Hatimaye: Serikali ya Tanzania yafuta mkataba wake na Kampuni ya Kenya (Indo Power Solutions LTD) iliyojinasibu kununua Korosho kwa Bil 400

Hatimaye: Serikali ya Tanzania yafuta mkataba wake na Kampuni ya Kenya (Indo Power Solutions LTD) iliyojinasibu kununua Korosho kwa Bil 400

Jiwe mpenda masifa ya kishamba aliahidi kugawa kilo mbilimbili, atekeleze sasa ahadi yake.

Mkuu wa nchi anakua na mizuka utadhani katibu kata.haya sasa na mwezi wa kumi huo korosho zingine zinaingia soko ni.
 
Afu siku ya kujifunga Kwny huo MKATABA pale Arusha, kulikuwa na ma-prof wawili wa sheria.. Prof Luoga, gavana wa BoT na huyo Kabundi, kumbe hakuna Cha maana, duuh!
Mkuu . ukishaona prof amekubali uteuzi wa jiwe basi piga magoti usali.
 
Jamani mzee magu si alisema tunaweza tukagawana hizi korosho kila mtu akapata japo kilo mbili mbili,HNi kheri tukazila wenyewe kisha tukasubiri msimu mwingine unaokuja tutakuwa tushapata mbia wa kununua
Hapo magu anauchunaaa utadhani hayupo bongo. Ahadi ni deni
 
HILI SUALALA KOROSHO NILIJUA HALINA UTOFAUTI NA ILE MVUA SIJUI YA MALYASIA SIJUI CHINA KWAMBA INATENGENEZWA NA INANYESHA USANII HUU MMMHHHMMMHHH NAWAANGALIA TU. TUNAKOENDA MUNGU ANATUONA WATANZANIA ITAFIKIA TUTAAAMBIWA HAKUNA KULIMA KWAKUWA CHAKULA KITANYESHA KAMA MVUA
 
I believe the best weed comes from Tanzania under CCM! Bange mbaya
tapatalk_1509731732046.jpeg
 
Serikali imeufuta mkataba huo uliowahi kutajwa kuwa na thamani ya Shilingi za Kitanzania Bilioni 400

Mwezi Februari mwaka huu Serikali iliweka wazi kuwa imeingia mkataba na Kampuni ya kutoka nchini Kenya ya Indo Power Solutions Ltd iliyojinasibu kuwa na uwezo wa kununua Korosho tani 100,000

Serikali kupitia Waziri wa Biashara, Joseph Kakunda imesema kampuni hiyo imeshindwa kutekeleza sehemu ya makubaliano

Aidha, JamiiForums iliibua madudu ya kampuni hiyo na kuyaanika wazi mapema mwezi Februari

Kwa Uzi ulioibua madudu ya Kampuni hiyo fungus kiunganishi hiki;

Je, hakuna wa kuishtaki serikali kwa kuingia mikataba na kampuni hewa?
 
Kumbe ulimuelewa tangu zamani sana!
Hii ndio mikataba anayoingia Profesa Kabudi. Nikashamuona Profesa Kabudi kwenye jambo lolote huwa najua kabisa hamna jipya hapo.
 
Inasikitisha sana
Sasa kwenye jambo dogo kama hili lakutambua uhalali wa uwepo wa Kampuni husika hatuwezi tutaweza kweli kupambna kwenye mikataba mikubwa na ma mafia wa ulaya na uchina?..

Serikali yetu pendwa ya wanyonge naomba tuchukue hatua kwa wahusika wote walioshiriki kwenye aibu hii pasipo kumuangalia mtu usoni, Hili lilipigiwa sana kelele humu JF na watu wakaleta mpaka very simple investigation ambayo hata mbumbumbu wa masuala ya kijasusi anaweza kung'amua.
 
Back
Top Bottom