Hatma ya maisha yangu ipo mikononi mwa kijana wa Buguruni

Hatma ya maisha yangu ipo mikononi mwa kijana wa Buguruni

Hakuna upande wa kubaki...

Kwanza umekosea sana kuingiza mapenzi sehemu za kazini, Acha kabisa...
Accountant atakuharibia kazi...

Hivyo huna kazi...

Pili umekuwa umekuwa unapenda vya bure, wewe mtoto wa kiume pambana kwa jasho...

Mzee anakupelekesha tu ka mtumwa...kama anataka kukusaidia mbona masharti...

Pia msaada angetoa yeye mwenyewe kwa hao watoto wa mtaaani...

Anataka kitu kutoka kwako mwishoe utaambiwa uoe mtoto wake...

Mi nafikiri Acha vyote ufanye biashara yako mwenyewe achana na Mzee na Achana na kazi ya mama Accountant
We ungeweza? yaani uache kazi hujajipanga! unafanya masiala nini![emoji16] Mtaani kuna balaaa
 
Anatunga lazima story iwe n Good ending ,,, any way jifunze kwa OMUGHAKA
 
Ilipoishia

Mzee: "Kabla sijafanya uamuzi, nataka kujua sababu zilizokufanya BM uache kazi"

Ghafla nilihisi joto wakati ndani full AC watu wote kimya mimi ndio natakiwa kuongea kwa wakati huo halafu Caryn akanipiga jicho flani hivi akakunja na mikono kifuani yani Ile kwamba "TUNAKUSIKILIZA"

Inaendelea

SEASON 2, Episode 2

Turudi nyuma kidogo tulipoishia

Ile siku Caryn alivyoniacha pale hotelini sikuchukua muda na Mimi nikasepa, zilipita kama siku mbili hivi sijawasiliana na Caryn, akaja kunipigia siku kama ya 3 ivi

Caryn: [emoji338]"Hey"

BM: "Mambo"

Caryn: "Poa, vip mbona kimya! umefikia wapi?"

BM: "Bado sijapata nyumba, nipo kwenye michakato"

Caryn: "So wale watoto wanaishi wapi kwasasa?"

BM: "Si wanaishi walipokuwa wanaishi"

Caryn: "Naona unaenda kufeli hili zoezi kabla hata jlhujalianza"

BM: "Kwanini? ni kama unataka nifeli sio?"

Caryn: "Hapana, ila kwa akili ya kawaida tu unadhani wale watoto wakiondoka kule unakowakutaga utawapata wapi tena? coz ulisema pale sio makazi yao permanent"

BM: "Dah! halafu kweli nilikuwa sijawaza upande huo kabisa"

Caryn: "Just act fast, you're wasting too much time" [emoji3513]

Caryn sometimes ni mzinguaji ila leo ameongea kitu Cha maana ambacho hata sikukifikiria, nikaona hapa nikisema niendelee kusubiri nyumba nikipata ndio nikawachukue wale madogo naweza nikafeli, Nikapata wazo, nikamvutia waya sister angu flani anaishi Yombo, nikampanga kwenye simu lakini hakupangika ikabidi jioni niende kwakwe nikamuelezea kwa kina zaidi, Lengo ni kutaka aishi na wale madogo kwa muda huku nikiendelea kutafuta nyumba ili nisije kupotezana nao

Kwa bahati nzuri sister akaelewa japo kishingo upande, maana anajua angenikatalia na mimi ningemfungia vioo kwenye mambo yake, na Mimi sikupoteza muda kesho yake tu nikaibuka Buguruni kuwacheki madogo, nikaenda hadi pale maskani yao lakini sikuwakuta nikazunguka mitaa yote karibu na lile eneo lakini hola, ikafika hadi mchana narudi yale maeneo bado sikukuta mtu, nikampigia sister kumuuliza kama ameshaandaa kila kitu maana Jana nilimuambia chakula Cha mchana aongeze kipimo kidogo atuhesabie na sisi chakula, nikamuambia kwamba huku madogo sijafanikiwa kuwaona

Ikabidi nitafute mahali nipate msosi, nimemaliza kula saa hiyo ni saa tisa kasoro na tangu asubuhi nipo Buguruni, ilivyofika saa 15:00 ikabidi niende Kinondoni Mkwajuni kwa mshkaji wangu flani maana tulipanga kuonana siku kadhaa sema ratiba zinavurugika kila tukipanga

Nikaibuka Kinondoni tukaenda kuchill Kitambaa Cheupe jamaa popote atakapokuwa utamkosa na vyote lakini sio laptop, ni wale wenzetu wa kufanya deal za Online, ila huyu mshkaji wangu yupo karibia kila sehemu kuanzia Forex, Cryptocurrency, ni freelancer pia hadi kubeti ana beti, na mchizi anaishi fresh mjini, anapokea kodi ya nyumba huko maeneo ya Goba lakini yeye kaamua kupanga Kino

Mshkaji anajua mambo mengi kuhusu mimi na mm Najua ya kwake Yani ni best friend, Nakumbuka hii siku nilivyoenda mchizi analikuwa ananishauri kutokuacha kazi, maana nilimuelezea situation niliyokuwa nayo

Mshkaji: "BM Unajua njia uliyochagua wewe kutafuta pesa inataka uwe na mahusiano mazuri na watu, so inabidi ucheze na akili zao ili uweze ku win"

BM: "Unamaanisha nini?"

Mshkaji: "Si namaanisha hicho nilichokiongea, Yani kama Mimi ningekuwa ni wewe kazi nisingeacha na kumgonga ningekuwa na mgonga kama kawa (Accountant) kwani wewe unachubuka wapi ukimgonga yule Demu?"

Huyu jamaa kwanza ni mtu wa mademu sana ndio maana sijashangaa hiki anachonishauri

BM: "Nikifanya kama unavyoniambia ndio nitazidi kumpa matumaini kitu ambacho mimi sitaki kukifanya"

Mshkaji: "Unajua the fight is against poverty, ukiendekeza sana Mapenzi Utaumia, mpe anachokitaka ili na wewe upate unachokitaka, huko mbeleni mambo yakinyooka ndio una nafasi ya kuchagua nani awe nani"

BM: "Kwa tafsiri nyingine hapa una maanisha nimuache Shemeji yako Annie sio?"

Mshkaji: "Hapana! Mimi sijasema hivyo ila huyo ambaye upo tayari kuacha Kazi ili tu uwe nae nina uhakika mambo kama yatakuendea hovyo atakuja kukuacha wewe"

BM: "Inawezekana lakini sio kwa yule mtoto"

Nilivyomuambia hivyo jamaa akacheka sana huku akitingisha kichwa left-right, nikaona huyu acha nimuage pengine zishaanza kumuingia, nikarudi zangu nyumbani, Sasa Wakati wa kurudi nipo kwenye daladala si tukapita Buguruni nikatamani nishuke nikacheki wale madogo lakini nafsi ikasita kwamba pengine nitapoteza tu muda kama nilivyopoteza mchana

Nimefika mjengoni nawaza kumpigia Caryn nimjulishe kwamba madogo sijawaona, nikaona huyu hata nikimjulisha hata nisaidia chochote zaidi ya kunisema, nikapiga zangu usingizi kesho yake nikatinga tena Buguruni, raundi hii nimeenda Asubuhi sana kama saa 2 na Dakika zake lakini nikakuta bila bila tena

Sasa yale maneno alioongea Caryn ni kama yanatimia ivi, nikarudi zangu home, unajua kipindi hiko sina ratiba maalum nipo nipo tu, siunajua tena ukipatiwa likizo ambayo hata hukuiwazia wala kuipanga unatamani kusafiri lakini huwezi juu ukisafiri kuna mambo yatasimama

Ilivyofika mida ya jioni nikarudi Mungu sio Mandonga nikamkuta yule Dogo wa kiume na mdogo wake wa kike Kaka yao alikuwa hayupo, Nikamuuliza yule Dogo janja Asubuhi mlikuwa wapi, na Jana pia nilikuja lakini sikuwakuta, Akanambia kama hawapo pamoja na kaka yao basi huwa wanakwenda kushinda na watoto wenzao huko mitaani,

Dogo akanielekeza Kaka yake anapopatikana kwa muda huo ambapo ni Ilala kuna mtaa unaitwa Ya Mungu Mengi

Ipo hivi, kumbe Kaka mtu asipopata kibarua Cha kumuingizia pesa basi humlazimu kwenda kuomba kazi kwenye migahawa ya kusafisha vyombo na malipo yake huwa ni Chakula

Basi nikaenda hadi kwa huo mtaa mgahawa kwa mgahawa sikufanikiwa kumuona nikarudi kule kwa madogo tukachoma sana mahindi tukimsubiria kaka yao hadi giza linakaribia kuingia ndio Kaka mtu anafika


Kaka mtu alikuja na kifuko ambacho alibebea msosi, Sasa muda wote nipo pale kumbe madogo walikuwa wamepiga pasi ndefu yani mchana hawajauona, kikatolewa kitu Cha wali pale kilikuwa kimefungwa kwenye foil, nikaacha wamalize kula baada ya kushiba nikawaambia Leo mnahama makazi hii sio sehemu sahihi ya kuishi

Nikawaelekeza Kila Kitu madogo wakaelewa, nikampigia simu sister kumjulisha kuwa madogo nimewapata, sisi hao tukafunga safari hadi Yombo tukafika kwenye saa mbili kasoro usiku

Sister katika harakati za kuandaa chakula kama mnavyojua familia zetu za hali ya chini kwenda na mahesabu ni lazima, sister akaniuliza kama nitakula ili anihesabu nikamjibu "hapana, hata hivyo nawaacha muda si mrefu, pia sidhani kama hawa wenzenu watakula" kusema hivyo yule dogo wa kiume akadakia "watuhesabu tu na sisi kaka"

Nilidhania wako sawa, basi sio kesi sister utawahesabu, Mimi sikupoteza muda nikahepa zangu japokuwa sister alisisitiza kesho niende kwaajili ya kumpeleka yule Dogo wa kike hospital maana afya yake ilikuwa hairidhishi,

Kweli kesho yake mapema tu nipo Yombo, nikamchukua Dogo nikampeleka hospital akakutwa na mataifodi malaria [emoji3082] nikaandikiwa dawa nikamrudisha nyumbani, tukashinda wote pale kwa sister mida ya jioni nikarudi zangu kwangu

Jumapili kama kawaida ni siku ya kwenye kwa Mzee ila kwa kipindi hiki ambacho amesafiri huwa naenda hata mara mbili kwa wiki, sasa hivi nikiwa nimeshazoeana na Caryn kidogo nikampigia simu kumuuliza kama yupo home akanambia kuwa ametoka ila anarudi muda sio mrefu nyumbani yupo Mama na Michelle

Nikaenda kweli nikamkuta Michelle na Mama yake, nilichogundua ni kwamba Michelle na Mama yake wanapatana sana halafu Caryn yeye kwa Mzee ndio humuambii kitu, hata kwenda Kazini Bi mkubwa anaongozana na Caryn kwasababu ya heshima ya Mzee tu ila kipenzi Cha Bi Mkubwa ni Michelle

Niliwakuta wanapiga story kama mtu na rafiki yake, nikawajoin japokuwa sikuwazoea kivile kama ilivyo kwa Mzee mwenyewe au Caryn japo kwa uchache.

Ilivyofika mida flani hivi ya jioni Caryn akafika kama kawaida yake yupo na Jeep Wrangler ya 2020 Diesel Engine akalipark, akatukuta mimi na Michelle tunapiga story Mama alituacha na kwenda kusaidiana na Dada wakazi jikoni

Caryn: "BM nilijua sitokukuta"

BM: "Hata hivyo ndio nataka kuondoka muda sio mrefu"

Michelle: "Leo itabidi ulale BM, Kila siku unakuja tu na kuondoka"

BM: "Dada Michelle nitalala siku nyingine wala usijali"

Basi nikamuaga Bi Mkubwa, Michelle akanisindikiza hadi nje getini nikaondoka

Zikapita kama wiki 2 ivi Caryn akanitafuta ilikuwa weekend akaniomba tukutane Morocco mida ya mchana, mimi ndio niliwahi kufika akanipitia, tulivyokuwa Morocco akapinda na ile njia ya kuelekea Kawe mbele tukaingia Barabara ya Masaki

Tulienda hadi kwenye Apartments flani akapark gari parkings za nje, tukaingia ndani tukamkuta mlinzi, Sasa kile kitendo Cha kuingia tu ndani ya geti Caryn akachange ghafla

Caryn: "BM naomba niletee simu yangu kwenye Gari"

Nikafata Simu lakini kinyonge sana nilihisi kama vile kanikosea heshima, huyu Binti nimempita miaka mitatu three good years nikampelekea simu yake ni kama kuna mtu alikuwa anataka kumpigia

Caryn: [emoji338]"Tell me where are you now, is this how you work
You call yourself an estate manager but you're nowhere you are managing, Nothing
Look at the whole compound so messy, look at trash everywhere, people are packing anyhow"

Kwa maongezi hayo nikajua tu kwamba huyu anayeongea na Caryn atakuwa ni Manager wa hizi apartments, kwa maana hiyo hizi apartments zitakuwa za Mzee, maana nilisikia Mzee ana apartments Masaki ila sikuwahi kuziona, muda huo Caryn anaendelea kuongea na huyo manager ila sikuwa namsikia manager anachokijibu


Caryn: "Get yourself another job because I no longer consider you fit to be my estate manager"[emoji3513]

Caryn akakata simu, nikamuuliza kwani kuna tatizo?

Caryn: "Huyu mtu anajiita manager lakini hana anachokifanya, ona kulivyokuwa hovyo, na Baba ndio anamuendekeza sasa mimi namuondoa hapa natafuta mtu mwingine"

BM: "Lakini Caryn mm naona ungewasiliana na Mzee kwanza kabla hujafanya maamuzi pengine anaweza kukushauri jambo"

Caryn: "Namjua yule Mzee hana atakachonishauri zaidi ya kunambia nimuache, hizi huruma zake ndivyo zinafanya watu wamuharibie kazi"

Wakati tunatoka nje ya Geti yeye akabaki sijui alikuwa anaongea Nini na mlinzi hata maongezi yao sijayasikia, tukaiacha Masaki tukaenda hadi Sinza tukaingia kwenye Duka kubwa la nguo za kike na za kiume


Hii siku nilikuwa kama mkia kila anapoenda Caryn mimi nipo nyuma yake, tulivyoingia kwenye lile Duka Caryn alienda moja kwa moja kwenye meza ya Muuzaji (Mdada) na mimi nikamfuata

Caryn: "Boss find your corner and hang yourself there"

Nikatafuta sehemu nikakaa nikamuacha na yule mdada wa Dukani, zimepita kama Dakika 15 akanifuata nilipokaa ikabidi nimchane

BM: "Caryn, this habit of yours has to stop"

Caryn: "I don't understand, what are you talking about?"

