Hatimaye Nime-Confirm Kuwa Balali Amefariki!

Hatimaye Nime-Confirm Kuwa Balali Amefariki!

Status
Not open for further replies.
haya mambo hatuwezi kujua jamani, na kuendeleza hizi chuki au mambo tusiyoyajua ndio maana pengine yalichangia yeye kutoa uamuzi wa kuzikwa marekani na si nchini mwake, maana we are judging even with no heart ! jamani tutajuaje nini kilichokuwa moyoni mwake ? maybe he decided to play a fool lakini moyoni alijua nini alichokuwa anafanya ! we never know. so lets not judge him !

KadaMpinzani ,

Wewe kama wewe una haki ya kutomjudge huyu bwana na mimi pia nina haki ya kumjudge ! Ni nasema tena ninahuzunika kwamba kifo kimemkuta uraiani
 
KadaMpinzani ,

Wewe kama wewe una haki ya kutomjudge huyu bwana na mimi pia nina haki ya kumjudge ! Ni nasema tena ninahuzunika kwamba kifo kimemkuta uraiani

sawa hapo sipingi hata moja ulilosema ! umauti ni kwa wote, tutamsema yeye leo, as long as tunajua tuliobaki ni marehemu watarajiwa then tuwe tayari kuchambuliwa umauti utakapotufika ! nakubaliana na wewe !
 
Kweli hapa inaonekana makosa ni ya marehemu

hahaa ! jamani tushaanza kuact kama JIBRIL duniani ?? duh napenda JF, kuna watu wanaojua makosa ya marehemu, wow !

sidhani kama ni kosa kwa marehemu kuwa na kosa ! hayo ni ya mola wake kumhukumu kulingana na hilo kosa lake, na hiyo sio kazi yetu ! hata wewe kama marehemu mtarajiwa una makosa chungu mzima pamoja na mimi pia ! je tuanze kuhukumiana ?
 
MKJJ na Mkuu Field Marshall mnawachanganya hata hawa. watanzania wa bongo..

Maziko ya Balali utata

2008-05-22 12:47:07
Na Simon Mhina na Restuta James


Wakati taarifa za kifo cha aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) Dk. Daudi Ballali, zimethibitishwa na serikali kupitia BoT, mazishi ya kiongozi huyo yamebaki kuwa na utata juu ya mahali atakapozikiwa.

Habari kutoka kwa wanafamilia zinaonyesha kuwa wamegawanyika kuhusu mahala pa kumzika, Marekani ama hapa Tanzania huku akisubiriwa mkewe atoe umauzi wa mwisho.

Wakati hayo yakitokea, Ubalozi wa Marekani umesisitiza kuwa licha ya kifo cha kiongozi huyo, wanachosubiri ni kuona ripoti ya uchunguzi wa BoT ikianisha matokeo ya kashfa iliyopoteza zaidi ya Sh. bilioni 133 zilizo kwenye akaunti ya madeni ya nje (EPA), kupitia nyaraka za kughushi na vielelezo feki.

Hali ya utata wa maziko ya Dk. Balali, ulianzia jana kwa Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Ikulu, Bw. Salva Rweyemamu, ambaye aliwaeleza waandishi wa habari kwamba hakuna utata kuwa Bw. Balali amefariki dunia.

Hata hivyo, Mkurugenzi huyo alisema mtu ambaye angeweza kutoa taarifa juu ya suala hilo ni serikali kupitia Mkurugenzi wa Idara ya Habari (Maelezo) Bw. Kassim Mpenda.

``Suala hili sio la Ikulu ni la serikali, tafadhali ngoja niwaitie Mzee Mpenda aweze kuwajibu maswali yenu,``alisema Bw. Rweyemamu.

Baada ya muda mrefu, Bw. Mpenda alikuja na kuwaeleza waandishi kwamba habari alizonazo ni kuwa kweli msiba huo umetokea.

Hata hivyo, alisema wamekubaliana kwamba BoT ndiyo itatoa taarifa kamili juu ya msiba huo.
``Tumekubaliana kuwa mzungumzaji katika jambo hili ni Benki Kuu,`` alisema.

