Hassan Mwakinyo apoteza kwa T.K.O dhidi ya Liam Smith | M&S Bank Arena | Liverpool

Hassan Mwakinyo apoteza kwa T.K.O dhidi ya Liam Smith | M&S Bank Arena | Liverpool

Greatest Of All Time

JF-Expert Member
Joined
Jan 1, 2017
Posts
23,620
Reaction score
52,790
Mabibi na mabwana, usiku wa leo kwa masaa ya Afrika Mashariki, Bondia mtanzania, Hassan Mwakinyo atakuwa anapambana na bondia Liam Smith katika dimba la M&S Bank Arena huko jijini Liverpool.

Liam Smith ana umri wa miaka 33 huku Mwakinyo akiwa na miaka 27.

Pambano hilo limekuja muda muafaka mara baada ya Mwakinyo kuwa nje ya ulingo kwa muda mrefu.

Liam Smith amepoteza mapambano matatu tu katika career yake ya masumbwi.

Yote kwa yote, tunamtakia heri Mtanzania mwezetu Mwakinyo aibuke na ushindi na kuendelea kuitangaza vema nchi yetu.

Tukutane hapahapa jukwaani kwanzia saa 3:00 usiku kwa live updates

Pambano litakuwa mbashara Azam Sports 1HD
88ADC0B8-5034-4AE4-83FA-8E2A73E8AE4E.jpeg

====

BONDIA MWAKINYO APIGWA TKO

Bondia Hassan Mwakinyo amepoteza pambano dhidi ya Liam Smith baada ya kupigwa kwa TKO

Pambano hilo lililokuwa na mizunguko 12 limeishia mzunguko wa 4 baada ya Mwakinyo kupiga goti wakati pambano likiendelea



MWAKINYO: WALINIPA VIATU VILIVYOKUWA VINANIUMIZA KIFUNDO CHA MGUU

Baada ya kupoteza pambano lake dhidi ya Liam Smith, Bondia Hassan Mwakinyo ameelezea kilichotokea huku akisema yupo tayari kurudiana na mpinzani wake

Amesema alipoteza begi lake alipokuwa Uwanja wa Ndege, hivyo ilibidi Wenyeji wake wampatie viatu vingine ambavyo vilikuwa vinamfinya na kumuumiza Kifundo cha Mguu

Amesema wakati wa pambano alipokuwa anakabiliana na hali hiyo ilibidi ateme 'MouthGuard' maana Sheria za Boxing zinasema Refa anatakiwa amsimamishe mpinzani na kuliuza nini kinaendelea

Ameongeza "Aliniuliza kama naweza kuendelea, nilimjibu naweza kuendelea lakini viatu vilizidi kuniumiza Kifundo cha Mguu nikaa chini lakini mpinzani akaendelea kunipiga na pamabano likaisha hapo"


 
Kama Mandonga hirizi yake hakuisahau nyumbani wakati wa kuondoka kwenda UK basi ni lazima Mzungu alambe sakafu asubuhi tu.
 
Kila la heri ila inatakiwa awe makini yule bondia ni mzoefu halafu ni sugu katika hayo mapambano aliyopigwa lipo na lile alilopigana na Canelo sasa fikiria mtu mpaka kapambana na Canelo c mchezo
You need to fight THE BEST to become THE BEST

Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom