Hatimaye zile Km 51 zilizokuwa na vumbi zimekamilka. Sasa kutoka Dar hadi Kigoma ni lami

Hatimaye zile Km 51 zilizokuwa na vumbi zimekamilka. Sasa kutoka Dar hadi Kigoma ni lami

ChoiceVariable

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2017
Posts
66,537
Reaction score
75,687
Mwaka Jana niliweka mada hapa kwamba Zimesalia km 51 za vumbi Ili Barabara yote kutoka Dar Hadi Kigoma iwe Lami.

Hatimaye km za mwisho kutoka Ilunde-Malagarasi zimekamilika na Sasa Kigoma sio mwisho wa reli tena.Serikali ya Rais Samia imewakomboa watu wa Kigoma na Tabora. Soma hapa Bado Km 51 ili Kigoma-Dar iwe lami. Rais Samia anaenda kuunganisha mikoa yote kwa lami.
Screenshot_20240924-154848.jpg


Sasa Serikali iweke Nguvu kwenye Barabara zifuatazo

-Mbeya-Tabora
-Songea-Morogoro
-Njombe-Morogoro
-Arusha-Musoma
-Mpanda-Kigoma
-Tanga-Singida
-Iringa-Morogiro-Lindi.
Screenshot_20240709-061801.jpg


1738216176920.png

===

Ujenzi wa barabara ya Kaliua - Malagarasi - Ilunde (km 156) na kipande cha Kazilambwa - Chagu (km 36) umekamilika kwa asilimia 100, huku kazi za nyongeza kwenye barabara ya Ugansa - Usinge (km 7.4) zikifikia asilimia 98.5.

Barabara hii, yenye umuhimu mkubwa wa kiuchumi na kijamii, imejengwa kwa kiwango cha lami kwa gharama ya shilingi 48.6 bilioni, ambapo Mfuko wa OPEC umefadhili asilimia 95 ya mradi huku Serikali ya Tanzania ikigharamia asilimia 5.

Mradi huu ulianza kutekelezwa tarehe 3 Agosti 2020, baada ya upembuzi yakinifu uliofanywa mwaka 2009 na kampuni ya Crowntech Consult Ltd kwa gharama ya shilingi 134.4 milioni.

Serikali ya Tanzania ilianza kufadhili ujenzi huo kwa asilimia 100, kabla ya Mfuko wa OPEC kuingia kama mfadhili mkuu mwaka 2021.

Wakazi 199 wa vijiji vya Ugansa na Malanga walilipwa fidia ya jumla ya shilingi 725.3 milioni kupisha ujenzi huo, huku gharama za usimamizi wa mradi zikifikia shilingi 2.2 bilioni kwa kipindi chote cha utekelezaji.

Aidha, mradi huu umesimamiwa na Kitengo cha Usimamizi wa Miradi cha Wakala ya Barabara Tanzania - TANROADS (TECU) kutoka Mkoa wa Tabora.

Pamoja na mafanikio ya mradi, changamoto kubwa imejitokeza ikiwemo wizi wa alama za barabarani.

Mpaka sasa, jumla ya alama 10 na mabango mawili ya mradi vimeripotiwa kuibwa, hali inayohatarisha usalama wa watumiaji wa barabara.

Katika juhudi za kudhibiti hali hiyo, vyombo vya ulinzi na usalama vikishirikiana na Meneja wa TANROADS Mkoa wa Tabora vimemkamata mtuhumiwa mmoja, Moshi Luponya, mkazi wa Kijiji cha Tarehe Moja, Kata ya Usinge. Mtuhumiwa anashikiliwa na kwa kesi ya kuhujumu miundombinu ya serikali chini ya RB Na. USNG/RB/37/2024 katika Mahakama ya Wilaya ya Kaliua.

Kwa sasa, kazi zinazokamilishwa ni pamoja na ufungaji wa taa za barabarani, ujenzi wa barabara za maingilio, na upakaji rangi.

