Hata tukifuzu kwa mazingaombwe hatuna timu ya kupeleka AFCON 2023

Hata tukifuzu kwa mazingaombwe hatuna timu ya kupeleka AFCON 2023

SAYVILLE

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
7,895
Reaction score
12,975
AFCON inatarajiwa kuanza huko Ivory Coast chini ya miezi 4 kutoka sasa. Unaenda kutafuta mechi ya ushindi lakini mategemeo yako ni kina Boko ambao hawajacheza mechi ya ushindani kitambo sana maana tayari wameonekana ni liability katika timu pamoja na kwamba kuna viongozi pale Simba wanamkingia kifua. Una Mbwana Samatta ambaye naye wote hata wasiojua mpira wanaona ni mzigo pale uwanjani. Kuna Msuva ambaye pamoja na kwamba amekuwa na bahati ya kuipatia magoli Stars ila naye ni machachari ila siyo hatari. Hawa ndiyo tunategemea kuwapeleka huko Ivory Coast maana usitegemee waachwe wakati ndiyo wanaonekana walioivusha timu. Wengine ndiyo kina Mzize, yaani ni masikitiko makubwa.

Halafu kuna ahadi ya yale mamilioni kama watafuzu. Unajiuliza hizo pesa zitagawanywaje kama wachezaji wanabadilishwa kila siku. Kuna waliopambana katika mechi za nyuma ili hata timu leo iwe na matumaini ila leo hii hawapo kwenye kikosi, kuna wengine wameitwa kwa mechi ya leo ila kwenye mapambano ya nyuma hawakuwepo wala kuonekana kama wana faida. Cameroon waliahidiwa nyumba walipofanya vizuri kombe la dunia 1990 ila imechukua miaka 30 kupewa hizo nyumba na sababu moja ya kuchelewa ilikuwa chama cha soka cha kule walipeleka majina ya wachezaji 44 wanaotakiwa kupewa nyumba badala ya wachezaji 22 ambao hasa ndiyo walikuwepo kwenye kombe la dunia. Toka 1990 wamekuja kupewa hizo nyumba 2020. Ngoja tuone.

Tukifungwa, tena tufungwe goli nyingi itatupunguzia visirani, rushwa na mengineyo. Itatusaidia pia kujenga utaratibu wa uwajibikaji katoka football siyo huu ujinga.
 
Mzize amewekwa kujaribu bahati na kumuondolea lawama kocha aonekane alijaribu silaha zote.

Ila Mzize ndio namashaka naye sana sijui lakini huwenda akatu-surprise kwa kufanya makubwa.
 
Mzize amewekwa kujaribu bahati na kumuondolea lawama kocha aonekane alijaribu silaha zote.

Ila Mzize ndio namashaka naye sana sijui lakini huwenda akatu-surprise kwa kufanya makubwa.
Ndiyo maana wanafanya mambo kisirisiri wakati timu ya taifa inabidi mambo yawe wazi, kuanzia uchaguzi wa wachezaji hadi maandalizi yake. Kuna watu wameona kwa sababu wana gundu wakiweka mikono yao katika timu basi wote tuwekwe mbali wafanye wanavyotaka bila kuwajibishwa.
 
Ndiyo maana wanafanya mambo kisirisiri wakati timu ya taifa inabidi mambo yawe wazi, kuanzia uchaguzi wa wachezaji hadi maandalizi yake. Kuna watu wameona kwa sababu wana gundu wakiweka mikono yao katika timu basi wote tuwekwe mbali wafanye wanavyotaka bila kuwajibishwa.
Lakini kwenye timu ya Taifa kuna muda TFF hawawezi kuepuka lawama.

Ingawa ni kweli tuna uhaba wa wachezaji bora wakuweza kutupambania kwenye michuano mikubwa ila kuna baadhi ya vitu tuna felishwa na TFF.
 
Lakini kwenye timu ya Taifa kuna muda TFF hawawezi kuepuka lawama.

Ingawa ni kweli tuna uhaba wa wachezaji bora wakuweza kutupambania kwenye michuano mikubwa ila kuna baadhi ya vitu tuna felishwa na TFF.
Ndiyo shida ya kuweka siasa kwenye mpira, mwisho wake unakuwa siyo mzuri na unafanana hivi. Hawafanyi mambo kwa weledi wa kimpira bali kufurahisha watu fulani
 
AFCON inatarajiwa kuanza huko Ivory Coast chini ya miezi 4 kutoka sasa. Unaenda kutafuta mechi ya ushindi lakini mategemeo yako ni kina Boko ambao hawajacheza mechi ya ushindani kitambo sana maana tayari wameonekana ni liability katika timu pamoja na kwamba kuna viongozi pale Simba wanamkingia kifua. Una Mbwana Samatta ambaye naye wote hata wasiojua mpira wanaona ni mzigo pale uwanjani. Kuna Msuva ambaye pamoja na kwamba amekuwa na bahati ya kuipatia magoli Stars ila naye ni machachari ila siyo hatari. Hawa ndiyo tunategemea kuwapeleka huko Ivory Coast maana usitegemee waachwe wakati ndiyo wanaonekana walioivusha timu. Wengine ndiyo kina Mzize, yaani ni masikitiko makubwa.

Halafu kuna ahadi ya yale mamilioni kama watafuzu. Unajiuliza hizo pesa zitagawanywaje kama wachezaji wanabadilishwa kila siku. Kuna waliopambana katika mechi za nyuma ili hata timu leo iwe na matumaini ila leo hii hawapo kwenye kikosi, kuna wengine wameitwa kwa mechi ya leo ila kwenye mapambano ya nyuma hawakuwepo wala kuonekana kama wana faida. Cameroon waliahidiwa nyumba walipofanya vizuri kombe la dunia 1990 ila imechukua miaka 30 kupewa hizo nyumba na sababu moja ya kuchelewa ilikuwa chama cha soka cha kule walipeleka majina ya wachezaji 44 wanaotakiwa kupewa nyumba badala ya wachezaji 22 ambao hasa ndiyo walikuwepo kwenye kombe la dunia. Toka 1990 wamekuja kupewa hizo nyumba 2020. Ngoja tuone.

Tukifungwa, tena tufungwe goli nyingi itatupunguzia visirani, rushwa na mengineyo. Itatusaidia pia kujenga utaratibu wa uwajibikaji katoka football siyo huu ujinga.
Lofa wewe...jivunie ulichonacho
 
AFCON inatarajiwa kuanza huko Ivory Coast chini ya miezi 4 kutoka sasa. Unaenda kutafuta mechi ya ushindi lakini mategemeo yako ni kina Boko ambao hawajacheza mechi ya ushindani kitambo sana maana tayari wameonekana ni liability katika timu pamoja na kwamba kuna viongozi pale Simba wanamkingia kifua. Una Mbwana Samatta ambaye naye wote hata wasiojua mpira wanaona ni mzigo pale uwanjani. Kuna Msuva ambaye pamoja na kwamba amekuwa na bahati ya kuipatia magoli Stars ila naye ni machachari ila siyo hatari. Hawa ndiyo tunategemea kuwapeleka huko Ivory Coast maana usitegemee waachwe wakati ndiyo wanaonekana walioivusha timu. Wengine ndiyo kina Mzize, yaani ni masikitiko makubwa.

Halafu kuna ahadi ya yale mamilioni kama watafuzu. Unajiuliza hizo pesa zitagawanywaje kama wachezaji wanabadilishwa kila siku. Kuna waliopambana katika mechi za nyuma ili hata timu leo iwe na matumaini ila leo hii hawapo kwenye kikosi, kuna wengine wameitwa kwa mechi ya leo ila kwenye mapambano ya nyuma hawakuwepo wala kuonekana kama wana faida. Cameroon waliahidiwa nyumba walipofanya vizuri kombe la dunia 1990 ila imechukua miaka 30 kupewa hizo nyumba na sababu moja ya kuchelewa ilikuwa chama cha soka cha kule walipeleka majina ya wachezaji 44 wanaotakiwa kupewa nyumba badala ya wachezaji 22 ambao hasa ndiyo walikuwepo kwenye kombe la dunia. Toka 1990 wamekuja kupewa hizo nyumba 2020. Ngoja tuone.

Tukifungwa, tena tufungwe goli nyingi itatupunguzia visirani, rushwa na mengineyo. Itatusaidia pia kujenga utaratibu wa uwajibikaji katoka football siyo huu ujinga.
Aahaaaaa
Wana Simba mnateseka sana

"Tukifungwa, tena tufungwe goli nyingi itatupunguzia visirani, rushwa na mengineyo. Itatusaidia pia kujenga utaratibu wa uwajibikaji katoka football siyo huu ujinga."
 
Football tz haitakua Kwa style hiii, lawama kila Nyuzi kulikoni.
Aahaaaaa
Wana Simba mnateseka sana

"Tukifungwa, tena tufungwe goli nyingi itatupunguzia visirani, rushwa na mengineyo. Itatusaidia pia kujenga utaratibu wa uwajibikaji katoka football siyo huu ujinga."
Kocha jana alifanya kosa moja kubwa la kiufundi kwa kumpanga Msuva ambaye ni juzi tu katoka kusajiliwa na klabu ya Algeria tena kama kwa kuipambania sana fursa hiyo. Jana Msuva asingeweza kuwa na madhara akijua angeweza kujijengea mazingira mabaya ya kazi.

Ndiyo maana hata Niger walivyokuja kucheza na Tanzania walimuweka benchi Adebayor kipindi ambacho tetesi kuwa Simba bado inamtaka zilikuwepo.
 
Lakini kwenye timu ya Taifa kuna muda TFF hawawezi kuepuka lawama.

Ingawa ni kweli tuna uhaba wa wachezaji bora wakuweza kutupambania kwenye michuano mikubwa ila kuna baadhi ya vitu tuna felishwa na TFF.
Uhaba wa wachezaji bora kwa kiasi kikibwa umechangiwa na hizi kanuni za tff za kurundika wachezaji wageni kwenye timu.

We angalia mechi za Simba, Yanga na Azam utaona idadi ya wazawa wanaocheza ni kiduchu mno. Unategemea hapo uwe na strong national team
 
Uhaba wa wachezaji bora kwa kiasi kikibwa umechangiwa na hizi kanuni za tff za kurundika wachezaji wageni kwenye timu.

We angalia mechi za Simba, Yanga na Azam utaona idadi ya wazawa wanaocheza ni kiduchu mno. Unategemea hapo uwe na strong national team
Idadi ya wachezaji wa nje wanaoweza kusajiliwa ipunguzwe au wanaoweza kucheza katika mechi moja ipunguzwe
 
Uhaba wa wachezaji bora kwa kiasi kikibwa umechangiwa na hizi kanuni za tff za kurundika wachezaji wageni kwenye timu.

We angalia mechi za Simba, Yanga na Azam utaona idadi ya wazawa wanaocheza ni kiduchu mno. Unategemea hapo uwe na strong national team
Hili kwangu sioni kama sababu

Kwasababu sifikirii kama kuna mchezaji ambaye anaweza akawa ni bora halafu hizi timu zikamuacha zikaenda kumsajili foreigner.

Otherwise kama unakusudia kuwa hizi timu zitumike kama taasisi za kukuza vipaji.

Zichukue wachezaji kwa lengo la kuwakuza na wakati huo huo hizo timu zinataka mafanikio kimataifa.
 
Hili kwangu sioni kama sababu

Kwasababu sifikirii kama kuna mchezaji ambaye anaweza akawa ni bora halafu hizi timu zikamuacha zikaenda kumsajili foreigner.

Otherwise kama unakusudia kuwa hizi timu zitumike kama taasisi za kukuza vipaji.

Zichukue wachezaji kwa lengo la kuwakuza na wakati huo huo hizo timu zinataka mafanikio kimataifa.
Hapa nakupinga mkuu Tanzania tunahusudu sana wachezaji wa kigeni
 
Back
Top Bottom