Harakati za Ben Saanane kupambana na Rais Magufuli, ni njia sahihi ya kuwaridhisha wafadhili wake?

Harakati za Ben Saanane kupambana na Rais Magufuli, ni njia sahihi ya kuwaridhisha wafadhili wake?

Kama Ben kaajiliwa na Lowassa na wewe umeajiriwa na nani kwa kazi ya kumshambulia Ben na unalipwa shilingi ngapi kwa kazi ya kumtukuza Magufuli?.
Angalia historia yangu Mkuu. Angalia pia mwelekeo wa post zangu
 
Hapo ni kama umnasemea chooni. Kama mnge kuwa na hoja msingezima bunge live, msingetunga sheria ya mtandao, msingepiga marufuku mikutano ya siasa, msingeleta sheria ya statics, msingeteua wanasiasa kwenye nafasi za utendaji zisizo husu siasa, msingeleta sheria za habari mlizoleta, msingemsaidia kwa kutumia polisi lipumba. Kifupi hamna hoja wala hamna hoja. Kam mnasema hao wapinzani wanatumia hotuba za mkuu kupata cha kusema si mrekebishe utaratibu wa anasema nini? badala ya kuacha aseme na nyinyi mpate kazi ya kufafanua au kuteteta hum JF. Wakati mwingine nachefuka kusikia watu wa namna hii wamesoma.
Msalimie Mange Kimambi
 
penye ukweli uzungumzwe huyu Ben maandako yake ni chungu kwa chama chetu maana mara nyingi anakuwa na fact though awe na adabu na aache kumuandika Rais wa nchi anavyotaka...
 
Jina lenyewe ni saa nane..[emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Eti Ben anasema alitangaza vita na raisi Dr. Magufuli, kichekesho hiki, Selasini tu kule Rombo alimnyoosha atamuweza raisi wa nchi?
 
Dj alishabadili gia angani tena.

Mpangusa viatu Vya wanene wa ufipa Ben , mwaka 2020 atalazimika kutunga mapambio ya kumsafisha mgombea urais wa Chadema Lugumi.

Kwa kuwa huwa hajifunzi 2020 ataifanya kazi aliyoifanya 2015 ya kusafisha aliowaita Mafisadi kwa muda mrefu.
 
Bavicha ni watu waliochanganyikiwa,na wala hawatafanikiwa kumtingisha Rais wetu
 
Mkuu uzi huu hautaondolewa kweli? Maana mada zinazotofautiana na Ben Saanane haziishi unaweza kufikiri Ben ni moja wa moderator wa jf.
 
Mwanzoni mwa mwaka huu, niliweka taarifa kwenye mitandao ya kijamii hususan hapa Jamiiforums juu ya Mkuu wa Sera na Utafiti CHADEMA, Ben Saanane kununuliwa vitendea kazi kama simu, kompyuta mpakato, ipad, tablets na zana nyingine. Nilieleza kuwa aliyemnunulia vitu hivyo ni Edward Lowasa. Nilitoa sababu za Lowasa kufanya hivyo ni kutaka Mkuu huyo wa Sera na Utafiti afanye kazi ya kumsafisha Lowasa kwenye mitandao ya kijamii lakini pia amshambulie Rais Magufuli ili tunapoingia 2020, asiaminike tena. Nilieleza kuwa Ben na Lowasa wamekubaliana kuwa malipo ya kazi hiyo ni milioni 4 kwa mwezi.

Kwenye uzi ule, nilieleza bayana kuwa Ben Saanane amepangiwa ofisi ya kufanyia kazi hiyo katika sehemu ambapo sikubainisha kwenye mtandao kutokana na sababu za kimkakati.

Hata hivyo, baada ya uzi ule kuwekwa, Ben Saanane alikosa uvumilivu. Aliishia kuporomosha lugha zilizokosa staha kwa lengo la kushinikiza mods waufute. Alifanikiwa. Uzi ule ukaenda na maji. Leo mdogo wangu Ben namuomba awe mvumilivu ili tujadili kwa staha.

