Hatma ya mradi Stiegler’s Gorge: Hatakama hatukubaliana kiitikadi, tukubaliane katika Ushauri wa kitaalam

Hatma ya mradi Stiegler’s Gorge: Hatakama hatukubaliana kiitikadi, tukubaliane katika Ushauri wa kitaalam

Mada zako ni bora ila unakosea kuweka matangazo ya biashara! Kitabu tulishasoma na kila mtu anajuwa njia ya kukipata ebu leta mada bila kuwa na mlengo wa kibiashara Yeriko
Nilivyoanza kusoma Uzi huu, nikajua nitapata mawe makubwa,
Ghafla napelekwa kununua kitabu na hata bila ABC za alichotaka kutuambia leo.

Inaonekana Soko haliendi vizuri ameamua kuja kiaina ili kupromote soko la vitabu vyake.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tuna Uhuru wa kuwafanya chochote wanyama wetu tukawala au tukawapiga kibiriti
Mpelekeni Selemani Nchambi tu mbona mnajifanya kumuhifadhi kelele ziiishe

Ili iwe Arabs contractors ya kwelikweli
 
Mimi
Mimi sio nabii, lakini angalau nikisema jambo nakuwa nimeona kijacho mbeleni, Naomba nikukumbushe jambo muhimu ambalo niliandika 13 March 2019 katika makala hii chini,

Katika makala hii nilianza kwakusema, "Vita vya Kiuchumi Tanzania chini ya mradi mtambuka wa maporomoko ya Rufiji, siasa ya Mazingira duniani na muundo na mienendo ya Shirika la Elimu, Sayansi na Udhibiti wa Mazingira duniani (UNESCO), vinanipa sababu ya kuiponeza TISS katika ulimbe huu wa vita vya kiuchumi.

Bonde la Rufiji liko kwenye urithi wa dunia kwamjibu wa Shirika la Uhifadhi wa Mazingira (UNESCO), Na hivyo ulinzi wa bonde hili ni kwa sheria za kidunia sio kwa sheria za Tanzania, hapa ndipo ambapo nataka kusifu idara za ujasusi na kumsifu Rais Magufuli kwa kuishinda dunia dhidi ya misimano na sera za mashirika haya ya kidunia ambayo Mwalimu yalimshinda, Mwinyi yalimshinda, Mkapa yakamshinda, Kikwete yakamshinda

Kwa wiki kadhaa nimekuwa nikipitia nyaraka za kijasusi za mashirika na taasisi mbalimbali ulimwenguni (Realiised docs), nimejiridhisha kuwa vita nikubwa kuliko wengi wanavyofikiri, na ikiwa mradi wa umeme bonde la Rufiji utafanikiwa, basi TISS itaingia kwenye historia ya mashirika bora kabisa ulimwenguni kwa counter intelligence hii. Palipo na uthubutu lazima tupongeze,

Awali mradi huu wa Umeme wa Stiegler's Gorge Ethiopia walikubali kujenga, lakini hakuna maelezo kama waliishia wapi ama walishindwa tenda. Zikawepo taarifa za Waturuki kuwa watajenga, nazo zikaishia hewani. Kisha tukashuhudia Arabb Contractors wa Misri wakisaini mikataba ya ujenzi. Bado ujenzi rasmi haijaanza, lakini hatua tu ya kuthubutu kusaini mkataba ni hatua kubwa inayostahili kupongezwa.

Bunge la Ujerumani liliweka azimo kuitaka serikali ya nchi hiyo kuzuia ujenzi wa mradi huo wa Rufiji na badala yake serikali ya Ujerumani isaidie kujenga vinu vya gesi kwaajili ya nishati ya umeme. Kwakuangazia jambo hili watu wengi wanaweza kujiuliza, itakuwaje nchi ya Ujerumani iingilie masuala ya ndani ya Tanzania? Mifumo ya kijasusi iko hivi, kwamjibu wa Nyaraka za idara ya ujasusi ya nchini Lithium (Anual report 2016) inaonyesha kuwa Ujerumani pekee ina majasusi 11 wa ngazi za juu ndani ya UNESCO, na kwa nadharia hiyo, Ujerumani ikitaka kuzuia miradi yoyote yenye uharibifu wa mazingira inatumia msukumo wa UNESCO.