Alipoulizwa kuwa ni vipi BoT wawe wasemaji wa kifo cha Balali, wakati alishafukuzwa kazi kwenye taasisi hiyo ya fedha, Bw. Mpenda alisema hiyo haiwezi kuwa sababu ya kuzuia chombo hicho kutoa taarifa zake kwa vile ni makubaliano yaliyoafikiwa na serikali.

Kundi la waandishi lilipofika BoT saa 7:00 mchana maofisa wa benki hiyo walisema taarifa kamili zitatolewa saa 8:30 na Mkurugenzi wa Itifaki na kuwataka wanahabari kuondoka na warejee muda huo.

Muda ulipotimu waandishi wa vyombo mbalimbali walirejea, maofisa hao waliwataka wasubiri hadi saa 9:00 alasiri. Waliendelea kusubiri na kuelezwa kuwa vigogo wako kwenye kikao nyeti kinachohusiana na mambo ya bajeti.

Waandishi hao waliambiwa waendelee kusubiri kwa dakika 45 kwa maelezo kwamba mkutano hujaisha.

Hatimaye muda wa saa 10:15 jioni, Ofisa Uhusiano Mwandamizi wa BoT Bw. Emmanuel Mwero, aliibuka na taarifa fupi ya maandishi ya tangazo la kifo cha Dk. Balali.

Hata hivyo, ofisa huyo kabla ya kugawa tangazo hilo, alitahadharisha kwamba hatojibu maswali yoyote ya waandishi kwa vile taarifa hiyo imetolewa na Gavana wa Benki Kuu, Profesa Beno Ndulu, yeye alitumwa tu kuigawa.

``Jamani sitasema lolote, kama kuna mtu mwenye swali anatakiwa kuwasiliana na Gavana, sikuja kuzungumza bali kuwapa hii taarifa kama nilivyoelekezwa na bosi wangu,`` alisema.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo fupi ya mistari nane yenye picha ya Dk. Balali akiwa ametabasamu, ilisema alifariki Ijumaa iliyopita jijini Boston nchini Marekani.

Bila kueleza sababu za kifo chake taarifa hiyo ilifafanua kwamba BoT ilipata taarifa za kifo cha Gavana wake wa zamani juzi usiku.

Taarifa hiyo haikuonyesha imetolewa na nani wala maradhi yaliyokuwa yanamsumbua licha ya kusema wana-BoT wamestushwa na kifo hicho.

``Ofisi ya Gavana ilipata taarifa za kusikitisha jana usiku (juzi) kuwa Gavana wa zamani, Dk. Balali, amefariki dunia Ijumaa nchini Marekani,`` ilisema taarifa hiyo na kuongeza: ``BoT tunaungana na familia ya marehemu na kuomboleza msiba huo na kumuomba Mwenyezi Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi, amina.``

Kwa mujibu wa taarifa hiyo marehemu Balali alijiunga na BoT Julai 14, 1998 hadi Januari 8, 2008 alipotimuliwa kazi na Rais Jakaya Kikwete kwa tuhuma za ubadhirifu kupitia akaunti ya madeni ya nje ya EPA.

Katika kashfa hiyo, inadaiwa kuwa Sh. bilioni 133 zililipwa kinyemela kwa makampuni yasiyo na stahili yaliyotumia vielelezo feki na nyaraka za kughushi.

Wakati hayo yakiendelea, nyumbani kwa marehemu Masaki Dar es Salaam, palikuwa na ulinzi mkali ulioshirikisha askari kanzu.

Mmoja wa wanafamilia wa marehemu huyo, ambaye aliomba jina lake lisitajwe, alisema amelazimika kulia kutokana na mazingira ya kifo cha mzee wao kilivyotokea.

Alisema licha ya kuhuzunishwa na kifo hicho, lakini ametafakari milima na mabonde na majaribu makubwa ambayo Dk. Balali ameyapitia kabla mauti hayajamfika.

