Hatimaye FRELIMO iko matatani, mwisho wake umefika!

Hatimaye FRELIMO iko matatani, mwisho wake umefika!

Sio mwa fisiem vs sisi manyumbu.. Unadhani bongo nyoso kiongozi akae ufichoni atoe maelekezo kuna mtu ataingia road, sisi ni maiti zinazotembea, labda vizazi vijavyo, wakikuta population tushagota kwenye milioni 100 huko, badari ishauzwa kwa mwarabu, gesi ya mchina.. Miradi yote imebinafsishwa, mfagizi wa ofisi ni muhindi, mbuga zote za wanyama zimepigwa bei, madini wameachiwa wachache, asilimia 10 tu ndio wanafaidika the rest kula ugali maharage ni anasa huenda hawa wakawa wamefufuliwa na ujio wa nabii issa.
 
Lakin suluhisho ni lipi huko Msumbiji?je wataenda Kwa second run off au nini kitatokea?
Yaani ninavyoona nguvu ya Umma ya watu iliyoko huku Viongozi wa chama tawala wataanza kukimbia mmoja baada ya mwingine kwa ajili ya kusalimisha maisha yao,hapo Huyu Mpinzani atajiludia kiulaini kuja kuunda selikali yake ya mpito
 
Yaani
Ila kwa Tanzania bado saana tena saana narudia bado saana
Sijui huu uoga tuliambukizwa na nani.

Ila kwa Tanzania bado saana tena saana narudia bado saana
Sijui huu uoga tuliambukizwa na nani.
Yaani kwa ninayoyaona huku kwa Tanzania bado sana,yaani hata wa kusimama kuitete Frelimo hakuna zaidi ya Polisi wanaotumwa kwenda kutawanya raia huku chuki ikizidi kupamba moto kila anapouwawa raia dhidi ya selikali
Mfano kunatukio nimeliona katika mji wa Nampula ni wakorofi kama mbeya, wamemchomoa polisi ndani ya gari alipoanguka akatimua mbiyo kukimbilia ndani ya nyumba ya mtu na wakamuungia wamempiga sana kama mwizi naona atakuwa amekufa,sasa chukulia raia kama hawa utawanyamazisha vipi?
 
Kwa wanaofuatilia siasa za Mozambique, hali ni mbaya kwa chama tawala cha Frelimo pamoja na serikali iliyoko madarakani. Baada ya uchaguzi kuisha na serikali kujitangaza kushinda kwa wastani wa asilimia sabini, wananchi wameikata, wakiongozwa na kiongozi wa upinzani Venancio Mondlane.

Kinachotokea sasa hivi ni kwamba huyu kiongozi wa upinzani ndiye mwenye nguvu na sauti kuliko serikali; yeye ndiye anayeamuru nini kifanyike. Anaratibu maandamano akiwa mafichoni, baada ya kukimbia nchi kufuatia mauaji ya wakili wake.

Hali si shwali. Mfano jana, ameamrisha kufanyika maandamano kwa siku tatu bila kupumzika, akilenga bandari kufungwa pamoja na mipaka. Kumeitikiwa kwa muitikio mkubwa katika miji yote mikubwa ya Maputo, Beira, na Nampula pamoja na miji mingine midogo, huku karibu watu 40 wakiwa wameuwawa na polisi.

Inchi inaongozwa na mtu aliyeko mafichoni, huku Rais Nyusi akiwa hana sauti. Ukiona mwenzako ananyolewa.

Soma, Pia: Yanayojiri kwenye Uchaguzi Mkuu wa Msumbiji: FRELIMO (Chama rafiki ya CCM) kushinda Uchaguzi 09 Oktoba?
Tutabakia kusoma na kuvihadisia vya wenzetu kila siku, kuweza kuunganika na kuwa na sauti moja kama wananchi kwa Nchi yetu katu haitawezekana.
 
Yatatoka tu. Unajua ccm wana-survive kwa sababu hatuna chama imara cha upinzani. Ukitaka kuona cdm kinaimarika mtoe Mbowe pale juu muweke Lema au yule jamaa wa Mkoa wa Mara
Upo sahihi kabisa ni kwamba CCM inaendelea kutawala kwa urahisi kwasababu amekosekana kiongozi imara wa upinzani huwa naamini kabisa Chadema inahitaji mwenyekiti aina ya Heche na makamu wake alitakiwa awe mtu kama Halima Mdee(yule wa zamani)
 
Kinachofurahisha binadamu ni wasaliti sana hakuna hata mtu mmoja anayeitetea Frelimo wala hata kuvaa nembo zake kipindi hiki mitaani,huku ofisi zake zikichomwa kila siku,kweli kifo kikikufikia hata marafiki zako hutawaona ili mradi ufe nao,utakufa peke yako
 
