Harakati za Baba Levo kwenye muziki wa Bongo Fleva

Harakati za Baba Levo kwenye muziki wa Bongo Fleva

ukwaju_wa_ kitambo

Senior Member
Joined
Sep 15, 2024
Posts
150
Reaction score
173
1726524035236.jpg
KUMBUKIZI YA WASANII MKOANI KIGOMA.

Cliton Revocatus Chipando a.k.a Baba Levo wa kwanza kutoka kushoto enzi za ubarobaro wake, picha ya kwanza akiwa kijana mdogo kabisa, picha inayofuata akiwa kwenye show na kundi lake la OBD & GAZ akiwemo Kijukuu Zero Sifuriii ooh, huyu Kijukuu Zero Sifuri Ooh, alikuwa ni bingwa sana wa mashairi au michano kwa lugha tata.

Hii ilikuwa ni mwaka 2003 katika ukumbi wa Cine Atlas Makondeko Ujiji, Baba levo alikuwa anatamba na wimbo wake wa Mapadri na Mashee

Clayton chipando alikuja akawa Diwani wa kata ya mwanga 2015-2020 kupitia chama cha ACT -Wazalendo.

Kigoma ilibarikiwa kuwa na wasanii wengi enzi hizo, na makundi mengi ya wasanii yaliundwa Kigoma ikiwemo kundi la ''Red spider'' kutoka Ujiji na kina Baba Levo walikuwa wakitokea Mwanaga.

Makundi mengi ya Ujiji yalisambaratika baada ya msanii wao mkubwa kutanganza kuacha muziki na kufariki siku chache mbeleni, huyu alikuwa ''Fad Moh'', alikuwa mwenye kipawa na talanta ya hali ya juu katika uimbaji na mipangilio ya sauti ya maghani. Ukiachana na Koffi Olomide katika kubadilisha ladha ya sauti pia ''Fad Moh'' alikuwa ni bingwa wa kubadili sauti kwenye Mic.

Miaka hiyo kulikwa na wasanii wa aina zote hapa kwetu Kigoma, hata midundo ya singeli ilianzia huku na iliendeshwa na mwamba 'Ali Sinina' na mauno.

Kigoma kulikuwa na wasanii wengi kama kina gado brain siwasikii, walikuwepo kina Igwee na pah one, tupo around na masela ni kolabo na kidman, ilisifika k.town RFA hewani, usiku uligeuka raha, chege chigunda mtoto wa mama saidi kwa kasim zaid hawa walikuwa Mwazimwi kutoka Ujiji kisha wakajiita Manyema Family, kwa kuwamiss kundi la change dollar-mambo hadharani, raha ikageuka shida, tambo la obd na gaz na wake mrembo, Iddi Nyundo a.k.a Chamjicho. Ujiji walimmiss Jasmin, r.i.p fad moe, lilo kilio kwa mtaa, mitoto ileee na leader walisema game bado, bring kuhit na mchumba, wapi subwenke ya zinja, grem na vuga wana dumba, Nagasaki pembe za chaki, kwenye mic hawakubaki, hizo zilikuwa fataki, zilizotamba na kuwika hapa kwetu Kigoma Ujiji. Hizi ni kumbukizi za burudani, mapumziko ya weekend, bangwe beach watu walispend, heshima kwa Kid, Hitman na Maximum Record.

Picha ya mwisho aliyevalia miwani na kupiga salut ni Malilo au Lilo Boy alikuwa rafiki kipenzi wa Marehemu 'Fad Moh'. (Mwasu)

Ukwaju wa kitambo


#funguka.

K town people fungukeni mtueleze kigoma kunani???
 
Mi naona videos tu humu kwa Internet, wanaume wenzetu kwa mfano yule Jux, yuko na mpenzi wake wamepamba maua mpaka kitandani, wanacheza na wanapigana mabusu dah.
Nafikiri ndio maana sisi wengine hawa madada hatuchukulii serious kwasababu hatuna Malavidavi kama yale
 
View attachment 3097977KUMBUKIZI YA WASANII MKOANI KIGOMA.

Cliton Revocatus Chipando a.k.a Baba Levo wa kwanza kutoka kushoto enzi za ubarobaro wake, picha ya kwanza akiwa kijana mdogo kabisa, picha inayofuata akiwa kwenye show na kundi lake la OBD & GAZ akiwemo Kijukuu Zero Sifuriii ooh, huyu Kijukuu Zero Sifuri Ooh, alikuwa ni bingwa sana wa mashairi au michano kwa lugha tata.