Miezi 5 imepita sasa tangu Ben Saanane anunuliwe. Matunda ya uwekezaji ule yameanza kuonekana. Ben Saanane na genge lake wameanza mashambulizi dhidi ya Rais kwa hoja ambazo kimsingi hazina mashiko.

Ben Saanane na genge lake wameshindwa kabisa kuona udhaifu wa Rais Magufuli kiutendaji na badala yake wanaegemea kwenye mipasho na mapambio. Wanafanya siasa za kuvizia. Niliwahi kuanzisha mada humu kwamba, ikitokea Rais akawa bubu, je CHADEMA watakuwa na ajenda zipi?

Tathmini yangu ya muda mfupi imebaini kwamba, hoja zinazojengwa na Ben Saanane na genge lake zinategemea nini Rais anaongea. Kwa maana utendaji wa Rais uliotukuka unasababisha Ben Saanane na Genge lake wakose hoja za kumkosoa. Hata kama wanapojaribu kukosoa utendaji, wanakosoa kwa hoja dhaifu. Mathalan, ziliponunuliwa ndege mpya mbili aina ya Bombadier Q400, walijenga hoja za kitoto eti ndege hizo hazina mwendo. Mara wanasema ni mapangaboi. Mara wanasema eti water salute haikufanyika kisawasawa. Almradi wanawaonesha wafadhili wao kuwa wametimiza wajibu wao. Utoto.

Uwezo wa vijana wa CHADEMA katika kujenga hoja ni mdogo. Kuna wakati Lusinde aliwahi kuwaambia kuwa akili zao zimeshikiliwa na Mbowe na ndio maana wanawaza kimbowembowe tu.

Hata hivyo, najaribu kuwaza, je kazi anayofanya Ben Saanane na genge lake inatosheleza matakwa ya wafadhili wake? Je watafanikiwa kushusha morali ya Rais Magufuli katika kuwatumikia wananchi? Je watakwamisha juhudi kubwa zinazofanywa na Rais Magufuli katika kutekeleza ilani ya CCM? Thubutu! Rais ameapa kuwa hakuna atakayekwamisha utekelezaji wa Ilani ya CCM. Ben Saanane na Genge lake wataishia kujadili water salute, kuomba Salary Slip ya Rais na kujipongeza kutokana na kauli ya Rais kuwa anatamani malaika afungie mitandao ya kijamii kwa mwaka mmoja ili itakapofunguliwa wakute Tanzania imepaa.

Nimhakikishie Rais wangu kuwa, hawa wapiga kelele mitandaoni hawatafanikiwa kukwamisha harakati zako za kuwaletea maendeleo wananchi. Waache wapige kelele. Wewe piga kazi. Mwisho wa siku kelele zao zitageuka kuwa kicheko kwako. Watanzania tuna imani kubwa kwako. Kazi unayofanya inapokelewa kwa mikono miwili na Watanzania. Utafiti wa Twaweza unabainisha kuwa 96% ya Watanzania wanakulibali. Endelea kupiga kazi ili ifikapo 2020, wapinzani waone aibu kumsimamisha mgombea Urais kupambana na wewe.

Wewe Ni Kama Nape AKA Waziri Rumbesa, aliyesema Kuwa Lowassa Kanunua Chadema, Unajua Tunakamataje Waongo, they pretend to have details ambazo kikawaida Haiwezekani Kuwa Nazo. Nani sasa anaamini Kuwa Lowassa alinunua Lowassa kwa Mbowe Kama alivyokuwa Akisema huyu Mwehu kwenye Kampeni? Kama Una akili Mwambie Rais Nani aliwaua Wale Askari wanne Pale Bank na Yule Mwingine Vikindu, Maana wanasema Kikulacho Kinguoni Mwako!



 
Usitulazimishe tukubali kile unachokiamini wewe bwana mdogo! CCM mtatuambia kitu gani tuwaamini sisi? kwa kifupi hamkubalili hata kidogo na mnalazimasha mambo muonekane mnakubalika! hiyo 96% ya TWAWEZESHWA waliwahoji wa TZ wawapi? acheni kutufanya kuwa hatuna akili, ogopeni jueni kuna Mungu na haya yote yana mwisho!
 
Magufuli hawezi kutoka kwenye reli kwa kelele za akina Saa nane na uwongo wao wa kutunga. Ile ya bukoba haitafutika kichwani mwangu kamwe na pale ndipo nilipomdharau sana huyu mtu ben saa nane. Yaani alikurupuka mbio humu eti Mbatia azuiwa na polisi asipeleke Msaada kwa wahanga. Raisi Magufuli Una vita kali sana. Kumbuka kuna watu wengi sana walikua wananufaika na mifumo ya ufisadi na dili na kwa sasa maisha yao yamebadilika hao ndo wanaojaribu kwa kila mbinu kuwatumia vijana mpaka wanasiasa maarufu ili kukudhoofisha katika jitihada zako hizi za kuwatumikia Watanzania. Kwa sasa upigaji hela serikalini umekua mgumu sana hapo awali ndo ulikua utaratibu.
 
Wewe Ni Kama Nepi AKA Waziri Rumbesa, aliyesema Kuwa Lowassa Kanunua Chadema, Unajua Tunakamataje Waongo, they pretend to have details ambazo kikawaida Haiwezekani Kuwa Nazo. Nani sasa anaamini Kuwa Lowassa alinunua Lowassa kwa Mbowe Kama alivyokuwa Akisema huyu Mwehu kwenye Kampeni? Kama Una akili Mwambie Rais Nani aliwaua Wale Askari wanne Pale Bank na Yule Mwingine Vikindu, Maana wanasema Kikulacho Kinguoni Mwako!




Hizi video zinahusiana vipi na mada?
 
Rais ni muacheni afanye yake huyo kijana apewe tu pesa lakn ninaiman kwa uwezo wa mungu Rais hawez kuchafuka hata kidogo....
 
Rais ni muacheni afanye yake huyo kijana apewe tu pesa lakn ninaiman kwa uwezo wa mungu Rais hawez kuchafuka hata kidogo....
Kinachosikitisha ni kwamba hawana hoja yoyote ya maana wanayotoa zaidi ya kumuattack tu binafsi. Washindwe kwa jina la Mwenyezi Mungu
 
Tunapata taabu sana kukuelewa unapoishia kulalamika kua Magufuli ni muovu bila kuuweka wazi huo uovu wenyewe sasa.
Mkuu, hao watu akili zao zote ameshika Mbowe. Hapo walipo hawajui hata wanaandika nini
 
Thread kama hizi ndizo zinazofanya Jf kuonekana ya Hovyo. Source ya habari yako? Ushahidi? Yan JF sasa imekuwa sehemu ya kushambulia watu binafsi bila ushahidi. Thread kama hii haina uwalali wa kukaa hapo kwa Heshima ya JF
Mkuu Kibosho, naunga mkono hoja kwa sababu jf was meant to be the home of great mind, ila kwa vile huu ni mtandao huru wa kijamii kila mtu yuko huru, matokeo yake ndio haya watu wenye sound mind wamejiunga na wanaleta hoja zenye mashiko kama Mkuu Ben Saanane ila pia watu wenye unsound mind pia wamo.

Bandiko kama hili ni uthibitisho Mkuu Lizaboni sio mzima, ni insane, kwa kifupi huyu ni kichaa kabisa, ila mtu kuwa kichaa sio lazima mpaka aokote makopo.

Kwa vile hawa vichwa wa jf ni wenzetu, hatuwezi kuwatenga, hatuwezi kuwatupa lazima tuendelee kuwa nao kwa kuwavumilia tuu.

Natoa ushauri kwa mode, tuanzishe jukwaa la umbeya na udaku wa kisiasa ili watu kama Lizaboni wawe wanapost kule huu utumbo wao kama huu.
Pasco
 
Last edited:
Back
Top Bottom