BM: "We jua tu sijapenda, nisiongee sana"

Caryn: "Achana na hizo habari, tujadili nilicho kuitia hapa"

BM: "Ushanikata mood, we ongea nakusikiliza"

Akagundua nipo off mood na sikuwa comfortable tena pale Dukani, akanambia basi tuondoke tutafute sehemu tunywe hata juice, tukaondoka pale Dukani tukaenda maeneo ya Mlimani City lakini sio kule ndani, hii inakuwa ni mara ya pili kuja hapa, mara ya kwanza tulitoka wote out kuanzia Bi Mkubwa, Mimi, Michelle pamoja na Caryn

Nikaagiza juice na msosi, Caryn akaagiza juice tu, maongezi yakaanza

Caryn: "BM umeliona lile Duka, ule mzigo wote ni kutoka Uturuki, nataka nichanganyie nianze kuagiza mizigo kutoka china"

BM: "Sasa si uagize mbona ni simple tu"

Caryn: "Ndio maana nikakuita ili unisaidie, nataka kuagiza mizigo kupitia Kampuni unayofanyia kazi Najua wewe ndio unaepokea mizigo ila Baba asijue"

BM: "Kwann hutaki Mzee ajue, unajua Kuna maamuzi mengine unayoamu ni muhimu sana kumshirikisha Mzee kwasababu huwezi jua risk itakayotokea badae"

Sasa mm nimeongea hivyo nikijua lile Duka nalo ni la Mzee ambapo Caryn ameambiwa asimamie

Caryn: "Tatizo unaongea sana halafu hutaki kufuatisha ninachokuelekeza, kwanza lile Duka ni la kwangu, ndio maana nimekuambia sitaki Mzee ajue, na sio Mzee tu, hadi Michelle na Mama"

Nikawa kama vile nimezubaa hivi, maana hilo Duka analodai ni la kwake nikahisi ni kamba napigwa

BM: "Bado hujanishawishi, kama Duka kweli ni la kwako kwanini umeniamini mimi nilijue halafu Mzee umemficha, nikivujisha Siri je?"

Caryn: "Siri Najua huwezi kuvujisha, na wewe kulijua duka haimaanishi wewe ni mtu spesho sana kwangu, bali imetokea tu kwasababu nataka tufanye kazi,"

BM: "Kazi gani?"

Caryn: "Kuna Suppliers kutoka china nimewapata lakini bei zao sio nzuri sana, so nilikuwa nakuomba unitafutie supplier mwenye bei Nzuri, Najua kwako itakuwa rahisi kwasababu kazi yako una deal na wafanyabiashara"

BM: "Sawa, acha tuone"

Caryn: "Kwani kazini una report lini?"

BM: "Bado kama wiki 2 ivi"

Tushamaliza kula, ule muda pendwa wa kulipa bill umefika, Dah! hapa Caryn aliniacha hoi, muhudumu kaja kuchukua pesa eti anamuuliza juice 2 ni shillings ngap? muhudumu akamuambia 10k, Caryn akatoa elfu 10 Kama ilivyo

BM: "Sasa mbona unalipia juice tu, na chakula?

Caryn: "Chakula analipa aliyekula, mimi nimetoka na hesabu ya juices mbili tu, kama ulikuwa na njaa ungesema mapema"

BM: "Kwahiyo unataka kuniambia hapo ulipo unakosa elfu 15 ya kulipa sahani moja ya chakula?"

Caryn: "Naweza kuamrisha mwenye hii hotel atoe watu wote humu ndani ubaki wewe tu na uagize unachotaka halafu wanilipishe kwa Kila meza na nikalipa bila shida, ila siwezi kufanya huo upuuzi coz haikuwa katika ratiba zangu"

Nikanote kitu kingine kipya kutoka kwa Caryn, Yani kila ninavyozidi kuwa karibu nae ndio nazidi kumsoma ni mtu wa aina gani, nikawa Sina budi kulipa Ile 15k ya msosi tukaondoka, Cha ajabu sasa tukapitia petrol station [emoji618] akaweka mafuta ya laki 2, nikashindwa kuvumilia

BM: "Ila Caryn hapa ndio sijakuelewa kabisa! kule restaurant umeniachia bill ya elfu 15 nilipe, hapa petrol station umeweka Diesel ya laki 2, na hii safari ni wewe ndio umeniita"

Caryn: "Yani bado ume catch! sikiliza nikuambie, Wakati natoka nyumbani nilitoka nikijua nitapita petrol station kuweka mafuta, so niliandaa pesa yake, na wakati tunatoka pale Dukani kwangu nilitoka na budget ya kunywa juice tu, elfu 15 ni pesa ndogo sana lakini haifai kutumia pesa eti kwasababu tu uko nayo"

BM: "Ni kweli lakini hujafanya poa, sijapenda kabisa...kama ningekuwa sina pesa je?"

Caryn: "Next time utajipanga, we Mwanaume utafikaje sehemu na kuanza kuagiza huku ukijua huna pesa"

BM: "Madam niache hapa hapa, na Asante kwa treatment"

Ilikuwa ni Tabata reli, nikashukia hapo maana niliona miyeyusho tu, Kesho yake mapema sana Annie akatinga mjengoni, wenzake wanakuja usiku yeye anakuja Asubuhi Sasa sijui ana maana gani, akanikuta nilikuwa bado sijaamka

Annie: "Babe ivi una matatizo gani? kwanini unanifanyia hivi lakini?"
(Annie aliongea hiyo sentensi kwa hisia za hudhuni sana)

BM: "Haya kumekucha! nimefanya nini tena?"

Annie: "Sikujua kama unaletaga Wanawake zako humu ndani nikiwa sipo, mwenyewe unajikuta mjanja kuwahi kuwatoa Asubuhi Asubuhi"

BM: "Unajua sikuelewi!"

Annie: "Hunielewi kitu gani Wakati humu Leo umelala na Mwanamke, Jana usiku nimepiga simu yako akapokea huyo mwanamke"

Duh! huyo atakuwa ni Caryn, si nilisahau simu yangu Jana kwenye Gari yao asee, sasa nikawa nawaza jibu la kumpa Annie huku nikiwaza kwann Caryn amepokea simu yangu na atakuwa amemjibu nini Annie hadi amepanic hivi


Itaendelea...
....
 
Ilipoishia

BM: "Ebu funguka sijakuelewa"

Mshkaji: "Labda nikuulize wewe, likizo yako inakaribia kuisha umeamuaje kuhusu kazi?"

BM: "Kazi nitapiga kama kawa, nitajua jinsi ya kumpanga yule mtoto (Accountant)"

Mshkaji: "Sasa acha nikupe mchoro mzima, hii ni kama ramani na uko vitani ukikosea kuisoma hii ramani unajikuta kwa adui na kumbuka huna siraha"

Muendelezo


SEASON 2 Episode 4


BM: "Nakusikiliza kiongozi"

Mshkaji: "Unajua sometimes inabidi utumie akili kwenye kufanya maamuzi, ukiweka hisia mbele kwenye kila kitu utafeli, kwanza kabisa mruhusu Demu wako aende Mwanza, usipomruhusu utajipiga pini mwenyewe"

BM: "Then nikishamruhusu?"