Kinachoweza kutokea ni kuwa UNESCO inaweza kuiandikia barua ya katazo nchi husika kwamba pale ni sehemu ya Urithi wa Dunia (World Heritage site.) na hairuhuriwi kupajenga. Na wanaonya kuwa ukiwa mbishi na ukaendelea kujenga utakuwa black listed. Na kampuni inayopata tenda ya kujenga nayo inapewa barua na kuonywa kuwa itakuwa black listed na Bank Account zako zitakamatwa. Kwakufanya hivyo wanashinikiza kampuni zijitoe katika mradi husika.

Majasusi hawa wamefanya hivyo kuidhibiti Iran, enzi za Reza Khan kwakutumia mashirika haya ya kidunia , ambayo mengi ni mashirika ya kijasusi. Pia nchi za Panama zimewahi kukumbana na nguvu ya mashirika haya.

Kwa namna yoyote naipongeza Serikali kwa ujasiri huu wa kufunga masikio na kelele za kidunia na kuamua kuanzisha mradi huu uliokwamba tangu miaka ya 60+. Hii ni hatua kubwa sana na ninaamini itaacha legacy kubwa sana kwa rais Magufuli na kwa vyombo vya ujasusi nchini ikiwa utafanikiwa, ingawa hakuna nchi au kikundi kilichowahi kushindana na mashirika haya ya kidunia na kikashinda, zaidi ya hapo labda ziwe ni siasa za kura. Bado naamini tumethubutu pakubwa sana, na katika ndoto tutashinda". Makala iliishia hapo.

Sasa mwaka mmoja na baadaa ya makala hii, Kampuni iliyokuwa ikijenga mradi huo imeandika taarifa hii ambayo inajumuisha ndani yake katazo la UNESCO. Isome hapa kwa lugha ya kitumwa....>>> ElSewedy Electric Co - Council on Ethics

Unaweza kujipa nafasi ya kusoma kwa undani zaidi kitabu cha Ujasusi kujua nama Ujasusi dhidi ya Ujasusi unavyofanya kazi na mifano hai toka katika viunga vya dunia ya ujasusi.

Nunua Kitabu kwa Ofa ya Mwezi Mtukufu na #Corona kwa 25,000 tu popote ulipo. Badala ya bei halisi ya 80,000/=

Nunua kwa Mpesa na Tigopesa 0715865544/ 0755865544 (Yericko Nyerere) kisha tuma majina yako na mahali ulipo.

Kwa Dar kitabu kitaletwa ulipo bure. Nje ya Dar nauli ni 8,000/=
Mimi niliahidi kikifika bei ya buku, ndio nitakinunua!
 
Ewe jasusi uchwara Ethiopia wanajengewa bwawa lao na Waitaliano halafu wangekuja kutujengea sisi?!

Ewe jasusi uchwara unayelima bamia Mbutu unawezaje kujua sehemu Ujerumani walipoweka majasusi wake duniani?

Ewe jasusi uchwara intelegensia yako inasemaje kuhusu kushindwa kwa bomba la gesi kutuletea umeme wa kutosha kama tulivyoahidiwa?
Hujambo ndugu, mengine hayana maana, naomba kidogo tuchombezi juu ya kisa cha bomba la gesi kuyeyuka.

Tanzania ilifanikisha kwa 💯, hili apongezwe Jasusi mkuu aliyeongoza vita Marehemu mzee Mahiga. Kenya walisanda kabisa.

Majasusi wa kimataifa kutoka USA, Ufaransa na Uchina wapigana vita wao kwa wao kupigania nani ajenge, nani asafirishe, na nani awe Sub-Contractor.

Mwenye tenda ya mradi alikuwa Mfaransa (Total), dili la kusafirisha akalishika USA, Sub Contractor akaidaka mchina, sasa vita vikaanzia hapo kwamba mchina kaingizwa na Mfaransa huku USA hajashirikishwa kumkubali. Hii inamaana kuwa USA alitaka alete mtu wake yule mjomba wale kutoka kutoka Cambridge. Mvutano ulipokuwa miubwa Mfaransa mwenye dili akasema sitoi mpunga na sijengi.... Hivyo sisi wengine tunasubiri wanyukane kisha mshindi tutajenga nae.... Tatizo ni je msindi atatoa hela?
 
