Harambee: Kuiona Mechi ya Brazil na Taifa stars

Nimesoma kule kwa Michuzi kuwa zile tiketi za laki mbili zimeisha! Sijaelewa zilikuwa chache sana (kama 10 tu hivi) au ni watu wana mkwanja wa kufa mtu?

Janja ya TFF mkuu ili kuwafanya watu waone bei ya Kiingilio ni za kawaida mkuu, juzi nilikuwa nacheki habari kabla ya Mwakalebela hajatangaza Viingilio akanza kwa kusema kuwa tiketi za 200,000 zimeisha sasa nikajiuliza hao walionunua walinunua kwa Shilingi ngapi wakati hata bei zilikuwa bado kuwekwa hadharani nikapata hisia kwamba Hizo za VIP watakuwa wamepewa Bure Mawaziri na Viongozi wengine wa Kisiasa. Tufumbuke Macho Serikali inataka sisi Masikini ndio tubebe Mzigo wa Kuileta Brazil yaani ukimsikiliza Tenga unaweza kufikiri labla Tanzania Soccer Fans ndio wamewaandikia Barua TFF kuiomba Tanzania kuieta Brazil! Teh teh teh
 
hAhha i saw this coming thats why I asked Charity which team she was supporting... :target:

Charity good luck baby Girl... ila make sure to take care of urself na hawakukanyagi huko kiwanjani...
 
Mi nilitaka kwenda lakini kuna mgomo kule umeanzishwa na Gembe,sasa niko njia panda niende au nisiende..
 
wee Kiranga unabore!wacha kuharibu mada ya mwenzio....
 
Mi nilitaka kwenda lakini kuna mgomo kule umeanzishwa na Gembe,sasa niko njia panda niende au nisiende..

Bora uende tu kama ndo mgomo angeitisha mgomo wa ufisadi unao endelea kufanyika nchini ambao ni zaidi ya hizo bil.3
 


sasa hapo meenda mbali, jamani kwa nilivyoelewa Charity alikuwa anaiburudisha j3 iliyokuwa imepooza tu, kuna thread alihangia kwamba hawezi kutoa hiyo pesa wakati ana majukumu yake kufanya zaidi ya kwenda kuwaangalia hao Brazil, watu mpo sensitive mpaka mnashindwa kutofautisha utani na mambo serious, wewe kataza jamaa/familia yako ichudhurie lakini wenye kuweza kuhudhuria iwe kwa kuchangiwa/kutoa mwenyewe waache wafanye hivyo, kapambane na serikali yako yenye matumizi mabaya na sio mtoa thread ambaye hata hivyo alikuwa anachangamsha mabo tu na blue monday...khaa.
 

yaani umejieleza vitu ambavyo havihusiani kabisa, usomeshe/ulishe na makorokoro yote yanawahusu wewe na hao uliowasaidia na huyo unaemwita demu, kifupi Charity hajakushikia gun umpe huo mchango, wewe unaona anasa lakini wengine ni ktu cha kawaida, umejieleza vicvyoelezeka kabisa......anzana na serikali yako, au hizo pesa zako we changia pia na serikali yako waendelee kufanya wafanyavyo kama charity anavyotaka kufanya afanyavyo.
 

kwa wewe ucemjua, wengine labda tunamjua zaidi ndio mana wenye kutaka kuchangia watachangia.....
 
 
 
Charity, FL1, Nyamayao na wengine,

Asanteni sana kwa posts zenu, mana kuna watu humu sura zimekunjamana kisa Charity kaamua kuburudisha baraza na kuitisha harambee!! Wanaanza kudiscuss watu badala ya mada. Kuna jamaa mmoja hamnazo kabisa, mara anasema kulipa kiingilio cha laki mbili kuiona Brazil ni anasa, wakati huo huo analeta ulimbukeni wake wa u Jack Pemba wa kutoa milioni 6 kwenye sherehe ya anasa! na anaona hiyo ni sawa!! na hapo hapo anataka watu wagome kwenda kwenye mechi, kisa kiingilio ni elfu thelathini.

Akili za watu zinatofautiana, na maana ya JF sio kupinga kila kitu ambacho wenzako wanakisema! Pinga basi mambo ya maana; hata hili la kufurahisha baraza unashupalia? Umeacha kazi zote zinazokupatia mamilioni (kama kweli) unabishania upupu!!