Mshkaji: "Ukishamruhusu utajua unaishi vipi na yule Demu wako wa Ofisini kule, unajua yule ndio amekuweka mjini, hata kama humpendi wewe igiza kumpenda hutapungukiwa chochote sana sana ndio una gain"

BM: "Huu Ushauri wako wa leo sijauelewa kabisa"

Mshkaji: "Hujauelewa kwasababu umeweka Mapenzi mbele hivyo unatumia sana hisia katika kuamua mambo, Leo upo tayari kuacha Kazi kwaajili ya mwanamke lakini nikuhakikishie mwanamke huyo huyo atakuja kukuacha wewe kwasababu huna kazi"

BM: "Sawa nimekuelewa, vipi ule mchongo wako wa mkoa, ulitiki?"

Nikachange mada makusudi, tukaendelea na story zingine hadi giza likaingia tukaagana, mimi nikarudi zangu home, nimefika mjengoni nimemkuta Annie kalala Sebuleni kwenye kochi,

Kabla sijamuamsha nikakaa kwenye kochi lingine nikakumbuka kile alichoniambia Mshkaji wangu kule Kinondoni, niliwaza sana na kuuchambua ule ushauri nikaona una make sense, nikamuamsha Annie

BM: "Vip mbona umelala mapema sana, uko sawa?"

Annie: "Niko poa, ni uchovu tu usingizi umenipitia muda sio mrefu"

BM: "Ungeenda kulala ndani, Vipi lakini Kuna chochote kitu?"

Annie: "Yeah, mimi nilishakula labda kama nakuwekea wewe tu"

BM: "Hapana, nitakula badae wewe nenda kalale tu...ila kabla hujaenda kulala Kuna jambo nataka nikuulize"

Annie: "Jambo gani?"

BM: "Kuhusu kazi uliyoniambia umepata, ni kazi gani?"

Annie: "Kazi ya Bank [emoji542]"

BM: "Ooh! Bank gani?"

Annie: "Bank flani ya Wahindi inaitwa I&M Bank"

BM: "Hii Kazi Annie umeipataje?"

Annie: "My Uncle ndio ameni connect ila yeye ananyia hapa Dar"

BM: "Ni sawa, unaweza kwenda hiyo kazi, ila utafanya kwa Mwaka mmoja tu"

Annie: "Usijali Mimi nimesha change mind siendi tena"

BM: "Kwanini!?"

Annie: "Si ulikataa wewe, kilichokufanya ukubali Sasa hivi ni nini?"

BM: "Kuna mambo mengi nimewaza nikahisi kama nilifanya maamuzi ubinafsi, unajua maisha yako pia inabidi yaendelee"

Annie: "Kweli nataka kwenda kufanya hiyo Kazi lakini nafsi yangu ghafla imekuwa nzito sijui kwanini"

BM: "Ni kawaida hiyo, we fanya maandalizi ya Kila kitu kwaajili ya safari"

Kwa mara ya kwanza kufuata ushauri wa mshkaji, maana jamaa nae miyeyusho kinoma, basi Annie akaenda zake kulala Mimi nikazuga na picha moja la Thriller ilivyoisha nikaunga tela kulala

Siku zikakatika Safari ya Annie ikakaribia hapo mm nimebakiza wiki moja tu likizo yangu kuisha, sasa ndio nikawa namlazimisha Annie kusafiri, Nakumbuka nilimkatia Ticket ya ndege nikampatia na milioni 3, nilivyompa hiyo Pesa Account yangu Balance ikasoma 4.1 m

But nilimpatia kiasi kile Cha pesa kwasababu sikutaka mshahara wake auingize kwenye kulipa Kodi ya nyumba,

Siku ya safari ikafika nikamsindikiza hadi Airport mtoto asianze kutoa machozi? nikamu hug hug kidogo nikahisi kama tuko Telemundo, mwisho wa picha Annie aliingia kwenye Air Precious

Plan A[emoji3514]

Nilivyotoka Airport straight nikaunga Kino kwa Mshkaji, unajua sikumwambia kama nimefata vile alivyonishauri, Mshkaji alinambia yupo maghetton nikamtimbia,

Nilivyofika Maghetton kwa mshkaji nikamuelezea kila kitu, nikamuambia yani hapa unavyoniona nimetoka Airport kumsindikiza Annie kaenda Mwanza, jamaa kama hakuamini akawa anaitikia Ile design ya mtu kumsapoti kile anachoongea

Alikuja kuamini Annie alivyonipigia simu kunijulisha kwamba amefika, Mshkaji ndio akaamini kumbe mchongo ni serious

Mshkaji: "Mimi nikajua unatania kumbe Demu ameng'oa kweli, Sasa hapa unaweza kufanya mambo yako fresh mwanangu"

BM: "Ila haya maamuzi nimefanya kwa kukurupuka sana, sikupata muda wa kutafakari vizuri"

Mshkaji: "Muda wa kutafakari ulishapita, Sasa hivi Cha kufanya mcheki Demu wako ****(Accountant) Anza kumsogeza taratibu hiyo ndio kazi iliyobaki"

Kwahiyo Plan B ilikuwa ni kumsogeza Accountant karibu, yani nianze kujibebisha kwake mbaya zaidi sikuwahi kumtafuta tangu nimeondoka pale ofisini na Cha ajabu yeye pia hajawahi hata kunibeep kitu ambacho sio kawaida yake

Basi Mshkaji akanipanga mambo ya kufanya, design sasa ikawa kama namsikiliza yeye kwa kila kitu,

Siku isiyokuwa na Jina nimeamka na mood Nzuri si nikampigia simu Accountant, hapo zimebaki siku 5 tu nirudi job ila kabla ya kurudi inabidi niwe nimefanya maamuzi ya kumkubali Accountant kimapenzi ili niendelee na Kazi (nimkatae Annie) au niache kazi nimkatae Accountant nibaki na Annie

BM: [emoji338]"Mambo"

Accountant: "Finally...hii simu nilikuwa naisubiria kwa hamu"

BM: "Ooh! uko wapi?"

Accountant: "Kazini"

BM: "Tunaweza kuonana Leo baada ya masaa ya kazi?"

Accountant: "Wewe tu"

BM: "Sawa basi nitakujulisha Mahali tutakapokutana"

Masaa nayo kwani yanakawia basi, jioni ndio hiyo Accountant nilishamtumia Location, tukakutana tena Mimi ndio nilimkuta yeye tukaagizia vinywaji story zikaanza, Wakati nampigisha story zingine nikawa nawaza jinsi ya kuingizia agenda yangu

BM: "Ivi ni Jumanne ndio likizo yangu inaisha eeh?"

Accountant: "Yeah, kwani unakuja kazini?"

BM: "Sasa kwanini nisije, si likizo imeisha"

Accountant akaniangalia kwa sekunde kadhaa Nikamuuliza "vipi kuna tatizo?"

Accountant: "Kuna Kitu una maanisha ila hutaki kufunguka, kama unakuja kazini ina maana umekubaliana na mimi yale matakwa yangu, right?"

BM: "Hayo mambo Tutaongea vizuri siku nyingine wala usijali"

Accountant: "Sasa hapa umeniitia Nini? umekuja kunipotezea muda wangu tu"

BM: "Okay! Relax, sasa hivi nimeamua kutulia na wewe lakini huku kupanic kwako ni moja ya sababu iliyonifanya nichelewe kufanya haya maamuzi"

Accountant: "Vipi kuhusu kidemu chako?"