Wakazi wa Tabora na Kigoma wamepokea mradi huu kwa matumaini makubwa, wakiamini utaimarisha uchumi kwa kuboresha usafirishaji wa mazao, biashara, na huduma za kijamii.

View: https://youtu.be/zv0jGPj2M8c?feature=shared
1738216176920.png
 
Mkuu hauna update za mradi wa rami kutoka Namanyere mpaka kirando ili kuweza kuunganisha Bandari ya kipiri ? Maana njia hii ni muhimu kwa uchumi wa wilaya ya Nkasi na mkoa kwa ujumla wake.
 
Mkuu hauna update za mradi wa rami kutoka Namanyere mpaka kirando ili kuweza kuunganisha Bandari ya kipiri ? Maana njia hii ni muhimu kwa uchumi wa wilaya ya Nkasi na mkoa kwa ujumla wake.
Hakuna chochote kwenye huo mradi ni stori kuliko uhalisia.

Serikali Ina priotise Rukwa-Katavi-Kigoka Link
 
Miaka 64 ya uhuru bado tuna hanahangaika na barabara, maji, umeme, matundu ya vyoo, madawati, madarasa, nyumba za walimu, dispensaries na una madini, tanzanite, almasi, bunga za wanyama, mito, makaa ya mawe, gas,bahari, maziwa, ardhi kubwa yenye rutuba, nguvu kazi ya kutosha n.k kweli tuna ongonzwa na wajinga haswa
 
Mwaka Jana niliweka mada hapa kwamba Zimesalia km 51 za vumbi Ili Barabara yote kutoka Dar Hadi Kigoma iwe Lami.

Hatimaye km za mwisho kutoka Ilunde-Malagarasi zimekamilika na Sasa Kigoma sio mwisho wa reli Serikali ya Rais Samia imewakomboa watu wa Kigoma na Tabora. Soma hapa Bado Km 51 ili Kigoma-Dar iwe lami. Rais Samia anaenda kuunganisha mikoa yote kwa lami

Sasa Serikali iweke Nguvu kwenye Barabara zifuatazo

-Mbeya-Tabora
-Songea-Morogoro
-Njombe-Morogoro
-Arusha-Musoma
-Mpanda-Kigoma
-Tanga-Singida
-Iringa-Morogiro-Lindi.

===

Ujenzi wa barabara ya Kaliua - Malagarasi - Ilunde (km 156) na kipande cha Kazilambwa - Chagu (km 36) umekamilika kwa asilimia 100, huku kazi za nyongeza kwenye barabara ya Ugansa - Usinge (km 7.4) zikifikia asilimia 98.5.

Barabara hii, yenye umuhimu mkubwa wa kiuchumi na kijamii, imejengwa kwa kiwango cha lami kwa gharama ya shilingi 48.6 bilioni, ambapo Mfuko wa OPEC umefadhili asilimia 95 ya mradi huku Serikali ya Tanzania ikigharamia asilimia 5.

Mradi huu ulianza kutekelezwa tarehe 3 Agosti 2020, baada ya upembuzi yakinifu uliofanywa mwaka 2009 na kampuni ya Crowntech Consult Ltd kwa gharama ya shilingi 134.4 milioni.

Serikali ya Tanzania ilianza kufadhili ujenzi huo kwa asilimia 100, kabla ya Mfuko wa OPEC kuingia kama mfadhili mkuu mwaka 2021.

Wakazi 199 wa vijiji vya Ugansa na Malanga walilipwa fidia ya jumla ya shilingi 725.3 milioni kupisha ujenzi huo, huku gharama za usimamizi wa mradi zikifikia shilingi 2.2 bilioni kwa kipindi chote cha utekelezaji.

Aidha, mradi huu umesimamiwa na Kitengo cha Usimamizi wa Miradi cha Wakala ya Barabara Tanzania - TANROADS (TECU) kutoka Mkoa wa Tabora.

