Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Nakubaliana na wewe kabisa. Ila je unadhan Ben Saanane anaandika kwa utashi wake? Alipoondoka Dr Slaa hakika alitamani na yeye kuhama chama. Ndio maana kwa sasa harakati zake zina mwelekeo wa kujipatia ugali tu na si kujenga chamaSi lazima kile unachokiona sawa kwako kiwe sawa kwa mwingine......
saanane anawachakaza mpaka mwenyekiti wenu anatoa choziHehehe vioja hivyo
Mmeishia wapi!!
Kila kukicha matamko yakijingajinga mbona hamjafanya lolote na huyo mropokaji,
Hilo kundi la mitandaoni analijua Lowassa lilivyo mchachavya 2015
Hana hamu
ahhhh ndio maana ole sanduku alikuwepo kuhakikisha mpishi anafanya kwa mujibu wa oda ya chakulaha ha haa mkuu...mbona nasikia kama kautafiti ka twajiweza kalipikwa?
Hapana Mkuu. Hiyo 4M Ben hali peke yake. Kawaajiri vijana anaowalipa kwa ujira mdogo. Wengi wapi facebookKwahiyo wewe kinachokuuma ni hiyo 4Mil? Au kwakua wewe unalipwa 210,000/=?(7000 perday*30days)
Mwambie boss wako na wewe aongeze mpunga kidogo maisha yamekua juu sana kuanzia bundle na bill za umeme hivyo kazi ya kupost imekua ngumu.
Hivi wahuni wahuni kama ninyi na mafisadi wenu kina Change na Tiba nani ana muda wa kujibizana na ninyi?Hehehe vioja hivyo
Mmeishia wapi!!
Kila kukicha matamko yakijingajinga mbona hamjafanya lolote na huyo mropokaji,
Hilo kundi la mitandaoni analijua Lowassa lilivyo mchachavya 2015
Hana hamu
Kwani wewe unaandika kwa utashi wako hapa ama ni mapenzi yaliyopitiliza juu ya chama chako hadi inapelekea kuona kila kinachosemwa na wapinzani hakifai...Mfano ulipinga sana mawazo ya Mh. Mbowe aliposhauri shule ile ya Ihungo ifungwe kwa ajili ya madhara yaliyotokana na tetemeko...Ulitokwa povu sana hapa ila kwa bahati nzuri wakubwa zako wao walimuelewa Mbowe na wakafuata ushauri wake....So jaribu na wewe kutumia utashi wako utagundua namba 9 na 6 zinazomeka sawa inategemea na upande ulioko...Nakubaliana na wewe kabisa. Ila je unadhan Ben Saanane anaandika kwa utashi wake? Alipoondoka Dr Slaa hakika alitamani na yeye kuhama chama. Ndio maana kwa sasa harakati zake zina mwelekeo wa kujipatia ugali tu na si kujenga chama
kweli mkuu,kwenye escrow na EPA uliwatetea sanaMimi ni mwana CCM kindakindaki. Sijipendekezi kwa mtu. Natetea maslahi mapana ya taifa na chama
Ben ni ''kifaranga'' muda ukifika wata''mdamp'' na kupatwa aibu kama yanayomkuta Mtatiro kwa sasa.Mwanzoni mwa mwaka huu, niliweka taarifa kwenye mitandao ya kijamii hususan hapa Jamiiforums juu ya Mkuu wa Sera na Utafiti CHADEMA, Ben Saanane kununuliwa vitendea kazi kama simu, kompyuta mpakato, ipad, tablets na zana nyingine. Nilieleza kuwa aliyemnunulia vitu hivyo ni Edward Lowasa. Nilitoa sababu za Lowasa kufanya hivyo ni kutaka Mkuu huyo wa Sera na Utafiti afanye kazi ya kumsafisha Lowasa kwenye mitandao ya kijamii lakini pia amshambulie Rais Magufuli ili tunapoingia 2020, asiaminike tena. Nilieleza kuwa Ben na Lowasa wamekubaliana kuwa malipo ya kazi hiyo ni milioni 4 kwa mwezi.