``Ngoja mzee akapumzike. Mzee amepata shida sana siku za hivi karibuni. Ugonjwa, majaribu fitina na kila aina ya kusemwa vimemkabili hali akiwa kitandani,`` alilalamika.

Alipoulizwa habari za maziko, alisema kwamba kumetokea utata mkubwa kwamba ni wapi Dk. Balali azikwe.

``Hata taarifa za kifo chake kuchelewa kutangazwa, zimetokana na mkanganyiko huo,`` alisema.

Alisema kuna watu wanasisitiza kwamba azikwe nchini Marekani na wengine arejeshwe.

Lakini akasisitiza kwamba mke wa marehemu, ndiye anatarajiwa kutoa uamuzi wa mwisho.

Alisema taarifa alizonazo ni kwamba upande wa serikali unataka Dk. Balali arejeshwe kwa vile inaona hatua yoyote ya kumzika nje, itachukuliwa kwamba kuna kitu kinafichwa.

Kwa upande mwingine, Ubalozi wa Marekani ambao marehemu Balali anadaiwa atazikwa nchini humo, umesema hauna taarifa zake mbali na kuzisoma katika vyombo vya habari.

Ofisa Uhusiano wa Ubalozi huo, Bw. Jeffery Salaiz, akizungumza na Nipashe kwa njia ya simu alisema kinachongojewa ni taarifa ya uchunguzi kuhusu ufisadi ndani ya BoT licha ya Balali aliyehusihusishwa na kashfa hiyo kufariki dunia.

Alisema Ubalozi hauna taarifa kuhusu mtuhumiwa huyo marehemu kwa kuwa haukuwahi kuombwa na serikali kusaidia kupata taarifa zake au kufuatilia mwenendo wake huko Marekani.

``Sijui alikokuwa anaishi, sifahamu alikuwa amelazwa hospitali gani kwa vile hatujaombwa kusaidia kumtafuta Balali,`` alisema.

Kuhusu maelezo ya kuwa na uraia wa mataifa mawili ya Tanzania na Marekani na kama nchi hiyo ina taarifa za marehemu huyo kuwekeza vitega uchumi vikubwa nchini humo, Bw. Salaiz, alisema mengi yamesemwa kuhusu Balali lakini nchi hiyo ilimfutia haki ya kuwa raia wa Marekani mwanzoni mwa mwaka huu na asingependa kuzungumzia masuala ya uwekezaji.
  • SOURCE: Nipashe
 
sawa hapo sipingi hata moja ulilosema ! umauti ni kwa wote, tutamsema yeye leo, ili hali tuliobaki ni marehemu watarajiwa then tuwe tayari kuchambuliwa umauti utakapotufika ! nakubaliana na wewe !


KadaMpinzani ,

Kifo ni part and parcel ya maisha ya mwanadamu , kwa hiyo mimi kama nilikuwa muovu basi nichambueni tuu. Unajua nimepata hasira sana kuona ni jinsi watanzania tulivyo wanafiki tunataka kumlabel Balali kama shujaa wakati amehusika kwa njia moja au nyingine katika kuifilisi nchi yetu . Na hiki kifo cha Balali kimenifundisha kitu kimoja kuwa Tanzania itaendelea kuwa maskini milele kwa sababu watu wako too emotional , wanatumia mioyo katika kufikiri. Kwa nini maoni yetu kuhusu Balali yabadilike ghafla baada ya kusikia amefariki ?

Maendeleo sio lele mama bali ni mapambano . Kwa hiyo Kada kwa kufuata logic yako hata Savimbi basi watu wa Angola wamzungumzie kwa mazuri kwa sababu amekufa . Let us stop pandering by caling a spade a spade .
 
Kumbe Ballali alifutiwa uraia mwaka huu na wamarekani?
Sasa watamfutiaje uraia halafu wasimdeport?
Eti mpaka ahitajike?
Mhn mhn Mhn!
 