Vitu vingine tunaandika humu naonaga ni delusions tu. Sioni role yoyote ya TISS kwenye huo mradi, kwa mfano TISS wamepambana na nani ili huo mradi uendelee au wameshauri nini.
Wataalam wa ndani na nje ya nchi waliandika na kusema huo mradi haufai, utaharibu mazingira na hata kuvuruga maisha ya watu downstream.
Global warming na uharibifu wa mazingira pia umeathiri kiwango cha maji kwenye mito mingi ikiwamo Rufiji.
Kimsingi huo mradi haufai, utaishia kuwa the only white elephant in Selous game reserve.
Halafu hapo ulipoandika realised documents nafikiri unamaanisha declassified documents. Tutaendelea kuelekezana taratibu jasusi Yericko Nyerere.
 
Mwenye Tenda ya mradi upi?

Kampuni inayozalisha gas nyingi inayosafirishwa ni kampuni ya Uingereza.

Aliyeshinda tenda ya kujenga bomba ni kampuni ya Kichina na kwa mkopo kutoka benki ya Exim ya China,bomba limejengwa na gesi inasafirishwa.

Hivyo visa vyako vya vita ya majasusi umevipata wapi kama sio stori za kutunga?
Hujambo ndugu, mengine hayana maana, naomba kidogo tuchombezi juu ya kisa cha bomba la gesi kuyeyuka.

Tanzania ilifanikisha kwa [emoji817], hili apongezwe Jasusi mkuu aliyeongoza vita Marehemu mzee Mahiga. Kenya walisanda kabisa.

Majasusi wa kimataifa kutoka USA, Ufaransa na Uchina wapigana vita wao kwa wao kupigania nani ajenge, nani asafirishe, na nani awe Sub-Contractor.

Mwenye tenda ya mradi alikuwa Mfaransa (Total), dili la kusafirisha akalishika USA, Sub Contractor akaidaka mchina, sasa vita vikaanzia hapo kwamba mchina kaingizwa na Mfaransa huku USA hajashirikishwa kumkubali. Hii inamaana kuwa USA alitaka alete mtu wake yule mjomba wale kutoka kutoka Cambridge. Mvutano ulipokuwa miubwa Mfaransa mwenye dili akasema sitoi mpunga na sijengi.... Hivyo sisi wengine tunasubiri wanyukane kisha mshindi tutajenga nae.... Tatizo ni je msindi atatoa hela?
 
Huyu ni jasusi uchwara anayetumia ujinga wa wabongo wengi kujipatia kipato kwa kuuza vitabu anavyoandika kwa kukusanya stori uchwara za mitandaoni na kufanya hadaa kwamba ni mambo halisi ya kijasusi.
Vitu vingine tunaandika humu naonaga ni delusions tu. Sioni role yoyote ya TISS kwenye huo mradi, kwa mfano TISS wamepambana na nani ili huo mradi uendelee au wameshauri nini.
Wataalam wa ndani na nje ya nchi waliandika na kusema huo mradi haufai, utaharibu mazingira na hata kuvuruga maisha ya watu downstream.
Global warming na uharibifu wa mazingira pia umeathiri kiwango cha maji kwenye mito mingi ikiwamo Rufiji.
Kimsingi huo mradi haufai, utaishia kuwa the only white elephant in Selous game reserve.
Halafu hapo ulipoandika realised documents nafikiri unamaanisha declassified documents. Tutaendelea kuelekezana taratibu jasusi Yericko Nyerere.
 
Labda sijui jambo hapa. Hizi pongezi kwa TISS zina maana gani huku ukimsifia Rais dhidi ya wenzake walioshindwa??

Tumechemka kwenye mtadi huu, tulipaswa kuutumia kama kigezo cha kuwalazimisha kufanya uwekezaji katika eneo lingine!! Tungeweza hata kupata umeme wa nyuklia. Iran na North Korea zimetumia vitu kadhaa kulazimisha haya mashirika ya kimataifa kufanya mambo kadhaa.

Ninadhani hukupaswa kupongeza TISS, ulipaswa kushauri vyombo vya serikali vitafute njia za kujadiliana ili kuwe na win-win situation. Katika swala la umeme, tunaonekana kama kuna zero sum!
 
Mkuu ninavyomjua jemedari wetu alivyojasiri wakigoma atawaweka wanajeshi wajenge! Piga kazi baba mabeberu hawawezi kukushinda.
 
Tutawasingizia mabeberu..bila wao mradi ungekamilika.

Wananchi watatuelewa.

Sent using iphone pro max
 
..tunahitaji umeme wa maji lakini siyo kwa style na utaratibu huu aliotumia bwana mkubwa.

