Hatimae nimeamua kuandika kitabu kuhusu mtindo wa maisha ya watu wa mikoa ya Kusini mwa Tanzania

Shida hujui, kusini Wanawake wanachezwa unyago wa Watu wa kusini ni tofauti na wazaramo, mzaramo anachezwa mara Moja akivunja ungo.

Kusini vinaenda unyagoni watoto wadogo wasizidi miaka 7 hakuna kitu chochote kinachofundishwa kuhusu ngono au mapenzi.

Mafundo yote Binti anayapata akizaa mtoto wa 1 kwanza au akichumbiwa.

Swala la watoto kujihusisha na ngono ni janga la maeneo mengi hasa vijijini.
 
Kuna vitu viwili jamii ya watu wa kusini wanafanya au jamii za kiyao.

Msondo, hapa ndo wanawacheza watoto wadogo, mambo wanayofundishwa ni namna ya kufanya mapenzi, usafi wa mwili, Etc

Unyago, hapa wanawacheza mabinti wakubwa na tayari wameshavunja ungo, wanafundishwa namna ya kulea mume, maisha ya ndoa, ujauzito, etc.

Ndo maana mtoto wa 13yrs tayari anajua kila kitu ktk mapenzi na anakua ktk mahusiano.

Ngono inaabudiwa sana ktk jamii hizo, mtoto wa kiume wa 12 yrs akitoka jandoni anatafuta mtoto wa kike wa 10 yrs wanafanya ufuska na wazazi wanajua, tena wanaona fahari.
 
Sidhani binafsi nimepitia unyago nikiwa na miaka 6 . Sijaona mahala tulipofundishwa ngono.
 
Watoto wadogo kuwa na wapenzi, kuoa na kuolewa.
Tena wazazi wanalipia mahari.
Duh watoto wa kiume wanao wakiwa na umri gani. Na watoto wa kike wanaolewa wakiwa na umri gani?
 
cocastic kwa bahati nzuri wenzako tumefanya utafiti kuhusu mila na desturi za akinamama mikoa ya Lindi na Mtwara (late 80s). Tunafahamu kitu inaitwa unyago, unyao etc. Mtoto wa kike kusema za ukweli huwa anafundishwa kutokana na umri wake na nini anategemea kukutana nacho. Mtoto wa kike kabla ya kuvunja ungo atapelekwa unyago ili ajiandae na MP na kuelezwa nini anategemea, atafanya nini na hatari zilizo mbele yake.

Binti akifika umri wa kuolewa atapata mafunzo jinsi ya kuhandle mwanaume etc, akiwa na mimba anachezwa ili afundishwe jinsi ya kulea mimba, atakapojifungua afanye nini ili kumlidhisha mwanaume ili asimbemende mtoto; jinsi ya kupanua nyonga ili mtoto asije kukwama wakati wa kujifungua (kumbuka Wamasai wao hukataza mama mwenye mimba asinywe maziwa etc ili mtoto asiwe mkubwa akashindwa kupita); jinsi ya kumkomaza mtoto kila asubuhi etc

Kwa bahati mbaya watu wengine huwa hawajui haya masuala. Kuna tofauti kati ya Wamakonde (Patrilineal) na wengineo kama Wamwera, Wayao etc ambao ni Matrilineal = Mwanaume akioa anaenda kukaa kwa wakwe zake na kuatumika (kama manamba). Naachia hapa
 
Hata mie nimeshaishi kwenye jamii hiyo ya watu kanda hiyo ndo nilivyojionea, wala cjatunga.
 
Hii jamii ina taratibu nzuri sana zimenivutia 😄
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…