Hatimaye Yanga yakabidhiwa kwa Manji aiendeshe kama club Binafsi

Sasa klabu inakodishwa hii mbona sijaelewa, kwa hiyo hizi klabu uwendeshaji hawa wazawa umewashinda kabisa yaani, kama mmeamua hivyo kwa nini hakuna michakato na tafiti mjue kiasi halali cha kukodishwa hiyo klabu maana imekuwa ghafla halafu mtu anatoa sauti halafu imepita hiyo, kaaazi kweli kweli.
 
Ukikosa akili ni shida...bora ukose mali
 
Leo ni ombi,ndo maana kamati ya wadhamini itakaa na kuona jinsi gan itakavyo kuwa
 
Leo ni ombi,ndo maana kamati ya wadhamini itakaa na kuona jinsi gan itakavyo kuwa
Ninachojiuliza ni kwamba kwenye huo mkutano hakuna mtu aliyeweza kupinga ama kudai njia nyingine ya uwendeshaji tofauti na huo mfumo wa hisa wa kukodishwa klabu mpaka pendekezo moja tu ndo lililochukuliwa na kujadiliwa na hiyo bodi ya wadhamini, hii maana yake hilo ombi limeshapita.
 
Dah! kuanzia leo mimi sio Shabiki wa YOUNG AFRICAN SPORTS CLUB mpaka pale Timu yetu wa Wananchi utakaporejeshwa baada ya 10!!!
 
Kwa mtu mwenye akili akili timamu hawezi asilali kukubali mkataba huo...
" eti ikipatikana hasara inabaki juu yangu ila faida club inapata 25% yeye 75% " seriously,? Wanachama wa Yanga wana akili timamu kweli ama walikua "intoxicated"??
 
tena jamaa anawaingiza chaka kwa akili kweli,faida ya wote hasara yake,waswahili tusivyopenda hasara na kupenda njia ya mkato hapo lazima tuingie tu kingi kiulainii
 
kwanini wapinge..? Huyo atakaepinga aseme ameisaidia nini Yanga
 
Dah! kuanzia leo mimi sio Shabiki wa YOUNG AFRICAN SPORTS CLUB mpaka pale Timu yetu wa Wananchi utakaporejeshwa baada ya 10!!!
ondoka tu umeisaidia nini yanga zaidi ya kuchekelea kuingizwa bure uwanja wa Taifa
 
Hakuna cha ajabu hapo. Kwani TP Mazembe inamilikiwa na mtu au wananchi?
 
Hadi leo nimekuwa mzee sijawahi kuona mswahili akipokea mabadiliko yoyote kwa fikra chanya. Yaani nikukosoa na kuwa na mashaka tu. Hata kama jambo lina tija. Mfano
1. Hoja ya vyama vingi au kimoja
2. Muungano
3. Ujio wa Rais Bush nakukaa siku 4
4. Ujio wa Rais Obama
5. Safari za Rais Kikwete nje ya nchi
6. Kutofanya safari nje ya nchi Rais JPM
7. EAC
8. Kuhamia Dodoma
9. Mo kuwekeza hisa club ya Simba
10. Manji kuikodisha Yanga kwa 75%
11. Hoja ya Yanga kuwa Kampuni
12. Mabasi ya mwendo kasi
13. Wafanyakazi hewa.
14. Wanafunzi wasio na sifa kujiunga vyuo viku
15. Vita ya kagera
16. Vijiji vya ujamaa
17. Siasa ni kilimo
18. Kilimo kwanza
19. Operation majangili
20. Matumizi ya EFD

Kila jambo mbogo ni kukosoa tu na kuwa na mashaka.

Simba na Yanga nusu karne yote wamefanya lipi la maana. Tuache uoga wa kufanya mabadiliko.

Nina imani waliokuwa wanakosoa uanzishwaji wa mabasi ya mwendo kasi, leo hii hawaishi kuyagombania kupanda tena wakali hao ukijaribu kuwahi kuingia kabla yao.

Acheni mazoea na akili mgando
 
Hawa jamaa kweli vilaza wa kimataifa. Wanakubaliana na manji bila kujua kwa Kina dhamira yake kwa miaka hiyo kumi ijayo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…