..kwanza, mradi wa stieglers ni mkubwa sana, unatumia fedha nyingi, na muda mrefu kukamilika.

..pili, ni mradi ambao unatugombanisha na marafiki na wadau wetu wa maendeleo.

..kwa maoni yangu, serikali ilipaswa kujenga miradi ya ukubwa wa kati. Na miradi hiyo ijengwe ktk vyanzo ambavyo havina migogoro na wafadhili wetu.

..advantage ya hatua hiyo ingekuwa kuingiza umeme kwa awamu bila kusuburi muda mrefu kama tunavyofanya kwenye mradi wa stieglers. Pia tusingekuwa na ugomvi na marafiki na wafadhili wetu. Zaidi tungekuwa na fedha za kugharamia miradi mingine muhimu kama viwanda, kilimo cha umwagiliaji, etc etc.

..Stieglers inatumia fedha nyingi, na imesababisha miradi mingine muhimu ikose fedha. Waswahili wana msemo kuwa " tumeweka mayai yote ktk kikapu kimoja ."
 
Mwenye Tenda ya mradi upi?

Kampuni inayozalisha gas nyingi inayosafirishwa ni kampuni ya Uingereza.

Aliyeshinda tenda ya kujenga bomba ni kampuni ya Kichina na kwa mkopo kutoka benki ya Exim ya China,bomba limejengwa na gesi inasafirishwa.

Hivyo visa vyako vya vita ya majasusi umevipata wapi kama sio stori za kutunga?
Unajua gesi ipi inayoongelewa ni liquified natural gas project likong'o na mchinga, sio iko kibomba Cha hapo kinyerezezi, usijifanye mjuaji alafu hujui vitu
 
'iko kibomba Cha hapo kinyerezezi' kinatoa gesi gani,kutoka wapi kwenda wapi?
Unajua gesi ipi inayoongelewa ni liquified natural gas project likong'o na mchinga, sio iko kibomba Cha hapo kinyerezezi, usijifanye mjuaji alafu hujui vitu
 
'iko kibomba Cha hapo kinyerezezi' kinatoa gesi gani,kutoka wapi kwenda wapi?
Tofauti kinyerezi na mradi wa likongo na mchinga ni miradi miwili tofauti, usipende lig kwa mambo ambayo yako wazi utaonekana mjinga
 
Kati ya miradi inayothibitisha ujinga wa serikali yetu ni pamoja na huu wa umeme...
Huu mradi una madhara makubwa sana siku zijazo kuliko Covid-19...
Najua wengi hawajui thamani ya mazingira... Na wengi zaidi hawajui madhara yatokanayo na mabadiliko ya tabia ya nchi...
Majuzi hapa si mlishuhudia mafuriko yaliyodumu wiki kadhaa kule RUMAKI na kule Mikumi? Basi ile ni trela... Majanga yajayo yanatisha....!!
Kifupi tu ni kuwa mtu yeyote mwenye akili timamu hawezi kuunga mkono ujenzi wa hilo bwawa...!!
Mwana kulitafuta.... Mwanakulipata!!
 
Mimi sio nabii, lakini angalau nikisema jambo nakuwa nimeona kijacho mbeleni, Naomba nikukumbushe jambo muhimu ambalo niliandika 13 March 2019 katika makala hii chini,

Katika makala hii nilianza kwakusema, "Vita vya Kiuchumi Tanzania chini ya mradi mtambuka wa maporomoko ya Rufiji, siasa ya Mazingira duniani na muundo na mienendo ya Shirika la Elimu, Sayansi na Udhibiti wa Mazingira duniani (UNESCO), vinanipa sababu ya kuiponeza TISS katika ulimbe huu wa vita vya kiuchumi.

Bonde la Rufiji liko kwenye urithi wa dunia kwamjibu wa Shirika la Uhifadhi wa Mazingira (UNESCO), Na hivyo ulinzi wa bonde hili ni kwa sheria za kidunia sio kwa sheria za Tanzania, hapa ndipo ambapo nataka kusifu idara za ujasusi na kumsifu Rais Magufuli kwa kuishinda dunia dhidi ya misimano na sera za mashirika haya ya kidunia ambayo Mwalimu yalimshinda, Mwinyi yalimshinda, Mkapa yakamshinda, Kikwete yakamshinda