Kuhusu maelezo ya kuwa na uraia wa mataifa mawili ya Tanzania na Marekani na kama nchi hiyo ina taarifa za marehemu huyo kuwekeza vitega uchumi vikubwa nchini humo, Bw. Salaiz, alisema mengi yamesemwa kuhusu Balali lakini nchi hiyo ilimfutia haki ya kuwa raia wa Marekani mwanzoni mwa mwaka huu na asingependa kuzungumzia masuala ya uwekezaji.
  • SOURCE: Nipashe



Swali la kujiuliza kama Balali alikuwa raia wa marekani alipeweje nafasi ya ugavana ? Naomba mnisahihishe kama nitakuwa nimekosea gavana lazima awe Raia wa Tanzania.
 


Swali la kujiuliza kama Balali alikuwa raia wa marekani alipeweje nafasi ya ugavana ? Naomba mnisahihishe kama nitakuwa nimekosea gavana lazima awe Raia wa Tanzania.

Kwa nini unadhani alikuwa raia wa US?
 
Kwa nini unadhani alikuwa raia wa US?


Kuhani Mkuu ,


Soma hiyo article hapa chini ya Nipashe especially the last paragraph you will know what a'm talking about ...



Ofisa Uhusiano wa Ubalozi huo, Bw. Jeffery Salaiz, akizungumza na Nipashe kwa njia ya simu alisema kinachongojewa ni taarifa ya uchunguzi kuhusu ufisadi ndani ya BoT licha ya Balali aliyehusihusishwa na kashfa hiyo kufariki dunia.

Alisema Ubalozi hauna taarifa kuhusu mtuhumiwa huyo marehemu kwa kuwa haukuwahi kuombwa na serikali kusaidia kupata taarifa zake au kufuatilia mwenendo wake huko Marekani.

``Sijui alikokuwa anaishi, sifahamu alikuwa amelazwa hospitali gani kwa vile hatujaombwa kusaidia kumtafuta Balali,`` alisema.

Kuhusu maelezo ya kuwa na uraia wa mataifa mawili ya Tanzania na Marekani na kama nchi hiyo ina taarifa za marehemu huyo kuwekeza vitega uchumi vikubwa nchini humo, Bw. Salaiz, alisema mengi yamesemwa kuhusu Balali lakini nchi hiyo ilimfutia haki ya kuwa raia wa Marekani mwanzoni mwa mwaka huu na asingependa kuzungumzia masuala ya uwekezaji.
 
KadaMpinzani ,

Unatumia vigezo gani kuilabel hii thread dead ? Hii thread aijafa kama wewe una la kusema kaa pembeni watu wakate ishu.
 
Alisema Ubalozi hauna taarifa kuhusu mtuhumiwa huyo marehemu kwa kuwa haukuwahi kuombwa na serikali kusaidia kupata taarifa zake au kufuatilia mwenendo wake huko Marekani. ``Sijui alikokuwa anaishi, sifahamu alikuwa amelazwa hospitali gani kwa vile hatujaombwa kusaidia kumtafuta Balali,`` alisema.

According to the dataz, ni kwamba hawa watu wa ubalozi, wamekuwa wakiwalilia familia ya marehemu ili nao waweze kuhudhuria mazishi kesho, lakini nasikia familia wamewakea ngumu mpaka dakika hii, sasa hapa wanasema nini? Ni bora wanyamaze tu!

Na wasiruhusiwe kwenda huko kwenye mazishi kabisaa!


 
Unatumia vigezo gani kuilabel hii thread dead ? Hii thread aijafa

Hiii thread aliyeianzisha ni mimi wakuu, bado inaendelea kwa sbabu kuna mengi yanakuja baada ya mazishi!
 
Kitu kilichonishtua ni kugundua ya kuwa Balali hakuwa raia wa Tanzania . Sasa ninachojiuliza ilikuwaje akapewa ugavana ? Nafasi muhimu kama hiyo ambapo moja ya vigezo ni lazima mtu awe raia wa Jamhuri ya muungano.
 
Kitu kilichonishtua ni kugundua ya kuwa Balali hakuwa raia wa Tanzania...