BM: "Huyo nishaachana nae, ni Bora hata hili limetokea mapema maana nilikuwa tayari kuacha Kazi kwaajili yake"

Accountant: "Ooh, now I got your point, so mimi nipo hapa kama Option"

BM: "Hilo sasa umelisema wewe, ninachojua tu Mimi kwasasa nimefanya maamuzi sahihi katika Wakati sahihi"

Accountant: "But you guys mlikuwa mnapendana sana kiasi kwamba nilijua hamtoachana"

BM: "You know Love can be really without being forever"

Accountant: "Bado ni ngumu kuamini, there something fish"

Nilivyomtamkia Accountant kwamba nataka kuwa nae alifurahi sana lakini Bado hakuamini kama ni kweli nimeachana na Annie ila nikaendelea kumpiga kiswahili hadi akanielewa

Nikaachana na Accountant pale kila mtu akielekea njia yake Wakati tunaagana eti akataka kuja kulala kwangu ili a confirm kama ni kweli Annie nimeachana nae, nikamkataa kiaina bila ya kumkwaza maana Sasa hivi ni mwendo wa kula na kipofu

Weekdays zikapita, Weekend ikaanza nakumbuka siku ya jumapili mapema sana Sister Michelle akanicheki akaniomba niende home kuonana nae after church,

Ilivyofika saa Saba Mimi ndio huyo mdogo mdogo hadi kwa Mzee, nilivyofika Kona ya mwisho ya kuelekea nyumbani kwa Mzee kwa mbali naliona Jeep, nikajua tu huyu atakuwa ni Caryn bila shaka na kweli alivyonikaribia akasimamisha Gari

Caryn: "Hata kama ni ubahili hapana aise, BM umekosa hata elfu 2 ya pikipiki kweli?"

BM: "Nipatie hiyo elfu 2 nirudi highway nikapande hiyo bodaboda"

Caryn: "Nyumbani unaenda kufanya nini Sasa watu wenyewe hawapo, aliyekuwa amebaki ndio huyu anaishia"

Sasa Michelle Atakuwa na Akili gani ya kuniita halafu tena atoke, nikajisemea tu mwenyewe moyoni, Basi Caryn akanilazimisha niingie kwenye Gari, sisi hao breki Sinza Dukani kwake

Caryn: "BM Ivi ni maeneo gani mazuri ya kununua viwanja?"

BM: "Maeneo ninayoyajua Mimi kwasasa ambayo ni potential ni Kigamboni na Bagamoyo"

Caryn: "Bagamoyo hapana, nataka eneo ambalo naweza kufanya makazi"

BM: "Basi Kigamboni pata kufaa, hata Mimi nataka kuhamia huko"

Caryn: "Umeshajenga Kigamboni?"

BM: "Nahamia kwenye vi appointment tu, pesa ya kujenga natoa wapi Mimi sasa hivi"

Caryn: "If I were you ningekuwa nishajenga, kazi unayofanya ina pesa sana the problem is, you don't know where to stand"

BM: "Ila Caryn bhana huwa unanifurahishaga sometimes, sasa mimi na wewe Kuna tofauti gani au ni nani anastaili kumcheka mwenzake?"

Caryn: "Mimi kama sio Biashara ningekuwa nishajenga, nilitaka kwanza Biashara yangu ikomae vizuri"

Majibu mdomoni yakaniisha, najibu nini tena hapo, ghafla nikawa mnyonge, moyoni nikasema hii chance safari hii sitaki kuichezea, yani hadi Caryn kajua ninapopiga kazi kuna hela na hadi sasa hivi sijafanya jambo la maana

Nikapata wazo la kumshirikisha Caryn kwenye kipengele nilichonacho kazini nione kama anaweza nishauri jambo ingawa tayari nishampanga Accountant akapangika, nimepata ujasiri na kuhisi ni salama kumshirikisha Caryn kwasababu nae naona ananishirikisha kwenye baadhi ya mambo yake


Nilichokifanya Sasa nikamuelezea Caryn mkanda mzima, jinsi nilivyopata kazi kupitia huyo mwanamke na kuniwekea kizingiti Cha kutokurudi kazini hadi nimkubalie, kifupi nilimueleza Kila kitu kasoro upande wa Annie Ndio sijamueleza chochote, Baada ya kusikiliza maelezo kwa makini Caryn alianza kwa kuniuliza tena swali ambalo kwenye maelezo lilishajijibu

Caryn: "Do you love her"

BM: "I don't love her"

Caryn: "So you have no feelings for her and you've been sleeping with her!?"

BM: "We've been sleeping together for fun, there's no attachments it's called friends with benefits"

Caryn: "Well she got attached while you were playing your game of friends with benefit she fell in love with you

BM: "That girl is not close to what I want in a wife, not mentally, not educationally, not psychological"

Caryn:"So what do you want?"

BM: "Your advice"

Caryn: "Quit"

BM: "Una maanisha niache kazi?"

Caryn: "We fanya kama nilivyokuambia"

Huu Ushauri umekuja too late wakati ambao nimeshafanya maamuzi, sasa kulikuwa na haja gani ya kumruhusu Annie kwenda Mwanza mbaya zaidi nishajishusha kwa Accountant na mambo yalikuwa yashanyooka,

Wakati naendelea kuongea na Caryn, Michelle akapiga simu, Sasa vile simu ilivyokuwa nikaiangalia halafu nikamuangalia na Caryn, Caryn akahisi kitu akaniuliza "ni nani?" nikamjibu ni Michelle anapiga, akanambia "Achana nae utaongea nae badae"

BM: "Labda Kuna emergency anataka usaidizi"

Caryn: "Usaidizi gani bhana mtu nimemuacha yupo nyumbani"

BM: "Dah! we si umeniambia ametoka wewe, au sio wewe?"

Caryn: "Sasa ulitaka kwenda kushinda nae nyumbani mkifanya nini?"

BM: "Alinipigia simu bhana alitaka mazungumzo na Mimi huwezi jua alitaka kunambia nini"

Caryn: "Mimi namjua Michelle vizuri kinachomsumbua sasa hivi ni Mapenzi hana anachowaza pale mwenzako zaidi ya hicho"

BM: "We umejuaje? usipende kumuongelea mtu pengine mwenzako ana mambo yake mengine"

Caryn: "Unajua wewe umetujua juzi tu hapa, Mimi yule sio Dada yangu tu, we used to be very close, we used to be friends, so nikikuambia kitu kuhusu yeye Jua Nina uhakika nacho

BM: "Sasa kwanini Sasa hivi hamna ukaribu huo tena?"

Caryn: "Alinikosea, Alinikosea sana Yani pakubwa mno"

BM: "Alikukosea nini?"

Caryn: "Kama nilivyokuambia Mimi yule sio Dada yangu tu Bali alikuwa rafiki yangu pia, na unaijua sifa ya urafiki? So siwezi kukuambia alichonifanyia ila we Jua tu alinikosea"

BM: "Ila yeye kanambia, kanielezea kila kitu

Caryn: "Sasa yeye ni sawa kufanya hivyo kwasababu yeye ndio mkosani ila nikianza mimi kuongea kwa kila mtu atajisikia vibaya"

BM: "Lakini wewe si ulimsema kwa Mzee"

Caryn: "Lini? na saa ngapi?"