Kwa wiki kadhaa nimekuwa nikipitia nyaraka za kijasusi za mashirika na taasisi mbalimbali ulimwenguni (Realiised docs), nimejiridhisha kuwa vita nikubwa kuliko wengi wanavyofikiri, na ikiwa mradi wa umeme bonde la Rufiji utafanikiwa, basi TISS itaingia kwenye historia ya mashirika bora kabisa ulimwenguni kwa counter intelligence hii. Palipo na uthubutu lazima tupongeze,

Awali mradi huu wa Umeme wa Stiegler's Gorge Ethiopia walikubali kujenga, lakini hakuna maelezo kama waliishia wapi ama walishindwa tenda. Zikawepo taarifa za Waturuki kuwa watajenga, nazo zikaishia hewani. Kisha tukashuhudia Arabb Contractors wa Misri wakisaini mikataba ya ujenzi. Bado ujenzi rasmi haijaanza, lakini hatua tu ya kuthubutu kusaini mkataba ni hatua kubwa inayostahili kupongezwa.

Bunge la Ujerumani liliweka azimo kuitaka serikali ya nchi hiyo kuzuia ujenzi wa mradi huo wa Rufiji na badala yake serikali ya Ujerumani isaidie kujenga vinu vya gesi kwaajili ya nishati ya umeme. Kwakuangazia jambo hili watu wengi wanaweza kujiuliza, itakuwaje nchi ya Ujerumani iingilie masuala ya ndani ya Tanzania? Mifumo ya kijasusi iko hivi, kwamjibu wa Nyaraka za idara ya ujasusi ya nchini Lithium (Anual report 2016) inaonyesha kuwa Ujerumani pekee ina majasusi 11 wa ngazi za juu ndani ya UNESCO, na kwa nadharia hiyo, Ujerumani ikitaka kuzuia miradi yoyote yenye uharibifu wa mazingira inatumia msukumo wa UNESCO.

Kinachoweza kutokea ni kuwa UNESCO inaweza kuiandikia barua ya katazo nchi husika kwamba pale ni sehemu ya Urithi wa Dunia (World Heritage site.) na hairuhuriwi kupajenga. Na wanaonya kuwa ukiwa mbishi na ukaendelea kujenga utakuwa black listed. Na kampuni inayopata tenda ya kujenga nayo inapewa barua na kuonywa kuwa itakuwa black listed na Bank Account zako zitakamatwa. Kwakufanya hivyo wanashinikiza kampuni zijitoe katika mradi husika.

Majasusi hawa wamefanya hivyo kuidhibiti Iran, enzi za Reza Khan kwakutumia mashirika haya ya kidunia , ambayo mengi ni mashirika ya kijasusi. Pia nchi za Panama zimewahi kukumbana na nguvu ya mashirika haya.

Kwa namna yoyote naipongeza Serikali kwa ujasiri huu wa kufunga masikio na kelele za kidunia na kuamua kuanzisha mradi huu uliokwamba tangu miaka ya 60+. Hii ni hatua kubwa sana na ninaamini itaacha legacy kubwa sana kwa rais Magufuli na kwa vyombo vya ujasusi nchini ikiwa utafanikiwa, ingawa hakuna nchi au kikundi kilichowahi kushindana na mashirika haya ya kidunia na kikashinda, zaidi ya hapo labda ziwe ni siasa za kura. Bado naamini tumethubutu pakubwa sana, na katika ndoto tutashinda". Makala iliishia hapo.

Sasa mwaka mmoja na baadaa ya makala hii, Kampuni iliyokuwa ikijenga mradi huo imeandika taarifa hii ambayo inajumuisha ndani yake katazo la UNESCO. Isome hapa kwa lugha ya kitumwa....>>> ElSewedy Electric Co - Council on Ethics

Unaweza kujipa nafasi ya kusoma kwa undani zaidi kitabu cha Ujasusi kujua nama Ujasusi dhidi ya Ujasusi unavyofanya kazi na mifano hai toka katika viunga vya dunia ya ujasusi.

Nunua Kitabu kwa Ofa ya Mwezi Mtukufu na #Corona kwa 25,000 tu popote ulipo. Badala ya bei halisi ya 80,000/=

Nunua kwa Mpesa na Tigopesa 0715865544/ 0755865544 (Yericko Nyerere) kisha tuma majina yako na mahali ulipo.

Kwa Dar kitabu kitaletwa ulipo bure. Nje ya Dar nauli ni 8,000/=
Kazi ipo!!
 
Back
Top Bottom