Hii ilikuwa ni mwaka 2003 katika ukumbi wa Cine Atlas Makondeko Ujiji, Baba levo alikuwa anatamba na wimbo wake wa Mapadri na Mashee

Clayton chipando alikuja akawa Diwani wa kata ya mwanga 2015-2020 kupitia chama cha ACT -Wazalendo.

Kigoma ilibarikiwa kuwa na wasanii wengi enzi hizo, na makundi mengi ya wasanii yaliundwa Kigoma ikiwemo kundi la ''Red spider'' kutoka Ujiji na kina Baba Levo walikuwa wakitokea Mwanaga.

Makundi mengi ya Ujiji yalisambaratika baada ya msanii wao mkubwa kutanganza kuacha muziki na kufariki siku chache mbeleni, huyu alikuwa ''Fad Moh'', alikuwa mwenye kipawa na talanta ya hali ya juu katika uimbaji na mipangilio ya sauti ya maghani. Ukiachana na Koffi Olomide katika kubadilisha ladha ya sauti pia ''Fad Moh'' alikuwa ni bingwa wa kubadili sauti kwenye Mic.

Miaka hiyo kulikwa na wasanii wa aina zote hapa kwetu Kigoma, hata midundo ya singeli ilianzia huku na iliendeshwa na mwamba 'Ali Sinina' na mauno.

Kigoma kulikuwa na wasanii wengi kama kina gado brain siwasikii, walikuwepo kina Igwee na pah one, tupo around na masela ni kolabo na kidman, ilisifika k.town RFA hewani, usiku uligeuka raha, chege chigunda mtoto wa mama saidi kwa kasim zaid hawa walikuwa Mwazimwi kutoka Ujiji kisha wakajiita Manyema Family, kwa kuwamiss kundi la change dollar-mambo hadharani, raha ikageuka shida, tambo la obd na gaz na wake mrembo, Iddi Nyundo a.k.a Chamjicho. Ujiji walimmiss Jasmin, r.i.p fad moe, lilo kilio kwa mtaa, mitoto ileee na leader walisema game bado, bring kuhit na mchumba, wapi subwenke ya zinja, grem na vuga wana dumba, Nagasaki pembe za chaki, kwenye mic hawakubaki, hizo zilikuwa fataki, zilizotamba na kuwika hapa kwetu Kigoma Ujiji. Hizi ni kumbukizi za burudani, mapumziko ya weekend, bangwe beach watu walispend, heshima kwa Kid, Hitman na Maximum Record.

Picha ya mwisho aliyevalia miwani na kupiga salut ni Malilo au Lilo Boy alikuwa rafiki kipenzi wa Marehemu 'Fad Moh'. (Mwasu)

Ukwaju wa kitambo


#funguka.

K town people fungukeni mtueleze kigoma kunani???

Kwahiyo unataka kusema Singeli ilianzia Kigoma?
 
Umenikumbusha kipindi fad moe efariki hakyanani wadau wa mziki tuliumia kichiz.Kipindi hiyo kidman wa hitman records alkuwa mkomboz wa muziki kgm.
Heshima kwao RFA presenterz akina
1.Sando George Mpanda(Kid-bwai)
2.Samwel Davids Kiama(uncle sam).
3.Fredrick Bundala(sky walker) bila kuwasahau akina Fredwa na sindano tano za moto
Hao waliitendea haki bongoflavor huko westzone na viunga vyake.
Naomba kama kuna mwenye wimbo wa Jasmin wa Fad moe na usiku wa raha wa Chenji dola autupie humu.
 
Umenikumbusha kipindi fad moe efariki hakyanani wadau wa mziki tuliumia kichiz.Kipindi hiyo kidman wa hitman records alkuwa mkomboz wa muziki kgm.
Heshima kwao RFA presenterz akina
1.Sando George Mpanda(Kid-bwai)
2.Samwel Davids Kiama(uncle sam).
3.Fredrick Bundala(sky walker) bila kuwasahau akina Fredwa na sindano tano za moto
Hao waliitendea haki bongoflavor huko westzone na viunga vyake.
Naomba kama kuna mwenye wimbo wa Jasmin wa Fad moe na usiku wa raha wa Chenji dola autupie humu.
Njoo whatsApp 0767 542 202
 
Back
Top Bottom