BM: "Kuna siku ulimsema bhana tena nikiwepo hiyo sijahadithiwa Wala nini, ulimsema kuhusu huyo Mwanaume wake mbele ya Mzee

Caryn: "Sasa vile ndio kumsema? vile si ni vitu vya kawaida tu, je ningeamua kusema vyote? and I'm sure hata wewe hajakuambia mambo yote"

BM: "Sioni Ubaya wa Sister Michelle ni kuteleza tu ameteleza, unajua sister ako yuko humble sana hana mambo mengi na ni muelewa"

Caryn: "Eti eeh! Okay"

Ilivyofika jioni nikamuacha Caryn Dukani kwake Mimi nikaenda kwa sister Yombo nikapiga na msosi huko huko nikarudi zangu Tabata

Kesho yake Jumatatu nakumbuka ilikuwa Nanenane hii siku sikutoka kabisa ndani ila mida ya jioni akaja Mshkaji wangu wa Kinondoni, alikuwa katika mishe mishe zake huku huku Tabata alivyomaliza akapitia mjengoni, akanikuta nabrash viatu

Mshkaji: "Nakubali mwanangu, kesho kazini sio"

BM: "Kama kawaida"

Mshkaji: "Nakubali, angalau siku hizi ushauri wangu unauzingatia....hujapika Mzee nina njaa kiseng*"

BM: "Mm huwa sipikagi, kwani hoteli zimefungwa huko ulipotoka?"

Mshkaji: "Hapo ndipo unapofeli"

Hii siku mshkaji aliangusha kwangu, mida mida tulienda kufinya msosi tukarudi mjengoni tukalala, ila sasa jamaa akagoma kulala chumbani akaenda kulala Sebuleni kwenye kochi

Tarehe 9 mwezi wa 8 (Jumanne) siku ya kuripoti kazini mapema tu nikajiandaa nikamuamsha na mshkaji sababu alitaka tutoke wote

Wakati nipo njiani nimeshaachana na mshkaji naelekea kazini kichwani nawaza kipi Cha kufanya na kipi Cha kuacha, kichwani wananijia watu wawili Caryn na mshkaji wangu, Caryn kanambia niache kazi huku Mshkaji kanambia niendelee na Kazi, Hadi nafika Ofisini Bado nipo njia panda

Nikasalimiana na staff wenzangu Accountant muda huo alikuwa hayupo nimeambiwa kaenda Bank ila Mama yake yani Bosi yupo Ofisini kwake, Mnyamwezi nikachoma ndani

Mama Accnt: "Karibu mwanang, Hujambo?"

BM: "Sijambo Mama Shikamoo"

Mama Accnt: "Marhaba mwanangu tulikumiss sana na umekuja Wakati muafaka huyu mwenzako uliyemuachia majukumu anaelemewa na Kazi?"

BM: "Bado haja Master tu? sababu akikwama huwa ananipigia simu namuelekeza"

Mama Accnt: "Tatizo ni kwamba mwenzako hajui kuongea na TRA kabisa, na hajui kubagain, kabla sijakuachia majukumu yangu itabidi uendelee kwenda nae trips kadhaa hadi atakapokuwa sawa"

BM: "Ni sawa, lakini Mama unajua Mimi nimekuja kukuaga, nimeona nikafanye majukumu mengine kwahiyo nilikuwa naomba ruksa yako"

Mama huwa anavaa miwani, kusikia hivyo akavua kwanza na mawani yenyewe, kuna vitu alikuwa anaandika akaacha akaweka peni chini yani ni kama vile hakutarajia kusikia nilichomuambia

Itaendelea
 
Ilipoishia

BM: "Ebu funguka sijakuelewa"

Mshkaji: "Labda nikuulize wewe, likizo yako inakaribia kuisha umeamuaje kuhusu kazi?"

BM: "Kazi nitapiga kama kawa, nitajua jinsi ya kumpanga yule mtoto (Accountant)"

Mshkaji: "Sasa acha nikupe mchoro mzima, hii ni kama ramani na uko vitani ukikosea kuisoma hii ramani unajikuta kwa adui na kumbuka huna siraha"

Muendelezo


SEASON 2 Episode 4


BM: "Nakusikiliza kiongozi"

Mshkaji: "Unajua sometimes inabidi utumie akili kwenye kufanya maamuzi, ukiweka hisia mbele kwenye kila kitu utafeli, kwanza kabisa mruhusu Demu wako aende Mwanza, usipomruhusu utajipiga pini mwenyewe"

BM: "Then nikishamruhusu?"

Mshkaji: "Ukishamruhusu utajua unaishi vipi na yule Demu wako wa Ofisini kule, unajua yule ndio amekuweka mjini, hata kama humpendi wewe igiza kumpenda hutapungukiwa chochote sana sana ndio una gain"

BM: "Huu Ushauri wako wa leo sijauelewa kabisa"

Mshkaji: "Hujauelewa kwasababu umeweka Mapenzi mbele hivyo unatumia sana hisia katika kuamua mambo, Leo upo tayari kuacha Kazi kwaajili ya mwanamke lakini nikuhakikishie mwanamke huyo huyo atakuja kukuacha wewe kwasababu huna kazi"

BM: "Sawa nimekuelewa, vipi ule mchongo wako wa mkoa, ulitiki?"

Nikachange mada makusudi, tukaendelea na story zingine hadi giza likaingia tukaagana, mimi nikarudi zangu home, nimefika mjengoni nimemkuta Annie kalala Sebuleni kwenye kochi,

Kabla sijamuamsha nikakaa kwenye kochi lingine nikakumbuka kile alichoniambia Mshkaji wangu kule Kinondoni, niliwaza sana na kuuchambua ule ushauri nikaona una make sense, nikamuamsha Annie

BM: "Vip mbona umelala mapema sana, uko sawa?"

Annie: "Niko poa, ni uchovu tu usingizi umenipitia muda sio mrefu"

BM: "Ungeenda kulala ndani, Vipi lakini Kuna chochote kitu?"

Annie: "Yeah, mimi nilishakula labda kama nakuwekea wewe tu"

BM: "Hapana, nitakula badae wewe nenda kalale tu...ila kabla hujaenda kulala Kuna jambo nataka nikuulize"

Annie: "Jambo gani?"

BM: "Kuhusu kazi uliyoniambia umepata, ni kazi gani?"

Annie: "Kazi ya Bank [emoji542]"

BM: "Ooh! Bank gani?"

Annie: "Bank flani ya Wahindi inaitwa I&M Bank"

BM: "Hii Kazi Annie umeipataje?"

Annie: "My Uncle ndio ameni connect ila yeye ananyia hapa Dar"

BM: "Ni sawa, unaweza kwenda hiyo kazi, ila utafanya kwa Mwaka mmoja tu"

Annie: "Usijali Mimi nimesha change mind siendi tena"

BM: "Kwanini!?"

Annie: "Si ulikataa wewe, kilichokufanya ukubali Sasa hivi ni nini?"

