiki wa chama la Milan chama lenye makombe mengi ya kimataifa kuliko klabu yoyote pale Ulaya, chama ambalo limechezewa na nyota wengi wa soka ulimwenguni, chama ambalo ili mchezaji akamilike basi ni lazima atue pale.
 
Hahahahahah..

Hongera dihno kwa kutimiza 35,

Lakini Duniani hapa kuna jamaa anaitwa MESSI jina uliloliacha pale barca lakini uwezo wake huu hukuuacha pale... Anaujua mpira, mpira unamjua na baya zaidi unampenda,, ana rekodi za kujaza mtungi wa bibi.
 
Huyu Messi sio wa dunia hii basi maana anachofanya huko Ulaya
 
Hahahahahah.. Hongera dihno kwa kutimiza 35, Lakini Duniani hapa kuna jamaa anaitwa MESSI jina uliloliacha pale barca lakini uwezo wake huu hukuuacha pale... Anaujua mpira, mpira unamjua na baya zaidi unampenda,, ana rekodi za kujaza mtungi wa bibi.


Hah hah hah hivi unajuwa kuwa kuna tofauti kubwa kati ya busha na shipa?

Ok may me nianze na kukutoa tongotongo, ishu ni kuwa huyo Nesi ktk ufungaji magoli pale Barca goli lake la kwanza kufunga alipewa pasi na huyu Nabii wa mwisho. na kama hio haitoshi Nesi anakiri ya kuwa hata kama angefumba macho siku ile basi angeweza kufunga tu, na ukikazia kuwa mpira unamjuwa Nesi na kumpenda basi unakuwa unachuma dhambi.
saint Gaucho hata ukimpigia shuti la dochi basi mwilini mwake mpira utaganda tu na utatulia.

Inaaminika pia kuwa kama mpira ungalikuwa na mdomo ungeomba kila dakika upelekwe kwa Dinho Magic ili akauchezee na kufurahi.

Kajipange tena kisha urudi.
 
Gaucho mchumba kwa Zidane, hata wabrazili wenyewe wanakiri. Ni taarifa tu


Taarifa zipo nyingi.

1. Taarifa za wapenzi kunasiana pale ktk hospital ya temeke...
2. Taarifa za mganga anaesafirisha wabeba madawa ya kulevya bila kuonekana airport...
3. Taarifa za mashambulizi ya panya road...

Ila yoote ni 9, kumi huo wako ni mtazamo tu kama jina lako.

Karibu tena
 
Huyo Ronaldinho wako hajafunga kama Messi
Hajachukua tuzo kama Messi
Hajaassist kama Messi
Hajavunja rekodi kama Messi
Hajaweka rekodi kama Messi

Messi nuksi sana tena sana
Rekodi(VITENDO)zinaongea sana kuliko mbwembwe(MANENO)... MESSI NITAMKUMBUKA KAMA MCHEZAJI HATARI ZAIDI KTK ZAMA ZANGU, NITAMWADITHIA NA MWANANGU PENGINE ATAKUA MESSI WA PILI
 
Gang Chomba mzee wa Jukwaa la Mapishi, naona umekuja kwa staili ya kantangaze xo xo...
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom