Hatimae hukumu imetoka tayari, siku ya kwanza tu ya kesi kusikilizwa

Hatimae hukumu imetoka tayari, siku ya kwanza tu ya kesi kusikilizwa

Hapo naomba unifafanulie kidogo mkuu, maana tumesha saini hukumu, japo baada ya 45 days itakaziwa rasmi. Je una maanisha kuna uwezekano mdai akakata rufaa kupinga matakwa yake mwenyewe? Kwamba alitaka taraka na sasa hataki??

Kwa Sababu alibaki anaweza tengeneza mazingira Kaka then mkarudi kwenye usuluhishi, trust me, either way Bro, nakupongeza, you have nothing to lose! Usikubali kesi, wala mazungumzo, na Kama akisema kabadili mawazo, ondoka kaa kimya tena hivyo hivyo!

Nakutia moyo Kaka, Umefanya jambo sahihi sana la kukukomboa na drama za huyo Shemeji yetu wa hovyo, at this stage you have nothing, I repeat again nothing to lose!
 
Ilinipa wakat mgumu sana kukubaki ukweli na uhalisia. Sikua nimetarajia. Ikanipa tabu

Yahp, alifikiri hivyo, na nili notice hilo kwenye session

Sijui kwann huwa hawafikirii kuwa wanatazamwaje na wanaodhan wanawahitaji. Kama umeweza mfanyia mwanaume mwenzake hiv , ataanzaje kukukuamini kuwa huwez mfanyia na yeye??

Shukran mkuu. Ila kuhusu wao kunitafuta sidhani. Wale ni viburi mnoo. Wana ego za hatari. Kilichotufkkisha hapa na wife n ego yake tu, nilikua tayar kumsamehe nkkawa nambembeleza
Ni kabila gani huyo wife wako?
 
Moja kati ya uzi wenye mengi ya kujifunza , tunakushukuru sana mleta mada kwa kutushirikisha.

Kwanza kabisa ni neno la faraja kwako , pole.
Pili neno la pongezi kwako, hongera sana.

Ukisoma maoni ya wengi kwenye uzi huu toka maoni ya kwanza hadi sasa lawama nyingi zinaelekezwa kwa mwanamke na kuonyesha ile maana ya maisha ya pamoja kati ya mwanamke na mwanaume haipo tena.

Ukweli hio maana au ule umuhimi haupo tena na si kwa sababu ya mwanamke pekee hadi sisi wanaume.

Binafsi naamini nature imemfanya mwanaume kuwa kama kiongozi kwenye familia au mahusiano tunayoweza kuyaita ndoa.

Inapotokea hayo mahusiano yanakuwa isivyo kawaida yule aliye kiongozi kuna sehemu ameshindwa kusimama katika nafasi yake.

Si zungumzii mume tu bali hata baba .
Kuna namna imefanywa mwanamke hakupaswa kutoka mikono mwa mwanaume kwa karibu kipindi chake chote, ata toka kwa baba atakuwa kwsa mume.

Sasa mwanamke anapo kosea sambamba na kumlaumu lakini tujiulize nasi kama waanaaume tumeweza kusimama katika nafasi yetu.



Maoni ya wengi kwenye uzi huu yamekubaliana na kauli iliyopo sasa ya kukataa ndoa, wengi walio toa maoni haikosi robo walio kwenye ndoa,

Na kama kuna yoyote aliye kwenye familia ama ndoa ambaye yupo na watoto, nadhani wanafahamu fika mtoto atakavyo kuwa mwaathika wa kwanza endapo kutakuwa na mgogoro .

Kuwa hio inapofika wakati wa mgogoro kama sababu hazikidhi haja heri kuvumilia kwa ajili ya nusura ya watoto...


Nadhani pia kuwepo na namna sauti ya mwanaume ipaaazwe serikali na watunga sera na watu wa dini waone namna ya kubadilisaha hizo sheria zinazo husu mambo ya ndoa na mahusiano.

Maisha ya mwanaume ni magumu sana , tokea siku ile anaitwa mwanaume ni mtu asie hitajika na dunia, anaye kandamizwa kwa kila namna na ambaye hatakiwi kuonewa huruma hadi siku ile atakapo rudi kwenye ardhi.

Embu watusaidie hao watu maana dunia imetuelemea mno, embu wafanye tu inavyo wezekana mwanaume nae asikilizwe.