BM: "Kuna mambo mengi nimewaza nikahisi kama nilifanya maamuzi ubinafsi, unajua maisha yako pia inabidi yaendelee"

Annie: "Kweli nataka kwenda kufanya hiyo Kazi lakini nafsi yangu ghafla imekuwa nzito sijui kwanini"

BM: "Ni kawaida hiyo, we fanya maandalizi ya Kila kitu kwaajili ya safari"

Kwa mara ya kwanza kufuata ushauri wa mshkaji, maana jamaa nae miyeyusho kinoma, basi Annie akaenda zake kulala Mimi nikazuga na picha moja la Thriller ilivyoisha nikaunga tela kulala

Siku zikakatika Safari ya Annie ikakaribia hapo mm nimebakiza wiki moja tu likizo yangu kuisha, sasa ndio nikawa namlazimisha Annie kusafiri, Nakumbuka nilimkatia Ticket ya ndege nikampatia na milioni 3, nilivyompa hiyo Pesa Account yangu Balance ikasoma 4.1 m

But nilimpatia kiasi kile Cha pesa kwasababu sikutaka mshahara wake auingize kwenye kulipa Kodi ya nyumba,

Siku ya safari ikafika nikamsindikiza hadi Airport mtoto asianze kutoa machozi? nikamu hug hug kidogo nikahisi kama tuko Telemundo, mwisho wa picha Annie aliingia kwenye Air Precious

Plan A[emoji3514]

Nilivyotoka Airport straight nikaunga Kino kwa Mshkaji, unajua sikumwambia kama nimefata vile alivyonishauri, Mshkaji alinambia yupo maghetton nikamtimbia,

Nilivyofika Maghetton kwa mshkaji nikamuelezea kila kitu, nikamuambia yani hapa unavyoniona nimetoka Airport kumsindikiza Annie kaenda Mwanza, jamaa kama hakuamini akawa anaitikia Ile design ya mtu kumsapoti kile anachoongea

Alikuja kuamini Annie alivyonipigia simu kunijulisha kwamba amefika, Mshkaji ndio akaamini kumbe mchongo ni serious

Mshkaji: "Mimi nikajua unatania kumbe Demu ameng'oa kweli, Sasa hapa unaweza kufanya mambo yako fresh mwanangu"

BM: "Ila haya maamuzi nimefanya kwa kukurupuka sana, sikupata muda wa kutafakari vizuri"

Mshkaji: "Muda wa kutafakari ulishapita, Sasa hivi Cha kufanya mcheki Demu wako ****(Accountant) Anza kumsogeza taratibu hiyo ndio kazi iliyobaki"

Kwahiyo Plan B ilikuwa ni kumsogeza Accountant karibu, yani nianze kujibebisha kwake mbaya zaidi sikuwahi kumtafuta tangu nimeondoka pale ofisini na Cha ajabu yeye pia hajawahi hata kunibeep kitu ambacho sio kawaida yake

Basi Mshkaji akanipanga mambo ya kufanya, design sasa ikawa kama namsikiliza yeye kwa kila kitu,

Siku isiyokuwa na Jina nimeamka na mood Nzuri si nikampigia simu Accountant, hapo zimebaki siku 5 tu nirudi job ila kabla ya kurudi inabidi niwe nimefanya maamuzi ya kumkubali Accountant kimapenzi ili niendelee na Kazi (nimkatae Annie) au niache kazi nimkatae Accountant nibaki na Annie

BM: [emoji338]"Mambo"

Accountant: "Finally...hii simu nilikuwa naisubiria kwa hamu"

BM: "Ooh! uko wapi?"

Accountant: "Kazini"

BM: "Tunaweza kuonana Leo baada ya masaa ya kazi?"

Accountant: "Wewe tu"

BM: "Sawa basi nitakujulisha Mahali tutakapokutana"

Masaa nayo kwani yanakawia basi, jioni ndio hiyo Accountant nilishamtumia Location, tukakutana tena Mimi ndio nilimkuta yeye tukaagizia vinywaji story zikaanza, Wakati nampigisha story zingine nikawa nawaza jinsi ya kuingizia agenda yangu

BM: "Ivi ni Jumanne ndio likizo yangu inaisha eeh?"

Accountant: "Yeah, kwani unakuja kazini?"

BM: "Sasa kwanini nisije, si likizo imeisha"

Accountant akaniangalia kwa sekunde kadhaa Nikamuuliza "vipi kuna tatizo?"

Accountant: "Kuna Kitu una maanisha ila hutaki kufunguka, kama unakuja kazini ina maana umekubaliana na mimi yale matakwa yangu, right?"

BM: "Hayo mambo Tutaongea vizuri siku nyingine wala usijali"

Accountant: "Sasa hapa umeniitia Nini? umekuja kunipotezea muda wangu tu"

BM: "Okay! Relax, sasa hivi nimeamua kutulia na wewe lakini huku kupanic kwako ni moja ya sababu iliyonifanya nichelewe kufanya haya maamuzi"

Accountant: "Vipi kuhusu kidemu chako?"

BM: "Huyo nishaachana nae, ni Bora hata hili limetokea mapema maana nilikuwa tayari kuacha Kazi kwaajili yake"

Accountant: "Ooh, now I got your point, so mimi nipo hapa kama Option"

BM: "Hilo sasa umelisema wewe, ninachojua tu Mimi kwasasa nimefanya maamuzi sahihi katika Wakati sahihi"

Accountant: "But you guys mlikuwa mnapendana sana kiasi kwamba nilijua hamtoachana"

BM: "You know Love can be really without being forever"

Accountant: "Bado ni ngumu kuamini, there something fish"

Nilivyomtamkia Accountant kwamba nataka kuwa nae alifurahi sana lakini Bado hakuamini kama ni kweli nimeachana na Annie ila nikaendelea kumpiga kiswahili hadi akanielewa

Nikaachana na Accountant pale kila mtu akielekea njia yake Wakati tunaagana eti akataka kuja kulala kwangu ili a confirm kama ni kweli Annie nimeachana nae, nikamkataa kiaina bila ya kumkwaza maana Sasa hivi ni mwendo wa kula na kipofu

Weekdays zikapita, Weekend ikaanza nakumbuka siku ya jumapili mapema sana Sister Michelle akanicheki akaniomba niende home kuonana nae after church,

Ilivyofika saa Saba Mimi ndio huyo mdogo mdogo hadi kwa Mzee, nilivyofika Kona ya mwisho ya kuelekea nyumbani kwa Mzee kwa mbali naliona Jeep, nikajua tu huyu atakuwa ni Caryn bila shaka na kweli alivyonikaribia akasimamisha Gari

Caryn: "Hata kama ni ubahili hapana aise, BM umekosa hata elfu 2 ya pikipiki kweli?"

BM: "Nipatie hiyo elfu 2 nirudi highway nikapande hiyo bodaboda"

Caryn: "Nyumbani unaenda kufanya nini Sasa watu wenyewe hawapo, aliyekuwa amebaki ndio huyu anaishia"

Sasa Michelle Atakuwa na Akili gani ya kuniita halafu tena atoke, nikajisemea tu mwenyewe moyoni, Basi Caryn akanilazimisha niingie kwenye Gari, sisi hao breki Sinza Dukani kwake

Caryn: "BM Ivi ni maeneo gani mazuri ya kununua viwanja?"

BM: "Maeneo ninayoyajua Mimi kwasasa ambayo ni potential ni Kigamboni na Bagamoyo"

Caryn: "Bagamoyo hapana, nataka eneo ambalo naweza kufanya makazi"

BM: "Basi Kigamboni pata kufaa, hata Mimi nataka kuhamia huko"

Caryn: "Umeshajenga Kigamboni?"

BM: "Nahamia kwenye vi appointment tu, pesa ya kujenga natoa wapi Mimi sasa hivi"

Caryn: "If I were you ningekuwa nishajenga, kazi unayofanya ina pesa sana the problem is, you don't know where to stand"

BM: "Ila Caryn bhana huwa unanifurahishaga sometimes, sasa mimi na wewe Kuna tofauti gani au ni nani anastaili kumcheka mwenzake?"