Rufiji;

Gazeti la Nipashe uliko pata habari hawajui wanachokisema. Hawajui tofauti ya Visa na Uraia. Marekani ilitengua Visa, sio Uraia. Ballali sio tu hakuwa raia wa US, bali hakuwa na Visa ya US wakati 'anafariki.'

Former BOT Governor's Termination Invalidates U.S. Visa


Press Release

Embassy of the United States
Dar-es-Salaam.Tanzania
January 16, 2008

The Tanzanian government recently inquired about the visa status of Mr. Daudi Ballali, the former Bank of Tanzania governor, in light of his recent termination. The United States Government has informed the Tanzanian government that it is revoking Mr. Ballali's visa because he no longer represents Tanzania.

Mr. Ballali visa was issued in his capacity as a representative of the Tanzania government. Simply put, because of the termination of his service, he no longer represents the government and is no longer eligible for his current non-immigrant visa status.


(Habari kamili: http://tanzania.usembassy.gov/pr_01162008.html)

Kwa hiyo, la Visa na Uraia halina utata. Mpasho wa Nipashe hapo juu ni Uwongo. Tanzani hakuna Press.
 
Rufiji;

Gazeti la Nipashe uliko pata habari hawajui wanachokisema. Hawajui tofauti ya Visa na Uraia. Marekani ilitengua Visa, sio Uraia. Ballali sio tu hakuwa raia wa US, bali hakuwa na Visa ya US wakati anafariki.

Former BOT Governor’s Termination Invalidates U.S. Visa

Press Release

Embassy of the United States
Dar-es-Salaam.Tanzania
January 16, 2008

The Tanzanian government recently inquired about the visa status of Mr. Daudi Ballali, the former Bank of Tanzania governor, in light of his recent termination. The United States Government has informed the Tanzanian government that it is revoking Mr. Ballali's visa because he no longer represents Tanzania.

Mr. Ballali visa was issued in his capacity as a representative of the Tanzania government. Simply put, because of the termination of his service, he no longer represents the government and is no longer eligible for his current non-immigrant visa status.

(Habari kamili: http://tanzania.usembassy.gov/pr_01162008.html)

Kwa hiyo, la Visa na Uraia halina utata. Mpasho wa Nipashe hapo juu ni Uwongo. Tanzani hakuna Press.

Na hiyo mika 23 aliyofanya kazi IMF alikuwa ana makazi yake wapi?
Na uraia wa nchi gani?
Maana inaonyesha huyu jamaa alikuwa na contract ya kuja kutekeleza masuala flani flani toka alipoajiriwa na Mkapa.
 
Na pia utaratibu wa kumvua mtu visa yake ina maana anakuwa statusless..Ama ilegal immigrant to be specific...Sasa alikuwa akiendelea kuishi vipi bila deportation regardless as to whether we needed him or not?
 
Na hiyo mika 23 aliyofanya kazi IMF alikuwa ana makazi yake wapi?
Na uraia wa nchi gani?
Maana inaonyesha huyu jamaa alikuwa na contract ya kuja kutekeleza masuala flani flani toka alipoajiriwa na Mkapa.

Taarifa inasema Marekani iliifahamisha Tanzania kwamba inatengua Visa yake. Hii ni absolutely conclusive proof kwamba alikuwa Mtanzania. Angekuwa ni Raia wa, tuseme Uchina, wangewafahamisha Uchina. Hapa wameifahamisha nchi ambayo mpewa Visa alitokea, yaani Tanzania.

Isitoshe, muda mchache baada ya ile taarifa, Marekani ilisema, na ikarudia siku tatu zilizopita, kwamba kama Tanzania ikimtaka US watamrudisha. Mtu akitenguliwa Visa halafu akarudishwa kwao, anarudishwa katika nchi ya Uraia wake. Hawawezi kum dampu Tanzania wakati ni Raia wa, mfano, Uchina.

Kwa hiyo hakuna utata kabisa katika Uraia wa 'marehemu' Ballali.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom