Happy valentine's day

Happy valentine's day

Hivi sio ruksa kuwa na Valentine zaidi ya mmoja ????, kwa mapenzi tofauti ofcourse..

Mpenzi mmoja...mama...dada...kaka...baba....mjomba...shangazi...mtoto....rafiki inaruhusiwa!!!
Wapenzi wakizidi ndio mbaya!!!!:coffee:
 
Acha watu wachakachue, muhimu kila mmoja asijue kama anachakachuliwa, Kwani ukiwa na watoto watano ukienda kupima DNA utapewa majibu? lakini unaishi raha mustarehe na mama watoto wako. TRUST IN GOD REST STRICLY CASH:roll:
 
Mpenzi mmoja...mama...dada...kaka...baba....mjomba...shangazi...mtoto....rafiki inaruhusiwa!!!
Wapenzi wakizidi ndio mbaya!!!!:coffee:
Ofcourse mpenzi wa as a couple ni mmoja tu.., The First, The Last and The Only..., mimi nilikuwa ninamaanisha kwamba huenda kesho ukawa na kadi tofauti kwa dada, kaka, shangazi etc..., lakini the chocolate, the wines and flowers na kutoka hilo ni special kwa mmoja tu..
 
Ofcourse mpenzi wa as a couple ni mmoja tu.., The First, The Last and The Only..., mimi nilikuwa ninamaanisha kwamba huenda kesho ukawa na kadi tofauti kwa dada, kaka, shangazi etc..., lakini the chocolate, the wines and flowers na kutoka hilo ni special kwa mmoja tu..
Thats what I said...mpenzi mmoja na ndugu plus marafiki inaruhusiwa!Inakua hujachakachua kama KKK anavyosema!
 
Wale wapendanao kesho kuweni macho msome mwenza wako kwani kesho lazima upigwe changa usiruhusu dharura shinda naye vinginevyo kesho maua yatatolewa kwa watu zaidi ya mmoja!Wajanja ukiona umeletewa maua asubuhi nakuondoka hukuakisema anadharura jua imekula kwako!!Akileta jioniii wakati umesha kata tamaa ya ujio wake basi ujue kuna mahali kaanzia wewe kaja kuhitimisha!!Happy Valentine!!

KK umeharibu.......ur statement ungeitoa after valentine. Kesho kazi ipo...............
 
Hivi kumbe kesho valentine?
Dah! Ya mwaka huu patupu.....
 
Na wewe pia mungu akulinde usipewe changa la macho siku hii
 
Thanx na wewe pia, nakukaribisha MMu kwa ukarimu mkubwa
 
Ahsante RealMan naona watu wote humu jamvini hawana vituko vya valentines day. Leo nahisi sina la kujipanga wala nini am all alone with my kids naona nitakuwa bize sana humu jamvini.American chips hahahahahaaaaa sina hamu na kuna valentines day tulienda bagamoyo gari bila spare tire na tulichelewa pia kutoka huku home pacha ilitupata aje??? mpaka saa tano na nusu tunahangaikia swala la tairi kutoka hapo tuligeuza moja kwa moja home! nina memories nyingi sana nyingine nzuuuur nyingine mbayaaaa
 
sina proper valentine almost mwaka wa sita huu, since nimetoka bongo, coz of long distance, na wala sikumbuki kama nilishawahi kuwa na kituko cha valentine,my all past valentine went well and perfect.
ila kitu ninachokumbuka na sitaweza kukisahau, kabla sijaja abroad, enzi za u teeneger(mapenzi ya kuibia), my best sister yeye ndio alikuwa anakaa ulaya, kuna mwaka mmoja alirudi home siku ya valentine halafu mitaa ya jioni(muda wa outing za valentine) kwa mara ya kwanza nilihisi kwamba sijammiss, na wala sijajali kama nimeletewa zawadi,na wala sijaenda kumpokea airport,maana ningefanya hivyo basi valentine yangu ingeharibika.
kwahiyo ikabidi nidanganye naenda kwenye msiba.
 
