Tetesi: Hatimaye "Chato International Airport" kuzinduliwa rasmi mwezi Aprili

Tetesi: Hatimaye "Chato International Airport" kuzinduliwa rasmi mwezi Aprili

Mnaweza kuweka uchambuzi mzuri sana ila ukakosa mashiko kwa kuwa tu una lengo la kiitikadi zaidi.

Mimi huwa najiuliza, je suppose tungechagua huko, kwa bahati mbaya sana umeshindwa kujiendesha wenyewe mkaamua kuturudishia walewale waliokimbia huku baada ya kukatwa je mngeweza kutujengea nchi kweli?, au mngeishia kuandika uchambuzi kama huu wakati mkishuhudia barabara ya Chalinze-Moshi ikiwekwa 4 ways, na kiwanja kama hicho cha chato kikijengwa Hai au Monduli?

Maana wenzetu wa upinzani mmekuwa mabingwa ya kuchambua msivyoviweza, mmekuwa wazuri theoretically but you are not practically oriented, mambo yenu mengi yanakwenda kinyume lakini kwa vile kafanya yule, basi you keep quite kama vile hamuoni huku ukisubiri uongee likifanyika upande wa pili.

Kaskazini ilijengeka mapema kwavile watu wa kaskazini walipata fursa, wakakumbuka kwao ili wapate kwenda mapumzikoni kila mwaka, sasa acha fursa zinapopatikana sehemu zingine basi wazitumie fursa hizo, huku mkiwa wavumilivu mkisubiri 2020 ,
Bravo
 
Najiuliza kwanini tumekataa majina yetu tukakubali ya wazungu na waarabu
Jiureze pia kwanini picha za Yesu na Mtume siyo zenye asili ya ngozi nyeusi na vazi la kiafrika. Na kwanini sula za devils na majini yanakuwa na ngozi nyeusi na sura za kiafrika tu.
 
Kipigi,

Wengine hatuongozwi na itikadi yoyote,ndio maana tunasifia na kutoa changamoto kwa nia njema.

Tulishangilia ujio wa Pangoboi katikati ya matusi na kashfa tele...Wakati huo hukutuona kama "wa kaskazini"!!Sasa tunahoji kwa staha na kwa nia njema unaamua kutupakazia "ukanda"

Mbona wengine hatutoki huko ulikokutaja?Hivi nani wa kuwekewa mshangao?Wewe unayeandika lugha ya kibaguzi au sisi tunaotoa changamoto?

Jenga hoja bila hisia za ukabila na ukada...Wengine hizo hatua tulishazipita!!Ndio maana tunapongeza na kukosoa kwa staha na nidhamu... Jifungue ktk minyororo ya ukada na ukanda, Utakuwa huru kiakili na kifikra
Kuhoji ujenzi kufanyika chato ni ukanda tayari
 
Tatizo lenu mmelewa ulevi wa madaraka, kama suala ni kupata upendeleo mngeanza na mambo ya msingi kwenu kama ugonjwa wa mnyauko wa migomba, awasaidie research na suluhisho mngeondokana na njaa kali mliyonayo sasa.

Basi la Sabuni au Lushanga kwenda Chato halijazi abiria nauli chini ya elfu kumi mtajaza ndege nyie? Tumieni upendeleo huu wa raisi kutoka kwenu awasaidie vya maana sio white elephants.

Hakuna mmiliki wa ndege Chato, hakuna kiwanda zaidi ya ginnery ya ushirika, hakuna hata Hotel pale zaidi ya tule tu Lodge tuchafu nani apande ndege kwenda Chato mtukufu akitoka. Mwanakijiji wa Ilyamchele atapanda ndege?
Ndo kinajengwa sasa,hata ufanyeje
 
Raisi ana akili nyingi sana sasa kwa sababu hamjui malengo yake ku ujenga ule uwanja pale si, kwasababu ni kwake, lengo lake kubwa ni kuwabana wezi wa dhahabu yetu, ni kwamba ndege zote zinazotua migodini itakua marufuku na viwanja vyote vidogo vidogo migodini vitafugwa
 
Sasa ni dhahiri kuwa, kuanzia mwezi Aprili katika mapumziko ya Pasaka, Mkuu wetu atakuwa na uhakika wa kwenda mapumzikoni kwa kutumia uwanja wa ndege mpya wa Chato, yaani Chato Airport.