Pia wanaume wenzangu kwenye kuijenga familia na ustawi wake , tufikirie kuwa na mji wa pili usiohusiana kabisa na familia,hii inaweza kusaidi inapotokea hali kama hii, au huko uzeeni watoto na mama yao watakavyo kosa umuhimu wako uwe na sehemu ya kwenda kuvutia faraja.
 
Picha lilipoanza ulionyesha ni jamaa Lia Lia + kulalamika .

Demu utombewe, ukute na picha za utupu, alafu wee ndio ulielie.

Anyway , X Mkeo alijua utazungusha suala la Talaka, Sasa haamini ndo Ivo Kawa mtalikiwa.

Mchepuko wake hawez kumuoa sababu keshazaa watoto wengi, Engine imechoka , na sababu kubwa kabisa ya kutomuoa ni kwamba kashuhudia demu anavunja ndoa yake mwenyewe .

Mwisho, Hongera , kuanza Upya Si ujinga.

Muda mfupi ujao, jiandae Ndugu zake na viongozi wa Dini kuanza kukubembeleza.
Pale anapoanza kuonekana mfalme ndio hapa Sasa.
 
Je huyo yf wako alichangia katika kuijenga Nyumba ?

Au umeamua kumnufaisha
Siwezi deny mchango wake kwenye ujenzi, lakini ni kwa sehemu ndogo sana, na nina vithibitisho vya kibenki kuhusu kila shilling 5 alioingiza bank, hivyo nimeamua kumnufaisha kwakua sikutaka hili shauri lipite jana liitwe tena aiku nyingine ndio maana nikaamua hivyo
 
Wakuu heshma kwenu.
Habari za jioni.

Nimeona ni vyema kuwa update kuhusu mwenendo wa suala ambalo nilileta hapa jukwaani siku ya jumatatu katika uzi huu 👇👇👇👇


"Samansi" ya mahakama ilielekeza nifike mahamani siku ya leo tarehe 12 Feb 025 nami nikafanya hivyo.
Katika kesi hii mimi kama mdaiwa na aliyekua mke wangu kama mdai.

Niseme tu kitu, katika mfumo wa serikali na personally katika suala hili, nimekuja kugundua, wanawake wame occupy sana nafasi nyingi serikalini, sasa sijui sababu ni nini?
Maana ;
- nilipoitwa dawati, incharge pale alikuwa mwanamke.
  • nilipoitwa baraza, kikao chote kilijawa na wazee wa baraza wanawake
  • leo hii mahakamani, hakimu alikua mwanamke.
Hakika wanawake wametaradadi everywhere, tukiendelea kwa mwendo huu, wanaume twafaaa
😁😁😁😁😁.

Anyway,.

Kama ambavyo nilikua nimeamua kuwa natamani hili suala liishe tu, na pia kwa kuzingatia ushauri wa baadhi yenu ndugu zangu wana JF, sikupemda kesi iwe na mambo mengi.

Tulipoitwa chamber na hakimu, alianza kwa kusema "hii kesi leo mmeitwa ili iweze kutajwa tu na kipangiwa siku nyingine, hivyo, mdaiwa utasomewa tu charges zako kisha kama una neno utatamka"

Akasoma,kama ilivyo ainishwa kwenye "samansi" niliopokea ,kuwa mdai anataka
1. Talaka
2. Mgawanyo wa mali
3. Kuishi na watoto
4. Matunzo ya watoto

Akauliza "unasemaje?"

Nikamjibu, "nimesikia na sina pingamizi juu ya lolote katika hayo, na kwasababu sina pingamizi naomba mahakama kama inaweza, hili suala tulimalize hapa hapa na leo leo mheshimiwa hakimu"

Akauliza "umekubaliana na haya yote?"

Nikamjibu "ndiyo, nakubaliana na dai lake la talaka, pia nakubaliana na dai la mgawanyo wa mali, japo nitaomba kujua muongozo wa mahakama unasemaje kuhusu hilo , pia muongozo wa mahakama unasema nini kuhusu matunzo ya watoto na kuishi ma watoto, maana yote niko tayari ku comply"

Akasema "kama ni hivyo, basi hii kesi ni nyepesi na itakwenda vizuri, kuhusu mgawanyo wa mali, mahakama ina suggest 50% 50%, unless kama kama mmoja wenu hajaridhika na mtahitaji tuingie katika ushahidi wa kuthibitisha mchango wa kila mmoja kwa vithibitisho.

Pia matunzo ya watoto yamejikita katika chakula, malazi, afya, na ada. Jukumu hili ni la baba kikawaida, lakini mahakama inaangalia kama mama naye anajiweza, basi jukumu hili wote mtagawana.

