Harmonize mtoto mbaya sana alichokifanya kwenye hii ngoma ni hatari tupu


Average...!naona Laizer karudia tena kutengeneza midundo ya matarumbeta unless hii midundo ni ya zamani maana nilimsifia sana kwenye Hallelujah,Harmonize anatabirika hataki kubadilika ni kama Mh Temba unajua tu ataimbaje hata kabla haujamsikia huwezi kuikataa video iko poa sana naona Mr Romantic kaangusha lugha ya Nyerere kwenye bridge pale imekaa poa.
 
Laizer ubunifu 0
 
Nyimbo karudia mjomba kuna wimbo ye mwenyewe alitoa unaitwa moyo
wimbo haujarudiwa,sema kuna baadhi ya vionjo kahamisha kutoka ktk wimbo wake wa Moyo...kitu ambacho sio kibaya coz hiyo Moyo yenyewe haikuwa official release,ilitolewa kama bonus track tu!
 
najua lengo lako upate likes nyingi na qoutes!

Ebu tuoneshe hapo alipomuiga Mondi.kwenye hiyo ngoma,kuhusu uimbaji ngoma imebalance kwa wote wawili Harmo na Korede...na labda unaona korede kafunika kwa kuwa kaimbishwa na kiswahili pia.
 
Huwaga nasikia nyimbo kujirudia leo ndo nmejionea. ... sijaenjoy honestly kama nmeshaisikia/iona zamani duh
jipe muda wa kuisikiliza na kuitazama zaidi,utaenjoy tu...vionjo vya kwenye Moyo ndo vimeipamba hii ngoma plus hizo nakshi nakshi mpya alizojaliza humo.
 
Kuna wakati lazima tukubali kuwa kila producer ana flavor/touches zake...matarumbeta style ndo touches za laizer,hii ni sawa na ukisikia beats za man walter au AM records,lazima tu utazijua coz kuna mitindo flani hivi lazima ijirudie.

Lakini pia ngoma hii ina mikono ya maproducer watu nazani...kuna sheddy clever wa burn records,laizer na producer wa Mavin...
 
Nimependa video, ila wimbo nah!! Same melody.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…