Kwa sasa uwanja huo unaotegemewa kukamilika mwanzoni mwa mwezi Aprili upo ktk kiwango cha vumbi na unaendelea kufanyiwa matengenezo hadi kiwango cha lami. Tayari ndege ndogo aina ya Beech Craft(King Air) mali ya kampuni binafsi ya TanzanAir imetua kwa mara ya kwanza ktk uwanja wa ndege wa Chato na hivyo kutoa uhakika kuwa sasa Chato inaenda kupokea ndege bila wasiwasi wowote.

Kwa mujibu wa taarifa,uwanja huo una kiwango cha "Aerodrome Reference Code 4D". Hizi "codes" hutolewa na ICAO (International Civil Aviation Organization) kulingana na ubora wa kiwanja kwa kuangalia aina ya ndege zinazoweza kutua, ukubwa wa ndege kwa maana ya uzito na upana wa mabawa.

Codes hizi zipo kuanzia 1A hadi 4F. Hivyo kwa kiwanja kuwa na Code 4D maana yake kimebakiza Code mbili tu kufikia kiwango cha mwisho cha ubora wa viwanja unaotambulika na ICAO.Uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere "Code" yake ni 4E, hivyo uwanja wa Chato upo nyuma ya JNIA kwa "code letter" moja lakini upo sawa kwa "Code number" na JNIA kwa sababu vyote vipo kwenye "Code number 4".

Mfululizo wa "Aerodrome Reference Codes" huanza na 1A, 2B, 3C, 4D, 4E, 4F. Hivyo ni hakika sasa Chato Airport kwa kuwa na "Code 4D" inaenda kuwa moja kati ya viwanja vitatu venye kiwango bora Tanzania ikikaa nyuma ya Julius Nyerere na KIA. Uwanja wa Mwanza ni "Code 4D" hadi hapo ukarabati utakapokamilika utakuwa na sifa ya "Code 4E".

Hatuididimizi dhamira ya Mkuu kujenga kiwanja chenye ubora Chato, bali tunahoji kwa uelewa mdogo tu wa kanuni za Uchumi. Kwamba kiwanja hiki huko Chato kinaweza kuwa na matokeo chanya ya kiuchumi kama ambavyo wangeweza kuboresha uwanja wa ndege wa Mwanza?

Tunauhitaji Uwanja wa Mwanza kuliko ule wa Chato kwa sababu za kiuchumi ktk sekta ya Utalii. Tumekuwa tukilalamika sana kwa mbuga yetu ya Serengeti kukosa watalii wa kutosha kisa njia za usafiri kufika huko zilivyokuwa duni kushinda majirani zetu tunaopakana na mbuga ya Maasai Mara.

Uwanja pekee unaohudumia mbuga ya Serengeti kwa njia ya anga ni "Seronera Aistrip" ambapo huwa busy sana na huchukua ndege ndogo zenye abiria wasiozidi 50. Hii ndio moja kati ya "busiest Airstrip" kwa Tanzania.

Ili ufike Serengeti kupitia uwanja wa KIA unahitaji kutembea kilomita 284 kwa gari toka uwanjani, kwa kupitia uwanja wa ndege wa Arusha inakupasa utembee kwa gari umbali wa kama kilomita 226 wakati kwa kupitia Uwanja wa Mwanza,mtalii anatembea kilomita 166 hadi kufika geti la Ndabaka(?).

Kwa mahesabu hayo,kama ujenzi wa Uwanja wa ndege Serengeti ulishindikana,basi Uwanja wa ndege wa Mwanza ndio suluhisho la haraka ktk kuwafikisha watalii kwa urahisi ktk mbuga hiyo.Tukiusahau uwanja huo na kutazama zaidi ule wa Chato, tunaweza kuhoji dhamira hii ya maendeleo ktk kufika uchumi wa kati. Na kuhoji kwetu kusiababishe "hasira" kwa wenye mamlaka, bali ichukuliwe ni kama changamoto za raia kwa serikali yao.

Ukisefu wa usafiri wa uhakika na hasa ule wa njia ya anga, ndio unatukosesha mapato na kupunguza idadi wa Watalii ktk mbuga yetu ya Serengeti na hivyo wengi kuishia Maasai Mara.

Licha ya kuwa Serengeti ina ukubwa mara sita ya Maasai Mara,lakini bado "Vitanda" vya kupokea watalii katika hotel za Serengeti hivizidi 970 wakati wenzetu Maasai Mara ktk mbuga yao, kuna "Vitanda" zaidi ya 4,700. Hakika kupanga ni kuchagua.

Mpaka sasa Serikali kupitia Mamlaka ya Viwanja vya ndege Tanzania inamiliki viwanja vya ndege 58(ukijumlisha na Chato itakuwa 59),na wakati Uwanja wa ndege wa KIA ukiwa mikononi mwa Kampuni ya KADCO. TANAPA inamiliki karibu viwanja 26(Vingi vikiwa ni Airstrips),NCAA 2 na viwanja binafsi 93.

Katika hivi vya binafsi,vingi vinamilikiwa na wawekezaji toka nje ambao huvitumia kufanya udanganyifu ktk maliasili zetu.Uwanja wa ndege wa mgodi wa Geita(Mchauru) na Uwanja wa ndege wa Tishwa(HTSW) kule Loliondo unaomilikiwa na mtoto wa mfalme wa UAE ni moja kati ya viwanja vinavyopswa kutazamwa vizuri na serikali hii.

Uwanja huu wa Tishwa Loliondo ndio "unatisha", kwani huku ndege za familia ya mfalme hushuka moja kwa moja na kunyanyuka na mali nyingi. Umejengwa kiasi cha kuweza kutua na kuruka ndege kubwa.

Huu ndio uwanja ulio ktk eneo ambapo ukifika na kuwasha simu unakutana na meseji inasema "Dear Guest,Welcome to the UAE.Enjoy the best network coverage and other unmatched services only with Etisalat.Please use <+> or <00> before the country code for international calls.For directory services call 181,for availability of GPRS,MMS 3G roaming services call Etisalat Travellers help line 8002300 & for inquiries on Tourism,entertainment,shopping,etc call 7000-1-7000(Roaming rates apply).Have a pleasant stay in the UAE"

Labda wengine hatuna utaalamu wa Telecomunication, lkn kweli inawezakana hii kitu iingie tu kwenye simu yako wakati hujafanya "roaming". Haya ndio mambo ya TCRA kututoa tongotongo, sio zile mambo zao za .co.tz

Tunatakiwa tuwekeze ktk usafiri wa anga,lakini tuwekeza kimkakati na kwa faida za uchumi wa pamoja kama Taifa.Tukipewa sababu za kiuchumi zinazoupeleka uwanja wa ndege Chato wenye "Aerodrome Reference Code 4D" hatutakuwa na maswali.Tusipapata majibu yenye faida za kiuchumi,tutaendelea kuhoji hata tukiwa mafichoni.

Tukumbusha umuhimu wa Mwanza ktk kuihudumia Serengeti National Park, tutawakumbusha kuwa mlikuwa na mradi wa kujenge Uwanja wa ndege Serengeti,ila mkapambana na wanaharakati wa Ikolojia. Uwanja wa Serengeti ulipaswa kujengwa kati wa Kiwanja cha Ndege pale Mgumu.

Serengeti International Airport ilikuwa ni Code 4F, ilipaswa kuwa na runway ya mita 3,800 hadi mita 4,200.Mradi huo ulififia,sasa "tumefufukia" Chato na Uwanja wa "Code 4D".Je huku ndio kupanga na kuchagua??