Upo sahihi kabisa ni kwamba CCM inaendelea kutawala kwa urahisi kwasababu amekosekana kiongozi imara wa upinzani huwa naamini kabisa Chadema inahitaji mwenyekiti aina ya Heche na makamu wake alitakiwa awe mtu kama Halima Mdee(yule wa zamani)
Yeah Heche au Lema hawa ni watu ambao huwezi kuwanunua. They canot trade you for money they are on the real course. Halima Mdee ana bei kesha nunulika
 
Tatizo wanapenda sana rushwa na wavivu.kuna sehemu ndani ya Mozambique inatumika shilingi ya Tanzania na wanaongea kiswahili na kalibu raia wa maeneo husika ni wa makabila tofautitofauti kutoka Tanzania
Yaani unakutana na wachimbaji madini, wanunuzi wa dhahabu mama ntilie mpaka machangudoa,lakini wao wako kimya wanachoitaji mnawapa rushwa na maisha yanaendelea na hayo maneneo yako poa yanahuduma zote
Hawapo makini na maisha wala vizazi vyao.Wakubwa serikalini ni wizi na starehe ndiyo vipaumbele vyao.
 
H

Hapa ndo mjue siasa za ki Frica ni upuuzi sentence ina sema hivi kiongozi wa upinzani anaamulu maandamano huku akuwa mafichoni alikokimbilia baada ya kuuawa kwa aliyekuwa mqasheria wake maana yake yeye anapenda kuishi ataki kufa au kuumizwa kulemazwa lkn anaotaka kuwatawala ana waamulu waandamane ili??alafu wakifanikisha hayo maandamano kwa kuumizwa na kulemazwa atakuja kumtawala Nani? Na kwanini nayeye asije kuandamana Kama watu wengine Kama akiumizwa ionekane kaumizwa au kafa kwa kutetea haki za watu wake?
Mbona ayatollah ruhola khomein aliongoza mapinduzi ya iran mwaka 1978 akiwa anaishi uamishoni ufaransa
Tatizo lako hujui historia
 
Yatatoka tu. Unajua ccm wana-survive kwa sababu hatuna chama imara cha upinzani. Ukitaka kuona cdm kinaimarika mtoe Mbowe pale juu muweke Lema au yule jamaa wa Mkoa wa Mara
Nina iman sana kwa Heche kuliko mtu yoyote Chadema.
Wanaosema Mbowe ni mtoto wa Nyerere nashawishika kukubari.
Huwezi kutumia mbinu ile ile kila mara na haileti matokeo na bado umo nayo tu.
Hata kama watanzania ndo raia pekee katika sayari hii hawadhaminiki!
Wanangoja matokeo mazuri bila kushiriki.
Madhara ya Ujamaa!
Haiwezekan chama makini hakina kill list. Unapigwa shavu la kushoto unageuzia la kulia!
 
Ni swala la muda tu, hata hawa majangili wa kijani nao watafurumushwa. Maana kama kuchokwa, tushawachoka. Imebaki kutolewa kwa mateke tu.
Hapa kwetu yametuweza. Tumezamishwa kwenye dini kama mambumbumbu. Akishika mkristo anatetewa na Wakristo na waislamu hivyo hivyo. Hata kama ni ujinga unafanyika.
 
Kwa wanaofuatilia siasa za Mozambique, hali ni mbaya kwa chama tawala cha Frelimo pamoja na serikali iliyoko madarakani. Baada ya uchaguzi kuisha na serikali kujitangaza kushinda kwa wastani wa asilimia sabini, wananchi wameikata, wakiongozwa na kiongozi wa upinzani Venancio Mondlane.

Kinachotokea sasa hivi ni kwamba huyu kiongozi wa upinzani ndiye mwenye nguvu na sauti kuliko serikali; yeye ndiye anayeamuru nini kifanyike. Anaratibu maandamano akiwa mafichoni, baada ya kukimbia nchi kufuatia mauaji ya wakili wake.

Hali si shwali. Mfano jana, ameamrisha kufanyika maandamano kwa siku tatu bila kupumzika, akilenga bandari kufungwa pamoja na mipaka. Kumeitikiwa kwa muitikio mkubwa katika miji yote mikubwa ya Maputo, Beira, na Nampula pamoja na miji mingine midogo, huku karibu watu 40 wakiwa wameuwawa na polisi.

Inchi inaongozwa na mtu aliyeko mafichoni, huku Rais Nyusi akiwa hana sauti. Ukiona mwenzako ananyolewa.

Soma, Pia: Yanayojiri kwenye Uchaguzi Mkuu wa Msumbiji: FRELIMO (Chama rafiki ya CCM) kushinda Uchaguzi 09 Oktoba?
Safii!
 
Back
Top Bottom