Teko Modise
JF-Expert Member
- May 20, 2017
- 2,331
- 7,733
Bojan Krkic Perez, mzaliwa wa Catalunya, Spain miaka 32 iliyopita hatmaye ametangaza kusatafu kabumbu.
Bojan ambaye akiwa katika shule ya soka (akademi) ya Barcelona (La Masia) alikuwa anatajwa kama mrithi wa Messi au Messi ajaye.
Alikuwa anacheza kama mshambuliaji au winga, kutokana na uwezo mkubwa aliouonyesha huko La Masia, akapandishwa timu ya wakubww kwa haraka mwaka 2007 na alidumu mpaka mwaka 2011 huku akicheza na role model wake Lionel Messi kikosini.
Miaka ikasogea, Bojan hakuwa yule tena aliyetabiriwa makubwa, akajikuta anaondoka Barcelona mara baada ya kupata muda mchache wa kucheza. Akazurura kwenye vilabu vingi Ulaya kikiwemo Stoke City FC.
Baadae akatimkia zake Canada kabla ya kwenda Japan na kisha kustaafu. Wachambuzi wengi wa soka wanashangaa mpaka leo ni namna gani Bojan alishindwa kufikia matarajio ya wengi. Ni kama ilivyotokea kwa akina Jack Wilshere, Dele Alli, Tom Cleverley na wengineo na ndio imetokea kwa Bojan.
Anastaafu soka huku akimuacha role model wake akiendelea kusakata kabumbu🤣🤣
Adios Amigo Bojan👋🏼
Bojan ambaye akiwa katika shule ya soka (akademi) ya Barcelona (La Masia) alikuwa anatajwa kama mrithi wa Messi au Messi ajaye.
Alikuwa anacheza kama mshambuliaji au winga, kutokana na uwezo mkubwa aliouonyesha huko La Masia, akapandishwa timu ya wakubww kwa haraka mwaka 2007 na alidumu mpaka mwaka 2011 huku akicheza na role model wake Lionel Messi kikosini.
Miaka ikasogea, Bojan hakuwa yule tena aliyetabiriwa makubwa, akajikuta anaondoka Barcelona mara baada ya kupata muda mchache wa kucheza. Akazurura kwenye vilabu vingi Ulaya kikiwemo Stoke City FC.
Baadae akatimkia zake Canada kabla ya kwenda Japan na kisha kustaafu. Wachambuzi wengi wa soka wanashangaa mpaka leo ni namna gani Bojan alishindwa kufikia matarajio ya wengi. Ni kama ilivyotokea kwa akina Jack Wilshere, Dele Alli, Tom Cleverley na wengineo na ndio imetokea kwa Bojan.
Anastaafu soka huku akimuacha role model wake akiendelea kusakata kabumbu🤣🤣
Adios Amigo Bojan👋🏼