Wakuu ukiyatafakari sana mambo ya nchi hii unaweza kuwa kichaa. Tuishukuru [HASHTAG]#Jamiiforums[/HASHTAG], inatupa wasaa wa kuhoji haya nyuma ya "keyboard". Mambo haya enzi za Waziri wa Maliasili Aboubakari Mgumia yaliondoa maisha ya Ndugu Stan Katabaro. Tunapouanza mwaka mpya, tuzame katika sala na maombi. Ili wale wanaoomba tuwaombee kila siku,tusiwaombee tu wawe na afya njema..Bali walegeze mioyo ktk kuishughulikia mitandao kama mtandao wetu pendwa wa [HASHTAG]#Jamiiforums[/HASHTAG].

Nawatakia Mwaka Mpya mwema. Ninafunga mwaka na "Chato Interantional Airport".... Panapo majaliwa hapo mwakani. Nitakuwa likizo huko kwetu porini.... Ciaoooo!!!!
African presidents are oftentimes greedy in disguise of serving the poor!! The most selfish African presidents are hiding under the dictatorship protection.
African presidents who are misusing their countries' resources while shattering the freedom of alternative opinion.
Oh I remember the hero stan Katabalo who died using the pen to defend the poor tanzanians resources.
We are doomed to live like devils!! while them the ruling goddesses and their home boys and girls are getting prepared to live like angels.
He promised us but we could not visualise this reality! he promised us if he becomes a president--out teeth shall become our own hand hoes; now it is the reality.

His principle--""No speaking/complaints while am strangling you all to death"' what a sadism!!
Oh God come and rescue us!!
 
Kwani
Chato International Airport ni project ya hovyo hovyo iliyo fanywa kwa kumuogopa Rais Magufuli
Wabunge wa Upinzani na Community yote ya Wapinzani mbona wamekaa kimya? Yetu macho na masikio. Hivi hapo Chato kila mkazi ana Maji safi ndani, hospital, shule,Na nyumba bora?
 
Kwani

Wabunge wa Upinzani na Community yote ya Wapinzani mbona wamekaa kimya? Yetu macho na masikio. Hivi hapo Chato kila mkazi ana Maji safi ndani, hospital, shule,Na nyumba bora?
Hakuna upinzani Tanzania
Nchi yenye upinzani Rais JPM asinge jenga Airport kwao na kubaki salama
Asingetafuna hela za rambirambi na kubaki salama
Asinge simamisha ajira na abaki salama
Lema asinge kaa jela kwa miezi mahabusu kwa kosa la kipuuzi kama hili

CHADEMA ndiyo wame ua upinzani na sasa we pay heavy price
Tunyooshe Magufuli
 
Jiureze pia kwanini picha za Yesu na Mtume siyo zenye asili ya ngozi nyeusi na vazi la kiafrika. Na kwanini sula za devils na majini yanakuwa na ngozi nyeusi na sura za kiafrika tu.
Mambo ndiyo hayo sasa uwanja ukianzishwa na mweusi utapingwa kwa nguvu zote akianzisha Mwarabu au Mzungu utakumbatiwa sana
 
Mambo ndiyo hayo sasa uwanja ukianzishwa na mweusi utapingwa kwa nguvu zote akianzisha Mwarabu au Mzungu utakumbatiwa sana
Naammm..then wanaishia tukugombanisha kwa misingi ya dini. Bola niwe mpagani tu
 
Raisi ana akili nyingi sana sasa kwa sababu hamjui malengo yake ku ujenga ule uwanja pale si, kwasababu ni kwake, lengo lake kubwa ni kuwabana wezi wa dhahabu yetu, ni kwamba ndege zote zinazotua migodini itakua marufuku na viwanja vyote vidogo vidogo migodini vitafugwa
Hivi dhahabu bado ipo kule? Mnakumbuka shuka asubuhi
 
Back
Top Bottom