Serikali imeufuta mkataba huo uliowahi kutajwa kuwa na thamani ya Shilingi za Kitanzania Bilioni 400
Mwezi Februari mwaka huu Serikali iliweka wazi kuwa imeingia mkataba na Kampuni ya kutoka nchini Kenya ya Indo Power Solutions Ltd iliyojinasibu kuwa na uwezo wa kununua Korosho tani 100,000
Serikali kupitia Waziri wa Biashara, Joseph Kakunda imesema kampuni hiyo imeshindwa kutekeleza sehemu ya makubaliano
Aidha, JamiiForums iliibua madudu ya kampuni hiyo na kuyaanika wazi mapema mwezi Februari
Kwa Uzi ulioibua madudu ya Kampuni hiyo fungus kiunganishi hiki;
Unapoambia fundi seremala kawa mpishi wa Serena Hotel, mtu unaweza tilia mashaka chakula atakachopika. Nimejaribu sana ku Gogle hiyo kampuni iliyonunua korosho na huyo kiongozi wao aliyetia saini na naibu Waziri, kidogo nimeingiwa na wasiwasi. 1. Kenya kuna kiwanda kimoja tuu cha kubangua...