Tuyaache hayo, tuendelee na story, Charity na mie ntakuchangia, ila sijui ni kiasi gani...na sina sharti lolote!!
 
Mundu we acha tu,watu wengine ndio hivyo inabidi tuwavumilie tu.Yani wewe hata ukiniambia nigome nisiende mie ntakukubalia kabisa sio yule mharibifu wa hewa.
Mie nakushukuru kwa moyo huo wa kunichangia bila masharti yoyote.
 
Mundu we acha tu,watu wengine ndio hivyo inabidi tuwavumilie tu.Yani wewe hata ukiniambia nigome nisiende mie ntakukubalia kabisa sio yule mharibifu wa hewa.
Mie nakushukuru kwa moyo huo wa kunichangia bila masharti yoyote.

Charity, au jamaa aliwahi kukutumia PM ukamchunia nini? Maana duh, naona ana hasira sana na wewe!

Nahisi nimendandia treni kwa mbele!!
 
Charity, au jamaa aliwahi kukutumia PM ukamchunia nini? Maana duh, naona ana hasira sana na wewe!

Nahisi nimendandia treni kwa mbele!!
Hahahahahaha.Masaki sivyo hivyo.Nadhani ndivyo alivyozaliwa na hapa tunamuamsha akikurupuka huko kuwahi kubeba maksi sijui itakuwaje.Mie nshaanza kumuogopa sio mzima huyu.
 
Hahahahahaha.Masaki sivyo hivyo.Nadhani ndivyo alivyozaliwa na hapa tunamuamsha akikurupuka huko kuwahi kubeba maksi sijui itakuwaje.Mie nshaanza kumuogopa sio mzima huyu.

Mwambie atulize mzuka, mbona mimi nipokufuata kwenye PM ukanitoa baru niliuchuna tu, kama sio mimi vile....!!!:rofl:
 
Mwambie atulize mzuka, mbona mimi nipokufuata kwenye PM ukanitoa baru niliuchuna tu, kama sio mimi vile....!!!:rofl:

:smile-big: teh teh ,kumbe ndo ulikuja na Aidii nyingine!!!!!!!! wewe!
 
Hamna haja ya Kuzodoana wana JF, JF iko open kwa kila mtu kwa maana kila mtu ana haki ya Kutoa Maoni yake na vile vile Kila Mtu ana haki ya Kukubali au Kukataa maoni ya Mwanachama mwingine kwa hoja.

Mimi ninaona Kiranga and Charity are delivering the same message but in different ways, Kwa mtazamo wangu wote wawili wanakerwa na vitu viwili

Charity yeye through her message inaonekana anakerwa na Viingilio vikubwa ambavyo vinaweza wafanya hata wale wasiomudu maisha yao wafanye kila linalowezekana ( Ikibid hata kuahirisha kwenda kununua dawa, kulipia karo za shule hata kumaliza mtaji wa Duka au Genge) ili mradi wakaione Brazil and this is because they love soccer

Kwa Upande wa Kiranga yeye anakerwa na namna pesa yetu inavyotumiwa vibaya ( Six Billions si Mchezo jamani Mkuu wa Kaya aliomba Msaada wa Milioni 70 kwa ajili ya vyandarua) wakati hatuna uhakika wa maji safi, bado kuna wanafunzi wanakaa chini, maisha ya watu ni duni, Barabara nyingi ni Mbovu na anaenda Mbali akitamani kama angekuwa na Uwezo watu wote wagomee kuhudhuria huu Mtanange

Jamani nimejaribu kwenda mbali Beyond Kiranga and Charity as indivuduals ( Or as people) nikaangalia na kujaribu kugundua kile walichokimaanisha katika maandisi yao

Kama nimewapata fresh basi Wote mko Sahihi

Note: Ili JF iwe na afya ni Lazima watu watofautiane, siku Watu wote ndani ya JF watapokuwa na Mawazo au mitazamo inayofanana huo ndio utakuwa mwisho wa JF

Idumu JF
 

Note: Ili JF iwe na afya ni Lazima watu watofautiane, siku Watu wote ndani ya JF watapokuwa na Mawazo au mitazamo inayofanana huo ndio utakuwa mwisho wa JF

Idumu JF
Tutofautiane kwa hoja ila sio kutukanana!!
 
Hongera!Unauwezo wa kuangalia vitu kwa JICHO LA TOFAUTI.
hivi ushawahi kuwa Mchungaji au mtumishi wa Bwana?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…