Unajua sijuagi kwanini watu hawataki wakulima wanufaika na kazi za jasho lao?
Mimi ni mwalimu nadhani hatutofautiani sana na hawa wenzetu wakulima
Yaani wanavyokandamizwa wakulima ndivyo na walimu tunavyokanyagiwa na hii awamu.
Mkulima anapelekeshwa hatakiwi kupata faida akipandisha bei ya bidhaa yake hata kwa msimu tu kelele lake na yowe hilo sio la mchezo ukipandisha bei ya mahindi, karubwagira, tembele , nyanya chungu au bamia kila mtu anaona kaonewa kama vile walimu yaani hamna posho ya chakula, wala makazi wala ya wenzi wala uniforms. Kibaya zaidi huku hata ukijiendeleza sijui Masters sijui PhD unaambiwa unajifurahisha haina acknowledge yoyote wala daraja.
Tunaimbiwa wimbo mzuri (waziri mkubwa) kuwa kuna bodi ya mishahara itamaliza tofauti na kibaya zaidi Mkuu kashasema hata yeye mshahara haumtoshi. Sasa kama wa 9mil haumtoshi pamoja na subsidy zote je Sisi wa 350K utatushea wapi minus subsidy?
Wakulima na Sisi walimu nadhani ni wahanga kuntu wa hii awamu!!!