Caryn: "Mimi kama sio Biashara ningekuwa nishajenga, nilitaka kwanza Biashara yangu ikomae vizuri"

Majibu mdomoni yakaniisha, najibu nini tena hapo, ghafla nikawa mnyonge, moyoni nikasema hii chance safari hii sitaki kuichezea, yani hadi Caryn kajua ninapopiga kazi kuna hela na hadi sasa hivi sijafanya jambo la maana

Nikapata wazo la kumshirikisha Caryn kwenye kipengele nilichonacho kazini nione kama anaweza nishauri jambo ingawa tayari nishampanga Accountant akapangika, nimepata ujasiri na kuhisi ni salama kumshirikisha Caryn kwasababu nae naona ananishirikisha kwenye baadhi ya mambo yake


Nilichokifanya Sasa nikamuelezea Caryn mkanda mzima, jinsi nilivyopata kazi kupitia huyo mwanamke na kuniwekea kizingiti Cha kutokurudi kazini hadi nimkubalie, kifupi nilimueleza Kila kitu kasoro upande wa Annie Ndio sijamueleza chochote, Baada ya kusikiliza maelezo kwa makini Caryn alianza kwa kuniuliza tena swali ambalo kwenye maelezo lilishajijibu

Caryn: "Do you love her"

BM: "I don't love her"

Caryn: "So you have no feelings for her and you've been sleeping with her!?"

BM: "We've been sleeping together for fun, there's no attachments it's called friends with benefits"

Caryn: "Well she got attached while you were playing your game of friends with benefit she fell in love with you

BM: "That girl is not close to what I want in a wife, not mentally, not educationally, not psychological"

Caryn:"So what do you want?"

BM: "Your advice"

Caryn: "Quit"

BM: "Una maanisha niache kazi?"

Caryn: "We fanya kama nilivyokuambia"

Huu Ushauri umekuja too late wakati ambao nimeshafanya maamuzi, sasa kulikuwa na haja gani ya kumruhusu Annie kwenda Mwanza mbaya zaidi nishajishusha kwa Accountant na mambo yalikuwa yashanyooka,

Wakati naendelea kuongea na Caryn, Michelle akapiga simu, Sasa vile simu ilivyokuwa nikaiangalia halafu nikamuangalia na Caryn, Caryn akahisi kitu akaniuliza "ni nani?" nikamjibu ni Michelle anapiga, akanambia "Achana nae utaongea nae badae"

BM: "Labda Kuna emergency anataka usaidizi"

Caryn: "Usaidizi gani bhana mtu nimemuacha yupo nyumbani"

BM: "Dah! we si umeniambia ametoka wewe, au sio wewe?"

Caryn: "Sasa ulitaka kwenda kushinda nae nyumbani mkifanya nini?"

BM: "Alinipigia simu bhana alitaka mazungumzo na Mimi huwezi jua alitaka kunambia nini"

Caryn: "Mimi namjua Michelle vizuri kinachomsumbua sasa hivi ni Mapenzi hana anachowaza pale mwenzako zaidi ya hicho"

BM: "We umejuaje? usipende kumuongelea mtu pengine mwenzako ana mambo yake mengine"

Caryn: "Unajua wewe umetujua juzi tu hapa, Mimi yule sio Dada yangu tu, we used to be very close, we used to be friends, so nikikuambia kitu kuhusu yeye Jua Nina uhakika nacho

BM: "Sasa kwanini Sasa hivi hamna ukaribu huo tena?"

Caryn: "Alinikosea, Alinikosea sana Yani pakubwa mno"

BM: "Alikukosea nini?"

Caryn: "Kama nilivyokuambia Mimi yule sio Dada yangu tu Bali alikuwa rafiki yangu pia, na unaijua sifa ya urafiki? So siwezi kukuambia alichonifanyia ila we Jua tu alinikosea"

BM: "Ila yeye kanambia, kanielezea kila kitu

Caryn: "Sasa yeye ni sawa kufanya hivyo kwasababu yeye ndio mkosani ila nikianza mimi kuongea kwa kila mtu atajisikia vibaya"

BM: "Lakini wewe si ulimsema kwa Mzee"

Caryn: "Lini? na saa ngapi?"

BM: "Kuna siku ulimsema bhana tena nikiwepo hiyo sijahadithiwa Wala nini, ulimsema kuhusu huyo Mwanaume wake mbele ya Mzee

Caryn: "Sasa vile ndio kumsema? vile si ni vitu vya kawaida tu, je ningeamua kusema vyote? and I'm sure hata wewe hajakuambia mambo yote"

BM: "Sioni Ubaya wa Sister Michelle ni kuteleza tu ameteleza, unajua sister ako yuko humble sana hana mambo mengi na ni muelewa"

Caryn: "Eti eeh! Okay"

Ilivyofika jioni nikamuacha Caryn Dukani kwake Mimi nikaenda kwa sister Yombo nikapiga na msosi huko huko nikarudi zangu Tabata

Kesho yake Jumatatu nakumbuka ilikuwa Nanenane hii siku sikutoka kabisa ndani ila mida ya jioni akaja Mshkaji wangu wa Kinondoni, alikuwa katika mishe mishe zake huku huku Tabata alivyomaliza akapitia mjengoni, akanikuta nabrash viatu

Mshkaji: "Nakubali mwanangu, kesho kazini sio"

BM: "Kama kawaida"

Mshkaji: "Nakubali, angalau siku hizi ushauri wangu unauzingatia....hujapika Mzee nina njaa kiseng*"

BM: "Mm huwa sipikagi, kwani hoteli zimefungwa huko ulipotoka?"

Mshkaji: "Hapo ndipo unapofeli"

Hii siku mshkaji aliangusha kwangu, mida mida tulienda kufinya msosi tukarudi mjengoni tukalala, ila sasa jamaa akagoma kulala chumbani akaenda kulala Sebuleni kwenye kochi

Tarehe 9 mwezi wa 8 (Jumanne) siku ya kuripoti kazini mapema tu nikajiandaa nikamuamsha na mshkaji sababu alitaka tutoke wote

Wakati nipo njiani nimeshaachana na mshkaji naelekea kazini kichwani nawaza kipi Cha kufanya na kipi Cha kuacha, kichwani wananijia watu wawili Caryn na mshkaji wangu, Caryn kanambia niache kazi huku Mshkaji kanambia niendelee na Kazi, Hadi nafika Ofisini Bado nipo njia panda

Nikasalimiana na staff wenzangu Accountant muda huo alikuwa hayupo nimeambiwa kaenda Bank ila Mama yake yani Bosi yupo Ofisini kwake, Mnyamwezi nikachoma ndani

Mama Accnt: "Karibu mwanang, Hujambo?"

BM: "Sijambo Mama Shikamoo"

Mama Accnt: "Marhaba mwanangu tulikumiss sana na umekuja Wakati muafaka huyu mwenzako uliyemuachia majukumu anaelemewa na Kazi?"

BM: "Bado haja Master tu? sababu akikwama huwa ananipigia simu namuelekeza"

Mama Accnt: "Tatizo ni kwamba mwenzako hajui kuongea na TRA kabisa, na hajui kubagain, kabla sijakuachia majukumu yangu itabidi uendelee kwenda nae trips kadhaa hadi atakapokuwa sawa"

BM: "Ni sawa, lakini Mama unajua Mimi nimekuja kukuaga, nimeona nikafanye majukumu mengine kwahiyo nilikuwa naomba ruksa yako"

Mama huwa anavaa miwani, kusikia hivyo akavua kwanza na mawani yenyewe, kuna vitu alikuwa anaandika akaacha akaweka peni chini yani ni kama vile hakutarajia kusikia nilichomuambia

Itaendelea
Caryn anakupoteza.[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Back
Top Bottom