Harmonize: Nilipewa Mkataba wa kuonewa na WCB na nilisingiziwa kumroga Diamond Platnumz

Kama hichi ulichokiandika ni kazi yako, basi wewe ni fundi mno. Watu kama ninyi ndiyo mlitakiwa muwe kwenye vyombo vya burudani na siyo wale wavuta bangi ambao hata kuchambua mambo hawawezi kazi kuharibu maadili ya watoto wetu. Again, umetisha sana mzee ✊✊✊
 
Ni Luqman Maloto
 
Hatukatai Kubebana hapa Duniani ni kawaida sana, na ndo Maisha!! hakuna mtu yeyote Duniani alisimama peke yake! akawa yeye! Mond! kabebwa sana tu!! hata Rais mbabe wa USA!! wana bebwa sana tu! na ukibeba watu tegemea iko siku watataka kujisimamia!!

Ni kujidanganya eti niwabebe milele! wawe hivo milele nooo!! ..... kubebwa ni maumbile yetu viumbe hai! sisi siyo visiwa!.....tunategemeana.. Israel na ubabe wake wooote wanabebwa na USA, chinga yeye nani asibebwe?

..so Maumbile ya asili yasiwe fimbo ya kumchapa Harmonise! kamwe!! .. wkt hata weye unae andika hapa umebebwa mpaka dakika hii na JF! Ni kuto kujijua tu! ..... kinacho wachoma Mond team! ni, Big talents, mfanikio ya dogo! na kukubalika kwa Harmonise kimuziki!!

Talanta ya Harmonise ndo shida inayo waumiza wale ''inner circle suppoters wa Mondi wengi! wivu wa mafanikio ya huyu kijana! amabao hao wanao piga kelele hawana! yanawachoma km moto wa rami! tena waziwazi hawajifichi!!

Narudia tena mnisikie wote! kubebana ni jadi yetu sisi km Binadamu!! haliepukiki wala siyo mjadala hapa! Sirikali yako tu inabebwa na misaada kedekede! uongo jamani?? ...

....Shetani na ubabe wake wote ana bebwa na Mungu, mpaka leo iko ivo!! umewahi kuona Mungu anapiga kelele? na Binadamu wameumbwa kwa mfano wa nani?! alisema tu Mungu atamchoma one day!! lkn hatujui labda atamsamehe...mwanae yule!

Ni kwelii hawa jamaa Diamond team!! wamejawa na wivu wa kimasrahi! na wa kitoto kabisaaaa!! iko siku hata Mondi watamgeuka tu! muacheni chinga aende zake siyo kumsimanga simanga! na mjue kwa kufanya ivo ndo mnamfungulia chinga njia kabisaa!!

itafika mahali mtakonda au mtakufa kwa kiroho cha korosho nyie watu! na mnao mpiga majungu huyo chinga wa watu!! atawasaidia tough! siku moja! mpaka myambe kifukuto! sijui sura zenu mtazificha wapi!

kuna mtu hasa Miafrica anakusaidia leo! ukinawili tu! anaanza chuki! mpaka ina fika mahali inakuwa kero! ndo km ivi sasa!!! Mondi aache kubeba!! beba watu km hawezi kuwavumilia wanapoondoka kwake, ya nini sasa?? umepata. wamepata shida iko wapi!

Mungu atawapa pa kutokea tu! na yeye Mond si Mungu, uone km na yeye hajafa kimuziki!! watu wanakuja kwako na nyota zao zinawaka hivi! na kweli unapaa!! wape msingi wajitegemee!

fanya piga bonge la sherehe ya siku ya kuondoka kwao! waombe msamaha km umewakwaza! wakaribishe tena nyumbani siku wakiona si salama kwao kimuziki! km wanao!! hapo sasa uone km utaanguka kimuziki! Daima dumu utasimama!

Mie ni shabiki wa Diamond kuliko huyo makonde lkn hapa nasema ukweli! lkn mjue fika kuwa Maisha haya hayatabiriki kamwe!! sema saaana leo!!! lkn kesho utabisha hodi kwa chinga na njaa kali ya mwaka inakuuma! ...sijui utakula kwanza ...au utasali kwanza!!

Hii Dunia ya Mungu ikanyage kwa Adabu!! ningekuwa chinga ningefanya kazi mara dufu, then piga kimya tu!
 
ukimsikiliza harmonize vizuri,yeye hakulalamika kwenye media kulipa mil 500 au hizo 600 (alikua anatambua mkataba wake) ila ni fitina zinazoendelea za chini kwa chini za WCB kuhakikisha wanampka matope na kuhalibu fan base wa mziki wake...same kama alikiba alivyowai kulalamika -INAONEKANA WCB WANAHII MICHEZO
 
mkuu kwa sasa sidhani kama wcb wana umia roho labda mashabiki ila diamodnd roho inamsuta kwa pesa ambayo kamtemesha harmonize katika hali ambayo sio fair yaani kama kamdhulumu may be kashamaliza iyo pesa kununua ndinga na hanasa nyingine sasa hapa anafuta ule utu kama alimsaidia hana nguvu tena


harmonize ndo ana kinyongo na wamuache atoe ya moyoni maana ile pesa ni ndefu karudi nyuma kimtindo kiuchumi
 
Mond! ange kuwa fair tu!! hela hiyo angepiga pasu kwa pasu! halafu wangepiga bonge la show moja matata sana! la kumtakia dogo maisha mema Harmonize! basi! amekaa nae kijana nyota imewawakia wote!!

aondoke kwa uzuri tu! wamepaa wote kiuchumi! safi!!..... inaonekana Chinga ana nyota kimuziki! mapato yalipaa!! Mondi asipotezee hii!

hivi Kampuni la muziki kubwa hivi!! halina washauri watu wazima???

hata wazazi tu!! wange fanya hii shughuli...
 
Lini diamond alisema harmonize ni mtumwa wake
Matendo. Ukimsikiliza ktk interview zake utagundua ni mtu mbinafsi. Ana ego sana. Hapendi wengine wafanikiwe anataka awe yy tu. Kwa nje Ni mtu mzuri lkn gizani/ndani anapambana sana kuwashusha wenzake.
 
Ukiambiwa ulete ushahidi wa himi ukisemacho utaleta?
Je hao waliomshawishi atoke ni akina nani? wataje
 
Ni mwandishi wa habari za sanaa katika Gazeti japo Sikumbuki ni lipi
Katikati ya 2017 nilimjua kupitia gazeti la KIU ila nowdays yuko MWANANCHI.kule KIU sijajua maana kipindi nipo skuli nililipata hilo gazeti kwa urahisi ila nowdays mpk niingie town.

Huyu bwana ni ANAJUA sana sijui kwa nn media hazimchukui yaani
 
Kumbe Magufuli kafa kwa mengi sana.
 
Ni tendo la kukubaliana na anachosema mhusika! Ndio maana hata watu wakipatana hupeana mikono. Kwa muktadha wa tukio husika Harmo angekubali kutoa mkono angetangaza vita rasmi Mondi
Pia inahusiana na kuchukua nyota yako. Huu ipo sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…