Na mwisho kuhusu kuishi na watoto, maadam wako chini ya miaka 18, wataishi na mama, ila baba una ruhusa ya kuwaona . Kama unahama mkoa, maana yake watoto watakuja kwako likizo ambapo, mama atagharamia nauli za kwenda likizo na baba atagharamia nauli za kurudi.

Hivyo basi , ndugu mdai nitakuuliza na utajibu hoja moja baada ya nyingine.

1. Talaka.

Hapa nikawaambia sina pingamizi, niko tayari mke wangu apewe haki yale kama anavyo hitaji. Hapo, wife nikaona kashusha pumzi ndedu nzito. Na muda mwingi alikua anajifuta jasho ingawa ndani pana feni. Katika session yote honestly, sikumtazama usoni. Na hatukusalimiana.

2. Mgawanyo wa mali.

Nikasema, kwakua kesi hii imeshanigharimu suala la muda , nakubaliana na pendekezo la mahakama la fifty fifty, kama mwenzagu, mdai anaona amebanwa naomba apewe uhuru wa kuchagua ratio itayompa comfort. Akasema mimi nataka 60%. Hakimu akauliza, mdaiwa (mimi yani) uko tayari, nikasema SINA PINGAMIZI, mahakama impe hiyo 60% anayotaka.

3. Matunzo ya watoto

Hapa nikasema, always nimekua nalipa ada miaka yote, hivyo hili nitae delea nalo, na pia nitawahudumia gharama ya chakula isiyozidi 150,000/= kwa mwezi kwa kuanzia kwasababu, suala hili limeniathiri biashara zangu pia nahitaji ku settle na kuanza upya maisha, hivyo nikitulia nita adjust.

4. Kuishi na watoto.

Nikasema, nakubaliana na pendekezo la mahakama hapo juu.

Hakimu akasema, aisee, hii kesi imeemda vizuri sana.

Wife akaomba "mheshimiwa naomba kidogo niongee na baba .... pembeni, kuhusu suala la mgawanyo wa mali"

Nikajibu "hakimu, sihitaji kuzungumza private , maana sioni kama kuna suala lolote ambalo kwasasa naweza ongea nae tukaelewana, kama ana jambo lolote aliseme hapa mbele yako"

Wife muda woote alikua anafuta jasho sijui maana yake ni nini, lakini katika vitu naamini, ni kwamba alitegemea confrontation na mimi labda nimuwekee kauzibe na vikwazo vya kukubali ombi la talaka, lakini akaona kila kitu nimekubaliana nae kama alivyotaka. Na kila alipotaka kuibua malalamiko, hakimu akawa anasema, naomba tusiguse sababu za mgogoro wenu kwakua sio sehemu ya madai yako mdai, yote uliyodai, tujikite hapo.

Hakim, akayasoma maandishi aliyoandika kisha akaita kila mtu asaini, nikasaini na yeye akasaini, lakini anaposaini akawa anajilalamisha chini chini, hata sijui anaongea nini.

Basi baada ya hapo tukaambiwa , baada ya siku 45 hati ya talaka itatoka na taratibu za utathmini zitaanza, hivyo tutakiwa kufika.

PIa nikatumia fursa hiyo kueleza kuhusu uharibu wa wa wizi uliotokea nyumbani kuonyesha RB ili ifahamike kuwa mali imeharibiwa na wezi.

Pia , ikafamika pale katika shauri kuwa mimi nilishahama nyumbani, na hii nikaona imem suprise mdai wangu, na sijui sababu ni nini!.

Baada ya yote, hakimu, akasema tumemaliza.
Nikanyanyuka na kutoka, japo niliona yf anaaga huku amekaa ana delay kutoka, like she was exhausted with the proceeding that ended.

Sijajua sasa kama walikua wanayapanga yao mengine au lah!!

Ikaisha hivyo.

Sasa baada ya siku ya 45 days ndio mengine yatafuata.
Kifupi nimefurahi hili suala halijawa extended, ngoma imeitwa leo na imetamatika leo, maana wengi walikua wanasema hii kitu inaweza ikaenda 2 months.

ADDITION:
Wakuu, kesi za kuvunjika ndoa ni nyingi sanaa nimekuatana nazo leo mahakamani. Hali sio nzuri kwenye hii taasisi ya kwanza kuanzishwa duniani

SHUKRANI WAKUU.
Usiku mwema
Hongera brother
 
Back
Top Bottom