Pamoja na mafanikio ya mradi, changamoto kubwa imejitokeza ikiwemo wizi wa alama za barabarani.

Mpaka sasa, jumla ya alama 10 na mabango mawili ya mradi vimeripotiwa kuibwa, hali inayohatarisha usalama wa watumiaji wa barabara.

Katika juhudi za kudhibiti hali hiyo, vyombo vya ulinzi na usalama vikishirikiana na Meneja wa TANROADS Mkoa wa Tabora vimemkamata mtuhumiwa mmoja, Moshi Luponya, mkazi wa Kijiji cha Tarehe Moja, Kata ya Usinge. Mtuhumiwa anashikiliwa na kwa kesi ya kuhujumu miundombinu ya serikali chini ya RB Na. USNG/RB/37/2024 katika Mahakama ya Wilaya ya Kaliua.

Kwa sasa, kazi zinazokamilishwa ni pamoja na ufungaji wa taa za barabarani, ujenzi wa barabara za maingilio, na upakaji rangi.

Wakazi wa Tabora na Kigoma wamepokea mradi huu kwa matumaini makubwa, wakiamini utaimarisha uchumi kwa kuboresha usafirishaji wa mazao, biashara, na huduma za kijamii.

Hapo Iringa - moro - lindi sijaelewa barabara inapitia wapi?
 
Ukisema serikali ya samia imewakomboa ni utaahira.Hizo bara bara zimejengwa kwa kiasi kikubwa na awamu zilizopita hasa JK.Toa credit kwa awamu zote
Una uhakika? Kama ndivyo si zingekuwa zimekamilika kitambo Sasa.

Kwa akili Yako ndogo unadhani aliyeongeza Bajeti kubwa kwenye Wizara ya ujenzi amejenga zaidi au kajenga kidogo?

Kuanza mradi miaka na mikaka sio kujenga zaidi.

Mwisho section iliyotajwa ilianzishwa 2022 mama akiwa Rais na imekamilika.
 
Mnazungumzia kuunganisha mikoa miaka 61? Hovyoooo
Kama sio vipaombele kubadilishwa na Magufuli Kwa Sasa Nchi yote ingekuwa lami na hivyo Nguvu ingekuwa kwenye Sgr.

By the way mama anaendelea kupiga mwingi sana kwenye Barabara,kabla ya 2030 Barabara zote kuu zitakuwa na lami.
 
Una uhakika? Kama ndivyo si zingekuwa zimekamilika kitambo Sasa.

Kwa akili Yako ndogo unadhani aliyeongeza Bajeti kubwa kwenye Wizara ya ujenzi amejenga zaidi au kajenga kidogo?

Kuanza mradi miaka na mikaka sio kujenga zaidi.

Mwisho section iliyotajwa ilianzishwa 2022 mama akiwa Rais na imekamilika.
Sasa ww taahira umesema section ya mwisho ndio ilianza 2022 ,maana yake hizo section nyingine zilijengwa na makalio yako?
Hizo section nyingine zina KM ngapi ukilinganisha na hiyo ya mwisho?
Akili yako ni finyu sana
 
Sasa ww taahira umesema section ya mwisho ndio ilianza 2022 ,maana yake hizo section nyingine zilijengwa na makalio yako?
Hizo section nyingine zina KM ngapi ukilinganisha na hiyo ya mwisho?
Akili yako ni finyu sana
Jikite kwenye mada.

Hata hizo section zingine licha ya kuanza kabla ya Mama ila alikuta hakuna iliyokamilika ,amezikamilisha yeye kuanzia Manyoni kuja Hadi Kigoma ila hii ya mwisho ni ya kwake 100% in less than 3 years imekamilika sio wengine wanajenga Barabara miaka na mikaka hazikamilikagi eg awamu ya Magufuli.
 
Back
Top Bottom