Kwenye uzi ule, nilieleza bayana kuwa Ben Saanane amepangiwa ofisi ya kufanyia kazi hiyo katika sehemu ambapo sikubainisha kwenye mtandao kutokana na sababu za kimkakati.
Hata hivyo, baada ya uzi ule kuwekwa, Ben Saanane alikosa uvumilivu. Aliishia kuporomosha lugha zilizokosa staha kwa lengo la kushinikiza mods waufute. Alifanikiwa. Uzi ule ukaenda na maji. Leo mdogo wangu Ben namuomba awe mvumilivu ili tujadili kwa staha.
Miezi 5 imepita sasa tangu Ben Saanane anunuliwe. Matunda ya uwekezaji ule yameanza kuonekana. Ben Saanane na genge lake wameanza mashambulizi dhidi ya Rais kwa hoja ambazo kimsingi hazina mashiko.
Ben Saanane na genge lake wameshindwa kabisa kuona udhaifu wa Rais Magufuli kiutendaji na badala yake wanaegemea kwenye mipasho na mapambio. Wanafanya siasa za kuvizia. Niliwahi kuanzisha mada humu kwamba, ikitokea Rais akawa bubu, je CHADEMA watakuwa na ajenda zipi?
Tathmini yangu ya muda mfupi imebaini kwamba, hoja zinazojengwa na Ben Saanane na genge lake zinategemea nini Rais anaongea. Kwa maana utendaji wa Rais uliotukuka unasababisha Ben Saanane na Genge lake wakose hoja za kumkosoa. Hata kama wanapojaribu kukosoa utendaji, wanakosoa kwa hoja dhaifu. Mathalan, ziliponunuliwa ndege mpya mbili aina ya Bombadier Q400, walijenga hoja za kitoto eti ndege hizo hazina mwendo. Mara wanasema ni mapangaboi. Mara wanasema eti water salute haikufanyika kisawasawa. Almradi wanawaonesha wafadhili wao kuwa wametimiza wajibu wao. Utoto.
Uwezo wa vijana wa CHADEMA katika kujenga hoja ni mdogo. Kuna wakati Lusinde aliwahi kuwaambia kuwa akili zao zimeshikiliwa na Mbowe na ndio maana wanawaza kimbowembowe tu.
Hata hivyo, najaribu kuwaza, je kazi anayofanya Ben Saanane na genge lake inatosheleza matakwa ya wafadhili wake? Je watafanikiwa kushusha morali ya Rais Magufuli katika kuwatumikia wananchi? Je watakwamisha juhudi kubwa zinazofanywa na Rais Magufuli katika kutekeleza ilani ya CCM? Thubutu! Rais ameapa kuwa hakuna atakayekwamisha utekelezaji wa Ilani ya CCM. Ben Saanane na Genge lake wataishia kujadili water salute, kuomba Salary Slip ya Rais na kujipongeza kutokana na kauli ya Rais kuwa anatamani malaika afungie mitandao ya kijamii kwa mwaka mmoja ili itakapofunguliwa wakute Tanzania imepaa.
Nimhakikishie Rais wangu kuwa, hawa wapiga kelele mitandaoni hawatafanikiwa kukwamisha harakati zako za kuwaletea maendeleo wananchi. Waache wapige kelele. Wewe piga kazi. Mwisho wa siku kelele zao zitageuka kuwa kicheko kwako. Watanzania tuna imani kubwa kwako. Kazi unayofanya inapokelewa kwa mikono miwili na Watanzania. Utafiti wa Twaweza unabainisha kuwa 96% ya Watanzania wanakulibali. Endelea kupiga kazi ili ifikapo 2020, wapinzani waone aibu kumsimamisha mgombea Urais kupambana na wewe.
Dah, sasa vijana wa facebook wanakupa presha? Au unafikiri KIONGOZI alipotoa ya moyoni kuhusiana na mitandao alilenga facebook?Hapana Mkuu. Hiyo 4M Ben hali peke yake. Kawaajiri vijana anaowalipa kwa ujira mdogo. Wengi wapi facebook