TUNDU mgombea urais Chadea 2020 alishindwa vibaya sana na John Pombe Magufuli Rais wa sasa na aliyekuwa mgombea kupitia CCM aliyemshinda vibaya sana TUNDU. Ieleweke uchaguzi ulikuwa Oktoba 28, 2020.
TUNDU alikuwa na wakili wake akijulikana Bob Amstardam, wakili huyo alitoa matamko kwa niaba ya TUNDU na kuandika barua NEC kutisha na kutaka maelezo.
Baada ya uchaguzi alisema anaenda ICC ambayo ni Mahakama ya Uhalifu wa Kimataifa. Tawi lake pia liliwahi kuwepo Arusha likishughulikia uhalifu wa Rwanda.
Sikujua chama cha upinzani kikishindwa linageuka kuwa uhalifu wa kimataifa na kupelekwa ICC the Hague. Nilikuwa naisubiri siku ya Jumatatu, Oktoba 23, 2020 siku iliyoahidiwa Robert Amstarda anafungua kesi ICC kwa kosa la mteja wake kushindwa vibaya uchaguzi na kugeuzwa uhalifu wa kibinadamu sawa na mauaji ya halaiki. Jumatatu, Oktoba 23 mara ikapita nikasikia tena viti maalum.
Mjadala wote umehamia viti maalum na suala la kesi ya mfano na ya kisanii kuendelea kufubaza akili za wafuasi wa chama limekwisha. Hakuna mtu anaweza kukumbuka kujadili na kuuliza ICC tena.
Ili kufubaza zaidi akili za wafuasi, viti maalumu vikaunganishwa na mfumo wa serikali. Kwamba serikali imeratibu viti maalumu Chadema. Sasa hapa, Mdee, Matiko na Bulaya wameratibiwa? Hawa kuna wajumbe wa vikao muhimu sana vya maamuzi ndani ya Chama mfano kamati kuu. Sasa, mjumbe wa kamati kuu anaratibiwa na mfumo w kiserikali. Mwenyekiti wa Bavicha anaratibiwa na mfumo wa kiserikali? Hii ni hatari kwa Chama.
Walid Kabour, Wilbroad Slaa, na Mashinji ni kati ya makatibu wakuu Chadema kuwahi kutokea na kuondoka. Hii nafasi imekuwa changamoto na Mnyika hivi karibuni ataondoka. Ni kwa sababu chama hakina mfumo. Juma Duni Haji mgombea mwenza wa Lowassa 2015 alisema, CHADEMA KILA MTU NI PAPA, baada ya hapo akarudi zake CUF. Katibu mkuu hapewi nafasi kutekeleza majukumu yake hasa linapokuja suala la kusimamia chama. Wakati wa Uchaguzi TUNDU na kampeni meneja wake BOB AMSTARDAM ndio walisikika zaidi kuliko Mnyika, katibu mkuu Chadema.
CHADEMA imara, ni CCM imara, na uchumi imara wa nchi. CHADEMA ijitafakari na kuondoa ubinafsi wa watu fulani ndani ya chama na kufanya kazi kama timu lakini kila mtu akitimiza wajibu wake.
Hatutegemei tena kuona akina Amstardam wakigeuka wasemaje wa CHADEMA.
Je, ikiwa kamati kuu hakuridhia kupeleka mashitaka ICC, kwanini itakiwe kuridhia viti maalumu