Hatari ya kuongezeka kwa mawazo ya kijamaa, hatamu za kiuchumi kushikiliwa na serikali

Hatari ya kuongezeka kwa mawazo ya kijamaa, hatamu za kiuchumi kushikiliwa na serikali

24 February 2024
Mwanza, Tanzania

CPA AMOS MAKALLA KATIKA KIKAO KIZITO NA WAFANYABISHARA WA SUKARI MKOANI MWANZA

RC MAKALLA: MWANZA TUMEPOKEA SUKARI TANI 255


View: https://m.youtube.com/watch?v=m2KFLB1Rfxk

Mkuu wa mkoa CPA Amos Makalla asikiliza hali ngumu ya sukari kutoka kwa wasafirishaji, wagavi na wenye maghala.

Amos Makalla serikali imetoa kibali na mkoa wa Mwanza umepojea tani 255 ingawa bado kuna foleni kubwa kwa SHAH muuzaji maarufu wa mjini Mwanza ...

CPA Amos Makalla asema bei elekezi ya Serikali Jumla ni shs 2650 hadi 2800 na rejareja ni shs. 2800 hadi Shs. 3000

Awahimiza Wakuu wa Wilaya na Maafisa Biashara kushirikiana kufuatilia bei sahihi. Aahidi kufuatilia bei ya Sukari wakati wa ziara yake Majimboni kuanzia Machi 2024 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.CPA Makalla leo Februari 26, 2024 wakati akiwa na kikao kizito kilichojumuisha wakuu wa wilaya, wafanyabiashara na wasambazaji wa sukari mkoani humo na kutangaza rasmi ujio wa tani 254.5 wa bidhaa hiyo na kusisitiza uzingatiaji wa bei elekezi ya Serikali.

Akizungumza nao kwenye ukumbi wa Ofisi ya mkuu wa Mkoa, CPA Makalla amesema kwa mujibu wa maelekezo ya Serikali bei ya Jumla itakuwa Tshs 2650 hadi 2800 na Rejareja ni Tshs 2800 hadi 3000 na kusisitiza bei hiyo itaendelea hadi viwanda vya sukari nchini vitakapo rejea katika uzalishaji wao wa kawaida.

CPA Makalla akaongeza kwa kusema "Ndugu zangu nimewaita hapa wote tunafahamu upungufu wa sukari uliojitokeza nchini kwetu, Serikali imetoa tangazo namba 40 b ya amri ya bei elekezi ya sukari naomba sana tuzingatie hilo ili kuwaondolea usumbufu wananchi wetu", amesisitiza CPA Makalla wakati akizungumza na wadau hao wa sukari.

Aidha, amewataka Wakuu wa Wilaya na Maafisa biashara kushirikiana kufuatilia usahihi wa bei ya sukari kwa muda wote ambao bidhaa hiyo itakuwa inauzwa dukani."Kuanzia Machi 4, 2024 nitaanza ziara ya kusikiliza kero za wananchi Majimboni na kipaumbele cha kwanza nitawauliza wananchi sukari wananunua kwa bei gani nikisikia tofauti nitajua viongozi hamkutimiza wajibu wenu."

"Tunashukuru kwa uamuzi huu wa Serikali wa kutoa vibali kwa wafanyabiashara kuagiza kutoka nje, hii inatupa unafuu sisi wafanyabiashara kuepuka malalamiko kutoka kwa walaji," Joyce Maduhu, msambazaji wa sukari.

Hivi karibuni Waziri wa nchi Ofisi ya Rais,TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa alitoa maelekezo kwa Wakuu wote wa Mikoa kuhakikisha wanasimamia bei elekezi ya Sukari baada ya bidhaa hiyo nyeti kupanda bei sana kutokana na upatikanaji wake kuwa mdogo na mahitaji kuwa makubwa

Source : MWANZA RS TV
 
Kwenye Sukari lengo ni kulinda Viwanda vya Ndani hata kama Viwanda hivyo havitoshelezi.
Viwanda vyetu vimekosa ubunifu.vinazalisha sukari kama ndio zao kuu,lakini viwanda vya Brazil havitegemei sukari katika mapato,vina by products zaidi ya 25 na kufanya bei ya sukari kuwa chini sana.
Hakuna haja ya kuendelea
kuwabeba wavivu hao ni mzigo kwa taifa,haswa mtumiaji wa sukari.
Ndio maana wameendelea kutuhadaa na upovu wao katika ubunifu wa viwanda vya miwa wakiogopa na kumzibia Brazil asijenge viwanda vyake hapa.
Kwa waziri Bashe,siku zao zimehesabika sio watu wakuhurumia hata kidogo ni sawa na wahujumu uchumi.
 
Viwanda vyetu vimekosa ubunifu.vinazalisha sukari kama ndio zao kuu,lakini viwanda vya Brazil havitegemei sukari katika mapato,vina by products zaidi ya 25 na kufanya bei ya sukari kuwa chini sana.

Hapo umetupatia habari za ziada kuhusu viwanda vyetu na wanaovimiliki Tanzania kushindwa kuwa wabunifu na kugeuka kuwa machinga wa kuuza sukari kutoka nje baada ya kupewa vibali na serikali.
 
Yesu alikuwa mjamaa na mtume Muhammad alikuwa mjamaa. Mawazo ya kijamaa hayajawahi, na hayawezi kuwa hatari.

Shetani anatumia nguvu sana kuwaaminisha hivyo.
Embu watueleze kama ujamaa ndio shida je... ubepari tulokumbatia kipindi chote umetufanya matajiri?
 
Hapo umetupatia habari za ziada kuhusu viwanda vyetu na wanaovimiliki Tanzania kushindwa kuwa wabunifu na kugeuka kuwa machinga wa kuuza sukari kutoka nje baada ya kupewa vibali na serikali.
Yaani kiwanda kimmoja cha miwa kingeweza kuzalisha by produts zaidi ya 25 kingeingiza mapato mengi,ajira nyingi na bei ndogo sana ya zao la sukari.By product mmoja wapo maarufu ni ethanol inayochanganywa na petrol kuedeshea magari.
Wakisikia Brazil antaka kupanda ndege kuja kuwekeza miwa Bongo wanasali uhamiaji amyime visa au TIC amkatae.
Viwanda vyetu vya miwa ni mzigo kwa mtumiaji wa sukari.
 
24 March 2024
Arusha, Tanzania

GAVANA ATANGAZA KIAMA JULAI 1 2024 WANAOBADILISHA DOLA MTAANI,HOTELI ZOTE ZICHUKUE LESENI

View: https://m.youtube.com/watch?v=-t5MfXr89I4

Gavana wa Benki Kuu Emmanuel Tutuba ametangaza leo alipokutana na wadau mjini Arusha ...

Gavana wa Benki kuu asema takwimu za nakisi ya Balance of Payment deficit ya import and export mwaka 2022 ilikuwa na nakisi ya 5.3 biliioni UDS Dollars na sasa hadi December 2023 nakisi imepungua hadi 2.7 Bilioni USD dollars ....
 
Back
Top Bottom