Harmonize kashuka kimuziki

Harmonize kashuka kimuziki

B M F ICONIC

JF-Expert Member
Joined
Jan 28, 2019
Posts
824
Reaction score
1,631
Moja kwa Moja kwenye mada.

Msanii Harmonize kashuka kimuziki upande wa international (nje ya mipaka ya Tanzania) na kawa msanii wa ndani (bongo) pamoja na Africa mashariki

kipindi bado yupo WCB alikua akitaftiwa collabo na wasanii wa nje ya nchi hasa Nigeria ili ali wini soko hilo la nje kimuziki. Na kutoa nyimbo na wasanii kama Sarkodie, Yemi Alade , Skales, Burnaboy.

Ikumbukwe kuwa hapo nyuma Harmoznize alikuwa na uhusiano wa karibu na msanii Burnaboy. ambapovShow ya Burna iliofanyika Rwanda alimuitaji Harmozize apande jukwaani licha ya WCB kumkazia na kutofanikiwa.

Kwa hali alionayo sahivi harmonize kimataifa sidhani Kama burnaboy anaweza kumpa nafasi ya collabo pasipo kumlipisha fedha au kwa barua.

Tangu Harmonize alipotoka WCB amekua akitoa ngoma nyingi za ndani kitu ambacho kina mrudisha nyuma na kuliua soko lake la muziki la kimataifa

Ame Base sana na Tanzania kitu ambacho kina mnyima show za nje ya bongo.

Amekua aki perfom kwenye majukwaa ya kisiasa na kutoa Album zisizo na mipango mizuri ya Marketing na ku li WIN soko la kimataifa.

Album hizo hazijamjengea soko lolote nje ya mipaka ya Tanzania. Mfano wa Album

Screenshot_20241028-162408_Opera Mini.jpg
HArmozize kaendelea kuwa Msanii wa ndani na kufanya vizuri kwenye kurasa za instagram kwa kusifika kwa kuwapata wnwke wenye Mashepu. japo ngoma anazozitoa ni nzuri na zinazopendwa na mashabiki hivyo kumpa nafasi ya kutumbuiza kwenye matamasha makubwa ya michezo na serikali.

Kwa kusema hayo Itoshe kusema kuwa Soko la Harmonize nje ya mipaka ya Tanzania limeshuka na kumfanya kuwa msanii wa ndani.

Abadilishe Uongozi wake na Management yake kwani hawana maono nae katika biashara ya muziki.
Nawasilisha . .. . Toa maoni yako.
 
Sasa kushuka kwake kunakuhusu nini?umeadhirika sehemu yoyote au umepungukiwa nini?kakuomba msaada?fanyeni yenu basi
MImi ni promota wa show huku Diaspora. Ulaji wangu ni kupitia hao wasanii. Maoni yenu yananisaidia kufanya Research yangu nisije kuingia cha kike kuwaleta hao wasanii huku
 
Kazi yako ni kufuatilia maisha ya watu tu na kuleta humu umbea,majuzi umemsema Rayvan kuwa kashika leo una harmoni,kenge wewe hina mambo yako ya kifanya?e
Pia na miliki Online Tv inayofanya vizuri bongo. Usiache ku subscribe maana huu ndo ulaji wetu sisi tuliowekeza kwenye sanaa na media
 
Apambane na hali yake kwani sisi tunamtegemea kwa lipi?
Tunakula kwake?
Maisha ni yake na cc tushughulike na yetu
Maoni yako yananisaidia katika biashara ya ya U promota ya kuwataftia na kuwaandalia wasanii show. Huu ndo ulaji wangu na nyie ndo wauzuliaji wa show hizo
 
MImi ni promota wa show huku Diaspora. Ulaji wangu ni kupitia hao wasanii. Maoni yenu yananisaidia kufanya Research yangu nisije kuingia cha kike kuwaleta hao wasanii huku
Sasa huna mawasiliano yao ?
Mbona kwenye Bio za mitandao yao kuna mawasiliano yao pale ?

Unajua nini B M F maisha hapa Tanzania ni magumu kinoma halafu hao wakina Harmonize kazi yao ni kumsifia Samia tu.

Wamepoteza mvuto na hakuna ambaye ana ushabiki kama kipindi cha nyuma.
 
Issue ya P didy imetrend Sana Hivyo ngoma zake alizoachia zote zimeshindwa kupenya kabisa.

Baada ya issues ya P didy ilifatia derby ya simba na yanga.

Means kuna strategies zinhitajika ili hawa wasanii wakae on trending.

Ikiwemo hiyo anayotumia diamond ya wanawake
 
Sasa huna mawasiliano yao ?
Mbona kwenye Bio za mitandao yao kuna mawasiliano yao pale ?

Unajua nini B M F maisha hapa Tanzania ni magumu kinoma halafu hao wakina Harmonize kazi yao ni kumsifia Samia tu.

Wamepoteza mvuto na hakuna ambaye ana ushabiki kama kipindi cha nyuma.
Na mawasiliano na meneja wake. Sema nachukua maoni kwa wana JF. Nisije kumuita kwenye Show pesa ya kuandaa show hisirudi.
Connection anayopata serikaln inamfanya apate vi show kwenye majukwaa ya MCC ndo maana anawasifia
 
Issue ya P didy imetrend Sana Hivyo ngoma zake alizoachia zote zimeshindwa kupenya kabisa.

Baada ya issues ya P didy ilifatia derby ya simba na yanga.

Means kuna strategies zinhitajika ili hawa wasanii wakae on trending.

Ikiwemo hiyo anayotumia diamond ya wanawake
Ishu pia ya nyimbo wanazoimba. Mtu anaimba "vitoto vya 2000" atapataje show

Nje ya nchi Msanii anaweza kupata Show kwenye club kubwa ata 10 Hvi kwa nyimbo moja tu ilio enda viral. Coma sava show ilipatikana Dubai
 
Ishu pia ya nyimbo wanazoimba. Mtu anaimba "vitoto vya 2000" atapataje show

Nje ya nchi Msanii anaweza kupata Show kwenye club kubwa ata 10 Hvi kwa nyimbo moja tu ilio enda viral. Coma sava show ilipatikana Dubai
Umewahi kufanya Biashara ya muziki?
 
Kimaokoto vipi? Wakati akiwa na kajala bank account ilikuwa inasoma milioni 800 au 900 lakini alivyokuwa na poshy bank acount inasoma milioni 100 au 120 alisema Mwijaku.
 
Back
Top Bottom