Harmo Rapa atimua mbio baada ya Mh. Nape kuoneshwa bastola

Harmo Rapa atimua mbio baada ya Mh. Nape kuoneshwa bastola

Watanzania wengi sana wako kama Harmorapa-maneno mengi kwenye keyboard ila frontline huwaoni. Na hapo kwenye kukimbia ndo mtaji wa wanasiasa wa chama tawala.
 
Nape Nnauye ni right handed ukimuangalia katika video hii huenda na yeye alikua ana silaha 9mm hand gun kama wengine mnavyooita Bastola, Chuma, Mguu wa kuku!

 
Hahaha ama kweli maisha matamu, ndo mwisho wa kimbele mbele, inabidi ucheke mbali ya kuona huruma kwa Nape
 
nimejaribu ku-upload video,imeshindikana.kwa aliye na ile video,ajaribu kuishusha hapa.

ila nimependa jinsi kijana harmorapa anavojaribu kucheza na matukio ya kijamii/kisiasa yanayotokea nchini ili kujiongezea umaarufu.
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] harmorapa kiboko ya mabishoo!! Mzee wa kutumia fursa[emoji23][emoji23]
 
Huyu jamaa leo kupunguza stress za watu juu ya Nape
 
Hiyo ni Namba ambazo Nape ameanza kusomeshwa bado mvua ya masiki inakuja kwa kuwa ameshawekwa tayari kwenye kapu la wapinzani angali ndani ya chama chake.
 
naona maulid kitenge akisaidia kutuliza ghasia na povu la yule askari kanzu
 
Msanii Harmo rapa leo alienda kwenye kikao cha Mh. Nape kilichokuwa kinafanyia kwenye hoteli ya Protea. Baada ya kutokea sintofahamu askari/usalama alitoa bastola na kumnyooshea Nape Nnauye, tukio lile lilimpa wazimu Harmo Rappa na kujikuta anatimua mbio asijue aendako.


Bastola yenyewe aliiweka mkono wa kushoto wakati yeye anatumia mkono wa kulia, huyu tiss hana uzoefu wa kutumia bastola, kwanza anaitoa bastola kishamba kabisa
 
Back
Top Bottom