Siku ya Valentines Day asili yake ni kutoka Dola ya Warumi. Ni siku ya kumbukumbu (memoria day) na sehemu nyingine ni (festum) maana yake siku kuu ya daraja la kwanza kwa kumkumbuka Padre Valentine aliyeuawa na utawala wa kirumi sababu ya kutetea waumini wake kufunga ndoa badala ya kuishi na vimada tu. Lakini sikukuu hiyo imeenea sana katika nchi za magharibi na baadaye karibu sehemu kubwa ya ulimwengu kuisherehekea kama siku yamapenzi kinyume cha dhamira ya Mt. Valentine.

Watawala wa dola ya kirumi walikuwa na fikra za kueneza dola ya kirumi duniani kote na hivyo vijana hawakutakiwa kuoa, ili wawe huru muda wote kwenda vitani kupigania nchi. Wakioa hawangekuwa na uhuru wa kwenda vitani bali kuwa na famiia zao. Vijana wengi wakawa na mtindo wa kuwa na vimada tu kitu ambacho kanisa lilikukwa linapinga.

Padre Valentine ambaye alikuwa Roma akawa anawahimiza vijana kufunga ndoa badala ya kufanya ngono bila ndoa kwani ni dhambi na kitu kisichokubalika mbele ya Mungu. Akawa anafungisha ndoa kwa siri kwenye makatakombe (mahandaki chini ya kanisa ambako kuna sehemu za ibada kwa watu wachache), alifanya hivyo kwa vile kufunga ndoa hadharani ilikuwa ni kukiuka amri ya wakuu wa dola ya kirumi.

Baadhi ya watu walifichua siri hiyo, hivyo Padre Valentin alishikwa na dola ya Warumi na kuuawa kama shahidi mfia dini kwa ajili ya kutetea waamini wake wafunge ndoa badala ya maisha ya ngono zembe bila ndoa.

Wakristo wakawa siku ya kumkumbuka Padre Valentin kama mfia dini sababu ya kutetea maisha ya wanakanisa kuwa wanandoa. Ikaenea katika kanisa nchi za magharibi na hata duniani ambako wanakanisa wanamkumbuka Mt. Padre Valentin. Baadaye ikapokeleka na watu hata wasio na imani ya kikristo kama ni siku ya kufanya kumbukumbu kwa Mt. Valentin kama mteteze wa Ndoa.

Maudhui ya siku hiyo kwa wasiowanakanisa imechukua maana nyingine ya kwamba ni siku ya wapendanao hata kwa wasio wanandoa bali mradi wanapendana, kitu ambacho ni kinyume cha malengo ya mfia dini Mt. Padre Valentin aliyetaka vijana wafunge ndoa badala ya kuwa na hawara tu (vimada).
 
Jamani tumeongelea tulivyotendwa na kila kitu embu tuongelee vituko vya valentine kama vile unanunua zawadi kumbe feki. unapanga dinner mara mtu anapata safari ya ghafla.
Mimi nina kituko kimoja hivi,valentine nafikiri 2002 hivi tumejiandaa kama couple nne tutoke dinner na ushamba wetu tukajifanya wengine tumehifadhi njaa ili tule five cse huko new africa hotel hata tusireserve tukaanza kuwasili tunawekwa tusubiri meza njaa inazidi mpaka nikaanza kutapika sababu ya njaa ilipofika saa tatu na nusu tukaambiwa meza bado na jiko linafingwa saa nne
Tukaondoka hoteli kama mbili hivi kote kumejaa basi tukaishia american chips kinondoni na magauni yetu nakwambia tukawekewa meza acha tule huku tukipeana zawadi kila mmoja wetu.kutoka hapo tukajikuta tumeingia kwenye mabendi ya kinondoni kila mmoja kachokaaaaa hoi haijafika saa nane tumbo zikaanza kuuma tukaondoka kesho yake kila mmoja anaumwa mbaya tuliharisha kila unaempigia anaharisha uzuri ilikuwa week end.duh
wapenzi pangeni dinner zenu mweke reserve mapema msijeishia msipotarajia.
Embu mwenye kituko cha valentine amwage hapa tucheke
Kuna kitu umrkiruka umetuchakachua mbona ujasema baada bend mliishia wapi habari hii siyo kamili!!
 
Babu nimetoswa na jamaa vipi huna marafiki zako :twitch::twitch::twitch::twitch:

hahaha...nani huyo kakutosa....afu misio babu MR..udalali siuwezi so will volunteer myself...lol mambo vipi lakini:clap2:
 
Back
Top Bottom